Kilichojiri kesi ya padri na wenzake wanane tuhuma za mauaji ya Asimwe
ฝัง
- เผยแพร่เมื่อ 27 มิ.ย. 2024
- Watuhumiwa wanane wa mauaji ya mtoto mwenye ualbino, Asimwe Novath (2) wamefikishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba akiwapo Paroko Msaidizi Elipidius Rwegashora wa Parokia ya Bagandika wilayani Misenyi Mkoa wa Kagera.
Mtoto Asimwe alichukuliwa Mei 30, 2024 na watu wawili wasiyojulikana akiwa nyumbani na mama yake, saa 2:30 asubuhi katika Kitongoji cha Mbale kilichopo katika Kijiji cha Bulamula, Wilaya Muleba mkoani Kagera.
Mabaki ya mwili wa marehemu Asimwe yalikutwa yametelekezwa kwenye mfuko wa sandarusi chini ya karavati katika Barabara ya Ruhanga Makongora, katika Kitongoji cha Malele, Kata Ruhanga, Juni 17, 2024 na kuzikwa siku iliyofuata Juni 18, 2024, nyumbani kwao.
Washtakiwa wote tisa, leo Ijumaa Juni 28, 2024 wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba na kusomewa shitaka moja la mauaji ya kusudiwa ya mtoto mwenye ualbino, Asimwe, ambalo ni shauri namba 17740.
Awali, Mkuu wa Mashtaka Mkoa Kagera, Waziri Magumbo amesema Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza shauri hilo, hivyo washtakiwa wote hawatakiwi kujibu chochote hadi watakapofikishwa Mahakama Kuu.
Jamhuri imefungua shauri hilo la mauaji ya kukusudia namba 17740 la mwaka 2024 ambalo limesomwa na Mkuu wa Mashtaka Mkoa Kagera, Waziri Magumbo, mbele ya Hakimu Mkazi wa Bukoba, Eliapokea Wilsoni, aliyesikiliza shauri hilo.
Baada ya kutajwa kwa shauri hilo na kusikiliza na Hakimu Mkazi Bukoba, Eliapokea Wilson amehairisha kesi hiyo hadi Julai 12, 2024, shauri litakapotajwa tena na washtakiwa wote tisa wamepelekwa rumande, gereza la Bukoba.
Pole
Wanyongwe hao kenge..
Padre tunamalizana nae kwenye Novena kwisha habari yako
Wanyongwe
Aibu kwa paroko na mzazi wa mtoto hao wamefunga kazi
Inasikitisha
Hatar mpaka mkuu wa kanisa ameshiriki!
Na wale walio muhwa kamanda mawaza mbona kwann wameachiwa?
Pingu Moja watu 3
Wèwe mtangazaji kuwa makini wanne wapi ujui kitu
Maandiko yalishasema aliyeua kwa upanga auawe kwa upanga sioni kwenda mahakamani wakati kila kitu kipo wazi nikupoteza makaratasi na kusumbua majaji tu
Padre? Makubwa duh
Uyo anajifanya kavaa suti alafu muaji wanyongwe kabisa
Sidhan kama waliitaji ulinz wowote mngewaachia2 wananchi wakawachoma moto
Msipoteze mda nao please please nyongeni kabisa
Mnaua mtoto kweli kwanini na nyie msiuwawe
Police nimewaheshimu Tena Kwa wale asikali wapelelezi alivyotengeneza nywele kama mchezaji wa mpira au muuingizaji fulani hivi kumbe askari
alikuwa ni kibu Denis kabla hajawa staa
Mbwa hao ni kunyonga ty
Wewe mbomba wa nne vip na tisa
Msipoteze muda nao wale ugali wa bure magereza hao pigeni chuma wana faida gani sasa napata uchungu nikimkumbuka asimwe jamani alivibebwa hana tumaini lolote yuko mikononi mwa wanyanganyi hapana wauwawe tu
Ndani ya police kuna vitengo aisee yaani kuna jamaa wawili hapo wamesokota nywele utadhani ni wavuta bangi ukiwakuta mtaani kumbe ni maaskari aisee.
Hao wapelelez wanafung ndevu
@@VeronicaAdam-lx8yd wanafuga ndevu na kusokota nywele,ndo maana sipendagi kuropoka kwa watu nisiyo wajuwa