Salama Na DORIS MOLLEL SE6 EP68 HALF WOMAN, HALF AMAZING PART 1 SendTip MPESA LIPA NO 5578460
ฝัง
- เผยแพร่เมื่อ 21 พ.ค. 2023
- #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Doris Mollel kwa kuanzia tu tuanze na jina lake, ni zuri lenye kukumbukwa ki rahisi, yeye mwenyewe pia ni mrembo na mkarimu, sana. Roho yake ni kama rangi yake, nyeupe na kwa bahati Mimi namfahamu yeye kiasi kwa kupitia rafiki zangu ambao yeye anafanya nao kazi na pia ana mahusiano nao mazuri, sana. Pia namfahamu mume wake ambaye tukianza shindano la kumtafuta nani mkarimu kati yao tunaweza kukamaliza kwa suluhu. Huwa naamini Mwenyezi aliwakutanisha ili kwa pamoja waweze kufanya makubwa kwaajili yao na familia zao na jamii ambayo imewanzunguka ambayo kwa kiasi kikubwa ina uhitaji wa yale ambayo wao wameyaona wanaweza kufanya jambo ili yawe mepesi.
Sasa tuanze kwa vipi Doris amekua akifanya ambayo anayafanya sasa ambayo baada ya kufanya kipindi hiki mengi ambayo aliyaongelea kama ya Serikali ya Uganda kumpa tuzo na kumkaribisha nchini mwao ili aweze kushirikiana nao bega kwa bega kwenye suala zima la kuwaokoa watoto wanaozaliwa kabla ya wakati yaani ‘NJITI’ na hivi karibuni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia S. Hassan kutoa MILIONI 70 kwaajili ya kuchangia mfuko wake wa Doris Mollel Foundation. Yeye alikua anataka tu kufanya kitu kwaajili ya kuisadia jamii yake, ananiambia wakati analizungumzia hilo huku akitafuta jambo la kufanya ndipo Mama yake alipomfugua macho kwa kumuambia masuala ya watoto njiti, taa iliwaka sasa baada ya Mama yake kumkumbusha kwamba hata yeye alizaliwa kabla ya wakati. Alipoambiwa hivyo hakukua na kurudi nyuma tena baada ya hapo.
Ananisimulia vikwazo ambayo aliwahi kupata mwanzo kuanzia nyumbani mpaka kwenye kutafuta hizo pesa ambazo zinasaidia mpaka leo hii, Doris ananihadithia jinsi ambavyo alipata bahati ya kuwa na watu ambao wamemsapoti na wanamsapoti mpaka leo kuanzia nyumbani kwa mume wake. Mtu ambae ndoa yao ilikua changa kuanza kuwa na vikao na watu mbali mbali mpaka usiku wa manane inamtaka mtu muelewa sana kuweza kuamini na kuyaacha mambo yaende. Mumewe alikua huyo mtu. Kwa ambao walimpigia simu mara ya kwanza baada ya kuona anchojaribu kufanya, watu kama Asas wa kule Iringa na wengine ambao wamekua wakijitokeza siku baada ya siku. Anakumbuka na anajua kwamba kutokata tamaa kwasababu ya changamoto kadhaa ndo ambapo kunamfanya awe ni mmoja ya watu wanao heshimika zaidi kwa mchango wake kwenye jamii yetu.
Binafsi naamini huu ni mwanzo tu wa mazuri mengi ambayo binti huyu halisi wa ki Tanzania anajaribu kufanya. Sekta ya kulea watoto ambao wamezaliwa kabla ya wakati inahitaji hela nyingi na kwasababu ambazo Mimi na wewe hatuzijui kumekua na vifaa VICHACHE sana vya kuwahifadhi watoto hao mara tu wanapo zaliwa. Doris na Foundation yake amekua akipigana vita hiyo kuhakikisha vifaa vinapatikana sio mjini tu, hata mikoani ili kuokoa maisha ya watoto hawa ambao wengine huishia kwenye debe la taka kwasababu tu walizaliwa kabla ya wakati wao.
Yangu matumaini utamuelewa na utapata nafasi ya kumfuatilia na kama utakua na lolote ambalo unaweza kuchangia basi yuko kwenye mitandao ya kijamii maana siku hizi kumpata mtu na kujua ambacho anakifanya imekua rahisi kupitia mitandao hiyo. Mimi najivunia sana yeye na yangu matumaini atafanikiwa sana kwenye sekta hii kama nasi tutaweza kumsaidia pale panapowezekana.
Tunahitaji kina Doris tele kwenye jamii yetu maana vya kusaidia viko vingi.
Yangu matumaini episode hii itasaidia kukufungua macho kwenye mengi ambayo jamii yetu ina uhitaji.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
TH-cam Link bit.ly/TH-camSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz - บันเทิง
Salama unafanya kazi kubwa sana kutuletea watu muhimu wanaozidi kutu'Inspire sisi wenye ndoto kubwa kuendelea kuzipambania. Allah akuweke sana I wish uendelee hivyo maana siku moja utakuja kunihoji hapo.
Tunaomba Salama na Madenge wa Twitter✊🏽
Sasa mtu kama Madenge ana lipi la kuinspire?
I love this girl
Finally nmesubiri sana
Always a get what a interview from my rolemodel ecejay
❤ safi
Mwanamke ataki usawa anataka kuwa juu ...anataka power...na women cant control power...limitation ya power....hakuna cha nafasi nje ..utaka kufanya kitu ambacho sio chako...nyie ndio mnatengeneza imbalance and confusion mnafanya kazi ya shetani wazungu wamewajaza na mmejaa ....
Salama na Dr.Isack Maro
Uvae dira ❎
Uvae dera✅
Salama na madenge wa twitter 🔥
Salama na George Iron Mosenya
Huyu kaka ni mwandishi mzuri sana wa vitabu, na Dhani pia ndiyo mwanzilishi wa simulizi za sauti Tanzania.
Nampenda sana nahitaji kufahamu zaidi kuhusu yeye na ninaamini anamchango mkubwa kwa vijana na waandishi wa vitabu chipukizi.
Salama na Mama Alaska🤲🏾
Salama Na Diamond na Ray kigosi
Leo nimekuwa wa kwanza😂😂🎉🎉
umepata bei gani
Good
Salama na harmorapa🏃
Afu mbona salama na doris wanafanana...aisee
Salama na mpoki...
Salama naomba umlete Hanscana
Salama na mpoki
Umejuaje yaan salama nampok iyo siku itakua poa mno
Tunaomba salama na Millard ayo
To be in the top of the hierarchy lazima uwe committed enough kushindana unatakiwa uwe Smart enough huwezi kutaka usawa usio kuwa na matokeo hasi nyie ambao ni radical feminist mnawadanganya wengine
Salama na mwijaku plzz
Tunaomba Lukas wa jua kali
First to comment can I please getting myself likes ??
😝😂ngedere
Dada Iyo upo katika Biblia mwanaume utakula kwa jasho ulimwengu wa Sawa sika masani kwa SS Kila MTU Ni jukumu lake
Salama mbona umeacha kuweka majina na umaarufu wa mtu wakati wa interview, inavutia kusikiliza