Zembwela Kuhusu Ndoa "Kuna Mke Mke, Mke Mke Wenu Na Mke Mkeo" | SALAMA NA ZEMBWELA PT 2
ฝัง
- เผยแพร่เมื่อ 4 ต.ค. 2024
- #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
MSAFIRI HUFIKIRI
Moja ya jambo ambalo nimejifunza kuhusu maisha na kufanikiwa ni KUTOKATA TAMAA wakati unatafuta ila kubwa kuliko ni wajibu wetu kutojiona tuko JUU zaidi ya wengine na kuamini kwamba pale ulipo hakuna siku ambayo utakuja KUTETEREKA. Katika makosa ambayo unaweza kuyafanya ni kuamini hilo jambo KUBWA.
Hillary Daudi ni Kaka yangu na Rafiki yangu, mimi nilianza kwa kumuona yeye kwenye TV kabla sijakutana naye rasmi kwenye mwanzo kwa miaka ya 2013 kupitia Rafiki yangu mwengine aneyeitwa Mussa Hussein, Mussa na Zembwela ni washkaji ambao wali click tu mara ya kwanza walivyoonana na Mussa alipomsikia tu Zembwela aliona atamfaa sana kama atakua partner wake kwenye kile kipindi alichokua akifanya cha kuanzia saa tatu asubuhi pale EA Radio.
Zembwela alikua mmoja wa waanzilishi wa kipindi cha vichekesho pale ITV akiwa na Rafiki yake Marehemu Max, na jambo ambalo mimi nilikua silijui ni kwamba Zembwela yeye ndiye aliyekua muandishi wa yale maigizo mafupi mafupi waliyokua wanafanya, na hilo swali nilimuuliza baada ya kusikia tetesi mtaani kwamba toka Max atangulie mbele ya haki yeye Zembwela amepoteza kabisa ile ladha na kwamba sasa si yule wa zamani. Ki kawaida tu kwanza hawezi kuwa kama yule wa zamani na zaidi ni kweli ladha pengine lazima ipotee maana sasa hivi yuko peke yake, ila je kipaji? Binafsi nadhani Zembwela ana kipaji na utashi wa hali ya juu ambao unamfanya aendelee kuwepo pale alipo na sasa akiwa anasimama kama Ndimu kwenye Radio ya Wasafi FM pale asubuhi anapokua anachambua magazeti.
Mwanzo nilikuambia Zembwela alianzia EA Radio baada ya kuvutwa na Mussa pale, na alikaa kwa kipindi hata baada ya Mussa kuondoka yeye aliendelea kuzungusha gurudumu la Super Mix ila baadae mambo yakabadilika na ikambidi aende kutafuta ustaarabu mwengine na sehemu nyengine. Maisha yako wakati mwengine yanaweza kukupeleka sehemu ambayo wala ulikua huitarajii.
Sasa pia amerudi kwenye TV na kaniibia siri pia kwamba hivi karibuni anatarajia kuanza series ambayo wao kama Wasafi TV wamekua wakiipika kwa kipindi sasa. Naamini hii itakua habari njema kwa wengi ambao wamekua wakiisubiria kwa hamu.
Na pia kasema itaanza hivi karibuni.
Mimi na Zembwela pia tumeongelea maisha yake binafsi, kuondoa kwa Max, kazi za kileo na mustakabali wa Siasa na wana Siasa na mengine tele. Moja kubwa ambalo naweza kukuahidi ni enjoyment na kucheka, hakika haya UTAYAPATA.
Tafadhali enjoy,
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahs...
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
Audiomack Link bit.ly/YahSton...
TH-cam Link bit.ly/TH-camS...
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
Kuna elimu na kuna kuelimika... Huyu jamaa kila nikimsikiliza naelimika sana... Asante kwa maisha yako Zembwela, jua kwamba kuna watu tupo tunapata elimu sana.
Mwamba huyu hapa, we are too blessed to have you till now. Akili nyingi mkweli mchekeshaji huchoki kumuangalia Wala kumsikiliza. Ahsante sana Salama kwa kutuletea huyu Mwamba muwe na afya njema tuendelee kujifunza
Nime enjoy Sana Leo sister salama jamaa mkweli sanaa
Yani nakipenda sana iki kipande cha mke mke. Mke mkiwenu. Mke mkeo. Nimejifunza mambo mazuri sana. Big up zembwela na salama bin jabir.
Waoo! Kipindi kimenielimisha na kuniburudisha sana😊 Big up sana salama na kwa kaka yangu Zembwela
Hebu muache km mienzi 2 halafu mlete tena salama huyo jambaa yuko vizuri sana na ana mambo mengi sana ya kutufunza
One of my favorite shows wow
Sister Salama na Zembwela mmeua sana , y’all very smart people. Binamu Mb, Master , Salama and Zembwela to mention a few … Yall are the Cream of your trade of choice and talent. Fanyeni jambo….❤️
Ppp
This guy is very fun, he made my night 😂😂😂😂
Asante dada salama, asante pia kwa zembwela babu nimeelimika sana leo napia nimeinjoy SHUKRANI 🙏🏻
Zembwela kwa hakika naku SALUTE. Nimefaidika na mifano uliyoyapeana. Ufafanuzi wako ni Elimu tosha.. pongezi sana bro. Mimi nakukubali..
Siku ya nne sasa nairudia hii daaah🙌🙌🙌bonge la interview
Allah akupe uhayy,huwa na enjoy nikimfwata zembwela anajuwa sana hadi anakera,Allah azid kukubarik
Gari bovu huvutwa na gari zima.... Fact Beberu 🍺
Asante salama, asante Hillary(Zebwela) mbarikiwe kwa somo la maisha.
Daa Nimekubali Sana
Thanks for the interview salama, madini ya kutosha, respect babuu zembwela
Babu kaongea ukweli mtupu mwishoni facts respect sana kwake
Tunajifunza mengi sana kupitia interview
Babu
Nampenda sana bro zembwela ni mkweli cku zote pia kazi zake nzuri
Asante dada salama kw kipindi chako naenjoy sana
One of the best Salama na episode.....kudos!!!
Thank you for you salama hua unatuletea watu kama hawa chuma kabari yao mbwa napata ziriki kwa mguu zake .I love him namejifunza vitu vingi sana kupiata Babu zembela Ak mume wangu 😂😂😂
Swali la kipofu hapo nadhani Salama umekosea kuuliza swali kama hilo, upofu sio swala la kuliwekea utani maishani kuna wanaotaabika na upofu
I like that mke mke,mke mkeo ,mke mke wenu😂😂😂
Thanks my mom for this interview 😀😀😀😀😃🤣🤣🤣😂😅😂 appreciate madame salma j
Madini ya kutosha Zembwela tunashukuru Sana kaka!
Wenye dini hawana imani na wenye imani hawa dini ..!
Watu wa dini, Bwana Yesu asifiwe, Shalom, Salaam aleykum, mi si mtu wa dini nisije tafuta dhambi mpya
Zembwela nomaaaa sanaaa!
Mke mke, mke mke wenu, mke mkeo🔥🔥🔥🔥
Nimeipenda sana show yenu, nzuri sanaaa
Shoo Kali Sana! Producer Tunamuomba Mb Dog Mzee Wa Latifa Kwenye Shoo
Zembwela bhana eti ooh! Bugger zinanenepesha!😆😆😆😆😆😆😆🤣🤣🤣🤣 , nimefurahi sana maneno ya Zembwela,
Oooh my Good one of the best busara nyingi na hekma thanks you for doing doing good job my sister
Nimefurai sana Leo kumuona zembwela. Big salama.
Very factual for sure Zembwela. I never knew u such an inspiration bro.i salute u man🤝👍👌🙏💯✔
Real zembwela mungu akupe kheri nyingi duniani
Msamiati wa Mke mke
Mke mke wenu na
Mke mkeo.
Umenimaliza kk vijana tulio wengi tupo hapo kwenye Mke mke wenu.
the show was great...nilitamani msingemalza☺
I think this is one of the shows ambayo salama ame enjoy sana
Safi saana nimenjoy saana pindi la lao zembwela katisha kinoma
Dah nime enjoy sana
One of the best interview all the time anaitwa BEBERU kabali yao or BABU
Zembwela👉🔥🔥🔥✌️
Hela ndo nguvu za kiume zilizobaki. Vijana tafuteni helaaaaaaaaaaaaa😅😅😅
salama and zembwela you guys are too smart ...
Zembwela big up
Asante kaka,🇧🇮
Naomba Zembwela arudi tena
Zembwela katisha sana
This is excellent show. Hongera sana Salam J . Zembwela is too real!~
Daaaaa dada asante Sana kwa kutuletea huyu jamaa n ukweli mtupu kaongea hapo
Dah ais
" Alaa moja panga mbili haikai, Babu zembwelaa chuma cha pua kabari yao." Naamia kamanda hujawai niangusha.
Full of lessons...!!
"Hela ndiyo nguvu ya kiume pekee duniani "by babu zembwela
Nimependa saan na nimejifunza vingi 🙏
mke, mkeooo... wanaumee na wavulaaana... safi sana Beberuuu
Best interview.......elimu ya kutosha nakukubali sana zembwela .......
Salama Tuletee yule Mbunge Mhe.Kishimba,mch.Gwajima au Mhe.Msukuma.
Kabisa aanze na mh.kishimba then msukuma
Kwa kwl salama nme enjoy sn kipindi cha leo
Awesome amazing 💙
Dah kipindi nimekiona kifupi san asee 😋😋, arudi tena ,ikibid muda uongezwe
Kweli kabisa.. Hapo sawa kabisa.
Asante sana kwa hili darasa
Great Show as usual Dada....
Twataka part 3 salama
Vichwa viwili, hatari.. safi sana.
Aisee...🙌🙌🙌
Nimeona muda wa kipindi mdogo leo jamaniii. ..Zembwela hachoshi kumskiliza wallah ukiplus na maswali yako Salama ndo kabisaaaa...
Kwenye mke nimekuelewa sana brother 🙏
Well said brother
Utakula alafu ule au utakulaa kwanza, mkunga mwenyewe ameshachika
Namkubali Sana Beberu,Nmejikuta Natamani Aendelee Kuongea,Hachoshi.
Dah madini special sana
dada unatufundisha maisha asante🙏
Nmependa sna hii interview ya zembwela sna na chumvi katupiga sehem zaman emoji hazikuwepo 🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Utakula alafu ule au utakula kwanza 😂😂😂😂😂
🤣🤣🤣🤣
Moja ya mahojiano bora yalopata kufanyika kwenye karne hii.big up zembwera
Zembwela siyo Zembwera
Zembwela siyo Zembwera
nimejifunza mengi sana katika interview hii ya zembwela ni maisha halisia kabisa
Hello, umepotelea wapi my dear
Nice one salama..big up sana.
Daaaah zebwela khatar saanna
Fresh akajibu hakuna mtindi kitambo sana,jamaa ana misemo uyu
Dada salama mlete pia Masoud Kipanya please!!!
Bonge la show....Zembwele moto
ZEMBWELA BABU... NAMKUBALI SANA HUYO
Huku wa prove wrong lakini ulihishi katk nyota za bahati may be za majina au ulikuwa unawategemea financially
nimeipenda
Mpaka machoz jamn
Ila Zembwela 😂😂😂🙌
Wanaosikiliza September 2024 tujuane.. bonge la kipindi..haichoshi
Beberu🙌
Nimechelewa Sana kuangalia hii interview mpaka Bwana zebwela ameanza ku trend huko tick tock na what's up stutus nikasema ngoja nije kuona utamu bonge moj ala rahaaaa na buridaniiii iliojaaa elimu toshaaaaa ama kweli junguu kuuu halikosi ukoko
Salama nakuomba huyu jamaa uweunamwita marakwara anaelimisha jamii
Nimependa sana watafute pesa sio mterezo wataanguka chali😂😂😂
Zambi mpya 🤣🤣🤣🤣🤣😭😭😭
Kwa max sikutegemea hiloo jibu umejibu kisilani
Nime enjoy na nimefurahi dada salama kumleta kaka zembwela kwenye kipindi chako nimejifunza mengi Sanaaaa kutoka kwa zembwela na kwako pia MSAFIRI HUFIKIRI
Vyuma vimekutana
Safi sana
Salama huyu mwamba inabidi awe na part 3 & 4