Dizasta Vina - Hatia IV

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 12 ธ.ค. 2020
  • Category: Music
    Song: Hatia IV
    Artist: Dizasta Vina
    Music: Ringle Beatz
    TH-cam: / jwa21m5eyl
    Mdundo: mdundo.com/song/1670618
    Audiomack: audiomack.com/dizastavina/son...
    Soundcloud: / hatiaiv
    Lyrics: genius.com/Dizasta-vina-hatia...
    Other Musical contents
    Audiomack - audiomack.com/dizastavina
    TH-cam - / dizastavina
    Deezer - www.deezer.com/artist/67967532
    Apple music - artists.apple.com/a/profile
    Mdundo - mdundo.com/a/2263
    Genius - genius.com/DizastaVina
    Boom play - www.boomplay.com/artists/3288... - artists.spotify.com/c/artist/...
    Connect with Dizasta Vina on social medias
    Instagram - / dizastavina
    Twitter - / dizastavina
    Facebook - / dizastavina07
    sw.wikipedia.org/wiki/Dizasta...
    Business: Pan.authentik@yahoo.com
    Website - bio.link/dizastavina
    Lyrics
    “JASIRI JOHN….. ALIYAANGALIA MAISHA YAKE
    HAKUONA JINSI ANGEWEZA KUISHI BILA JANE
    MSICHANA ANAYEMPENDA
    LICHA YA KUZONGWA NA UMASIKINI
    ALIJITAHIDI KUMPA JANE MAHITAJI MADOGOMADOGO KADRI ALIVYOWEZA
    LAKINI ALIFAHAMU SHUBIRI YA KUSUBIRI KUPENDWA HUKU ANAFAHAMU KUSUBIRI KUPENDWA NI
    MATUMAINI YANAYOUMIZA. KAMA WANAVYOSEMA, MTAFUTAJI HACHOKI AKICHOKA KASHAPATA…
    .ALIENDELEA KUNGOJA”
    Ah! Sikuwa na zali sikuziamini ndumba
    Sikuwa na mali za kufuja
    Nilijitahidi kuuza mitumba kufuga mipunga
    Ili siku nimpe gari nimpe nyumba. Nilishindwa…
    Niliishia kumpa chai, ‘chipsi’ mayai na ‘vocha’
    Nywele za kimasai na mkoba
    Pesa za magauni, majuba na viatu vya kuzuga
    Nilimpa muda ila bado haikutosha, kwani…
    Nilipomwambia nampenda hakujibu
    Akaweka moyo wangu maumivu
    Na mtima wangu akauweka ‘solemba’
    Nikaapia kuwa sitakuja kupenda ‘forever’
    Ah! Nilimpa upendo nilimpa sifa
    Niliweka mitego ya faida, haikuwa shwari
    Nikabadili mwenendo wa maisha
    Niliweka malengo sikutimiza, hakunikubali
    Alikuwa na ndoto kubwa kushinda mimi
    Alikuwa na misimamo kuipita dini
    Aliniambia ameomba nije kuokota utajiri
    Amengoja sana na sasa amechoka kusubiri
    Ah! Sikuwa na hali ya kuikosha roho yake
    Nilimwacha aende aufate moyo wake
    Alipata bwana wa kizungu magharibi
    Alimwahidi kuishi maisha ya ndoto zake
    Nilipata uchungu niliishia kuhamaki nilitaka nijiue
    Nilitaka nimzuie abaki nikakumbuka
    Ukipenda ua haulikati unaliacha likue
    Duka langu nilifunga biashara niliacha zote
    Uchumi uliyumba kwa maana nilianza pombe
    Niliumwa bado kidogo moyo uzime
    Nilimfanya ndoto kumbe naye ana ndoto nyingine
    Alisema anakwenda jiji la Miami
    Hakuna alichowaza zaidi ya kuishi kifahari
    Kamtumia picha na ‘mchizi’ kazikubali
    Na yupo tayari kumlipia gharama za safari
    Aliondoka na kipande kimoja cha mwili
    Nilikonda nilipata ugonjwa wa akili
    Haikuwahi kupita hata sekunde nisilie
    Nilitamani mpaka ardhi ipasuke niingie
    Ah! Muda ukaenda nitapata ‘Mwanamwali’
    Nikamwomba awe mwenza wa maisha akakubali
    Nikamvisha pete nikalipia mahari
    Sikumpenda lakini nilijifunza kumjali
    Aliuliza kama nampenda, nilimjibu
    Sikutaka kuweka moyo wake maumivu
    Sikutaka kuuweka Mtima wake solemba
    Kiasi aseme hatakuja kupenda ‘‘forever’’
    Ah alinikumbatia nikamfunga kwa ishara
    Akanikabidhi tunda nikala
    Akaniamini tukajuana nikapanga kumwoa
    Akaidhisha na tukaanza na mipango ya ndoa
    “Habari naamini u bukheri wa afya
    Unaendeleaje maisha na huyo mpenzi wa sasa
    .nashukuru nahema ughaibuni si kwema
    Nakiona cha mtema mpaka naona ni heri nikafa…
    Ah! Maisha niliyowaza yote ni uongo
    Nauzishwa madawa nalazimishwa ngono
    Nafungiwa ndani kama mtumwa ufungwani
    Roho yangu rehani kiasi sasa naitamani Bongo
    Ukubwa umekuja kunisafisha jicho
    Ndoto imeisha na taswira imenionyesha sivyo, ah
    Naomba unifate uniondoshe kwenye hichi kifo
    Na hii namba ya msamaria atakueleza nilipo”
    Sherehe ilikuwa na mipango madhubuti
    Kabla mimi kuichukua michango ya Harusi
    Nikatoroka ughaibuni kufuata hisia zangu
    Kwenda kumfata njiwa wangu mahususi
    Nilivuka majangwa na majabali
    Sehemu ya safari anga sehemu nyingine bahari
    Niliacha kila kitu nyuma upendo na huruma vilinijaa
    Penzi likanipeleka mbali
    Nikakutana na bopa la kizungu
    Lenye sura ya kuichachisha mboga kwenye chungu
    Kiko kwenye mdomo,Tatuu kila kona na wapambe
    Pamoja na vishoka wenye mtutu
    Sio siri alizungukwa na wasichana wengi
    Sikujua umri walikuwa wadogo ka’ “madent”
    Baadhi walikuwa uchi wanahesabia “chenchi”
    Wengine masaji huku wengine wanamchezea nyeti
    Hata nilipomuuliza kama ananipenda hakujibu
    Akaweka moyo wangu maumivu
    Nilijua hawezi kufa kwa sababu hakunipenda
    Na ni rasmi nikapoteza shilingi kwenye msitu
    Nilikiambia kifo kama unakuja njoo
    Maana sikuwa mtu ilishakufa roho
    Sikuumia kama alivyoniumiza yeye
    Kwahiyo sikujali jinsi nilivyoteswa na wale mbwa no
    Aliambiwa ambusu bosi hakubisha
    Alipewa bunduki hakusita
    Aliishika risasi akaiingiza
    Akaambiwa anipige kwenye kichwa
  • เพลง

ความคิดเห็น • 643

  • @joshmangi
    @joshmangi 3 ปีที่แล้ว +9

    "Nilimfanya ndoto, kumbe naye ana ndoto nyingine"

  • @dizastavina
    @dizastavina  3 ปีที่แล้ว +94

    “JASIRI JOHN….. ALIYAANGALIA MAISHA YAKE
    HAKUONA JINSI ANGEWEZA KUISHI BILA JANE
    MSICHANA ANAYEMPENDA
    LICHA YA KUZONGWA NA UMASIKINI
    ALIJITAHIDI KUMPA JANE MAHITAJI MADOGOMADOGO KADRI ALIVYOWEZA
    LAKINI ALIFAHAMU SHUBIRI YA KUSUBIRI KUPENDWA HUKU ANAFAHAMU KUSUBIRI KUPENDWA NI
    MATUMAINI YANAYOUMIZA. KAMA WANAVYOSEMA, MTAFUTAJI HACHOKI AKICHOKA KASHAPATA…
    .ALIENDELEA KUNGOJA”
    Ah! Sikuwa na zali sikuziamini ndumba
    Sikuwa na mali za kufuja
    Nilijitahidi kuuza mitumba kufuga mipunga
    Ili siku nimpe gari nimpe nyumba. Nilishindwa…
    Niliishia kumpa chai, ‘chipsi’ mayai na ‘vocha’
    Nywele za kimasai na mkoba
    Pesa za magauni, majuba na viatu vya kuzuga
    Nilimpa muda ila bado haikutosha, kwani…
    Nilipomwambia nampenda hakujibu
    Akaweka moyo wangu maumivu
    Na mtima wangu akauweka ‘solemba’
    Nikaapia kuwa sitakuja kupenda ‘forever’
    Ah! Nilimpa upendo nilimpa sifa
    Niliweka mitego ya faida, haikuwa shwari
    Nikabadili mwenendo wa maisha
    Niliweka malengo sikutimiza, hakunikubali
    Alikuwa na ndoto kubwa kushinda mimi
    Alikuwa na misimamo kuipita dini
    Aliniambia ameomba nije kuokota utajiri
    Amengoja sana na sasa amechoka kusubiri
    “JOHN ALIFAHAMU HALI YA JANE, KUWA JANE ALIZALIWA KWENYE
    FAMILIA MASIKINI, NA ALIUCHUKIA MNO UMASIKINI.
    ALIFAHAMU UMASIKINI ULIVYOCHUKUA UHAI WA MAMA YAKE KIPENZI,
    ALIYEFARIKI KWA KUKOSA MATIBABU. ALIIFAHAMAU NADHIRI ALIYOIWEKA JANE YA KWAMBA
    HATOKUBALI TENA KUISHI KWENYE MAISHA YA KIMASIKINI, NADHIRI ILIYO MWEKA JOHN NJIAPANDA”
    Ah! Sikuwa na hali ya kuikosha roho yake
    Nilimwacha aende aufate moyo wake
    Alipata bwana wa kizungu magharibi
    Alimwahidi kuishi maisha ya ndoto zake
    Nilipata uchungu niliishia kuhamaki nilitaka nijiue
    Nilitaka nimzuie abaki nikakumbuka
    Ukipenda ua haulikati unaliacha likue
    Duka langu nilifunga biashara niliacha zote
    Uchumi uliyumba kwa maana nilianza pombe
    Niliumwa bado kidogo moyo uzime
    Nilimfanya ndoto kumbe naye ana ndoto nyingine
    Alisema anakwenda jiji la Miami
    Hakuna alichowaza zaidi ya kuishi kifahari
    Kamtumia picha na ‘mchizi’ kazikubali
    Na yupo tayari kumlipia gharama za safari
    Aliondoka na kipande kimoja cha mwili
    Nilikonda nilipata ugonjwa wa akili
    Haikuwahi kupita hata sekunde nisilie
    Nilitamani mpaka ardhi ipasuke niingie
    “JANE ALIPOONDOKA ALIMWACHIA JOHN KIDONDA KILICHOCHELEWA SANA KUPONA
    NA YEYE AKAWEKA NADHIRI YA KUTOJIHUSISHA NA MAPENZI TENA MAISHANI MWAKE.
    ALIKAA KWA MUDA MREFU BILA MAHUSIANO. LAKINI…
    HAKUNA DAKTARI MZURI KAMA MUDA, JOHN ALIPONA MAUMIVU NA ALIIRUDIA HALI YAKE YA KAWAIDA”
    Ah! Muda ukaenda nitapata ‘Mwanamwali’
    Nikamwomba awe mwenza wa maisha akakubali
    Nikamvisha pete nikalipia mahari
    Sikumpenda lakini nilijifunza kumjali
    Aliuliza kama nampenda, nilimjibu
    Sikutaka kuweka moyo wake maumivu
    Sikutaka kuuweka Mtima wake solemba
    Kiasi aseme hatakuja kupenda ‘‘forever’’
    Ah alinikumbatia nikamfunga kwa ishara
    Akanikabidhi tunda nikala
    Akaniamini tukajuana nikapanga kumwoa
    Akaidhisha na tukaanza na mipango ya ndoa
    “WAKATI KARNE YA 21 INAINGIA, JOHN ALIKUWA NI MIONGONI MWA
    VIJANA WALIOKUWA ‘FASCINATED’ NA UKUAJI WA TEKNOLOJIA YA MITANDAO YA KIJAMII.
    ALIJIUNGA NA DUNIA HII MPYA, MARA KADHAA ALIKAA KWENYE UBARAZA, AKIANGAZA SIMU YAKE.
    AKIPAPASA KILA KITUFE, NDIPO SIKU MOJA AKAPATA UJUMBE KUTOKA KWA JANE”
    “Habari naamini u bukheri wa afya
    Unaendeleaje maisha na huyo mpenzi wa sasa
    .nashukuru nahema ughaibuni si kwema
    Nakiona cha mtema mpaka naona ni heri nikafa…
    Ah! Maisha niliyowaza yote ni uongo
    Nauzishwa madawa nalazimishwa ngono
    Nafungiwa ndani kama mtumwa ufungwani
    Roho yangu rehani kiasi sasa naitamani Bongo
    Ukubwa umekuja kunisafisha jicho
    Ndoto imeisha na taswira imenionyesha sivyo, ah
    Naomba unifate uniondoshe kwenye hichi kifo
    Na hii namba ya msamaria atakueleza nilipo”
    Sherehe ilikuwa na mipango madhubuti
    Kabla mimi kuichukua michango ya Harusi
    Nikatoroka ughaibuni kufuata hisia zangu
    Kwenda kumfata njiwa wangu mahususi
    Nilivuka majangwa na majabali
    Sehemu ya safari anga sehemu nyingine bahari
    Niliacha kila kitu nyuma upendo na huruma vilinijaa
    Penzi likanipeleka mbali
    “JOHN ALIFIKA UGHAIBUNI, AKAMTAFUTA MSAMARIA ALIYETAMBULISHWA NA UJUMBE,
    MSAMARIA AKAMWELEKEZA NJIWA WAKE ALIPO, NA NIKWELI… HAPAKUWA PEMA”
    Nikakutana na bopa la kizungu
    Lenye sura ya kuichachisha mboga kwenye chungu
    Kiko kwenye mdomo,Tatuu kila kona na wapambe
    Pamoja na vishoka wenye mtutu
    Sio siri alizungukwa na wasichana wengi
    Sikujua umri walikuwa wadogo ka’ “madent”
    Baadhi walikuwa uchi wanahesabia “chenchi”
    Wengine masaji huku wengine wanamchezea nyeti
    “MASIKINI JOHN, ALIDANGANYA KWA KUJITAMBULISHA KAMA KAKA KWA JANE,
    AKIMSIHI YULE MAFIA AMRUHUSU AONDOKE NA JANE WAKAANZE MAISHA MAPYA,
    LAKINI… PALIPOSHINDWA SHOKA WEMBE HAUWEZI TAMBA. KWA KUZIDIWA NA UOGA WA KUUAWA…
    JANE ALIMKANA JOHN KWA KUSEMA HAMJUI…”
    Hata nilipomuuliza kama ananipenda hakujibu
    Akaweka moyo wangu maumivu
    Nilijua hawezi kufa kwa sababu hakunipenda
    Na ni rasmi nikapoteza shilingi kwenye msitu
    Nilikiambia kifo kama unakuja njoo
    Maana sikuwa mtu ilishakufa roho
    Sikuumia kama alivyoniumiza yeye
    Kwahiyo sikujali jinsi nilivyoteswa na wale mbwa no
    Aliambiwa ambusu bosi hakubisha
    Alipewa bunduki hakusita
    Aliishika risasi akaiingiza
    Akaambiwa anipige kwenye kichwa
    JOHN ALIKUWA NI JINA JIPYA LA WAHANGA WA UPENDO WA DHATI, VIPOFU WA MAPENZI, WAJINGA WA MAHABA...
    JOHN ALIKUWA ROMEO KWENYE ROMEO AND JULIETH, ALIKUWA SAMSON KWA DELILAH KWENYE WAHUKUMU WA AGANO LA KALE, ALIKUWA JACK KWENYE TITANIC, FRED WEASLEY KWENYE HARRY POTTER..
    JOHN ALITUKUMBUSHA KUWA UPENDO NI SADAKA, SADAKA YA MUDA NA PESA, ALITUKUMBUSHA UPENDO NI SADAKA YA DAMU
    JOHN, ALIPOTEZA UHAI AKIWA KWENYE SAFARI YA KUTAFUTA UPENDO WA MTU ALIYEMHUSUDU NA
    JANE ALIPOTEZA AMANI NA THAMANI YAKE KAMA MTU AKIWA KWENYE SAFARI YA KUTAFUTA UTAJIRI ALIOUHUSUDU
    Hatia iko wapi?

    • @challymchaff374
      @challymchaff374 3 ปีที่แล้ว +1

      Daaah dizasta wewe ni vina hivi naanzaje kuchoka kusikiliza nyimbo zako

    • @wilsontonga3728
      @wilsontonga3728 3 ปีที่แล้ว +1

      🤝🏾

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 3 ปีที่แล้ว +4

      Naskiza ngoma mpaka moyo unataka kupasuka. Dizasta vina, MC Mahiri, Mc Katiri. Yaan hauishi kbs katika dunia tunayoishi sisi!
      Huku kwetu kitaa kizima wanajua n kiasi gani Mwamba unawika, wameacha kuniita jina langu, sikuhizi wananiita Dizasta Vina.
      Ngoma zako ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri na hana hatia. Ngoma zako zinaweza kumfanya mtu akatishe ktk msitu mnene wenye kutisha na asiogope. Ngoma zako zinamfanya mtu ajifunze kuwa mwenye maamuzi magumu bila kuhofia lawama la mwenye kulaumu!
      Dizasta vina, katika ulimwengu wa Hip Hop zaidi yako wewe bado sijamuona mwingine. Hata Fareed Qubanda umemtupa kule, kabakia jina tu!
      Hebu pitia hii ili uone uzao wa tungo zako broo
      th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html

    • @castorymwaipopo290
      @castorymwaipopo290 3 ปีที่แล้ว

      Nakukubali sana bro 💪

    • @sautidawa2222
      @sautidawa2222 3 ปีที่แล้ว

      Real talent

  • @emilysaimon481
    @emilysaimon481 3 ปีที่แล้ว +7

    Dizasta vina bro we ni mkaliii
    Sikumpenda lakini nilijifunza kumjali Kama tupo pamoja tia like 25-12-2020

    • @dizastavina
      @dizastavina  3 ปีที่แล้ว

      Thanks.. Please share. Usisahau kuorder my new album

    • @emilysaimon481
      @emilysaimon481 3 ปีที่แล้ว

      @@dizastavina pamoja bro nigei no yako

    • @dizastavina
      @dizastavina  3 ปีที่แล้ว +1

      @@emilysaimon481 pre order kupitia tigo pesa 0655696811 au Mpesa 0762158871

  • @maishacenter-eastafricatv3976
    @maishacenter-eastafricatv3976 3 ปีที่แล้ว +8

    Duuhh nlichelewa😪😪😪
    Dizzasta's fan number one from +257🇧🇮🇧🇮🇧🇮

  • @camillomakongwa8308
    @camillomakongwa8308 3 ปีที่แล้ว +45

    This dude is a script writer, story teller inshort ni Verteller,,, he can compose a movies of 2 hrs in 7 mins,, daaaamn🔥🔥🔥🔥

    • @dizastavina
      @dizastavina  3 ปีที่แล้ว +8

      Thanks, please share

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 3 ปีที่แล้ว

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
      th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html

    • @mussabutanwa8693
      @mussabutanwa8693 3 ปีที่แล้ว +2

      @@dullywamashairi121 yes he's a genius we should support him lol!!!

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 3 ปีที่แล้ว

      @@mussabutanwa8693 dats true my blood
      Dizasta vina:
      The man one army 💪💪

    • @mussabutanwa8693
      @mussabutanwa8693 3 ปีที่แล้ว

      @@dullywamashairi121 yes for really man

  • @winfredykahwili1513
    @winfredykahwili1513 3 ปีที่แล้ว +5

    Huu mziki wako ni dawa ya ubongo asee Viva dizasta vina 💪💪💪👊👊💥💥💥

  • @shabannyamsalika8959
    @shabannyamsalika8959 3 ปีที่แล้ว +21

    Hii ngoma ni zaidi ya albamu nzima ya Weusi, Prof Tungo we ni 🔥🔥🔥🔥🔥

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 3 ปีที่แล้ว +1

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
      th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html

    • @shabannyamsalika8959
      @shabannyamsalika8959 3 ปีที่แล้ว

      @@dullywamashairi121 Hip hop inahitaj wenye uwezo mkubwa wa kufkr, pole sana kwako mwny uwezo mdogo nkushauri kasikilize waaah!!!

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 3 ปีที่แล้ว +1

      @@shabannyamsalika8959 inaelekea wewe ndo hujanielewa Mimi. Wewe bado mbana pua. Wagumu wakipita wataelewa nimemaanisha nini.
      Umekurupuka mzee, maana kitaani wamenibatiza jina wananiita Dizasta vina!!💪💪💪

    • @shabannyamsalika8959
      @shabannyamsalika8959 3 ปีที่แล้ว

      @@dullywamashairi121 We ndo umekurupuka kusema huu wimbo ni wawagumu, hii ngoma anasikiliza mtu yeyote na anaelewa. Tuondoe mawazo finyu ya kudhania kuwa hip hop inasikilizwa na watu wagumu, cjui makatiri km wewe ulivyosema mwanzo...

    • @obeidjoseph3610
      @obeidjoseph3610 3 ปีที่แล้ว

      @@dullywamashairi121 mwanangu ww bado Sana na hilo jina la dizasta mwalichafua kitaan kwenu

  • @kelvinshayo608
    @kelvinshayo608 3 ปีที่แล้ว +8

    Nilikwambia unajua na ctoacha kukwambia unajua💪💪

  • @wawesttv
    @wawesttv 7 หลายเดือนก่อน +2

    ... nilipo mwambia nampenda hakujibu... 2024

  • @jamesngadaya2791
    @jamesngadaya2791 3 ปีที่แล้ว +3

    dizasta unao uwezo mkubwa sana wenye nguvu kama meli ya mizigo aiseee

  • @louiskhan7372
    @louiskhan7372 3 ปีที่แล้ว +6

    Hii True story nimesikiza ×10....song imenipeleka mpaka gaibuni ....utahisi mkono wa mungu umeandika Hii✔✔#KingOfRap

  • @tiktoktv8678
    @tiktoktv8678 3 ปีที่แล้ว +4

    Wasanii kama hawa Bongo ni wachache Sana... Big up bro....

  • @ARUSHA_NAILS
    @ARUSHA_NAILS 3 ปีที่แล้ว +16

    Dah dizasta umezigusa hisia umenifanya nijione mwenye hatia

    • @erastompongo8400
      @erastompongo8400 3 ปีที่แล้ว

      Dah Kama umeniimba mimi vile
      Haso za mapenzi duniani zinaumiza wengi

  • @benyvoice9415
    @benyvoice9415 3 ปีที่แล้ว +1

    Kaka hii ngoma naomba niifanyie cover yn nmeikubal Kias kwmb mpk nawaboa watu Everyday nackiliza

  • @jeovangisc7957
    @jeovangisc7957 3 ปีที่แล้ว +1

    Daaaa bro unajua mpaka unaboa.. masikio yetu hayalali njaa kila unaposhika kipaza!!

  • @ashuramuhammed3257
    @ashuramuhammed3257 ปีที่แล้ว +1

    Dizasta hii nyimbo ni funzo tosha yani ww ndo mwalimu wangu najifunza vitu vingi nkasikiliza nyimbo zako$

  • @hassanihanzel
    @hassanihanzel 3 ปีที่แล้ว +5

    Wa KUMI kutazama 🙌

    • @dizastavina
      @dizastavina  3 ปีที่แล้ว

      👏🏾 👏🏾 👏🏾 👏🏾

  • @hon-mlenga
    @hon-mlenga หลายเดือนก่อน

    🎶🎶🎶🎶Dizasta nadownlod nyimbo zako zote

  • @alextanzania
    @alextanzania 3 ปีที่แล้ว +5

    Dizasta vina ni akina Joh 70.
    Mtiririko mzuri ,kazi nzuri. Big up brother.

  • @blacklion3672
    @blacklion3672 3 ปีที่แล้ว +6

    This is the kind of music I expect to listen to in heaven.

  • @emmabelljohn4086
    @emmabelljohn4086 3 ปีที่แล้ว +3

    Nomaa sanaa

  • @mwajumakarim8520
    @mwajumakarim8520 3 ปีที่แล้ว +5

    Wewe wewe weeeeeewe🥺🥺🥺ulishushwa ututeke🇹🇿❤️

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 3 ปีที่แล้ว +1

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
      th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html

  • @rachelgmartin6850
    @rachelgmartin6850 3 ปีที่แล้ว +1

    Sauti yako tu mi hoiiiii🙆🏻‍♀️🙆🏻‍♀️🙆🏻‍♀️🙆🏻‍♀️🙆🏻‍♀️🙆🏻‍♀️🙆🏻‍♀️🙆🏻‍♀️🌹🥰❤️

  • @kelvinseif9928
    @kelvinseif9928 3 ปีที่แล้ว +5

    Dizasta vina ✍️💯

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 3 ปีที่แล้ว

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Ngoma zake zinaweza kumfanya mtu akatishe ktk msitu mnene wenye kutisha na asiogope. Ngoma zake zinamfanya mtu ajifunze kuwa mwenye maamuzi magumu bila kuhofia lawama la mwenye kulaumu!
      Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti
      th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html

  • @abdfattah883
    @abdfattah883 ปีที่แล้ว

    Kitu kinachoniuma ni kuona jamii inasikiliza miziki isiyo ya mafunzo yoyote na kuacha mziki wenye mafunzo Kama huu

  • @user-ie4ch2cf1g
    @user-ie4ch2cf1g 29 วันที่ผ่านมา

    Muziki unaishi na unajenga na kuponya hakika hii ni dawa kwenye kufkiria kabla ya kutenda❤❤🧠

  • @michaelmasanja6343
    @michaelmasanja6343 3 ปีที่แล้ว +1

    Verteller ...Dah huwezi amini nimeiona movie yote kichwani mwangu the way Mwamba unavoflow... nilichofeli ni kuipata sura ya Jane.

  • @binyezanch8271
    @binyezanch8271 3 ปีที่แล้ว +5

    Wimbo wangu wa mwaka kbsa Asante dizasta 2020

    • @dizastavina
      @dizastavina  3 ปีที่แล้ว

      Apreciate, umeshaweka order ya album

  • @danielmalimi9890
    @danielmalimi9890 3 ปีที่แล้ว +1

    Duuuhhh.... hii inabeba sababu muhimu ya muziki kwenye maisha....

  • @legawayz6093
    @legawayz6093 3 ปีที่แล้ว +7

    Hii ni movie kabisa bro one day andaa scripts then simama as diirector naamini itakuwa kazi kubwa BIG UP DIZASTA VINA

  • @learntoearn9588
    @learntoearn9588 3 ปีที่แล้ว +1

    Muda utafika Inshaallah dizasta utakua jina kubwa na ramani ya maarifa kwa kizazi kijacho

  • @KelvinEmersonSteven
    @KelvinEmersonSteven 3 ปีที่แล้ว +5

    Aisee hii ni ya moto kushinda jua🔥🔥🔥🔥

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 3 ปีที่แล้ว

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
      th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html

  • @meshack2559
    @meshack2559 3 ปีที่แล้ว +1

    Mistar unachora Broo!!! Ni nomah ,we mkali aise,big up

  • @sayeedally8152
    @sayeedally8152 3 ปีที่แล้ว +1

    kazi nzuri bro,,,, nakubali kazi zakoo

  • @msolidwagalilaya6094
    @msolidwagalilaya6094 4 หลายเดือนก่อน +1

    Brother ushaandika HATIA nyingi sana lakini hii hatia IV ni funga kazi brother

  • @chibalevicent822
    @chibalevicent822 ปีที่แล้ว +1

    You are so Genius, asante kwa uwezo wako wa kunifanya niamini kuwa wewe ndie Rapper Bora

  • @user-yo4yf7kw9n
    @user-yo4yf7kw9n ปีที่แล้ว +2

    naikubali kinoma hingoma bigp bro

  • @awetubello5399
    @awetubello5399 3 ปีที่แล้ว +2

    Brother unawezaaaaah na xo unaweza 2 we ni MWALIMU

  • @GerrardTryphorn
    @GerrardTryphorn หลายเดือนก่อน

    Daaa hiingom Kali

  • @fundi_nyata
    @fundi_nyata 3 ปีที่แล้ว +3

    THE VERTELLER!! Wachache watakuelewa na kukusifia!!

  • @mosesbond202
    @mosesbond202 3 ปีที่แล้ว +1

    Wewe mwamba ni mwehu sema tuu unafikiri sana
    Yaani movie moja classic

  • @johnkerrysibomana9062
    @johnkerrysibomana9062 ปีที่แล้ว +1

    Nimerudi hapa baada ya mistari mingi kunigusa na kuendana na ninachikipitia kwenye maisha ya mahusiano

  • @lonely8682
    @lonely8682 3 ปีที่แล้ว +1

    Najivunia kua shabiki ako bro...hujawahi kuniangusha🙏🙏🙏🙏🔥🔥🔥🔥

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 3 ปีที่แล้ว +1

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
      th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html

  • @shaddyqualityfurniture3595
    @shaddyqualityfurniture3595 3 ปีที่แล้ว +2

    Ukipenda ua haulikati unaliacha likue 🎶

  • @jofreymfugale4752
    @jofreymfugale4752 3 ปีที่แล้ว

    Aliondoka na kiungo cha mwili 😃🔥🔥

  • @nashonshimba7997
    @nashonshimba7997 3 ปีที่แล้ว +1

    Imenitoa machoz hii ngoma mapenz yanauma sana

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 3 ปีที่แล้ว

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
      th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html

    • @ramadhanally138
      @ramadhanally138 3 ปีที่แล้ว

      My broo really umenitoa mazur kweli VINA NI HAFAHI KABISA

  • @erickpaschaljr8667
    @erickpaschaljr8667 3 ปีที่แล้ว +1

    Ahsante sana Dizasta Vina Kwa Muziki Mzuri unaoacha/utakaoacha Alama ya Milele

  • @Gomsrap
    @Gomsrap 3 ปีที่แล้ว +19

    I'm Doing Music Because Of You That's It, You Are Extraordinary Man

    • @dizastavina
      @dizastavina  3 ปีที่แล้ว +1

      Appreciate the love brother

    • @alextanzania
      @alextanzania 3 ปีที่แล้ว +1

      Angusha ngoma Trickson ,tutakusupport tu

  • @octavianmushi928
    @octavianmushi928 3 ปีที่แล้ว

    Brazaaa umegusa maisha ye2 kwa hii ngoma

  • @salehekasangas3291
    @salehekasangas3291 ปีที่แล้ว +1

    Umeshushwa.brooo...yan.unajuaa.brooo

  • @kangeyg6879
    @kangeyg6879 3 ปีที่แล้ว +3

    Master vina fan toka 🇰🇪🔥✅ tumengoja sana umewakilisha kama kawaida

    • @dizastavina
      @dizastavina  3 ปีที่แล้ว +1

      Thanks, please share

  • @cosmasdonasian7248
    @cosmasdonasian7248 3 ปีที่แล้ว +2

    Sikisanga na nusu

  • @Therealgayakidy
    @Therealgayakidy 3 ปีที่แล้ว +1

    Kumamakeeeeee

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 3 ปีที่แล้ว

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha💪💪
      th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html

  • @novatusanthony8563
    @novatusanthony8563 3 ปีที่แล้ว +1

    Hii goma inatakiwa wasambaziwe wanafunzi Tanzania mzima maana hili ni somo linajitegemea.

  • @saidamour2635
    @saidamour2635 3 ปีที่แล้ว +2

    Disasta unaweza sana amini wanakuelewa ila wanabana tu, fans wako tunasubri collabo yako na kaa la moto.

    • @jumangala
      @jumangala 11 หลายเดือนก่อน

      Ausio

  • @deciphertz
    @deciphertz 3 ปีที่แล้ว +1

    Emotional 🔥🔥🔥🙌🙌

  • @geofreymboyelwa614
    @geofreymboyelwa614 2 ปีที่แล้ว

    Nyimbo nzur sana

  • @robifilosomaniofficialonli4272
    @robifilosomaniofficialonli4272 3 ปีที่แล้ว

    Waaaaaah...
    Dizasta vina..tisha sana..
    Kenya tunakuaminia.

  • @muddyjumaa604
    @muddyjumaa604 3 ปีที่แล้ว +1

    Umetisha sana mzee baba bonge moja la ngoma

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 3 ปีที่แล้ว +1

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
      th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html

  • @SPM_Mukong
    @SPM_Mukong 3 ปีที่แล้ว +9

    The pure art of storytelling! I love it man. Great job

  • @richardtitus8539
    @richardtitus8539 3 ปีที่แล้ว

    Daaah black maradona.. home boy unajua

  • @obeidjoseph3610
    @obeidjoseph3610 3 ปีที่แล้ว +1

    Unatishaaa yaaaani hiii ngoma mengne live

  • @dullyhaleem6962
    @dullyhaleem6962 2 ปีที่แล้ว

    Hii nyimbo itungiwe movie kummmke duuh😓😓🔥🔥🔥

  • @RamaSwalehe-kc9kr
    @RamaSwalehe-kc9kr ปีที่แล้ว

    Unyama sana broo

  • @wilsontonga3728
    @wilsontonga3728 3 ปีที่แล้ว

    Ahsaante tena kwa
    💣💣💣 bomu la kufungia mwaka 2020..

  • @intavides
    @intavides 3 ปีที่แล้ว

    daah..💯💯 shukrani sana

  • @revocatuscharles1512
    @revocatuscharles1512 ปีที่แล้ว +1

    Jamaa unaimba sana aiseh🔥🔥🔥🔥

  • @henrytanji8874
    @henrytanji8874 3 ปีที่แล้ว

    Dah Dizasta ...salute

  • @tinnohaugustineh6193
    @tinnohaugustineh6193 6 หลายเดือนก่อน

    Vina vingi sana humu👑

  • @ombenedwin136
    @ombenedwin136 3 ปีที่แล้ว +1

    Mungu ametupaga disaster vina

  • @SoulfulPrayersSanctuary
    @SoulfulPrayersSanctuary 3 ปีที่แล้ว

    Moto Kwa anga

  • @abottymlamba8075
    @abottymlamba8075 3 ปีที่แล้ว +1

    So much blessings....vina for real..

  • @ellyscarlxrd7380
    @ellyscarlxrd7380 3 ปีที่แล้ว +4

    Disasta vina

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 3 ปีที่แล้ว

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
      th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html

  • @benjaminchokela3577
    @benjaminchokela3577 ปีที่แล้ว +1

    REST IN PEACE MAGUFULI ULIPAMBANA SANA NA HIYO VITA! MUNGU AKUPUNGUZIE ADHABU YA KABURI NASI SOTE TWAJA! Ameen

  • @vigangwaya8802
    @vigangwaya8802 3 ปีที่แล้ว +2

    The best hiphop rapper kwa sasa nchini, hakuna wa kumzidi Dizasta vina kwa sasa

  • @shabannyamsalika8959
    @shabannyamsalika8959 3 ปีที่แล้ว +2

    Bongo movie mpo wapi, Chukueni huu wimbo mkatengeneze movie ya masaa 3. Prof Tungo kasimulia kwa dk 7 tu!!

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 3 ปีที่แล้ว

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
      th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html

    • @shabannyamsalika8959
      @shabannyamsalika8959 3 ปีที่แล้ว +1

      @@dullywamashairi121 Akili yako ndo ngumu kuelewa, Hip hop usikivu km huwez kasikilize waaah!!

    • @midopestjr5297
      @midopestjr5297 3 ปีที่แล้ว +1

      @@shabannyamsalika8959 sahihi bro awahi uko kwa wanenguajii🤣🤣🤣

    • @shabannyamsalika8959
      @shabannyamsalika8959 3 ปีที่แล้ว +1

      @@midopestjr5297 ,😂😂😂

    • @midopestjr5297
      @midopestjr5297 3 ปีที่แล้ว

      @@shabannyamsalika8959 watu wengine chengu kweliiii 😜😜

  • @mohammedyjshemweta1390
    @mohammedyjshemweta1390 3 ปีที่แล้ว

    Daaah jiji lina habar kamil mzee,🙌🙌🙌

  • @johnmosha8285
    @johnmosha8285 3 ปีที่แล้ว +1

    Makini sana mzee

  • @nafsitukuf7671
    @nafsitukuf7671 3 ปีที่แล้ว +1

    Noma sana 🔥🔥

  • @allymarumbo1088
    @allymarumbo1088 3 ปีที่แล้ว +1

    What a lesson..daaaaaah
    We jamaa ni zaidi ya hip hop bro.

  • @harunahozzah5847
    @harunahozzah5847 3 ปีที่แล้ว

    Haya banah bwana John 🙏🙏🙏

  • @danchalzndyanabo9200
    @danchalzndyanabo9200 3 ปีที่แล้ว +1

    Dizasta vina noma sana

  • @peterbenjaminpeterbenjamin9566
    @peterbenjaminpeterbenjamin9566 3 ปีที่แล้ว +1

    Aisee dizastar noma Sana mshkaji wangu darasa Hilo namimi napenda Nije nipate mautundu ya asali ya hip-hop

  • @mrundumo1326
    @mrundumo1326 3 ปีที่แล้ว

    Namkubali Dizasta

  • @pudaboytz4956
    @pudaboytz4956 3 ปีที่แล้ว

    Dizasta vina ujawai kosea big ✊✊

  • @furahinandrew9704
    @furahinandrew9704 3 ปีที่แล้ว +1

    We jamaa nomaa

  • @mrcoolboy5475
    @mrcoolboy5475 2 ปีที่แล้ว

    Dah hatar sana

  • @ellyscarlxrd7380
    @ellyscarlxrd7380 3 ปีที่แล้ว +5

    🔥🔥🔥🔥🔥🔥

    • @dullywamashairi121
      @dullywamashairi121 3 ปีที่แล้ว

      Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Ngoma zake zinaweza kumfanya mtu akatishe ktk msitu mnene wenye kutisha na asiogope. Ngoma zake zinamfanya mtu ajifunze kuwa mwenye maamuzi magumu bila kuhofia lawama la mwenye kulaumu!
      Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti
      th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html

  • @erastomichael9840
    @erastomichael9840 5 หลายเดือนก่อน

    My all time Banger..!! ❤

  • @nocerinocarterabdalla4247
    @nocerinocarterabdalla4247 3 ปีที่แล้ว

    Hii ni zaidi ya nyoko.Hainaga kufeli🔥🔥🔥

  • @balikiabdala823
    @balikiabdala823 ปีที่แล้ว

    🤔🤔🤔🤔 Noma sana ngoma kali sana

  • @kladsman
    @kladsman 3 ปีที่แล้ว

    Safi 💯🔥

  • @jistusngowi721
    @jistusngowi721 3 ปีที่แล้ว

    Noma sana, bonge la ujumbe kwenu walengwa

  • @musamwakalinga6191
    @musamwakalinga6191 3 ปีที่แล้ว +1

    Asante kaka dizasta

  • @facebmzeewakimba1546
    @facebmzeewakimba1546 3 ปีที่แล้ว +2

    Wejamaaa weeeeee!!!! Ninomaaaaa

  • @abdulrahmantiger6957
    @abdulrahmantiger6957 3 ปีที่แล้ว +1

    Umeuaaaa🔥🔥🔥🔥

  • @sylvestermtweve2895
    @sylvestermtweve2895 3 ปีที่แล้ว +4

    Dizasta..... you're very UNIQUE broo...Mungu akuzidishe maarifa na afya tele just because unajua kutupa Raha mashabiki zako..GOD BLESS TOUR TALENT

  • @sabrisaleh1720
    @sabrisaleh1720 3 ปีที่แล้ว

    We dizasta fundi ni kweli nikitaka mziki mzuri nimtafute dizasta

  • @bonnifacewilly3026
    @bonnifacewilly3026 3 ปีที่แล้ว +1

    Daaah huyu jamaa anafanya mziki kwa bongo hakuna tena kama dizasta amani kwako brother

  • @franciscojonja1164
    @franciscojonja1164 3 ปีที่แล้ว +1

    Asie elewa kazi ya hiki kichwa aisee hatokuja kuelewa milele @dizasta vina ndio nembo ya hip hop isio vunja nguzo ata moja ya hip hop brother umetisha sana

    • @dizastavina
      @dizastavina  3 ปีที่แล้ว +1

      Thanks, please share