Dizasta Vina - Hatia IV
ฝัง
- เผยแพร่เมื่อ 12 ธ.ค. 2020
- Category: Music
Song: Hatia IV
Artist: Dizasta Vina
Music: Ringle Beatz
TH-cam: / jwa21m5eyl
Mdundo: mdundo.com/song/1670618
Audiomack: audiomack.com/dizastavina/son...
Soundcloud: / hatiaiv
Lyrics: genius.com/Dizasta-vina-hatia...
Other Musical contents
Audiomack - audiomack.com/dizastavina
TH-cam - / dizastavina
Deezer - www.deezer.com/artist/67967532
Apple music - artists.apple.com/a/profile
Mdundo - mdundo.com/a/2263
Genius - genius.com/DizastaVina
Boom play - www.boomplay.com/artists/3288... - artists.spotify.com/c/artist/...
Connect with Dizasta Vina on social medias
Instagram - / dizastavina
Twitter - / dizastavina
Facebook - / dizastavina07
sw.wikipedia.org/wiki/Dizasta...
Business: Pan.authentik@yahoo.com
Website - bio.link/dizastavina
Lyrics
“JASIRI JOHN….. ALIYAANGALIA MAISHA YAKE
HAKUONA JINSI ANGEWEZA KUISHI BILA JANE
MSICHANA ANAYEMPENDA
LICHA YA KUZONGWA NA UMASIKINI
ALIJITAHIDI KUMPA JANE MAHITAJI MADOGOMADOGO KADRI ALIVYOWEZA
LAKINI ALIFAHAMU SHUBIRI YA KUSUBIRI KUPENDWA HUKU ANAFAHAMU KUSUBIRI KUPENDWA NI
MATUMAINI YANAYOUMIZA. KAMA WANAVYOSEMA, MTAFUTAJI HACHOKI AKICHOKA KASHAPATA…
.ALIENDELEA KUNGOJA”
Ah! Sikuwa na zali sikuziamini ndumba
Sikuwa na mali za kufuja
Nilijitahidi kuuza mitumba kufuga mipunga
Ili siku nimpe gari nimpe nyumba. Nilishindwa…
Niliishia kumpa chai, ‘chipsi’ mayai na ‘vocha’
Nywele za kimasai na mkoba
Pesa za magauni, majuba na viatu vya kuzuga
Nilimpa muda ila bado haikutosha, kwani…
Nilipomwambia nampenda hakujibu
Akaweka moyo wangu maumivu
Na mtima wangu akauweka ‘solemba’
Nikaapia kuwa sitakuja kupenda ‘forever’
Ah! Nilimpa upendo nilimpa sifa
Niliweka mitego ya faida, haikuwa shwari
Nikabadili mwenendo wa maisha
Niliweka malengo sikutimiza, hakunikubali
Alikuwa na ndoto kubwa kushinda mimi
Alikuwa na misimamo kuipita dini
Aliniambia ameomba nije kuokota utajiri
Amengoja sana na sasa amechoka kusubiri
Ah! Sikuwa na hali ya kuikosha roho yake
Nilimwacha aende aufate moyo wake
Alipata bwana wa kizungu magharibi
Alimwahidi kuishi maisha ya ndoto zake
Nilipata uchungu niliishia kuhamaki nilitaka nijiue
Nilitaka nimzuie abaki nikakumbuka
Ukipenda ua haulikati unaliacha likue
Duka langu nilifunga biashara niliacha zote
Uchumi uliyumba kwa maana nilianza pombe
Niliumwa bado kidogo moyo uzime
Nilimfanya ndoto kumbe naye ana ndoto nyingine
Alisema anakwenda jiji la Miami
Hakuna alichowaza zaidi ya kuishi kifahari
Kamtumia picha na ‘mchizi’ kazikubali
Na yupo tayari kumlipia gharama za safari
Aliondoka na kipande kimoja cha mwili
Nilikonda nilipata ugonjwa wa akili
Haikuwahi kupita hata sekunde nisilie
Nilitamani mpaka ardhi ipasuke niingie
Ah! Muda ukaenda nitapata ‘Mwanamwali’
Nikamwomba awe mwenza wa maisha akakubali
Nikamvisha pete nikalipia mahari
Sikumpenda lakini nilijifunza kumjali
Aliuliza kama nampenda, nilimjibu
Sikutaka kuweka moyo wake maumivu
Sikutaka kuuweka Mtima wake solemba
Kiasi aseme hatakuja kupenda ‘‘forever’’
Ah alinikumbatia nikamfunga kwa ishara
Akanikabidhi tunda nikala
Akaniamini tukajuana nikapanga kumwoa
Akaidhisha na tukaanza na mipango ya ndoa
“Habari naamini u bukheri wa afya
Unaendeleaje maisha na huyo mpenzi wa sasa
.nashukuru nahema ughaibuni si kwema
Nakiona cha mtema mpaka naona ni heri nikafa…
Ah! Maisha niliyowaza yote ni uongo
Nauzishwa madawa nalazimishwa ngono
Nafungiwa ndani kama mtumwa ufungwani
Roho yangu rehani kiasi sasa naitamani Bongo
Ukubwa umekuja kunisafisha jicho
Ndoto imeisha na taswira imenionyesha sivyo, ah
Naomba unifate uniondoshe kwenye hichi kifo
Na hii namba ya msamaria atakueleza nilipo”
Sherehe ilikuwa na mipango madhubuti
Kabla mimi kuichukua michango ya Harusi
Nikatoroka ughaibuni kufuata hisia zangu
Kwenda kumfata njiwa wangu mahususi
Nilivuka majangwa na majabali
Sehemu ya safari anga sehemu nyingine bahari
Niliacha kila kitu nyuma upendo na huruma vilinijaa
Penzi likanipeleka mbali
Nikakutana na bopa la kizungu
Lenye sura ya kuichachisha mboga kwenye chungu
Kiko kwenye mdomo,Tatuu kila kona na wapambe
Pamoja na vishoka wenye mtutu
Sio siri alizungukwa na wasichana wengi
Sikujua umri walikuwa wadogo ka’ “madent”
Baadhi walikuwa uchi wanahesabia “chenchi”
Wengine masaji huku wengine wanamchezea nyeti
Hata nilipomuuliza kama ananipenda hakujibu
Akaweka moyo wangu maumivu
Nilijua hawezi kufa kwa sababu hakunipenda
Na ni rasmi nikapoteza shilingi kwenye msitu
Nilikiambia kifo kama unakuja njoo
Maana sikuwa mtu ilishakufa roho
Sikuumia kama alivyoniumiza yeye
Kwahiyo sikujali jinsi nilivyoteswa na wale mbwa no
Aliambiwa ambusu bosi hakubisha
Alipewa bunduki hakusita
Aliishika risasi akaiingiza
Akaambiwa anipige kwenye kichwa - เพลง
"Nilimfanya ndoto, kumbe naye ana ndoto nyingine"
“JASIRI JOHN….. ALIYAANGALIA MAISHA YAKE
HAKUONA JINSI ANGEWEZA KUISHI BILA JANE
MSICHANA ANAYEMPENDA
LICHA YA KUZONGWA NA UMASIKINI
ALIJITAHIDI KUMPA JANE MAHITAJI MADOGOMADOGO KADRI ALIVYOWEZA
LAKINI ALIFAHAMU SHUBIRI YA KUSUBIRI KUPENDWA HUKU ANAFAHAMU KUSUBIRI KUPENDWA NI
MATUMAINI YANAYOUMIZA. KAMA WANAVYOSEMA, MTAFUTAJI HACHOKI AKICHOKA KASHAPATA…
.ALIENDELEA KUNGOJA”
Ah! Sikuwa na zali sikuziamini ndumba
Sikuwa na mali za kufuja
Nilijitahidi kuuza mitumba kufuga mipunga
Ili siku nimpe gari nimpe nyumba. Nilishindwa…
Niliishia kumpa chai, ‘chipsi’ mayai na ‘vocha’
Nywele za kimasai na mkoba
Pesa za magauni, majuba na viatu vya kuzuga
Nilimpa muda ila bado haikutosha, kwani…
Nilipomwambia nampenda hakujibu
Akaweka moyo wangu maumivu
Na mtima wangu akauweka ‘solemba’
Nikaapia kuwa sitakuja kupenda ‘forever’
Ah! Nilimpa upendo nilimpa sifa
Niliweka mitego ya faida, haikuwa shwari
Nikabadili mwenendo wa maisha
Niliweka malengo sikutimiza, hakunikubali
Alikuwa na ndoto kubwa kushinda mimi
Alikuwa na misimamo kuipita dini
Aliniambia ameomba nije kuokota utajiri
Amengoja sana na sasa amechoka kusubiri
“JOHN ALIFAHAMU HALI YA JANE, KUWA JANE ALIZALIWA KWENYE
FAMILIA MASIKINI, NA ALIUCHUKIA MNO UMASIKINI.
ALIFAHAMU UMASIKINI ULIVYOCHUKUA UHAI WA MAMA YAKE KIPENZI,
ALIYEFARIKI KWA KUKOSA MATIBABU. ALIIFAHAMAU NADHIRI ALIYOIWEKA JANE YA KWAMBA
HATOKUBALI TENA KUISHI KWENYE MAISHA YA KIMASIKINI, NADHIRI ILIYO MWEKA JOHN NJIAPANDA”
Ah! Sikuwa na hali ya kuikosha roho yake
Nilimwacha aende aufate moyo wake
Alipata bwana wa kizungu magharibi
Alimwahidi kuishi maisha ya ndoto zake
Nilipata uchungu niliishia kuhamaki nilitaka nijiue
Nilitaka nimzuie abaki nikakumbuka
Ukipenda ua haulikati unaliacha likue
Duka langu nilifunga biashara niliacha zote
Uchumi uliyumba kwa maana nilianza pombe
Niliumwa bado kidogo moyo uzime
Nilimfanya ndoto kumbe naye ana ndoto nyingine
Alisema anakwenda jiji la Miami
Hakuna alichowaza zaidi ya kuishi kifahari
Kamtumia picha na ‘mchizi’ kazikubali
Na yupo tayari kumlipia gharama za safari
Aliondoka na kipande kimoja cha mwili
Nilikonda nilipata ugonjwa wa akili
Haikuwahi kupita hata sekunde nisilie
Nilitamani mpaka ardhi ipasuke niingie
“JANE ALIPOONDOKA ALIMWACHIA JOHN KIDONDA KILICHOCHELEWA SANA KUPONA
NA YEYE AKAWEKA NADHIRI YA KUTOJIHUSISHA NA MAPENZI TENA MAISHANI MWAKE.
ALIKAA KWA MUDA MREFU BILA MAHUSIANO. LAKINI…
HAKUNA DAKTARI MZURI KAMA MUDA, JOHN ALIPONA MAUMIVU NA ALIIRUDIA HALI YAKE YA KAWAIDA”
Ah! Muda ukaenda nitapata ‘Mwanamwali’
Nikamwomba awe mwenza wa maisha akakubali
Nikamvisha pete nikalipia mahari
Sikumpenda lakini nilijifunza kumjali
Aliuliza kama nampenda, nilimjibu
Sikutaka kuweka moyo wake maumivu
Sikutaka kuuweka Mtima wake solemba
Kiasi aseme hatakuja kupenda ‘‘forever’’
Ah alinikumbatia nikamfunga kwa ishara
Akanikabidhi tunda nikala
Akaniamini tukajuana nikapanga kumwoa
Akaidhisha na tukaanza na mipango ya ndoa
“WAKATI KARNE YA 21 INAINGIA, JOHN ALIKUWA NI MIONGONI MWA
VIJANA WALIOKUWA ‘FASCINATED’ NA UKUAJI WA TEKNOLOJIA YA MITANDAO YA KIJAMII.
ALIJIUNGA NA DUNIA HII MPYA, MARA KADHAA ALIKAA KWENYE UBARAZA, AKIANGAZA SIMU YAKE.
AKIPAPASA KILA KITUFE, NDIPO SIKU MOJA AKAPATA UJUMBE KUTOKA KWA JANE”
“Habari naamini u bukheri wa afya
Unaendeleaje maisha na huyo mpenzi wa sasa
.nashukuru nahema ughaibuni si kwema
Nakiona cha mtema mpaka naona ni heri nikafa…
Ah! Maisha niliyowaza yote ni uongo
Nauzishwa madawa nalazimishwa ngono
Nafungiwa ndani kama mtumwa ufungwani
Roho yangu rehani kiasi sasa naitamani Bongo
Ukubwa umekuja kunisafisha jicho
Ndoto imeisha na taswira imenionyesha sivyo, ah
Naomba unifate uniondoshe kwenye hichi kifo
Na hii namba ya msamaria atakueleza nilipo”
Sherehe ilikuwa na mipango madhubuti
Kabla mimi kuichukua michango ya Harusi
Nikatoroka ughaibuni kufuata hisia zangu
Kwenda kumfata njiwa wangu mahususi
Nilivuka majangwa na majabali
Sehemu ya safari anga sehemu nyingine bahari
Niliacha kila kitu nyuma upendo na huruma vilinijaa
Penzi likanipeleka mbali
“JOHN ALIFIKA UGHAIBUNI, AKAMTAFUTA MSAMARIA ALIYETAMBULISHWA NA UJUMBE,
MSAMARIA AKAMWELEKEZA NJIWA WAKE ALIPO, NA NIKWELI… HAPAKUWA PEMA”
Nikakutana na bopa la kizungu
Lenye sura ya kuichachisha mboga kwenye chungu
Kiko kwenye mdomo,Tatuu kila kona na wapambe
Pamoja na vishoka wenye mtutu
Sio siri alizungukwa na wasichana wengi
Sikujua umri walikuwa wadogo ka’ “madent”
Baadhi walikuwa uchi wanahesabia “chenchi”
Wengine masaji huku wengine wanamchezea nyeti
“MASIKINI JOHN, ALIDANGANYA KWA KUJITAMBULISHA KAMA KAKA KWA JANE,
AKIMSIHI YULE MAFIA AMRUHUSU AONDOKE NA JANE WAKAANZE MAISHA MAPYA,
LAKINI… PALIPOSHINDWA SHOKA WEMBE HAUWEZI TAMBA. KWA KUZIDIWA NA UOGA WA KUUAWA…
JANE ALIMKANA JOHN KWA KUSEMA HAMJUI…”
Hata nilipomuuliza kama ananipenda hakujibu
Akaweka moyo wangu maumivu
Nilijua hawezi kufa kwa sababu hakunipenda
Na ni rasmi nikapoteza shilingi kwenye msitu
Nilikiambia kifo kama unakuja njoo
Maana sikuwa mtu ilishakufa roho
Sikuumia kama alivyoniumiza yeye
Kwahiyo sikujali jinsi nilivyoteswa na wale mbwa no
Aliambiwa ambusu bosi hakubisha
Alipewa bunduki hakusita
Aliishika risasi akaiingiza
Akaambiwa anipige kwenye kichwa
JOHN ALIKUWA NI JINA JIPYA LA WAHANGA WA UPENDO WA DHATI, VIPOFU WA MAPENZI, WAJINGA WA MAHABA...
JOHN ALIKUWA ROMEO KWENYE ROMEO AND JULIETH, ALIKUWA SAMSON KWA DELILAH KWENYE WAHUKUMU WA AGANO LA KALE, ALIKUWA JACK KWENYE TITANIC, FRED WEASLEY KWENYE HARRY POTTER..
JOHN ALITUKUMBUSHA KUWA UPENDO NI SADAKA, SADAKA YA MUDA NA PESA, ALITUKUMBUSHA UPENDO NI SADAKA YA DAMU
JOHN, ALIPOTEZA UHAI AKIWA KWENYE SAFARI YA KUTAFUTA UPENDO WA MTU ALIYEMHUSUDU NA
JANE ALIPOTEZA AMANI NA THAMANI YAKE KAMA MTU AKIWA KWENYE SAFARI YA KUTAFUTA UTAJIRI ALIOUHUSUDU
Hatia iko wapi?
Daaah dizasta wewe ni vina hivi naanzaje kuchoka kusikiliza nyimbo zako
🤝🏾
Naskiza ngoma mpaka moyo unataka kupasuka. Dizasta vina, MC Mahiri, Mc Katiri. Yaan hauishi kbs katika dunia tunayoishi sisi!
Huku kwetu kitaa kizima wanajua n kiasi gani Mwamba unawika, wameacha kuniita jina langu, sikuhizi wananiita Dizasta Vina.
Ngoma zako ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri na hana hatia. Ngoma zako zinaweza kumfanya mtu akatishe ktk msitu mnene wenye kutisha na asiogope. Ngoma zako zinamfanya mtu ajifunze kuwa mwenye maamuzi magumu bila kuhofia lawama la mwenye kulaumu!
Dizasta vina, katika ulimwengu wa Hip Hop zaidi yako wewe bado sijamuona mwingine. Hata Fareed Qubanda umemtupa kule, kabakia jina tu!
Hebu pitia hii ili uone uzao wa tungo zako broo
th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html
Nakukubali sana bro 💪
Real talent
Dizasta vina bro we ni mkaliii
Sikumpenda lakini nilijifunza kumjali Kama tupo pamoja tia like 25-12-2020
Thanks.. Please share. Usisahau kuorder my new album
@@dizastavina pamoja bro nigei no yako
@@emilysaimon481 pre order kupitia tigo pesa 0655696811 au Mpesa 0762158871
Duuhh nlichelewa😪😪😪
Dizzasta's fan number one from +257🇧🇮🇧🇮🇧🇮
This dude is a script writer, story teller inshort ni Verteller,,, he can compose a movies of 2 hrs in 7 mins,, daaaamn🔥🔥🔥🔥
Thanks, please share
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html
@@dullywamashairi121 yes he's a genius we should support him lol!!!
@@mussabutanwa8693 dats true my blood
Dizasta vina:
The man one army 💪💪
@@dullywamashairi121 yes for really man
Huu mziki wako ni dawa ya ubongo asee Viva dizasta vina 💪💪💪👊👊💥💥💥
Hii ngoma ni zaidi ya albamu nzima ya Weusi, Prof Tungo we ni 🔥🔥🔥🔥🔥
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html
@@dullywamashairi121 Hip hop inahitaj wenye uwezo mkubwa wa kufkr, pole sana kwako mwny uwezo mdogo nkushauri kasikilize waaah!!!
@@shabannyamsalika8959 inaelekea wewe ndo hujanielewa Mimi. Wewe bado mbana pua. Wagumu wakipita wataelewa nimemaanisha nini.
Umekurupuka mzee, maana kitaani wamenibatiza jina wananiita Dizasta vina!!💪💪💪
@@dullywamashairi121 We ndo umekurupuka kusema huu wimbo ni wawagumu, hii ngoma anasikiliza mtu yeyote na anaelewa. Tuondoe mawazo finyu ya kudhania kuwa hip hop inasikilizwa na watu wagumu, cjui makatiri km wewe ulivyosema mwanzo...
@@dullywamashairi121 mwanangu ww bado Sana na hilo jina la dizasta mwalichafua kitaan kwenu
Nilikwambia unajua na ctoacha kukwambia unajua💪💪
Thanks kev
... nilipo mwambia nampenda hakujibu... 2024
dizasta unao uwezo mkubwa sana wenye nguvu kama meli ya mizigo aiseee
Hii True story nimesikiza ×10....song imenipeleka mpaka gaibuni ....utahisi mkono wa mungu umeandika Hii✔✔#KingOfRap
Wasanii kama hawa Bongo ni wachache Sana... Big up bro....
Dah dizasta umezigusa hisia umenifanya nijione mwenye hatia
Dah Kama umeniimba mimi vile
Haso za mapenzi duniani zinaumiza wengi
Kaka hii ngoma naomba niifanyie cover yn nmeikubal Kias kwmb mpk nawaboa watu Everyday nackiliza
Daaaa bro unajua mpaka unaboa.. masikio yetu hayalali njaa kila unaposhika kipaza!!
Dizasta hii nyimbo ni funzo tosha yani ww ndo mwalimu wangu najifunza vitu vingi nkasikiliza nyimbo zako$
Wa KUMI kutazama 🙌
👏🏾 👏🏾 👏🏾 👏🏾
🎶🎶🎶🎶Dizasta nadownlod nyimbo zako zote
Dizasta vina ni akina Joh 70.
Mtiririko mzuri ,kazi nzuri. Big up brother.
This is the kind of music I expect to listen to in heaven.
Nomaa sanaa
Wewe wewe weeeeeewe🥺🥺🥺ulishushwa ututeke🇹🇿❤️
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html
Sauti yako tu mi hoiiiii🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🌹🥰❤️
Thank you........
Dizasta vina ✍️💯
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Ngoma zake zinaweza kumfanya mtu akatishe ktk msitu mnene wenye kutisha na asiogope. Ngoma zake zinamfanya mtu ajifunze kuwa mwenye maamuzi magumu bila kuhofia lawama la mwenye kulaumu!
Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti
th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html
Kitu kinachoniuma ni kuona jamii inasikiliza miziki isiyo ya mafunzo yoyote na kuacha mziki wenye mafunzo Kama huu
Muziki unaishi na unajenga na kuponya hakika hii ni dawa kwenye kufkiria kabla ya kutenda❤❤🧠
Verteller ...Dah huwezi amini nimeiona movie yote kichwani mwangu the way Mwamba unavoflow... nilichofeli ni kuipata sura ya Jane.
Wimbo wangu wa mwaka kbsa Asante dizasta 2020
Apreciate, umeshaweka order ya album
Duuuhhh.... hii inabeba sababu muhimu ya muziki kwenye maisha....
Hii ni movie kabisa bro one day andaa scripts then simama as diirector naamini itakuwa kazi kubwa BIG UP DIZASTA VINA
Hopefully one day
Muda utafika Inshaallah dizasta utakua jina kubwa na ramani ya maarifa kwa kizazi kijacho
Hopefully
Aisee hii ni ya moto kushinda jua🔥🔥🔥🔥
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html
Mistar unachora Broo!!! Ni nomah ,we mkali aise,big up
kazi nzuri bro,,,, nakubali kazi zakoo
Brother ushaandika HATIA nyingi sana lakini hii hatia IV ni funga kazi brother
You are so Genius, asante kwa uwezo wako wa kunifanya niamini kuwa wewe ndie Rapper Bora
naikubali kinoma hingoma bigp bro
Brother unawezaaaaah na xo unaweza 2 we ni MWALIMU
Thanks bro
Daaa hiingom Kali
THE VERTELLER!! Wachache watakuelewa na kukusifia!!
Wewe mwamba ni mwehu sema tuu unafikiri sana
Yaani movie moja classic
😂 😂 😂
Nimerudi hapa baada ya mistari mingi kunigusa na kuendana na ninachikipitia kwenye maisha ya mahusiano
Najivunia kua shabiki ako bro...hujawahi kuniangusha🙏🙏🙏🙏🔥🔥🔥🔥
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html
Ukipenda ua haulikati unaliacha likue 🎶
Aliondoka na kiungo cha mwili 😃🔥🔥
Imenitoa machoz hii ngoma mapenz yanauma sana
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html
My broo really umenitoa mazur kweli VINA NI HAFAHI KABISA
Ahsante sana Dizasta Vina Kwa Muziki Mzuri unaoacha/utakaoacha Alama ya Milele
I'm Doing Music Because Of You That's It, You Are Extraordinary Man
Appreciate the love brother
Angusha ngoma Trickson ,tutakusupport tu
Brazaaa umegusa maisha ye2 kwa hii ngoma
Umeshushwa.brooo...yan.unajuaa.brooo
Master vina fan toka 🇰🇪🔥✅ tumengoja sana umewakilisha kama kawaida
Thanks, please share
Sikisanga na nusu
King
Kumamakeeeeee
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha💪💪
th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html
Hii goma inatakiwa wasambaziwe wanafunzi Tanzania mzima maana hili ni somo linajitegemea.
Disasta unaweza sana amini wanakuelewa ila wanabana tu, fans wako tunasubri collabo yako na kaa la moto.
Ausio
Emotional 🔥🔥🔥🙌🙌
Nyimbo nzur sana
Waaaaaah...
Dizasta vina..tisha sana..
Kenya tunakuaminia.
Umetisha sana mzee baba bonge moja la ngoma
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html
The pure art of storytelling! I love it man. Great job
Daaah black maradona.. home boy unajua
Unatishaaa yaaaani hiii ngoma mengne live
Hii nyimbo itungiwe movie kummmke duuh😓😓🔥🔥🔥
Unyama sana broo
Ahsaante tena kwa
💣💣💣 bomu la kufungia mwaka 2020..
daah..💯💯 shukrani sana
Jamaa unaimba sana aiseh🔥🔥🔥🔥
Dah Dizasta ...salute
Vina vingi sana humu👑
Mungu ametupaga disaster vina
Moto Kwa anga
So much blessings....vina for real..
Disasta vina
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html
REST IN PEACE MAGUFULI ULIPAMBANA SANA NA HIYO VITA! MUNGU AKUPUNGUZIE ADHABU YA KABURI NASI SOTE TWAJA! Ameen
The best hiphop rapper kwa sasa nchini, hakuna wa kumzidi Dizasta vina kwa sasa
Hip hop 👍👍👍
Bongo movie mpo wapi, Chukueni huu wimbo mkatengeneze movie ya masaa 3. Prof Tungo kasimulia kwa dk 7 tu!!
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha
th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html
@@dullywamashairi121 Akili yako ndo ngumu kuelewa, Hip hop usikivu km huwez kasikilize waaah!!
@@shabannyamsalika8959 sahihi bro awahi uko kwa wanenguajii🤣🤣🤣
@@midopestjr5297 ,😂😂😂
@@shabannyamsalika8959 watu wengine chengu kweliiii 😜😜
Daaah jiji lina habar kamil mzee,🙌🙌🙌
Makini sana mzee
Noma sana 🔥🔥
What a lesson..daaaaaah
We jamaa ni zaidi ya hip hop bro.
Haya banah bwana John 🙏🙏🙏
Dizasta vina noma sana
Aisee dizastar noma Sana mshkaji wangu darasa Hilo namimi napenda Nije nipate mautundu ya asali ya hip-hop
Namkubali Dizasta
Dizasta vina ujawai kosea big ✊✊
We jamaa nomaa
Dah hatar sana
🔥🔥🔥🔥🔥🔥
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Ngoma zake zinaweza kumfanya mtu akatishe ktk msitu mnene wenye kutisha na asiogope. Ngoma zake zinamfanya mtu ajifunze kuwa mwenye maamuzi magumu bila kuhofia lawama la mwenye kulaumu!
Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti
th-cam.com/video/_vGu4l1MoMw/w-d-xo.html
My all time Banger..!! ❤
Hii ni zaidi ya nyoko.Hainaga kufeli🔥🔥🔥
🤔🤔🤔🤔 Noma sana ngoma kali sana
Safi 💯🔥
Noma sana, bonge la ujumbe kwenu walengwa
Asante kaka dizasta
Wejamaaa weeeeee!!!! Ninomaaaaa
Umeuaaaa🔥🔥🔥🔥
Dizasta..... you're very UNIQUE broo...Mungu akuzidishe maarifa na afya tele just because unajua kutupa Raha mashabiki zako..GOD BLESS TOUR TALENT
Thanks bro
We dizasta fundi ni kweli nikitaka mziki mzuri nimtafute dizasta
Daaah huyu jamaa anafanya mziki kwa bongo hakuna tena kama dizasta amani kwako brother
Asie elewa kazi ya hiki kichwa aisee hatokuja kuelewa milele @dizasta vina ndio nembo ya hip hop isio vunja nguzo ata moja ya hip hop brother umetisha sana
Thanks, please share