Salama Na DR TULIA SE6 EP50 | BULYAGA 1976 PART 1 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 15 ม.ค. 2023
  • #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
    Tulia Ackson ni jina kubwa kati ya majina makubwa kwenye Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na kwa sisi kuweza kulipata jina kubwa na kukubali kuja kuketi kwenye kiti chetu chakavu ilikua ni BARAKA sana. Ila ukiachana na kwamba ni jina kubwa ila yeye ni binadamu, tena wa kawaida tu. Ni Mama, ni mke, ni Dada, ni Binti kwa Mama yake na ni Mbunge kwa wana Mbeya mjini lakini pia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wadhifa ambao baada ya uchaguzi wa 2020 alirudi bungeni kama Naibu Spika ila baada ya aliyekua Spika kujiuzulu Dr Tulia aliona fursa ya yeye kuvaa viatu hivyo na wabunge nao walimpa kura zao zote za kuridhia Mwana Dada huyu AWAONGOZE.
    Baada ya uchaguzi wa 2020 na yeye alirudi bungeni kama MBUNGE kamili, si tunakumbuka baada ya 2015 alienda bungeni kama Mbunge wa kuteuliwa ila mwaka 2020 aliamua kwenda kugombea jimbo la Mbeya mjini ambako Gwiji wa Bongo Flava Kaka yangu Joseph Mbilinyi aka Sugu alikua ndo Mbunge wake? Sugu alikaa kule kwa miaka 10 ilikua ni moja ya ngome za wapinzani ambazo walikua wanajivunia nazo, kwa Dr Tulia kuamua kwenda kugombea pale iliwafanya watu wengi watake kufuatilia mchuano huo mkali ambao mwisho wa siku Dr Tulia aliibuka kidedea. Na haya yalikua ni moja ya maswali ambayo nilikua na hamu ya kumuuliza na kwa urefu alinijibu tu vizuri sana.
    Sasa nchi yetu inaongozwa na Rais mwanamke kwa mara ya KWANZA toka tulipopata uhuru wetu mwaka 1961, na hii haikuja kwa kupangwa ila baada ya kutokea ambalo Mwenyezi alikua ameliandika, na hata hili la kuwa na Spika Mwanamke (ingawa huko nyuma Mama Anne Makinda alishawahi kuwa) nalo halikua limepangwa maana Spika tayari tulikua naye baada ya Uchaguzi wa 2020. So suala la kuwa na Rais mwanamke na Spika mwanamke bila ya shaka linalipa Taifa letu utofauti na HESHIMA flani hivi ambao mataifa mengi yanavutiwa nayo.
    So kwake yeye nini hasa kimebadilika? Yaani kutoka kuwa Naibu mpaka sasa Spika? Ilikua easy kwake kuichukua nafasi hiyo baada ya kuwepo na nafasi hiyo? Alifikiria mara mbili?
    Kwa maongezi yetu haya pia nimegundua Dr Tulia alikua hapendi kabisa siasa, yeye aliyapenda zaidi maisha yake ya kuwa Lecturer pale Chuo Kikuu, alipenda zaidi kuandika na kusoma na kujifunza. Alikua akiwaona wana Siasa kama watu flani ambao pengine wanajiona tofauti na watu wengine, pengine wanajiona wa MUHIMU sana. Je na yeye sasa? Akiwa nao kule bungeni wanaishi vipi? Sasa pia kama Kiongozi wa mhimili huo wa NCHI nini zaidi kimebadilika? Nini zaidi kigumu?
    Maongezi yetu yalianzia nyuma kiasi na mbele pia yakafika, pia humu tumeongelea Tulia Trust na vitu ambavyo inafanya ili kuwafikia wale ambao wana uhitaji. Na sasa amekua naye MWANASIASA, nini kimebadilika? Msemo wa Siasa ni mchezo mchafu, kwake yeye una maana gani?
    Yangu matumaini uta enjoy na kujifunza jambo kutoka kwa Kiongozi huyu ambaye pia ni Dada yetu.
    Love,
    Salama.
    Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
    SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
    Listen our Podcast on
    Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
    ‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
    GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
    Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
    ‪TH-cam Link bit.ly/TH-camSalamaNa
    Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
    Follow:
    Twitter: / yahstonetown
    Instagram: / yahstonetown
    Facebook: / yahstonetown
    Channel Administered by Slide Digital
    Instagram: slidedigitaltz
  • บันเทิง

ความคิดเห็น • 76

  • @drmdee
    @drmdee ปีที่แล้ว +2

    Naomb salama ukianza kuwahoj Hawa uwe unaulizia historia zao walipozaliwa,waliposoma na maisha yao

  • @ramadhanomar8346
    @ramadhanomar8346 ปีที่แล้ว +4

    km na wew umesoma HKL KM MAMA TULIA ACKOSON LIKES HAPA. HUWAGA TUNAONGEA

  • @hopxzbahati1078
    @hopxzbahati1078 ปีที่แล้ว +10

    As a member of the Comment Reading Association (CRA), I’m only here to read comments. Please keep the comments short and simple. We do appreciate your typing effort. Also please watch your spelling. Thank you and have a great day!

  • @davidwillson4894
    @davidwillson4894 ปีที่แล้ว +6

    Dr Tuli, you are smart, jeeembe letu la Mbeya

  • @mzizirashid709
    @mzizirashid709 ปีที่แล้ว +12

    Huyu Mama Yupo Vizurii Jaman Anavyojibu Maswaliii Huchoki Kumsikiliza Yaani Hadi Rahaaa 🥰
    Tanzania inawatu Jaman Vichwaa Haswaaaa

  • @mohamedismail2662
    @mohamedismail2662 ปีที่แล้ว +2

    Akili kubwa ambayo bado naona haijatumika vzur tunaitumia kisiasa zaidi Mungu akubariki Dr Tulia nakuona mbali sana endelea ivyo ivyo

  • @seinabelimi2296
    @seinabelimi2296 ปีที่แล้ว +12

    Naam kwanza ss wanaume tutambue thamani ya mwanamke ktk maisha yetu mfano tu hai kitendo cha mwanamke kazi ya kulea mimba miez 9 heka heka anayopitia mwanamke hata uuze dunia na vilivyomo huwez katu kumlipa hapo bado kwenda leba kwa uchungu na kuzaa na kunyonyesha mtoto hv una kipi cha kumlipa mwanamke huyo zaid ya kumfanyia ihisani mapenz huruma na upole kwao kitendo cha mwanamke kuweka kiumbe tumbon ni hekima ya Mwenyezi Mungu wanawake wanaweza tuwaheshimu na kuwapa elimu ya kutosha ya dini na dunia na tuwathamini tuliingia ktk kupitia tupu zao na humo humo ndo njia ya ss kutokea namuomba mola wangu awalinde na kila baya na kila shari na kila hasad tupate kufaulu ktk huu mgongo wa dunia✍✍

    • @edwinmandela5658
      @edwinmandela5658 ปีที่แล้ว

      ko ulitaka wote tunyonyeshe mngekula nini

    • @mwaminitindwa7131
      @mwaminitindwa7131 ปีที่แล้ว +1

      Mwenyezi mungu akubariki sana kwa hekma hizo, no wachache sana wanaotambua thamani ya mwanamke

    • @seinabelimi2296
      @seinabelimi2296 ปีที่แล้ว

      @@mwaminitindwa7131 shukrani kipenz cha Allah ikiwa unatambua kuna Allah bs utatambua kuna viumbe vya Allah☝️

  • @noeljuvenalmunishi75
    @noeljuvenalmunishi75 ปีที่แล้ว +12

    Beauty, Brain and confidence (BBC) in one person @Dr Tulia Ackson...

    • @dostovan5142
      @dostovan5142 ปีที่แล้ว

      Beauty is questionable

    • @skteller5039
      @skteller5039 ปีที่แล้ว

      😂minus one B tafadhali

  • @gertrudegwarasa632
    @gertrudegwarasa632 2 หลายเดือนก่อน

    Here I am Mama. Nilisoma HKL pia🤝🥰

  • @jescalaurenti4970
    @jescalaurenti4970 ปีที่แล้ว

    She's my role model and my mentor@ Mh Tulia ..... As a youth we should have mentors who inspire us on chasing our dreams en goals..
    Big up mom... 💪 Let's start dreaming big as the upcoming leaders.

  • @nassornassor9678
    @nassornassor9678 ปีที่แล้ว +4

    Talent women big up nimefurahi umetofautisha kazi na siasa umependa kazi kuliko siasa that good 👍

  • @mimmyjijimmy5235
    @mimmyjijimmy5235 ปีที่แล้ว +2

    Tunamuomba Halima Mdee nadhan itapendeza sana

  • @januaryrashid8844
    @januaryrashid8844 ปีที่แล้ว +1

    Speaker ( Akson)
    Mama uko vzr saaana,unajibu maswali kwa confidence ya juu saana,
    Salama asant kwa kumleta speaker

  • @gladnesskombe1664
    @gladnesskombe1664 ปีที่แล้ว

    Nimefurahi sana kumuona huyu jemedari wetu wa uongozi Mungu amlinde awe na maisha marefu ya baraka tele

  • @G.r.e.a.t.I.Q
    @G.r.e.a.t.I.Q ปีที่แล้ว +2

    Kibonge Salamaaaa!👋👋

  • @mussachabonga9595
    @mussachabonga9595 ปีที่แล้ว +1

    Sister Salama big up, this my super woman, fantastic interview 2023

  • @ilhamsalum6815
    @ilhamsalum6815 ปีที่แล้ว +1

    Msuko wa ki Zanzibari kabisa # chana la ndizi 🥰 umependez sis SALAMA

  • @seinabelimi2296
    @seinabelimi2296 ปีที่แล้ว +1

    maisha lazima kutafakar huko ndo kufaulu ktk kila lko ktk maisha kuchukua muda wako na kulifanyia kaz huko ndo kunazalika hekima busara na utu ni muhimu mno maishan mwetu mola atusimamie atutangulie sote ktk hilo ndo msingi wa maisha yetu✍✍

  • @rommelmauma8081
    @rommelmauma8081 ปีที่แล้ว

    Zamani, kazi zilijigawa sana, kijinsia, kulingana na nguvu za misuli yetu. Leo hii, kazi hazitegemei nguvu ya misuli. Teknolojia ya mashini imetuokoa na utegemezi wa misuli; *tunategemea ubongo*! Na uwezo wa ubongo *transcends the gender divide*, japo mila za *kikabila* bado nyingi *work at the advantages of the boys and at the disadvantages if the girls*.

  • @MandrivaShinnyFirstMedia
    @MandrivaShinnyFirstMedia ปีที่แล้ว +1

    Always good job salama

  • @jasmineedamu6089
    @jasmineedamu6089 ปีที่แล้ว +1

    Salama na tulia 💕

  • @yusufmohamed8874
    @yusufmohamed8874 ปีที่แล้ว

    Salama umetisha sana

  • @rosemofuga8101
    @rosemofuga8101 ปีที่แล้ว

    Yaani da Salama umependeza sana haki ya mzungu tena wala sikutanii

  • @stellah3844
    @stellah3844 ปีที่แล้ว +1

    Dr Tulia 💞💞💞💞💞💞

  • @ashooraashoora1180
    @ashooraashoora1180 ปีที่แล้ว

    Tumefrah kweli Allah akuongoze katika Khery duniani na kesho akhera

  • @abuujuhayfa4321
    @abuujuhayfa4321 ปีที่แล้ว

    Big up kwa muheshimiwa 🤝

  • @aminaomary5567
    @aminaomary5567 ปีที่แล้ว

    Salama safi sana,kualika viongozi,mimi binafsi naomba umwalike Mh.Majaliwa

  • @saumusalimuhassan2499
    @saumusalimuhassan2499 ปีที่แล้ว

    Napenda anavyojibu Mheshimiwa Tulia.

  • @nahyialetomia9284
    @nahyialetomia9284 ปีที่แล้ว +1

    Goal 3 in the Millennium development goals - promote gender equality and empower women

  • @hansmwasakyeni3038
    @hansmwasakyeni3038 ปีที่แล้ว

    Bunge saizi lina spika kwakweli! Dada namuelewa sana saizi!

  • @massawemrlowprice3949
    @massawemrlowprice3949 ปีที่แล้ว +1

    Namba 3

  • @amrimtiti9054
    @amrimtiti9054 ปีที่แล้ว

    Namkubali sana spika wa bunge letu na nawish kama ningekutuna nae siku moja

  • @buberwadeus3158
    @buberwadeus3158 ปีที่แล้ว

    👏👏👏

  • @yahyahamad1802
    @yahyahamad1802 ปีที่แล้ว +1

    salama mlete dada Sofia mjema

  • @maryamtanzania9743
    @maryamtanzania9743 ปีที่แล้ว

    Salamama umenenepa umependeza

  • @KamodiTV
    @KamodiTV ปีที่แล้ว

    Kamodi star ✴️

  • @tausonsamwel8736
    @tausonsamwel8736 ปีที่แล้ว

    Bulyaga my home from Tukuyu (took you)

  • @mzizirashid709
    @mzizirashid709 ปีที่แล้ว +2

    Anayefuata Ni Mr Polepole 🥰

  • @stevewanga957
    @stevewanga957 ปีที่แล้ว

    from🇶🇦🇶🇦 2ko locked

  • @tanzaniamycountry9308
    @tanzaniamycountry9308 ปีที่แล้ว +2

    Kumbe waheshimiwa kama Hawa inawezekana kuja mezan eh?
    Sasa niombe umwalike mama yetu uvunje rekod kabisa😊

  • @sheikhmuharammwaita
    @sheikhmuharammwaita ปีที่แล้ว +1

    Mashallah, umenenepa salama

    • @jaymwinyi6957
      @jaymwinyi6957 ปีที่แล้ว

      Mashaallah 👏 tabarakallah Tena sana 🤣mashavu mashavu

  • @donnietommie8444
    @donnietommie8444 ปีที่แล้ว

    #SalamaNaDrLeaky

  • @bedabenson6576
    @bedabenson6576 ปีที่แล้ว +1

    Lete Mgunda

  • @athumanimtengo3350
    @athumanimtengo3350 ปีที่แล้ว

    Napenda sana uelewa wa Huyu mama, namkubali katika hilo suala kwa kweli..ana akili mno na navutiwa kumsikiliza 🙏🙏🙏🙏🙏

  • @Johnsonkayila
    @Johnsonkayila ปีที่แล้ว

    Salama fanya ufanyavyo umlete Mh Khasim Majaliwa;alafu baada yake Mlete Mzee Mwinyi Rais wa Zanzibar

  • @msowamhokole7714
    @msowamhokole7714 ปีที่แล้ว +1

    Mlete konde ama mengi ya kutujibu maana katrend sana

  • @edwardmwakanolo1259
    @edwardmwakanolo1259 ปีที่แล้ว +2

    Mama mwenye Jimbo lake..Mbozyo mwenyewe,mama asiye na makuu,kimbilio la wengi,mfuta machozi wa Wanambeya,mama piga kazi ,mama mwenye HEKIMA,mama bingwa ,Jimbo la Mbeya limetulia na Dr.Tulia

  • @assumaninadja315
    @assumaninadja315 ปีที่แล้ว +1

    Natamani nimuone Diamond kwenye hio meza please

  • @marygregory7566
    @marygregory7566 ปีที่แล้ว +1

    Nimejifunza umuhimu kutafakari

  • @faudhiasalum7279
    @faudhiasalum7279 ปีที่แล้ว

    Salama na juma lokole 😝please please please please

  • @raiyansaleh9255
    @raiyansaleh9255 ปีที่แล้ว

    Milard ayo mlete

  • @kilamiko8299
    @kilamiko8299 ปีที่แล้ว

    Hata kuchunga ng'ombe huwezi kusoma utalisha mazao ya watu ama mifugo kupotea hahah

  • @mountaincoffee7
    @mountaincoffee7 ปีที่แล้ว

    Mlete ayo tz

  • @ahmedahzab9439
    @ahmedahzab9439 ปีที่แล้ว

    Ndani ya dakika 9 nzima wa kuongea pumba ukiachia kukosea Matamshi licha yakua ni gwiji wakusema.👌🏽

  • @Nyimbozainjil
    @Nyimbozainjil ปีที่แล้ว

    Mbeya for TULIA Ackson

  • @kakakuona57
    @kakakuona57 ปีที่แล้ว

    Spika,je unaridhika kuongoza bunge lenye wabunge wa chama chako TU?

  • @johnsahani4182
    @johnsahani4182 ปีที่แล้ว

    Mlete na ndugai

  • @michaellagwen8198
    @michaellagwen8198 ปีที่แล้ว

    Huu msuko wa Salama unaitwaje mwenzenu Mpaka nimewaza kwa sauti

  • @fadhilshafi2947
    @fadhilshafi2947 ปีที่แล้ว

    she's smart

  • @semsimbazisemsimbazi2866
    @semsimbazisemsimbazi2866 ปีที่แล้ว

    Tuleteeni mzee Mwinyi jamani....

  • @paulsibu5770
    @paulsibu5770 ปีที่แล้ว

    Mlete Mama Samia Kiongozi Shupavu.

  • @hendrycomonsiwenga1128
    @hendrycomonsiwenga1128 ปีที่แล้ว

    Nimefurai kumuona Mhe, Dk. Tulia Akson ( Spika Wa Bunge La Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania ) Hongera umeongea point ☝️🤣

  • @samsonmwakikuti5318
    @samsonmwakikuti5318 ปีที่แล้ว

    Unastahili nafasi hiyo,si bahati tu!!