Dizasta Vina - Mbuzi

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 7 ก.พ. 2025
  • Official Lyric video of the record MBUZI as prepared and performed by Dizasta VIna. Off the studio album, A father figure
    Stream/Download
    TH-cam - • Dizasta Vina - Mbuzi
    Mdundo - mdundo.com/son...
    Boomplay - www.boomplay.c...
    Audiomack - audiomack.com/...
    Apple music - / mbuzi-single
    Other Musical contents
    Audiomack - audiomack.com/...
    Boom play - www.boomplay.c...
    TH-cam - / dizastavina
    Mdundo - mdundo.com/a/2263
    Spotify - open.spotify.c...
    Apple music - / dizasta-vina
    Deezer - www.deezer.com...
    Spotify Playlist - open.spotify.c...
    Connect with Dizasta Vina on social medias
    Instagram - / dizastavina
    Twitter - / dizastavina
    Facebook - / dizastavina07
    sw.wikipedia.o...
    Business: Pan.authentik@yahoo.com
    Website - bio.link/dizas...
    Lyrics
    Mbuzi alipata wadudu kwenye kwato
    Iliathiri furaha na nguvu alizonazo
    Mchungaji alihakikisha mbuzi ananawa
    Aliondoa wadudu wote kisha akamweka dawa
    Alikampangusa chawa akampa chakula kwa wakati
    Akamjengea chumba kwa nafasi
    Ajisikie huru, Akashika ratiba na itifaki
    Muda ukapita afya mbuzi ikatamalaki
    Mtaa ikahamaki ukasukwa uvumi
    Kuwa bwana Kheri Anatoa muda kisha sumni
    Japo hali yake ya uchumi ilikuwa ni duni
    Aliuza matunda mboga chache na kuni
    Hakuna siku mbuzi alipiga kelele kwa njaa
    Watu walimwonea gere balaa
    Alinawiri kwa kilele cha umaridadi
    Majambazi walipiga misele kadhaa
    Na usiku hauwi mwanana akisikia mbiu
    Mbuzi akilalama kwamba anahisi kiu
    Mchungaji alikuwa macho, Akatambua kuna
    Magonjwa nyemelezi akavumbua chanjo
    Mbuzi aling’ara alinona
    Manyoya yalitawala kuashilia afya kila kona
    Hakuwepo hata mwanga mmoja wa kuroga
    Hata Waliojaribu kuchanja walikoma
    Najiuliza maana ya upendo nini
    Mpaka uwe na kingi ndio ushee?
    Au pesa kipindi michango ya sherehe?
    Au mzazi anayetamani uendelee?
    Ndio maana anakulea ile umlee
    Inasadikika kuwa upendo wa kweli ni kujali
    Mama mzazi homa ikikushika tu halali
    Tabasamu analokupa unaposhika Masarali
    Ungekuwa hai ingekuwa kutoa mimba ni halali?
    Wazalendo wanahitaji hela na nyadhifa
    Wanalipwa kutetea sera za taifa
    Wadini wanakumbatia itikadi na imani yao
    Mpaka wanamwaga damu wenzao
    Au mapenzi kwenye timu inapoingia mtimani
    Unaumia inashika mkia na hauhami
    Kufichiana dhambi tabia wanayoisifia masela
    Au mjeshi anavyofia bendera
    Nani anajua siri ya kupenda penda?
    (Ni) kujitoa sadaka kwa ajili ya mwenza?
    Wapo wanaosema kuwa kupenda ni ushupavu
    Wanaumizwa wanachukia wanaandika vitabu
    Ukijua mwenza wako ana mtu anampenda
    Utampa nafasi aende upige moyo konde?
    Mama akifariki na una dawa ya kusahau maumivu
    Swali ni utakula vidonge?
    Je upendo wa kweli ni mpaka aagize mungu?
    Aliyesema ufuge paka alafu umchinje kuku
    Amemmtoa mwanaye kama mdhamini msalabani
    Awafie watu ambao dini hazifanani
    Bado Mawazo yananisumbua nasinzia
    Nawaza ingekuwaje tungechagua familia
    Je mtoto angempenda baba angekuwa lofa?
    Au Baba angemchagua mtoto angejua ni shoga?
    Wanandoa tungekuweka kwenye Time Chamber
    Muda urudi ungemchagua patner wako tena?
    Wangapi wanawish wangepita sehemu hii?
    Wangapi wangemchagua Justin Bieber na Jay Z?
    Kabla ndoa haijakufunga pini
    Jiulize kama mkeo angekuwa na wewe ka' ungekuwa chini?
    Licha ya hizi nyimbo zinazofanya watu walie sana
    Washikaji walingoja niwe msanii ndio niwe mwana
    Pengine inabadili maana ya upendo
    Na kuacha swali upendo je ni haja au matendo?
    Mchungaji alifuga mbuzi alifuga na ajenda
    Alimjali lakini si kwa sababu alimpenda
    Kwani ilipofika sikukuu alitoa vitu
    Sufuria jungu kuu akanoa visu
    Yule mbuzi mzuri aliyenona sana
    Ndiye aliyechinjwa na adhuhuri alichomwa nyama
    read more about Mbuzi genius.com/Diz...

ความคิดเห็น • 756

  • @dizastavina
    @dizastavina  9 หลายเดือนก่อน +234

    Nunua nakala yako ya A FATHER FUGURE Kwa whatsApp, Email au telegram. Tuma 10,000tzs au 650ksh kwa Mpesa +255 762 158 871 au Tigopesa +255 655 696 811 (Jina Edger Vicent Mwaipeta). Kisha tuma jina au sms ya malipo kwa hizo namba.

    • @hamismbwana8592
      @hamismbwana8592 9 หลายเดือนก่อน +2

      Ina nyimbo ngap?

    • @thomaslima921
      @thomaslima921 9 หลายเดือนก่อน +4

      Poa big brain rapper,ndyo maana DUBO alisema mc mbovu utakata tamaa ukimsikiliza dizasta we ni darasa tosha

    • @Mungopark187
      @Mungopark187 9 หลายเดือนก่อน +3

      Jamn mkuje sasa mnunue albamu yenye magoma makali.. Verse kali, beats kali.. Yani kilakitu kikali.

    • @terminal_tz
      @terminal_tz 9 หลายเดือนก่อน +6

      Despite being an MC, I bought this Albam na sijajutia ...nafikiri vijana wengi wangefata failsafA za dizasta maana nawaona Akina Karl max Napoleon hill na wengine wengi Sana ktk history...walioongelea kuhusu ukombozi wa kifikra...dizasta katuletea mawazo Yao in a simple form Kwa Lugha adhimu Sana ya Kiswahili akiilenga jamii yetu....AFF ni album yangu pendwa na nasikiliza Kila siku ubongo unapata Chakula...Dizasta is the master Art, and the only orchestrated symphony...

    • @Brunoh90Tv
      @Brunoh90Tv 9 หลายเดือนก่อน +1

      Pamoja san kaka👏👏🔥🔥🔥

  • @insectondama798
    @insectondama798 9 หลายเดือนก่อน +9

    Mchungaji alifuga mbuzi
    Alifuga na agenda
    Alimjali, lkn si kwa sababu alimpenda
    Kwani.....
    Ilipofika sikukuu ..alitoa vitu
    Sufuria jungu kuu.. akanoa kisu
    YULE MBUZI MZURI ALIENONA SANA , NDIE... ALIECHINJWA NA ADHUHURI ALICHOMWA NYAMA

  • @magotimtani2180
    @magotimtani2180 9 หลายเดือนก่อน +27

    Sehemu ya kwanza ya wimbo inaonekana kuashiria uhusiano kati ya mchungaji na mbuzi kama mfano wa uhusiano kati ya watawala na wananchi, au hata kati ya watu katika jamii. Mchungaji anawakilisha nguvu au serikali, wakati mbuzi anaweza kuwakilisha raia au watu wa kawaida. Mchungaji anajitolea kumtunza mbuzi, ikionyesha wajibu wa serikali kwa wananchi wake, lakini kuna maudhui ya utata kuhusu nia ya mchungaji - je, anamtunza mbuzi kwa upendo wa kweli au kwa sababu ya faida zake binafsi?
    Sehemu inayozungumzia bwana Kheri inaonesha changamoto za kiuchumi na jitihada za kujikimu katika jamii. Ingawa bwana Kheri anajitahidi na hali yake ya uchumi ni duni, anaonyesha uvumilivu na ujasiri katika kukabiliana na changamoto za maisha.
    Katika sehemu inayohusu upendo, wimbo unachunguza maana ya upendo na kujitolea kwa wengine. Inaleta mifano mbalimbali kuhusu jinsi upendo unavyoweza kueleweka na kutekelezwa katika maisha ya kila siku, iwe ni katika uhusiano wa kimapenzi, uhusiano wa kifamilia, au hata katika uhusiano kati ya watu na imani zao au utamaduni wao.
    Mwisho wa wimbo unatoa picha ya kusikitisha ambapo mbuzi, licha ya kutunzwa na kustawi chini ya uangalizi wa mchungaji, anakatwa na kuliwa. Hii inaweza kuashiria udanganyifu wa watawala au nguvu kuu katika kutumia na kudhulumu watu wa kawaida kwa manufaa yao binafsi, huku wakionekana kama wachoyo au wasiojali.
    Na hii verse ya mwisho ndio inasahihisha nia ya utata inayotajwa katika verse ya kwanza.
    Verse ya kati, ni kama anaonesha tu upendo wa kweli ni nini, ili aje afanye hitimisho vema kwenye verse au eneo la mwisho

    • @alphanlukombe3774
      @alphanlukombe3774 9 หลายเดือนก่อน +2

      Upo sahihi mwamba

    • @ferdnandshija2334
      @ferdnandshija2334 9 หลายเดือนก่อน +2

      swadakta

    • @Brunoh90Tv
      @Brunoh90Tv 9 หลายเดือนก่อน +2

      Asantee kwa uchambuzi👏👏👏

    • @MaulidiHimidi
      @MaulidiHimidi 9 หลายเดือนก่อน +3

      Oya, huu mbona kama unamuhusu sana Lunya

    • @munixpicentertainment
      @munixpicentertainment 9 หลายเดือนก่อน

      @@MaulidiHimidi😂😂😂😂 ila watu n wasen

  • @gotintito4455
    @gotintito4455 9 หลายเดือนก่อน +16

    Rafiki zangu wengi wamekuwa wafuasi wa dizastavina baada ya kuwasikilizisha ngoma kazaa...Jana Tu Kuna mwana mmoja kaisifia sana hii ngoma alafu Leo umekuwa released aisee...tunaomba uandae show moja Yako mwenyew tutaingia kwa gharama yoyote.

  • @lukasbuyamba4135
    @lukasbuyamba4135 9 หลายเดือนก่อน +8

    Hem ngojeni kwanza. Mna hakika huyu jamaa ni mwanadamu wa kawaida.. aseeee big up brother Ediga

  • @ibni_H2TL6r
    @ibni_H2TL6r 9 หลายเดือนก่อน +6

    Coment Yangu Ni Ya 99 Dizasta Vineration 17 April 2024 when you read My Comment In 2099 Generation this Dude Was The Best & Genius

  • @QoberConstant
    @QoberConstant 9 หลายเดือนก่อน +5

    Aseee nmeelewa kuwa ukiskiza nyimbo za vina ni sawa na siskilizi nyimbo za wanadamu wenzetu..bado natafuta jina la kiumbe wa kumuita tofaut na binadam wa kawaida ila sijafankiwa kupata asee👊🏼🙌

  • @Yeah-k3h
    @Yeah-k3h 9 หลายเดือนก่อน +4

    Marafiki zangu wamebadilika na wamekuwa wakielimisha wengine kupitia mistari ya huyu mwamba wengine walipata wapenzi kweli huyu ni Mungu wa Rap 100%

  • @jovinkivelege7604
    @jovinkivelege7604 9 หลายเดือนก่อน +6

    SIO POA WE JAMAA UNAJUA

  • @ismailmtengwa8370
    @ismailmtengwa8370 9 หลายเดือนก่อน +8

    Jamaa kipindi unajiita dizasta vina ulikuwa unajua kuwa jina lako litakuwa linaendana na vina vyako mwanangu unajua sana sioni wakukufananisha nae

  • @JirashJamali-s6d
    @JirashJamali-s6d 29 วันที่ผ่านมา +4

    vina anajuwa sana

  • @YunusYahya-gr6ks
    @YunusYahya-gr6ks 9 หลายเดือนก่อน +8

    Waliorudiaa hio nyimbo Zaid ya.mara 10 piga like hapa Jamaa anauwasha Hakuna kama hii kichwaa

  • @robygeniuz
    @robygeniuz 9 หลายเดือนก่อน +5

    Nadiliki kusema tangu niwe mshabiki wa HIPHOP uyu mwamba ndio msanii wangu bora tangu niijue hiphop nikiipokea mikononi mwa prof J oyaaaaa 👊

  • @user-badboyrozay
    @user-badboyrozay 9 หลายเดือนก่อน +8

    Vina juu ya vina humu ndani Kuna bonge la disaster kiufupi hamna usalama🔥🔥❤

  • @msimika_III
    @msimika_III 9 หลายเดือนก่อน +4

    Nadhani ni muda wa kukubali sasa kuwa Dizasta vina ndie msanii mwenye maarifa mengi zaidi na ana namna nzuri zaidi ya kufikisha kuliko msanii yeyote wa hip hop kwa sasa
    Asilimia 90 ya nyimbo za hip hop bongo humalizi hata verse moja unaona unazichosha tu ngoma za masikio yako, lakini ukimsikiliza muwa wa Dizasta vina unatamani hata uwe na verse kumi
    Dizasta vina ndie msanii pekee ambaye huwa nakuwa na shauku sana ya kusikia his next project, bro is pure genius, too good for this industry
    Sijui hii nyumba ya hip hop imebaki na mihimili mingapi mpaka ianguke ila Dizasta vina ni miongoni mwa mihimili inayofanya ili jumba la hip hop lisianguke
    All the best Dizasta vina natumai utakuwa na Madusko yanayoendana na kipawa chako na juhudi ulizowekeza kwenye sanaa yako

  • @godblessluvanda9808
    @godblessluvanda9808 9 หลายเดือนก่อน +8

    Kweriii huyuu jamaa NI NYOKOMBILI 🙌🙌🙌🙌🙌🎧🎧🎧🎤🎤

  • @dankirunda1796
    @dankirunda1796 9 หลายเดือนก่อน +6

    Daaah peni imezingatiwa sana humu 🔥

  • @susumantalanta8505
    @susumantalanta8505 9 หลายเดือนก่อน +6

    Siku zinakuja hili Taifa litabadilika, vijana hawata kuwa inspired na machawa bali ngoma kama hizi....thamani yako itakuwa ya juu sana....Big Up Rasta

  • @Omry_Sinyangwe_2024
    @Omry_Sinyangwe_2024 3 หลายเดือนก่อน +10

    Nasema Hivi Hakuna cha fid q wala killer wala Stamina huyu Vina ndo Mwandishi Bora currently

  • @lampadshigonko3006
    @lampadshigonko3006 9 หลายเดือนก่อน +5

    Nimeelewa kipande cha mbuzi kinanikumbusha tukio la ngwajima kula muhumini wake.

  • @omarabdulaziz3786
    @omarabdulaziz3786 9 หลายเดือนก่อน +4

    Level 5 sorcerer kutoka far future!!

  • @allychilinga1958
    @allychilinga1958 9 หลายเดือนก่อน +11

    Ina pigwa violin inapigwa guitar Tunasikia neno baada ya neno..mpangilio mzuri wa Mashahiri hakuna yo-yo..

  • @ayubukaduma1017
    @ayubukaduma1017 9 หลายเดือนก่อน +4

    vina tungo imesimama mzee , n wateule wachache sanaaa tunaelewa izi chuma unatuachia keep moving broo tunakufuata

  • @user-badboyrozay
    @user-badboyrozay 9 หลายเดือนก่อน +6

    Vina juu ya vina humu ndani Kuna bonge la disaster kiufupi hamna usalama🔥🔥

  • @JREMPIRE-jd1ms
    @JREMPIRE-jd1ms 9 หลายเดือนก่อน +7

    mifumo ya taifa letu d..vina umeuwa...🙄🙄 yule mbuzi mzuri aliyenona sana ndiye aliyechinjwa na adhuhuri alichomwa nyama......

  • @khatibkapire877
    @khatibkapire877 9 หลายเดือนก่อน +3

    Dizasta nataka nimguse huenda sio binadam

  • @mchattachattanoga7795
    @mchattachattanoga7795 9 หลายเดือนก่อน +3

    Kweli dizasta akiwaka anaweza kumgeuza fid akawa sajna

  • @YunusYahya-gr6ks
    @YunusYahya-gr6ks 9 หลายเดือนก่อน +5

    Yanii huyui mwambaa anapigaa mamboo ambayoo hata fid q anakubalii mwambaa anajua kufichaa maana huyu ni kama langaa wa pilii ila mwambaa sijuii wakumgananisha naee dizastaa ni zaidiii yaoooo aiseeee

  • @Yegon254
    @Yegon254 9 หลายเดือนก่อน +4

    Hii ni aina ya mziki ninaoupenda haswa wakati nimetulia

  • @rockonsonmlandi2818
    @rockonsonmlandi2818 9 หลายเดือนก่อน +7

    Mimi naomba bifu ya vina na Rapcha tena 🤤...

  • @Antary9
    @Antary9 9 หลายเดือนก่อน +6

    BLACK MARADONA. SALUTE KWA MADINI BRO.

  • @tariqkhassim4059
    @tariqkhassim4059 9 หลายเดือนก่อน +4

    SOON HUU MZIKI UNAANZA KUA NO 1 ON TRENDING INSHAALAH

  • @ahutamorris
    @ahutamorris 9 หลายเดือนก่อน +3

    Utaratibu au mpangilio wa kutuma pesa kutoka Kenya hadi Tanzania ni upi kakangu @Dizasta Vina

  • @VictorKotein
    @VictorKotein 9 หลายเดือนก่อน +2

    Wewe mwamba unajua sana unafanya ubongo wangu utafakari sana

  • @antonyngao131
    @antonyngao131 9 หลายเดือนก่อน +3

    Vina! Vina! Vina,nimekuita ngapi? Noma sanaa

  • @rigajunior8487
    @rigajunior8487 9 หลายเดือนก่อน +4

    Mwanangu...! Sema tu kiki ndo hunaga but katika watu ambao ni blessed na branded upo kaka yan ni wewe na darassa yani ni brand za kitofauti mno na ladha kali❤❤. Mbeyahood.

  • @CertifiedStoic
    @CertifiedStoic 9 หลายเดือนก่อน +8

    Tulionunua Album day one tu ilivyotoka tunakosa cha ku-comment maana tulishachambua wimbo mpaka tukauchambua tena. Big Up Vina 🙌

  • @JosephRobert-uf5dr
    @JosephRobert-uf5dr 9 หลายเดือนก่อน +3

    Dizasta aseee sema media za bongo chai sana hawasikiagi hivi vyuma kutoka kwa mwana kuvichaka...

    • @terminal_tz
      @terminal_tz 9 หลายเดือนก่อน

      Sisi hatutaki media za Bongo....tununue Albam Kwa Dizasta ...Vina

  • @emmanueljames9215
    @emmanueljames9215 9 หลายเดือนก่อน +5

    👊 vina kisha somo, umesomeka vina uwezo wako hauwezi kupimwa kwa tuzo za pombe

  • @Vers456
    @Vers456 9 หลายเดือนก่อน +3

    UNatumia muda gani dizasta ku create golds kaMA hizi 🫡🤗🫢🫢🫢

  • @rama_cholobi
    @rama_cholobi 9 หลายเดือนก่อน +2

    Nakupenda Sana HIP HOP

  • @BockrrineMadizaina
    @BockrrineMadizaina 17 วันที่ผ่านมา +2

    Vina best songs 🎉🎉

  • @DennisUnju
    @DennisUnju 9 หลายเดือนก่อน +5

    Kudadekiiii unajua we Fara

  • @runtown____3587
    @runtown____3587 9 หลายเดือนก่อน +3

    Bro this guy deserves more support nunueni album much love dizasta.

  • @hashimswalehe1550
    @hashimswalehe1550 9 หลายเดือนก่อน +2

    ukijuwa mwenza wako ana anampenda
    utampa nafasi aende upige moyo konde🔞🧠🎤🎤

  • @wilbardlameck8025
    @wilbardlameck8025 9 หลายเดือนก่อน +4

    Aliyeelewa hii ngoma anieleweshe tafadhari

  • @shenamtukufu1224
    @shenamtukufu1224 9 หลายเดือนก่อน +4

    Asante sana homie hujawai tufelisha wana.

  • @dmgaya8856
    @dmgaya8856 9 หลายเดือนก่อน +4

    @Mbuzi 💥💥💥

  • @pcthemaster9096
    @pcthemaster9096 9 หลายเดือนก่อน +3

    Ujawai kosea mzee. Nice

  • @mbegumohammed7398
    @mbegumohammed7398 9 หลายเดือนก่อน +3

    Yani huyu mwamba kashashindikana kabisaaa🙌🙌

  • @patrickmgaza9927
    @patrickmgaza9927 8 หลายเดือนก่อน +7

    hapa ndipo tunapopimwa IQ zetu huyu jamaa kama umezoea kuskiliza singeli huwezi muelewa bonge moja la ngoma

  • @matugarecords
    @matugarecords 9 หลายเดือนก่อน +2

    Kazi kali na ni kazi kubwa sana my brother 🔥🔥🔥🔥🔥

  • @Almarsprince254
    @Almarsprince254 9 หลายเดือนก่อน +3

    Nmedakia juu kwa juu,,,❤❤

  • @DullahXella-xb4cz
    @DullahXella-xb4cz 9 หลายเดือนก่อน +4

    DVN is G.O.T

  • @bashirusalehenandoro3128
    @bashirusalehenandoro3128 9 หลายเดือนก่อน +5

    Upendo nipamoja na kumtendea mwenzako mema,dhana ya upendo ni pana sana ila kwenye upendo jambo kubwa linalotafsir upendo ni uvumilivu, sabab binadamu ni lazima akosee tu so upendo ndio utafanya chuki isiwagawe anapokosea unaempenda au anaekupenda

  • @abelmsaki
    @abelmsaki 9 หลายเดือนก่อน +2

    Kazi nzuri sana mwana fanya kazi moja na bele 9 am sure it will be a banger

  • @boygavana4674
    @boygavana4674 9 หลายเดือนก่อน +3

    VINAAAAAA

  • @yasinimalya4001
    @yasinimalya4001 9 หลายเดือนก่อน +3

    Love from 🇺🇸, albam kali kama tindikali, Maji ya betri 🔥💯

  • @JafetPaul-xy1mt
    @JafetPaul-xy1mt 8 หลายเดือนก่อน +4

    Daaaah ifikie hatua watanzania hususa ni wanasanaa wamziki wa hip hop waungamane kwapamoja ili kuweza kuumudu uzito wahuyu jamaa

  • @chidi_don
    @chidi_don 9 หลายเดือนก่อน +4

    Unyama ni mwingi sana bro unajua sana 🔥💯✈️

  • @allyhabibu1117
    @allyhabibu1117 9 หลายเดือนก่อน +2

    Acha wajisifie nimarapa bora ila wewe ndo mwalim wao✊✊✊

    • @thomaslima921
      @thomaslima921 9 หลายเดือนก่อน +1

      🎉🎉🎉🎉

  • @insectondama798
    @insectondama798 9 หลายเดือนก่อน +3

    This ma'faka is an alien💥💥

  • @LudeofficialXworldwide
    @LudeofficialXworldwide 9 หลายเดือนก่อน +2

    Hii Hot Kabsa🔥

  • @langemwepesi
    @langemwepesi 9 หลายเดือนก่อน +6

    Kama vile nazama namuona mwamba kadondosha sijui niseme nizare la professa😂❤

  • @elizajafaphary6559
    @elizajafaphary6559 9 หลายเดือนก่อน +3

    Umetisha mkali wa vina 🔥🔥🔥

  • @josephmasenga7718
    @josephmasenga7718 9 หลายเดือนก่อน +2

    Nipo kwenye top 2 and iam not second ile ngoma uliua sana

  • @cauyadibo9653
    @cauyadibo9653 9 หลายเดือนก่อน +2

    Dizasta mungu azidi kukuweka uachie vigongo we ndo msanii wa hip-hop Wang wa milele

  • @hasanibakari6924
    @hasanibakari6924 9 หลายเดือนก่อน +4

    Serikali hainitambui na ushairi Wangu shule 😂👏👏👏🙌

  • @gaddibullahtzg5635
    @gaddibullahtzg5635 9 หลายเดือนก่อน +2

    Dizasta vinaaaaa umetisha sana nasubiri uchambuzi but you deserve great Honor in Hip-hop Industry

  • @nickbway2052
    @nickbway2052 9 หลายเดือนก่อน +2

    Mbn kama bado haija isha mkuuu🎉

  • @MichaelMtei
    @MichaelMtei 9 หลายเดือนก่อน +3

    Uyu mwamba ni makl wa hip hop

  • @Scott_lit
    @Scott_lit 9 หลายเดือนก่อน +5

    Dizasta vina ni Extraordinary 😂💥💥

  • @jrluhombo
    @jrluhombo 9 หลายเดือนก่อน +3

    Mwisho wa siku mbuzi akaliwa nyama😂

  • @talebanistudio4513
    @talebanistudio4513 9 หลายเดือนก่อน +1

    Oya wanangu wa mziki mzuri kama huu tusiishie ku like na kusifia tununuue ngoma na tisapoti mziki mzuri ili mwana aendelee kutudondoshe ngoma Kali kama hizi Kuna vitu vingi vya kuimba ila wasanii wa bongo banaa mapezi mapenzi wana boa sana dizasta tuna kuaminia wapige msasa wasani wa mapenzi kila siku❤

  • @MalickMazikublood-gq2fs
    @MalickMazikublood-gq2fs 9 หลายเดือนก่อน +3

    Hivi dizasta unavyo andika wimbo kichwa kinakua kinauma au kuna machine unatumiga kutungia nyimbo zako, mm nahis sio kichwa cham2 kinacho andikaga

  • @mukrimkhamis678
    @mukrimkhamis678 8 หลายเดือนก่อน +6

    Uyu mwamba kma akili yako ya kawaida huwezi kumuelewa kbsa###@dizasta🔥🔥🔥

  • @JosephRobert-uf5dr
    @JosephRobert-uf5dr 9 หลายเดือนก่อน +1

    This man is not a human asee dizasta ni monster

  • @MILTONFASHA-kf5pm
    @MILTONFASHA-kf5pm 9 หลายเดือนก่อน +2

    Broo uko vizuri up stair Mimi shabiki yako iam above 50 big up keep it up

  • @stapinuswilliam
    @stapinuswilliam 9 หลายเดือนก่อน +4

    Japo hali yake ya uchumi ilikuwa duni liuza matunda mboga chache na kuni

  • @emmanuelpius6387
    @emmanuelpius6387 9 หลายเดือนก่อน +2

    Nasubiria uchambuzi wake,

  • @SAMAMBIRE
    @SAMAMBIRE 9 หลายเดือนก่อน +10

    Mnasifia sana tungo za vina ila mnajifanya kama hamuoni namba za kutuma iyo miamala mazee afu kesho na kesho kutwa vina aka pause music mtasema vina kapotea

  • @tistarbilly
    @tistarbilly 9 หลายเดือนก่อน +4

    Uyu Dizaster vina anapaswa kuwa msanii wa juu sana

  • @ammyskills5588
    @ammyskills5588 9 หลายเดือนก่อน +3

    Huyu jamaa ni noma 🔥

  • @ammyskills5588
    @ammyskills5588 9 หลายเดือนก่อน +3

    Sema kuna sehemu Dizasta vina umeandika mchugaji badala ya mchungaji (Sehemu ya mwisho mchugaji,msiba wa mbuzi badala ya sehemu ya mwisho mchungaji,msiba wa mbuzi)👍

  • @facarapper5388
    @facarapper5388 9 หลายเดือนก่อน +3

    Washikaji walingoja niwevshujaa ndo niwe mwana😮😮😮

  • @josephatthadeo6119
    @josephatthadeo6119 8 หลายเดือนก่อน +5

    Stamina Dizasta Nacha toxic Roma Nay killer nawakubar kchz

  • @blasiohaule6767
    @blasiohaule6767 9 หลายเดือนก่อน +1

    Mchungaji asitufanyue ivo bs dah salute

  • @LatifaAnuary
    @LatifaAnuary 9 หลายเดือนก่อน +2

    Jamaa kabalikiwa kipaji chakweli ❤

  • @shaddyqualityfurniture3595
    @shaddyqualityfurniture3595 9 หลายเดือนก่อน +4

    Goat 🐐

  • @AmanHaonga-c7u
    @AmanHaonga-c7u 5 หลายเดือนก่อน +6

    Oooh no Dizasta... Mbeya we feel high..reee to have you wish u well 🔥 fire man straight from the cold hooray green town.

  • @antoniomwangi8347
    @antoniomwangi8347 9 หลายเดือนก่อน +2

    What the hell bro🤯🤯. Mad Genius Vina. Big up and salute from🇰🇪

  • @StephanoMbila-ec9lh
    @StephanoMbila-ec9lh 9 หลายเดือนก่อน +2

    Kk umetisha

  • @AhmedYasseen-eg2kz
    @AhmedYasseen-eg2kz 9 หลายเดือนก่อน +1

    Black maradonaa.....
    Vinaaaa🙌🏾🙌🏾🙌🏾

  • @soudyruge-fi9xv
    @soudyruge-fi9xv 9 หลายเดือนก่อน +4

    Huyu mwamba nilichelewa kumjua ila nilivomjua nikamfanya Best RAPPER wa muda wote haiwezi kupita siku bila kusikiliza ngoma zake kama 5, nikianza na TRIBULATION, ACHIA JALA, WACHEZAJI WA TIMU, NO ONE IS SAFE, (zote) na HATIA (Zote)

  • @peter_masawe
    @peter_masawe 9 หลายเดือนก่อน +2

    We proud of you rasta, endelea kutupa ivi vitu🇹🇿

  • @jjokochamwakyusa3626
    @jjokochamwakyusa3626 9 หลายเดือนก่อน +3

    This kind of vina hatuna tena kwa dunia hii.

  • @wilsonjonas5481
    @wilsonjonas5481 9 หลายเดือนก่อน +1

    Walipita wengi lakn huyu ndo msanii wang Bora wa hip-hop

  • @AdveraPhilipo
    @AdveraPhilipo 9 หลายเดือนก่อน +2

    nikiwa mkubwa niwe kama wewe, sijui unamaanisha Nini huu wimbooo😢😢😢😢😢😢😢

  • @Beastlaude
    @Beastlaude 9 หลายเดือนก่อน +3

    Hivi vina ni dizasta 👀🎉

  • @lucasjonas2987
    @lucasjonas2987 8 หลายเดือนก่อน +6

    Kubababakee umu tu unajua sana mwanangu sema ndo ivo hauishi angani