Salama Na DEO GRATIUS SE6 EP64 | PRIVILEGED?! PART 1 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 24 เม.ย. 2023
  • #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
    Deo Gratias, jina tu linatosha kujielezea kama wewe nawe utakua kama mimi wa kutaka kujua maana ya majina ya watu ili uweze kujua tabia zao au ujiulize wazee wake walikua wanafikiria nini wakati wanaamua kumpa jina hilo mtoto wao. Kwa Deo maana imejibeba na imejikamilisha na kwa yeye kuamua kubaki na jina lake hilo hilo mpaka kwenye stage ambako ndo sehemu yake ya kazi inabidi hilo nalo likuambie jambo kuhusu yeye na jinsi ambavyo anajichukulia na kuyachukulia mambo ambayo ameyachagua kuyafanya.
    Shukrani ziende kwa Mungu ndo maana ya jina lake, shukrani ziende kwa Mungu kwa kila alifanyalo leo, shukrani ziende kwa Mungu maana baada ya wazee wake kumsomesha kwenye shule ambayo walikua wameianzisha wao na kuhakikisha kijana wao anapata elimu ambayo anastahili lakini yeye akaamua kuiacha fani ambayo aliisoma na kuamua kuwa mchekeshaji basi nadhani Shukrani ziende kwa Mungu, Shukrani ziende kwa Mungu kwa wazazi wake kuelewa, Shukrani pia ziende kwa Mungu kwasababu mwanga umeanza kuonekana kwenye lile alifanyalo sasa.
    Yeye na rafiki zake ambao ni vijana wenzake wamejikusanya na kuanzisha kundi lao linaloitwa Watu Baki, ila hawakuamka tu wakaanzisha, kuna ka story hapo nyuma yake ambapo ndo panaleta maana kwenye maisha yetu na yao kama watafutaji. Deo anakumbuka audition ya kwanza ya Stand Up Comedy ambayo aliwahi kuifanya na akashinda huko Mbagala, chini ya shindano lililokua likisimamiwa na Evans Bukuku, Deo anakumbuka kushinda MILIONI nadhani kwenye shindano hilo ingawa alipofika home aligundua kuna mwana alichomoka na elfu kumi yake, yaani kuna mwana alimuangalia Deo, kisha akakiangalia kibunda alafu akasema nah, hawezi kumpa yote lol.
    Courage ya kufanya mengine mengi ikiwa na pamoja na ambayo yanaendelea leo ilianzia hapo. Mengine yakabaki story!
    Story ya kujikusanya na wanae enzi za Cheka Tu na baadae kuamua kundoka na kuanzisha WatuBaki ilikua mmoja inabidi awe na uthubutu na uthubutu huo uliwezekana na mpaka leo wamesimama na wana time yao kwenye DSTV ambayo inatoa burudani nzuri tu kwa watu wao na vile vile bado matamasha ya nje wanafanya wao kama wao.
    Kwa wengi ikiwa pamoja na mimi tulipewa story kwamba Deo ni mtoto flani wa kishua alokua kutoka kwenye familia inayokula wali kwa kijiko na ndo maana baadhi ya mambo ilikua rahisi kwake kufanyika kwasababu ana uwezo wa kurudi nyumbani kwa Baba na Mama na akarudi na mzigo wa kutosha ambao unasaidia mambo yaende. Ila kwa mujibu wake, hiyo si habari na wala yeye hajatoka kwenye mazingira hayo ambayo wengi wanadhani ametokea.
    Bado safari ndo kwanza imeanza na kwa wenzake yeye akiwa kama kiongozi anaamini kama wakitulia pamoja na kufuata maono yao basi mengi mazuri tu yatakuja, ila sasa huo uwezo wa kuweza kutulia pamoja na kutengeneza kitu kikubwa na kizuri ndo inawezakana ikawa mtihani. Si wengi wameweza ingawa wapo ambao wameanza pamoja na mpaka leo wanaunguruma pamoja. Inawezekana na yangu matumaini wao pia wataendelea kuwa WatuBaki kwa muda wote ulobaki.
    Love,
    Salama.
    Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
    SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
    Listen our Podcast on
    Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
    ‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
    GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
    Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
    ‪TH-cam Link bit.ly/TH-camSalamaNa
    Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
    Follow:
    Twitter: / yahstonetown
    Instagram: / yahstonetown
    Facebook: / yahstonetown
    Channel Administered by Slide Digital
    Instagram: slidedigitaltz
  • บันเทิง

ความคิดเห็น • 70

  • @fadhilimwakaje154
    @fadhilimwakaje154 ปีที่แล้ว +2

    This guy deserves more recognition than he got..keep up deo 👊

  • @dorisfabian4776
    @dorisfabian4776 ปีที่แล้ว +6

    My favorite comedian.. Deo gratius

  • @camillah1097
    @camillah1097 ปีที่แล้ว +2

    Mungu mwema kaka utafika mbl sana unatisha kwenye jua kali nakupenda sana kk Deo

  • @aloyceshaban1348
    @aloyceshaban1348 ปีที่แล้ว +7

    Duke on 🔥🔥🔥🔥

  • @sumayaishengoma4543
    @sumayaishengoma4543 ปีที่แล้ว +4

    Genious himself Deoooooooooi🎉🎉🎉🎉🎉🎉🎉🎉🎉

  • @skigen
    @skigen ปีที่แล้ว +1

    I love listening to Deo, he's a talented story teller.

  • @agnesmussa197
    @agnesmussa197 ปีที่แล้ว +3

    Salama Tunaomba Wachambuzi Wa Mchongo pia 🙏🙏🙏

  • @Lugonela
    @Lugonela ปีที่แล้ว +1

    Very smart guy

  • @sarahsesa8851
    @sarahsesa8851 ปีที่แล้ว +1

    Napenda kingereza chako very super

  • @chiccynaturaldamnhot877
    @chiccynaturaldamnhot877 ปีที่แล้ว +1

    Wow nimependa sana when he explained about Utu baki!!

  • @movierecapsswahili1042
    @movierecapsswahili1042 ปีที่แล้ว +1

    I truly love this guy

  • @goodlucktemu3149
    @goodlucktemu3149 ปีที่แล้ว +4

    Deo ni mchekeshaji bora kuliko wote apa Tz kwa anaebisha amfatilie.

  • @jasirimjasirimedia7940
    @jasirimjasirimedia7940 ปีที่แล้ว +1

    This man is genius keep it up brother

  • @asterialucas4680
    @asterialucas4680 ปีที่แล้ว +1

    I like this 👍

  • @johnwilfred3920
    @johnwilfred3920 ปีที่แล้ว +5

    Joel Arthur Nanauka

  • @JonasMbilinyi-py2hg
    @JonasMbilinyi-py2hg ปีที่แล้ว

    Love this guy

  • @KaijageNdyanabo-xx3eq
    @KaijageNdyanabo-xx3eq ปีที่แล้ว +1

    Huyo broo wetu kioaji kutoka ifoza mtoto wa mzee mboya Daah broo mm nàkukubali mno

  • @JoeMziwanda
    @JoeMziwanda ปีที่แล้ว

    msera ni genius sana huyuuu

  • @bigdaddy_faustinjumong4427
    @bigdaddy_faustinjumong4427 ปีที่แล้ว

    Bro Juwa kama unapendwa saaaana 🔥💪

  • @christinasinderema3005
    @christinasinderema3005 ปีที่แล้ว +2

    Hahaaa linda linda

  • @masalakulwa7601
    @masalakulwa7601 ปีที่แล้ว +4

    Nampendaga huyu kaaka...anawaigiziaga lafudhi watu wa ifakara utacheka ufe ..very genious aise

  • @heightsmays5963
    @heightsmays5963 ปีที่แล้ว +2

    Tunamuomba Moto Mabanga

  • @faudhiasalum7279
    @faudhiasalum7279 ปีที่แล้ว +4

    🤣😂Linda Linda 🤣

  • @masalakulwa7601
    @masalakulwa7601 ปีที่แล้ว +1

    Anaongea deep sana kisomi..mabongolala hawawez mwelewa

  • @BIGBOSS-hl3bu
    @BIGBOSS-hl3bu ปีที่แล้ว +1

    Sauti ya huyu mwamba inafanana sana na idriss sultan😂😂

  • @dankirunda3368
    @dankirunda3368 ปีที่แล้ว +1

    Safi HomeBoi #Deo

    • @ashaidd2912
      @ashaidd2912 ปีที่แล้ว

      Plz Joel nanauka salama

  • @maryamconstantine2232
    @maryamconstantine2232 ปีที่แล้ว +9

    Nilivyomuona huyu kaka nikaja mwenyewe 😂😂

  • @faudhiasalum7279
    @faudhiasalum7279 ปีที่แล้ว +7

    Joel nanauka please

  • @dullah5733
    @dullah5733 ปีที่แล้ว +3

    Salama katoka London innit that’s why there was money involved innit 😅😂innit innit 😂

  • @Angle-lm3sb
    @Angle-lm3sb ปีที่แล้ว

    🙏🙏

  • @faudhiasalum7279
    @faudhiasalum7279 ปีที่แล้ว +1

    Juma lokole please

  • @official-madudu4959
    @official-madudu4959 ปีที่แล้ว

    Namsikia kyombo deo akiongea

  • @JoeMziwanda
    @JoeMziwanda ปีที่แล้ว +2

    ANAKITUUU ATAFIKA MBALII😂

  • @azizaedina8088
    @azizaedina8088 ปีที่แล้ว

    🥰🥰🥰🥰

  • @zebedayobiswalo1924
    @zebedayobiswalo1924 ปีที่แล้ว

    Diamond platnumz please

  • @dianerditto
    @dianerditto ปีที่แล้ว +3

    I love deogratius much, good interview 🥰

  • @rehematawalani733
    @rehematawalani733 ปีที่แล้ว

    RRINDA RRiNDA umemuacha wapi weee no unaweza na RRiNDA RRINDA

  • @rizikiurio1133
    @rizikiurio1133 ปีที่แล้ว

    Joel nanauka pleaseeeeee 😊

  • @haphsamaulid304
    @haphsamaulid304 ปีที่แล้ว

    Mtot WA mama mboya😂😂😂

  • @haniphadaud667
    @haniphadaud667 ปีที่แล้ว

    Wachambuzi Wa Mchongo 🏃🏃🏃

  • @priscamnzava2656
    @priscamnzava2656 ปีที่แล้ว

    Home boy

  • @ishe_ngo8926
    @ishe_ngo8926 ปีที่แล้ว

    Siku nyingine tumia lugha moja kiingereza haieleweki kiswahili haieleweki pia. Siku nyingine tumia kiswahili hutaeleweka vizuri.

    • @fadhilimwakaje154
      @fadhilimwakaje154 ปีที่แล้ว +1

      Sio kwamba wewe ndo una uelewa mdogo 🤔

    • @Unique653
      @Unique653 ปีที่แล้ว

      Jifunze kingereza ndugu yangu, utateseka sana

  • @bahatijonas2183
    @bahatijonas2183 ปีที่แล้ว

    Tuletee WACHAMBUZI WA MCHONGO Ganslay na Headmaster

  • @rehematawalani733
    @rehematawalani733 ปีที่แล้ว

    Kweli comedy imekukontro yaani nacheka kwa kuchekesha

  • @julianamaganga4803
    @julianamaganga4803 ปีที่แล้ว +1

    Toomuch talking but he's goodguy

  • @fakiikibakola1300
    @fakiikibakola1300 ปีที่แล้ว

    Swali moja majibu 100

  • @godfreymiho4927
    @godfreymiho4927 ปีที่แล้ว

    Huyo jamaa ni hatar

  • @lucydelina1749
    @lucydelina1749 ปีที่แล้ว

    Salma naomba uniite na mim jamn

    • @olicej7837
      @olicej7837 ปีที่แล้ว

      Siku ukiitwa uniambie na mimi nikusindikize🤣🤣🤣🤣🤣🤣😂😂😂

  • @officialbntrasool5223
    @officialbntrasool5223 ปีที่แล้ว

    Salama uniite mim siku moja 😊

  • @vonniemarry2680
    @vonniemarry2680 ปีที่แล้ว

    Hachoshi kumsikiliza

  • @domycossan1395
    @domycossan1395 ปีที่แล้ว +1

    Kwa mara ya kwanza ndo najua maana ya Mtu Baki au Watu Baki

  • @derickdepota101
    @derickdepota101 ปีที่แล้ว

    Deogratius mtu na nusu

  • @mrs2918
    @mrs2918 ปีที่แล้ว

    STIFF Ifakara moja,

  • @emmamatemu8225
    @emmamatemu8225 ปีที่แล้ว

    Hii kuchanganya kiswahili na Kienglish sometimes inakera

  • @Bongodailyhabari
    @Bongodailyhabari ปีที่แล้ว +2

    Mtu umezaliwa na MD na afisa af useme sio wa kishua c'mon we ni wakishua manzee period. acha kutuchora

    • @kokusimabayona4179
      @kokusimabayona4179 ปีที่แล้ว

      Kwakweli anatuchora,. Gari wamenunua akiwa form 2 wakati wengine wazazi wao wanastaafu bila hata gari Ila wabongo

  • @maggieluvuno4666
    @maggieluvuno4666 ปีที่แล้ว +1

    Dereva wa Bobo na Linda Linda

  • @bm4tv602
    @bm4tv602 ปีที่แล้ว +1

    Kingereza Cha mjinga huyu ni super

  • @julianamaganga4803
    @julianamaganga4803 ปีที่แล้ว +3

    Toomuch talking but he's goodguy