UADUI WA FAMILIA KISA MZUNGU | NILIKUA NABANDUKA NGOZI | NIMEBAKI NALEA MTOTO MWENYEWE
ฝัง
- เผยแพร่เมื่อ 25 ก.ค. 2023
- Chendwa ameeleza Safari yake ilipoanza kuingia mahusiano na Mzungu, changamoto alizokutana nazo kwenye Safari hii, Uadui kutoka kwa ndugu na kuingia kwa nguvu za giza.
Changamoto za uzazi na kuvunjika kwa safari yake ya kwenda Ulaya baada ya Mzungu wake ambae ndio baba wa mtoto wake kupata kiharusi cha ghafla.
Katika Haya maisha nimejifunza kitu, kabla mambo yako hayajafanikiwa sio vema kumshirikisha kila mtu. Huwezi kujua Nani mwema kwako na Nani mbaya kwako. Mara nyingi watu hawapendi kuona unafanikikiwa/ kupiga hatua/ kuwazidi. Binadamu hawana huruma, anayeweza kukuonea huruma ya kweli au kufurahia mafanikio yako kwa moyo mkunjufu ni wazazi wako.
Mimi watu ni bora wanichukie kwa kutowashirikisha mambo yangu lakini nifanye kimya kimya, Mimi maranyingi sishirikishi progress zangu ila nita share Success tuu. Hapo hata kama kuna anaetaka kupinga hawawezi ila watakubali tuu.
Karibu sana kwa kipindi +4367764790884
@@OfficialDatingAssistance asante
Ndugu wamemfelisha Sana maskin nayeye Kwasababu alikuwa mdogo akashindwa kujisimamia vyema na akawaamin ndugu zake lakin wakamfanyia husda na roho mbaya na wakamroga yeye na mzungu wake ... kiukwer waswahili wanaroho mbaya Sana..mungu atakulipia kipenzi..pole sana
Naanza kuamini kweli uchawi upo. Ashukuriwe MUNGU atupaye kushinda Asante dada Shena kwa hili
Nimejifunza kitu, adui yako ni yule unayekula naye sahani moja, familia wamemharibia kabisa huyu binti na mtoto wake. Na nafikiri hata huo ugonjwa wa mjerumani ni bomu lililorushwa na babu na sio kazi ya mungu. Tuzidi kumuombea baba ya mtoto mungu akatende muujiza hatimaye siku moja skaweze tena kuongea kwa kinywa chake na kuikuta familia yake.
Very moving story ina mafundisho mengi. Dada shana you are exceptional 👏 umebarikiwa bring people together. Let be short
1> pole sana kwa yote been through a lot.
2> katika maisha Kuna watu huletwa na Mungu. This guy ndio alikuwa ame amekuwa your story yako.
3. Katika maisha kila mtu ana bahati yake. Uswahili kwamba ni lazima na sisi tutokee hapo hapo ni ujinga na kubebeshana mizigo. Ndugu yako hawezi kukusahau mwache aendee na maisha yake mwombe mema. Kama sio mtu wa kusaidia sio mtu wa kusaidia.
Sasa maisha yake yamechelewa kisa ndugu ambao wamekucha nganyia madawa 😮 at times tunashikana sana too much na sio maisha ni kurudishana nyuma. What a topic ya kujifunza uswahili tupa kule
Usipozaliwa familia ya kichawi ni baraka. Pole Chendwa
Hizi familia zinatutesa sana wakiona mtu na watu weupe tu basi mtu atakufanya chochote kile anachojisikia,pole sana dada angu
Nimeumia sana
Yaani mnoooo
Huyu dada Mungu amlinde kama mboni ya jicho,Binadamu nimekosa maneno ya kuongea juu yao hao ndugu yani hata sielewi nyie 🙌🙌🙌
🙏🙏
Tabia ya wazungu wakipenda wanapenda ila yote aliokuwa anafanya tz alikuwa anawaambia familia na inaonekana katumia pesa nyingi sana uyo mzungu alikuwa namawazo yaliopitiliza ndugu zako wamechangia sehemu kubwa sana, mimi nilipata mzungu nikamtambulisha kwa mama kaka yangu alivyosikia ninamzungu akaja eti nisiondoke na mzungu mpaka atowe mali nilitowa maamuzi kuwa hakuna mali wala nini nikaondoka.
Kuna family nyingine wanakuwa na tamaa nyingi sana
Inasiikitisha sn hii jamani. Familia nyingi zina watu wanateswa na ndugu zao wenye tabia za kichawi ila hawajulikani. Kusali na kupata watu wa Mungu wa kweli, inasaidia sana kuwabaini wanga ndani ya familia ila inatakiwa kuwa na kifua maana unaweza kuzimia maana unakuwa hauwezi kutarajia.
Mungu awalaani, ila tulishaambiwa katika kitabu cha Kutoka 22:18 Usiache mwanamke mchawi kuishi... Ni kuwaua kwa kutumia neno la Mungu tu shenzi kabisa.
Dada wewe Mungu awabariki na huyo mzee wako apone mufurahie maisha yaliyobaki. Mume bila shaks alichezwa na hawo jamaa zake, Wabongo.
Jaman haya mambo yapo sana kwenye familia nyingi hata mm yalinikuta baada ya kuonekana nimeolewa na familia yenye uwezo. Ila baada ya kuokoka Mungu alinisaidia sana maana walifunga tumbo nisizae na pia ndoa yangu ivunjike. Ndoa yangu ilivunjika ila Mungu alinisaidia kabla sijaachana na mume wangu nikapata mtoto. Mungu mwema dada usimwache Mungu
Pole sana dear this should be a lesson kwake and others usiseme mazuri yako hata kwa ndugu yako ni bora lawama kuliko shari
Mdogo mzungu wako akija au kufanya mipango ya kwenda kaa kimya paka ukishafika ndo useme..
Maskini mtoto anapata shida na wewe pia na huyo babu yako hana anachofaidika
Shendwa usithubutu tena kuwashirikisha hao ndugu zako hata hali inavyoendelea ya baba mtoto wako usiwafahamishe, tena uwaeleze kuwa huna mawasiliano nao tena. Na akipona ikibidi kwenda sepa kimya kimya achana nao hso wanga hata huyo kaka yako usimfahamishe cho chote.
Pole sana Mungu wako Yuko hai atakutetea,ila jifunze usiwape ndugu nafasi kubwa kwenye maisha yako
Pole sana ndungu.Hzi family sa nyingine sio za kuamini sana.pengine ni family yako ndo chanzo ca yte hayo.Mungu awe nawe. na ukifanya mambo yko usiwashirikishe. Yamenikuta na mm nimelia hadi nishajinyamazia zangu tu.
Uchawi upo maisha bila kua na imani ya mungu ni changamoto pole sana binaadam hatuaminiki
Jamani niwambie watanzania unapotaka kusafiri usiwambie ndugu wala marafiki uchawi upo
Adui mkubwa ni wale wa nyumbani kwako. What's a sad story. Walimfanya kitega uchumi. Mungu amtetee. Ikiwezekana ahame tu kwenye hiyo familia hao sio ndugu kabisa.
Absolutely 💯
Mzungu wa watu alienda kukuta bank yake hata haisomi tena wabongo washamfilisi akapata stroke.
dada wafrica wivu ,uchawi upo sana kwa hawa ndugu zetu,ukiondoka tena usiage mutu,wenzako hata hatuagagi mtu ,mshike huyu Mungu dada..ndio mtetezi wako,dada ndugu wabaya mdogo wangu ,yametukuta hayo ,ila Mungu arituvusha , Mungu akutetee dada na baba watoto wako, mdumu sana kwa maombi, damu ya Yesu wanazareti iwafunike ,
Tatizo letu sisi watu weusi hatuna upendo ukizingatia wazazi wote wametangulia mbele ya haki waliobaki ni shida sana kujaliana kwa dunia hii ya sasa mungu ampe roho ya subra na uvumilivu katika mapitio apitayo mungu ni mwema mwenyewe Rehema
Huyo Dada Anachosema Ni ukweliii kabisa Africans family’s ni shida Aisee 😢😢😢😢😢😢
Wangapi wapo hapa Leo baada ya ushuhuda wa Chendwa kweli MUNGU mkuu🙏
Whuue Ogopa Binadamu kwa kweli ,He Will be Well in the Mighty Name Of Jesus Christ 🙏🏿🙏🏿😢😢😢❤️❤️🇰🇪
Endelea kuomba, pia nenda ubalozi wa Austria na mtoto. Waombe mtoto akamwone baba yake. Tumwamini Mungu, ukiwaelezea watawapa nafasi ya kwenda kumwona. Tuachane na haki nyingine kwanza. Ni muhimu wakaonane kwanza. Pole sana binti yetu
Yes vile mtoto ni wao watafanya DNA kila kitu kitakua sawa.
My dya pole sana. Ndg zetu ni mashetani sana. Ila tumuombe sana Mungu roho mbaya za kichawi ziitoke familia
Dah!Familia hizi ni shida..Adui huwa hatoki mbali kwakweli..Mungu awafanyie wepesi kwa dada yetu huyu..😨
Hakikaa
Pole sana mdogo wetu
Ndo mana siku hizi watu kusaidia ndugu hakuna tena
God is the great physician and the miracle worker. God has the final answer! Receive restoration with compensation 🙏
Absolutely!!
Nawe mjinga Sana unheondoka Kunaa mambo ya kuhusisha familia Ila sio hayo mie dada angu alitilia sumu kbs eti mdogo wangu mie Niko kivyangu na watu ukiwaeleza watakuona mswahili nyokoo hayajakuta mie dada yangu kabisa tumbo moja
Poleee
@@LucyKapinga-fg4dk Asante mwaya hii dunia hii we acha kabisa Kuna watu tunapitia maisha ambayo watu Wala wasikuchukie .haya kikuta wewe shukuru Ila hkn kitu kinachooumiza km kutendwa na ndugu huwezi kueleweka Ila daah
Baba wa Mbinguni aka tende jambo kwa binti huyu na mtoto wake MAANA Yeye ni Baba asiye shindwa 🙏🏾 , PIA aka mrudishie furaha na kutimiza yale maombi yake makuu🙏🏾.
Praying for you Chendwa, hugs ❤️❤️
Amen 🙏
Mpaka nimelia Sanaa namuombea kwa Mungu akae sawa
Inasikitisha sana ,binadamu kutokuwa na Hutu ,Mungu ni mweza Wa yote furaha itarudi maradufu.Yeremia 33:-3 niite nami nitakuitikia nitakuonesha mambo makubwa magumu usiyoyajua.Ameen
Don't share your plans to anyone Don't trust people people are evil
🙏
Sure
Mungu atakufanyia wepesi,kila jaribu Lina mlango wa kutokea,Kuna siku usiyotegemea atakufanikisha maana Mungu yeye hachelewi Wala hawai na tena hana choyo adui zako atawaaibisha
pole dada Shedwa aende kwa padre RIMISHO yupo chuo kikuu mliman amesaidia watu wengi aende aombewe mambo yatakaa saw
Pole sana shendwa . Endelea na maombi kumuombea ķuti atakaa sawa. Pengine akiona mtito wake na wewe atapona
Nimeamua ku like hii post hata kabla sijaiskiliza coz I'm sure itakua nzuri sanaaa big up Shena
Inasikitisha hii Story
Pole sana shendwa anaekuchoma ni wakaribu yako mungu akupganie.
Amen kwake 🙏
Mungu aponye tu jamani mungu yupo nimelia Kwa ajili Yako Amen na hakika utamuona tu mungu aponye huyu baba
Mungu amjalie maisha marefu dada huyo amuondoleye mitihani iyi ni Kama storie yangu mimi, nilijikuta nabakia mjane na mtoto wa miezi 9 ,ila alicho andika mwenyezi mungu akuna wakuki badilisha watachelewesha tu ila Allah atakamilisha ,Leo hi nipo Norwey na mzazi wangu ndugu zangu ,walio yafanya Leo mimi nakuwa msada kwao.Allah akupe maisha marefu.vita utaishinda❤❤
Pole tunakuombea. Mungu hatakuondolea yote. Amen. ❤❤❤❤
Pole sana Dada!Shida ya watu wetu ni wivu. badala ya kutumia mafanikio ya mmoja kwenda mbele.
Jamani, mama yako na baba yako wakiondoka duniani, huna familia. Baba yako akiondoka kwenye maisha ya mama yako , pia sio baba yako tena. Usingewashirikisha hao familia, ungeondoka kimyakimya.
Pole sana.
Mbona Kama vitiligo jmn, sio kila kitu kurogwa, pole sana Chendwa, familia yako ni mfano wa familia nyingi sana Tanzania
Kuna watu. Wanarogezewa magonjwa ili mjue hii vitgo kumbe sio
@@anastaziamathias8861 kama unaamini uchawi hata magonjwa ya kawaida utachelewa kutibiwa, hayo ni maoni yangu I’ll not go back and forth with this
Pole sana Chendwa pole asante sana Shena kwa kwa hii story atafutiwe namna aende kwa mume wake.
Aisee jamani, pole sana dada kwa uliyoyapitia ni mengi na mazito sana, story inahuzunisha mno...nimeumia dah😢 Mungu aendelee kukutia nguvu mpendwa. Lakini ulikosea kuwashirikisha watu wa familia yako ilihali ulishawajua ni wachawi😢
Mtihani
Tumuombe mwenzetu
@@OfficialDatingAssistanceHabari Shena!! naomba na cm yako binafsi ya whatsapp. Asante
@@OfficialDatingAssistance kabisa jamani🙏
Doooh ndugu wachawi kweli wameweza kukufanyia hivo pole sana.😊
Pole sana,Kazana na maombi, Mungu atakushindia
Jamani pole sana. Kama inawezekana arudi part 2 kama Hani 🙏🏾😕
Omg😢😢. Mungu akupiganie dada yangu. Mungu akapigane vita yako yote.
Shetani mbaya sana. Ndugu zako wana roho mbaya na ni wachawi. They had something to do with it. Vitu vizuri kama hiv you keep it to yourself. Adui akijua your next move ana jua pa kukuattack.
Ameen ameen
Mwamini MUNGU USIACHE MAOMBI SHETANI YUKO KILA MAHALI
Pole sana dada angu mungu akutie nguvu hata hili litapita ucjl uso wa mungu ukatembee pamoja na ww na mwanao mzungu wako❤
Amen kwake
Tumuombee mwenzetu
Pole sana dada hivyo familia yako inaroho ya kimskini sana , yani wanaona wivu mpaka wana kupa magojwa , khaaaa
Pole sana dada omba mungu sana
Pole sana sada Mungu akuondokee ukiwa wote akupe furaha AMINA
Pole sana mdongo wangu mungu akupe subira yaani nimeumia sana njamani
🤔 very sad story, huyo kaka yake alikuwa tapeli tu. Mungu ampiganie huyo mme wake. Kama ni ischemic stroke Mungu atamsaidia kwake yote yawezekana.
Mtihani sana
Pole sana. Uchawawi upo.
Pole sana dada mwenyezimungu akufanyie mambo rahisi.
Inshaallah mola atamnyanyuwa mumeo na mtaanza maisha mapya na mtoto wenu. Mola hamtupi kiumbe chake.
Pole sana sana inabidi haende ubalozi wa austra apste msaada wajua pia mtu haki yake wasimzulumu
Daaah nimeumia sana hizi familia zetu pamoja na ndugu zetu mungu atusaidie tunapokuwa tunapambana sio wote wanapenda imenigusa sana hii story pia nimejifunza kitu unapokuwa unataka kufanya maamuzi juu ya jambo furani jiangalie wewe kwanza ndugu watafuata pia huenda alishindwa kufanya maamuzi kwasababu alishakuwa amelogwa hakujua nini chakufanya alikuwa anapelekwa kama upepo daaah 😢
Mungu ni mwema na mwaminifu atatenda tena kwa wakati🙏🙏🙏🙏
Dunia shikamoooo …. Ndugu mtatuua jamani tunapitia mateso kutafuta hao wazungu bado mnaturoga 🙌🙌🙌🙌🙌🥲🥲🥲 MUNGU tusaidie peke yetu hatuwezi
Dada umefanyiwa uswahili, kaka zako kaa nao vizuri, wamekutumia kama kitega uchumi
Duhhh pole sanaaa
Hapo ndio umuhimu wa kuwa na maamuzi binafsi kuliko kutegemea ndugu
Ni kweli atamimi yalinikuta mambo kamaayo sikuwa namaamuzi binafsi😌.
Pole sana dear, hakuna lisilowezekana kwa Mungu dear, Mungu azidi kukuimarisha
Amen 🙏
Mungu ATAKUSAIDIA atamnyanyuwa na atakuwa Kama zamani mtaishi pamoja. Amin🎉 kweli huyo kijana ni MUUGWANA SANA na nimzungu huyo.
Pole sana shendwa sad sad ndugu shikamooni🙌 mungu akutie nguvu
🙏
Keep on praying God is going to make a name for himself to your situation
🙏
Very sad story wallah😢 Mungu ampe nguvu na amsimamie yeye na mtoto wake pole sana beautiful
Shena napenda nywele zako, it's so beautiful ❤️
Ahsante 🙏
Dada nenda kwenye maombi na picha ya mumeo usikate tamaa mungu yupo mumeo atapona
Amen 🙏
Pole sana mdogo wangu Allah akupe nguvu na subra kwa sababu ya Mtoto wako Aamee 😢
Jamani ndugu, ndugu ndugu, hapana aiseee ndugu wanaumiza mnooo
Mimi siagi siku yakuja wala kuondoka, msiseme mambo yenu kwa ndugu iwe mama wala dada wote , usiamini mtu kirahisi.
Pia kuzungukwa na ndugu na marafiki wengi nayo tatizo wakikuona wewe ni mtu wakutoboa watakubock.
Allah akufanyie wepesi dear pole
😢😢nimelia jamani uwii....haya mambo yapo jamani🙌nilipata mchumba sweden tulikuwa tunawasiliana poa tu ma mwanangu alimpenda ni mtanzania anaishi huko eeh ghaflaa 😢tuu yaani ananitxt "sorry endelea na maisha yako" nyie wanadam 🙌
Pole
🙏
@@hamida2187 🙏🏻
Nina choamini Yesu hajawahi kushindwa jitoe Kwa Yesu kikamilifu.Damu ya Yesu Ina nguvu ita damu ya Yesu atafunguliwa TU atapona.majibu ya daktari silo majibu ya Mungu..Mungu wetu ni Mungu wa yasiyowezekana.
Good blessings, mungu atakusaida mama
Ndugu zake wamemloga mzungu wa watu sema ulikuwa mtoto kazana kusali sana watamuua baba mtoto wako
Jamani Afrika tuna Wivuuu mbayaaaa haaaa dada simama na maombi sana, na ujitambue sana mana ndugu zako waweza wakukua na mwanao.
Mungu ATAKUSAIDIA atamnyanyuwa na atakuwa Kama zamani mtaishi pamoja. Amin🎉
Naitamanu no yk nikuombee kiopiga hio roho iliyotuma kuharibu maisha yk Kwa jina la Yesu
kuna story zinaumiza sana so sad Mungu atafanya jambo kubwa sana kwenye maisha yake
Aiseeeee saiz naona maana halisibya kufanya vitu kimyakimya khaaa🙌🙌🙌🙌🙌 ila watu wa karibu sometimessss 😂🙌🙌🙌🙌
Sana
😢😢😢so sweet and lovely story❤❤❤
Pole shendwa wabaya ni ndug zako na hao ndo wanakuchezea wewe pamoja na huyo baba inauma sana jmn
🙏🙏
Daahh pole saana jamani!.story inaumiza hii
Mimi sijaolewa na mzungu Ila nilishawahi kupitia Hali hiyo Tena ndugu tumeshea tumbo moja tumezaliwa siku moja kisa tu nilikuwa nasikilizwa Sana na wazazi wangu
Mtihani
Pole
Pole Sana Mungu,anakwenda kufànya maajabu ya uponyaji juu ya mzazi mwenzako Kwa mamlaka aliyotupa Mungu uponyaji upo juu Yako na juu y mzazi mwenzako.sema Amina.
Amen 🙏
Hongera sana Kwa kuweza kuwaibua Hawa watu wanaoitaji msaada unanfanya kazi ya utumishi wa aliyetuumba.
Ubarikiwe Sana shughuli zote hizi njema unazifanyia Tanzania au nje ya nchi yetu ya Tanzania?
Pole sana.
Pole sana Chendwa.
Damu ya Yesu ikafanye uponyaji kwa baba mtoto wa Shendwa. Amen
Pole sana Shendwa
What a sad story aki nimelia sana mungu akusaidie mdogo wangu
Tutamuombea shendwa..Mungu atamvusha hapo
Amen 🙏
Dada acha kulia Anza kuamini fuatilia TH-cam arise and shine kila saa tatu usiku shida zako hizo zimeisha tena Ni ndogo Sana,hatujamaliza live imekatika cjui mume wako anaendeleaje atapona haraka tu utakuja kunishukuru hapa.
🙏🙏
Exactly Haya mauzauza, dada chendwa nenda Kwa mwamposa tena omba appointment Nae ..Mungu atawafungua hivyo vifungo...hayo Ni mazingaombwe
Kwa kweli asimame na maombi atafanikiwa
Pole binti hizi familia za kiafrica. Acha mungu akutetea
Nipe namb ya whatsap nikupigie notake ushauri kwako
Kuna lakujifunza hapa , chendwa ulivyongundua ndugu zako ni wapigaji juu ya mzaz mwenzio, usingewaambia kitu kuhusu kwenda huko wala taarifa zako zozote na angekuja huyo mzungu wako kwania kukuchukua ungeondokea mwanza kwa yule bimkubwa na hata wangefunga ndoa yake ya simple sana akasepea hukohuko mwanza na angefika huko akaendelea na maisha yake kimyaaa
Mpaka nimelia jamani lakini Mungu atafanya Nina Imani Mungu atafanya lakini Kaa mbali na family yako si watu wazuri watakumaliza na Kinga yako na siraha yako ni maombi tu Mungu hajawahi kushindwa jambo kama amefanya kwa wengine na kwako atafanya kwa Imani yote yanawezekana,Tulio olewa na wazungu tunaelewa vzr anachoongea huyu Dada📖❤️🙏
anajikaza Sana asilie 😢tuishi na ndugu kwa maarifa Sana
🤝
Anaonekana Ana uchungu sana, Yesu akufungue
Jamn napenda sana kusikia Mambo mazur
Inasikitisha sana 😢😢😢pole sana my Mungu yupo pamoja nawe
Jamani machozi yamenitoka !! Mungu amtie nguvu
Pole sana shendwa
Tunawasubili. ❤❤❤❤
Mpe pole sana, nasisimuka sana
Amen 🙏