Tazama Misemo Ya Mchungaji Hananja Ilivyomvunja Mbavu Salama | SALAMA NA RICH BILIONEA PT 2
ฝัง
- เผยแพร่เมื่อ 2 ต.ค. 2024
- #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Kipindi cha nyuma kidogo nilifanya lile ambalo huwa nafanya la kuwashirikisha rafiki zangu na team kuhusu list ya watu ambao wangependa kuwaona kwenye kiti chetu chakavu na sababu za kwanini hasa waje kwenye meza ile yenye kigae kwa juu maana tukisema tutaje majina tu bila ya sababu thabit za wao kuja pale tunaweza tukaondoa maana yenyewe ya kuwa na watu wenye story za kuvutia na kutufunza kama ambavyo tumekua tukifanya. Jina la mgeni wetu huyu lililetwa kwangu na Michael (Mx) Mlingwa na Ndugu yangu Elbogast Myaluko ndo alinipatia mawasiliano naye na kuanzia hapo mengine yamebaki kukhadithiwa kama hivi.
Sikua namfahamu Mchungaji Richard Hananja mpaka Michael alipo niambia nami nikachukua muda wangu wa kwenda kufanya ka research kangu kabla hajaja mezani, ambacho nilijifunza ni kwamba Mchungaji alikua ni mtu mashuhuri sana ambaye ana watu wengi sana pia wanao mskiliza. Ilinichukua takriban miezi miwili kuweza kumpata maana kila weekend (mara nyingi rekodi za kipindi huwa zinafanyika weekend) yeye huwa yuko safarini. Huitwa sana sehemu mbali mbali, na sasa Serikali nayo imekua ikimuita pia katika matamasha na mikutano mbalimbali. Kwahiyo mara utamsikia yuko Dodoma, mara Moshi, mara Iringa ilimradi yuko busy. Na wakati mwengine Jumapili yake inakua ya yeye kualikwa kwenye Makanisa mbalimbali ili akatoe neno, siku hizi yeye ameshastaafu kuhubiri kanisani na sasa zilizobaki ni hizo za mialiko maalum.
Kama kawaida mimi na wenzangu tulitaka kuanza kwa kumfahamu mgeni wetu maana kama nilivyokuambia hapo awali mimi sikua namfahamu zaidi tu ya kumuona kwenye mitandao akimwaga cheche, tulianzia kwenye kuzaliwa kwake na kukua kwake, mitihani mbalimbali ya ujana, bishara na kazi ambazo ashawahi fanya, na wakati naandika hii nimejifunza pia kuwa Mchungaji hana ambalo anaongeza chumvi maana baada ya sisi kufanya nae maongezi haya, nimeona ameenda sehemu tofauti tofauti na story yake haijawahi kubadilika.
Ujasiri wa ziada huhitajika ili tuweze kufanikiwa kwenye maisha yetu na pia kuwa kwenye mstari ili usiingie kwenye matatizo na vyombo vya sheria. Mchungaji ananiambia jinsi ambavyo alikua ana hustle kila kona, kusafiri bila ya kibali cha kuvuka mipaka ya nchi na boxing ambayo aliifanya kwenye kipindi flani kwenye maisha yake. Boxing imemuachia kovu ambalo kila siku linamkubusha mapambano ambayo ameshawahi kuyafanya kwenye maisha yake.
Boxing pia ndo ambayo imemfanya awe na discipline ya hali ya juu. Kwenye maisha yake ya sasa Mchungaji Hananja anatoa nafasi kwa kila aliye kata tamaa au ambae watu wamemkatia tamaa, yeye ndo huwachukua hao na kuwapa nafasi nyengine kwenye maisha yao, na amini usiamini wengi wao hunyooka na kuanza upya. Kwenye nyumba yake huko Madale Mchungaji anafanya mambo mengi ikiwa pamoja na kilimo na ufugaji. Swali langu lilianza kwa kutaka kujua hizo pesa za yeye kuweza kufanya mambo yote hayo, huwa zinatoka wapi?
Mchungaji Hananja ni MUME, na kwa mujibu wa maelezo yake, alichelewa saana kuoa na mkewe ni Rafiki yake wa kwanza. Yangu matumaini moja mbili tulizopiga humu zitakupeleka sehemu.
Tafadhali enjoy.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahs...
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
Audiomack Link bit.ly/YahSton...
TH-cam Link bit.ly/TH-camS...
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
Funny, educational, humble, inspirational, loving, caring what an interview. Respect to you Salama and the billionaire.
Nilijihisi kuwa nipo kwenye lecture room nakula nondo ❤
Wallahi nimecheka sana, pia nimejifunza kwa nondo za Hananja
Aslam aleikum salama hope everything well on your side, I'm from Kenya and I really enjoyed your interview with rich billionaire and the previous interviews too.. Wanna request if possible to bring him back again coz he's educate so many people in this world. And it's gives people not to give up in life.. SALAMA we love you and Allah bless you good things happen to you. xxx
Dada leo hakuna msosi wala juisi😊😊..ni nondo mwanzo mwisho. Nice interview..Mwamba sio wakuulizwa maswali meengi. Ni kumchokoza na kumwacha atambae
🤣🤣🤣
❤❤❤❤❤❤❤😂😂😂😂😂😂
Amini😂😂😂
Hii like 100 ni yangu natamani nilike Mara Mia Mia what an interview!
"Shetani haonei mtu asiyekuwa na akili." 🙌🤛
Nikweli kbs
umenifanya nicheke
Nimepata majibu ya mengi kupitia Interview hii kuhusu maisha, uchumi, Imani na mengine mengi 🤝💪
Hii ntarvew imenifunza na imeongeza kitu kwenye Maisha Yangu kupitia hii interview naenda kua tajiri huu Mwaka imenipa ujasir Zaid ya kutafuta ishi Sana Salama na Father apo rich billionea mchungaji
JAMANI TUCHICHEENI BASATA WAMPE TUZO YA KUFAFANUA KUHUSU MTU NA DINI ALIYO TOKEA... THIS IS REALLY REALLY REALLY HARD TALK
Hakuna kushindwa kwenye maisha,bado maisha yapo,maisha yamapambano yanakufanya uwe imara...asante Mchungaji Rich..
Salama ni mwandishi bora... umemwacha mzee aongee,nasi tumepata elimu. Kuna waandishi wengine wangemkatisha... salama ni type ya Millard ayyo
Salama naangali Mtumishi ananipa raha mbavu zangu
Hakika
yes
Salama always the best interviewer
hii mimi pia nimeliona salama is professional ever
Hongera salama Kwa kipindi mie nakufuatilia sana unatujenga sana ,hakika mungu akutie nguvu
Huyo baba nii was aiana yake, humble, helpful and passionate. Hatuchoki ukimsikiliza. Ujumbe wa kutosha! Tutaufanyia kazi . Thanks Salama. Good work!!
Masha'Allah Tabaraka'Allah
Yani mda mdogo sana, Salama tunamuhitaj tena please
The best of the best interview.....
Sisi sote ni wa Tanzania 🇹🇿 hakuna cha udini,ukabila wala rangi.. tusigombanie maini kabla mwenye ng'ombe hajachinja
"Jambo la kwanza siyo maombi. Jambo la kwanza ni Ukombozi wa fikra." 🤛🙌
Daah one of the best interviews from Bongo in recent times, Salama you are the best keep this up. Your interviewees give us relevant information and education and I'm sure I'm among many who appreciate this show.
Ubarikiwe dada kwa kutuletea huyu mtumishi wa Mungu
"Umeletwa ili usaidie, siyo usaidiwe." 🙌🤛
Tufanye ibada ndugu zangu, Mim Huwa naumia Sana napokuta mtu wa dini fulani anamchukia wa dini nyingine,
Mchungaji wa kweli unamuona, sio kwa ubinafsi na kuahidi magar na miujiza, ila kwa kujitoa. Billionea mfano wa kuigwa.
Dada salama pole sana leo kwa kijasho
Japo leo umeyakanyaga
Salama, swali lako kuhusu imani na dini pamoja na sayansi ni zuri mno na limewagusa wengi sana, pia nashukuru kwa patience uliyonayo wakati unamuuliza maswali.
"NDANI YA UJANA KUNA UTAYARI WA KUFANYA KAZI"
#WALK_THE_TALK
Best interview 2023🙌 nmepata majibu ya maswali
Nakupenda alafu najifunza sana kwako baba Mungu akutunze
Kwa kweli Aliposema kuhusu muda ameni inspire mambo mengi
Hongera sana dada mungu akubariki na Asante sana mchungaji kwa ushauri mzuri 🙏🙏🙌🙌💯❤️❤️❤️❤️🤝
Yani natamani msimalize maana nabarikiwa sana nacheka hadi nashangaa najihisi mpya kwa maongezi ya MCH Hananja Mungu akulinde na akutunze mpendwa
kipindi cha kwanza kama hukueleweka vzr bt hiki cha pil,daaah big up sanaa
Yaaan mpaka nashindwa ni comments how ntacomment maana ni mgodi tena wenye kila Aina ya madini
😅😅😅 for sure
Salama , ubarikiwe sana , kutuletea mtu na nusu , bonge la elimu , billionaire ni full package abarikiwe sana 🤝🤲
MPIGANIA UHURU WA UCHUMI🙏👍
Jihurumie uhurumiwe. Jitese uhurumie wengine
Asanteeeeeeeeee"watu huwa wanauliza mbona hunywi pombe majibu hayo"akili yangu yenyewe pombe🤣🤣🤣🤣ikinywa ni hatari
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Hatari sana
Hata mimi. Najiona hivyo, kuwa sinywi pombe bado huwa najitafakari maamuzi na matumizi yangu naimagine ningekuwa mnywaji ningekuwa je sasa!! 😂😂
@@filamupictures9349 tungekuwa wehuuu😂😂😂
Uyu mzee ni Mzalendo ...i wish to meet you Mentor wa Taifa.
Salama asante mzee ametufunza mengi.#One Love
"Imani siyo kuelewa, Imani ni kukubali." 🙌🤛
Interview Bora sana kwangu imenipa majibu mengi,good job salama kip it up.
... Interview Bora kabisa kutokea kwenye ubora wako #SERMON
Sasa Mchungaji wewe unawaelekeza Watu Safari ya mbinguni usio Na hakika Nayo? wewe Huna uhakika na ufalme wa Mungu?.
ni inspire sanaaa hyu mchungaj anatoa nondooo sanaaa mungu akuweke
Dah huyu mzee kichwani yupo vizur sana ubarikiwe
Fedha ni ulinzi....bila fedha huna ulinzi...👊
📌
Nondo mzee
Mtumish Nimekpenda Sana nimejifunza vtu we ni jasiri Mungu azidi kukupa nguvu na uishi miaka 10000000
Salama we mzur sanaaaa, na be blessed kwa kutuletea watu wa kutujenga
"Mpigania uhuru wa kiuchumi", Asante sana Mchungaji.
Hongera sana Dada Salama, Unajua sanaaaa, interview inaubora wa hali ya juu, inavutia kusikiliza. Nimejifunza sana. SHUKRANI....
Huyu mtu namuona mkubwa sana hadi anatisha.Sijawahiona mtu anaongea hivyo hslafu vya maana tupu.Hakika atukuzwe Mungu kwa uumbaji.🙏
kabisa yan mm ndio nimechoka kabisa kwasababu yakutafakari anachoongea yeye na kila neno lake ni point big IQ aisee
Nimeangaliaaa nikajua Salama ndio anahojiwa!
Mimi ni muisilamu Ila uyo mzee mchungaji ,nampenda sana mafundisho yake ni bora
😂😂kwani waislamu hawapendi mafundisho yake😂
I'm blessed through this interview
Thanks God and to U Salama and Young Rich
Salama umemleta mtu na nusu mwenye fact za maisha.
Salama leo umepatikama hata swali Huna nafasi ya kuuliza😆😅😅🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Jamaniii...."Jicho lako linaona nini".. hii ni muhimu sana...
MUNGU yupo jamani huyu mzee ameletwa apo na MUNGU ili tupate chakula cha UBONGO
Hii ni interview bora zaidi kuwahi kuitazama.
Asante Salama kwa umahiri wako ktk uandishi. Big up!
This is the best interview ever🙌🏽
Daah mwalimu wangu kitambo sana...leo nmecheka...naomba nipate number yako ...mwanafunzi wako msasani Luther an church 2002
Nimeguswa sana sana sana na mchungaji huyu... Daah!! Barikiwa salama kwa exposure ya watu hawa!! We need this things to trend 📈 jaman
Kama mmenotice salama haonekani sana atakuwa hana mbavu muda mwing sanaaa
Hakuna kushindwa kweye maisha. Maisha ni kupambana jiamini.
"Mnajenga majengo kutega uchumi, sisi tunajenga kutega huduma." 🙌🤛
Best Interview 2023..MCHUNGAJI HANANJA KIBOKO
This man has such fidelity to humanity; nonetheless, he speaks really fast for Kenyan ears.
Ubarikiwe sana mchungaji,umetoa madini ya thamani sana.❤❤❤
Huyu mzeee anafanya nikose usingizi kwa kumsikilizaa
Tusisifie tu interview jamani tubonyeze na kitufe cha support ....Salama you the best Kuna mengi wenye digital media zao wana cha kujifunza kwako....keep going!
Wew ushabonyeza?
Kule unaenda kutiwa moyo tu, muhimu FANYA KAZI. 🤛🙌
Mchungaji Hana njaa anaongea kama kanywa maji ya chooni hatar mpaka salama kaganda.
Nakupenda sana maneno yko yananipa moyo nguvu na usabiti
The best lesson, utoto utumwa ,ujana maswali,uzee ugonjwa
This will be interview of the decade.
Kabisa ✊🏾
He talks real and reality.... Nice and good thanks for this fantastic show
😊😊😊 ety Imani zingine ukifa unakamuliwa hili urudi ukiwa mtupu.
I love this pastor.. lazima nije kutoa chochote kwenye kituo chako kabla robo ya kwanza ya Mwaka huu kuisha.. Serious naguswa sana na mission hizi
Please don’t forget if you haven’t 🇬🇧😁
I wish to meet this man one day, very humble, very intelligence man, he is third eye opened, he is just see life in a spiritual way. he see love 😍.
I think he meditate
Hata mimi nimetamaani
Umetu inspire sana....
Hongera sana Salama kwa kubuni kipindi kizuri Mungu akusimamie ufike pale unahitaji
BWANA YESU ASIFIWE.
TUMSIFU YESU KRISTO.
Hakikaaa mungu awe nawe daima mchungaji
Jamani watu wa📷📸 leo nahisi wanakufa kwa kucheka🤣🤣🙌🙌🙌🙌🙌🙌 HAPANA jamani 🤣🤣🤣🤣🤣
😅🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Natamani sana vijana wote wangeisikiliza hii interview. Kwa kweli ni mafundisho muhimu kwao. Asante sana.
Hananja Mungu akusaidie usirudi nyuma katika huduma yako,unaongea ukweli mtupu
Salama huu mwaka umetufungulia na mazuri sana kwa kila jambo vijana tunajioliza tumepewa majibu hongera sana salama salut kwa mzee wetu mchungaji nipo KENYA nainjoi
Salama ni hatari. Elimu tumepata❤
Mwamba huyu hapa..anatoa sana Elimu
Wewe sio secretary wa MUNGU
Salama mrudishe tena Rich billionea atupe madini mengine
Hii interview 😀😀salama hana haja ya kuuliza maswali yote anajieleza tu mchungaj wa watu
Yani🤣🤣🤣🤣
Maneno n mengi na hapotezi point🙌🙌
Point inabaki imesimama
machali wa arusha musiyopenda kazi munajambo la kujifunza hapo
Mchungaji ananikumbusha marehemu Mzee majuto Mungu ailaze roho yake. Mchungaji Rich Bilionea unafunza injili kiualimu
M. Mungu amfishe haliyakua ksmridhia
Best interview ever
❤😂Nakupata sana billionaire Rich 5/5 från Stockholm Sweden Ubarikiwe sana
Mchungaji Thanx ur genius
Giant wa Tanzania 🇹🇿 🤝🤝🤝👊👊
am rich kid..inspired by rich bilioner..lifee is good. thanks much SALAMA JABIRI for this message ..always you are at the Top ❤
In whatever he does, he sees and encourages live for one another, nampenda sana very open minded. Thanks for a great listening skill @Salama
Hii ndio ya Yahstone town👍👍