RAIS DKT.JOHN MAGUFULI AMTEMBELEA MAMA MARIA NYERERE NYUMBANI KWAKE MSASANI

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 11 ก.ย. 2024
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amesema Serikali ya Awamu ya Tano itaendelea kumuenzi Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere kwa kuhakikisha fikra na mipango mizuri aliyoiweka inatekelezwa kwa manufaa ya Watanzania wote.
    Mhe. Rais Magufuli ametoa kauli hiyo tarehe 14 Oktoba, 2018 wakati akizungumza na Mjane wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere nyumbani kwake Msasani Jijini Dar es Salaam alikokwenda kumtembelea muda mfupi baada ya kushiriki Ibada ya Misa Takatifu ya Jumapili iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Petro, Oysterbay.
    Mhe. Rais Magufuli amebainisha kuwa Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere alifanya kazi kubwa ya kujenga misingi imara ya nchi kuwa na amani, umoja na mshikamano na pia kujenga misingi ya uchumi wa kujitegemea kupitia Azimio la Arusha.
    Ametoa wito kwa Watanzania wote hasa vijana kuungana na Serikali katika kuyaenzi yaliyofanywa na Baba wa Taifa, na pia kuliombea Taifa.
    Mjane wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kuendelea kumuenzi Baba wa Taifa na amemhakikishia kuwa yeye na wanamaombi wenzake pamoja na Watanzania wote wanamuombea heri yeye, viongozi wote na Taifa kwa ujumla.
    Aidha, akiwa nyumbani hapo Mhe. Rais Magufuli aliyeongoza na Mkewe Mhe. Mama Janeth Magufuli amekutana na mtoto wa Baba wa Taifa Bw. Makongoro Nyerere na Wajukuu wa Baba wa Taifa.
    Mapema leo asubuhi Mhe. Rais Magufuli ameungana na Waumini wa Kanisa la Mtakatifu Petro, Oysterbay Jijini Dar es Salaam kusali Misa Takatifu ambapo Waumini hao wamemuombea Baba wa Taifa, aliyefariki dunia tarehe 14 Oktoba, 1999.

ความคิดเห็น • 291

  • @fredytarimo9107
    @fredytarimo9107 5 ปีที่แล้ว +262

    Safi sana mjomba.we ndo rais watanzania tumeanza kukuelewa.nchi iko shwari kama unamkubali magu gonga hapa.

  • @Eniola0ne
    @Eniola0ne 4 ปีที่แล้ว +24

    When I saw Madaraka Nyerere at Julius Nyerere International in Dar Es Salaam, I was shock with his simplicity, Not like other African President Sons bragging and strolling in land cruiser. He was just Walking like every Tanzania. I walk past before, I realize that, This Nyerere Son. I wanted take Picture with him, but he already went far. He was very wonderful guy, with his humility

  • @70SIXER7
    @70SIXER7 5 ปีที่แล้ว +53

    Mungu Amlinde Kaka Yetu Magufuli Pamoja na Very Humble!...First Lady Mama Janet!

  • @mumbisdesigns
    @mumbisdesigns 3 ปีที่แล้ว +45

    I'm watching all of Dr. Magufuli's videos while he was alive and loving him and his pure, kind heart even more. I wish I could have met him. Such loss and pain! Poleni sana ndugu zetu waTanzania, mie mwenzenu hapa USA 😢😢😢😭😭😭🙏.

    • @happymariki824
      @happymariki824 3 ปีที่แล้ว

      Sana kaka tumepoteza jaman

    • @juliansjuicebarmalindi1156
      @juliansjuicebarmalindi1156 2 ปีที่แล้ว

      Iam a Kenyan too watching all of his videos since he was alive may God rest his soul in eternal peace

    • @salummfaume4767
      @salummfaume4767 2 ปีที่แล้ว

      @@happymariki824 lp

  • @mumyhendry2919
    @mumyhendry2919 3 ปีที่แล้ว +38

    Baba leo wewe ndio tunakuzungumzia hvyo kweli😭😭😭
    Namuomba Mungu akupe pumziko la Milele Baba🙏🙏🙏

    • @nyotawauniquem7462
      @nyotawauniquem7462 3 ปีที่แล้ว +4

      Mpaka machozi yamentoka 😢😢😢

    • @mumyhendry2919
      @mumyhendry2919 3 ปีที่แล้ว +3

      @@nyotawauniquem7462 pole sana mpndwa,ndio maisha haya kesho hatujui tutaamkia wap

    • @karanichris2007
      @karanichris2007 2 ปีที่แล้ว +1

      Imagine 😭😭😭

  • @rezegerezege691
    @rezegerezege691 3 ปีที่แล้ว +25

    😭😭😭😭😭 R.I.P BABA YANGU NAWE TUTAANZA KUKUOMBEA 17/3/2021 TUTAKUENZI HAKIKA.

  • @Eniola0ne
    @Eniola0ne 5 ปีที่แล้ว +40

    Tanzanian are Special People, they are kind, humble People
    I am very happy to be associated with this great humble People

    • @sylversserubiri3765
      @sylversserubiri3765 4 ปีที่แล้ว +1

      You're 100%✓

    • @agnesndetaramo7209
      @agnesndetaramo7209 3 ปีที่แล้ว

      🙏🙏🙏

    • @everkabete6645
      @everkabete6645 3 ปีที่แล้ว

      thank you,so can we be friends ?

    • @machoguhameri7757
      @machoguhameri7757 2 ปีที่แล้ว

      Mh:Magufuri kiongozi aliyepatikana bila watu kutegemea,na akatutoka bila watu kutegemea (Alitufaa zaidi kuliko waliotegemewa)

  • @japhetdaud3889
    @japhetdaud3889 5 ปีที่แล้ว +43

    JPM unafaa Mungu na akusaadie pia kwa kazi unayoifanya 👍👏👏💪

    • @prospermauki7304
      @prospermauki7304 4 ปีที่แล้ว

      Huyu magufuli ni mfano wakuigwa na kama ukutangulia baba wa taifa basi angekua yeye. Tunakupenda raisi wetu

  • @nyanchokachacha6975
    @nyanchokachacha6975 5 ปีที่แล้ว +33

    Hongera sana RAIS wetu, Mama yetu Janeth, na Bibi yetu Mama NYERERE Mungu awabariki sana na Maisha Marefu.

  • @DottRoBroc
    @DottRoBroc 3 ปีที่แล้ว +7

    I am an italian man. I studied Magufuli, a politician I discovered and appreciated for his complaint against the effectiveness of tampons. He was a great and courageous president, an honest man who had reduced his salary (from $ 15,000 to $ 4,000) defended the interests of the people. I also appreciated his position on covid and against dangerous vaccines. In my opinion they killed him even though he officially died of heart problems. Magufuli will forever remain a political example of integrity for all. I agree about Magulification of Africa!

  • @nyanchokachacha6975
    @nyanchokachacha6975 5 ปีที่แล้ว +21

    Big up my president I am very happy to see you struggling to bring up Tanzania with industrial Economy.

  • @mansarayify
    @mansarayify 3 ปีที่แล้ว +9

    This man was really humble, I I'm loving him more in his grave than ever even than when he was alive as more evidences of his panafrican spirits are coming out. RIP my hero.

  • @abuunomaz2323
    @abuunomaz2323 5 ปีที่แล้ว +31

    Rais wangu uko vzr....Mungu ibariki Tanzania Mungu m'bariki Magufuli

    • @peacelove1572
      @peacelove1572 4 ปีที่แล้ว +1

      Amen

    • @aime2937
      @aime2937 3 ปีที่แล้ว

      mungu pokeya mtotoyako rais njoni pombemangufuri tunamuririya Africa yote

  • @mansarayify
    @mansarayify 3 ปีที่แล้ว +13

    I'm not from Tanzania nor do I speak swahili but i love the humbleness and the peaceful nature of the Tanzanians.

  • @hasnathamza8438
    @hasnathamza8438 3 ปีที่แล้ว +16

    Hatimae umemfata baba wa taifa pia kakumzike kwa amn bb yetu maguful tutendelea kukuombea kipenz cha watanzania wotee😭😭😭

  • @saidbarawa9096
    @saidbarawa9096 5 ปีที่แล้ว +18

    Jpm umejaza nafasi ya baba wa Taifa Nyerere vizuri sana kushinda waliokutangulia,heko jpm, heko tena kwa uongozi wako bora,Mimi ni mkenya Lakini naenzi utawala wa Nyerere na utawala wako,mungu akubariki

    • @albertulikaye5951
      @albertulikaye5951 4 ปีที่แล้ว

      Mtu akimsema vibaya Raise wetu mpendwa Dr. Magufuli akili yake haiko vizuri, anatakiwa kuombewa. Raise anayemtanguliza Mungu katika Kila Jambo!

    • @asantekwahuuwimbozubeda873
      @asantekwahuuwimbozubeda873 4 ปีที่แล้ว +1

      Asante baba magufuli kwa wema wako tunaouwona wa kumkumbuka mama maria mke wa baba wa taifa letu la tanzania ubarikiwe sana rais wetu mungu akupe maisha marefu yenye kheri na anae kutakia mabaya mungu amuwaibishe

  • @happinessjoseph3146
    @happinessjoseph3146 5 ปีที่แล้ว +26

    Magufuli Mungu akupe maisha marefu baba napenda busara zako

  • @JoyceAudax
    @JoyceAudax 5 หลายเดือนก่อน

    Asante Sana baba yetu unafa kuigwa kwa kazi yako nzuri unayoifanya mungu akulinde na kukuongoza kwa kila ulifanyalo katika maixha yako yote.Amina tutaixhi Kama alivyotuelekeza 🙏

  • @samuelmusungu1056
    @samuelmusungu1056 2 ปีที่แล้ว +2

    Very humble President,
    I wish I was a Tanzanian...... very calm n with pure heart.
    RIP Rais

  • @undulemwakibabala8119
    @undulemwakibabala8119 3 ปีที่แล้ว +2

    Asante Mwenyezi Mungu kwa zawadi ya Rais Magufuri kwa kuzaliwa Tanzania yawezekana angezaliwa Nchi nyingine lakini ulipenda atokee Tanzania, Nina Imani huko uliko umeshafika kwa Mkombozi wetu YESU KRISTO amekupeleka kwa Muumba wetu 🙏🏼🙏🏼🙏🏼🙏🏼

  • @wilondjanyengawilliam4893
    @wilondjanyengawilliam4893 2 ปีที่แล้ว +2

    je préfère avoir cette gentillesse , cette humilité 🙏🙏🙏

  • @mbabaziscovia4832
    @mbabaziscovia4832 4 ปีที่แล้ว +11

    Tanzania's ur so lucky n blessed to be led by a leader who's full of love, humanity n with a mind of peace. Come test museveni, hmmm Uganda is in hell. N thx to Nyerere the work he did on liberating Tz

    • @sylversserubiri3765
      @sylversserubiri3765 4 ปีที่แล้ว +1

      Thanks for your compliment. We need people like us who stand by the truth . God bless you 🙏.

  • @sankungyork6665
    @sankungyork6665 ปีที่แล้ว +1

    I never see a such leader like him in my life a very humble man to earth and he respect everyone

  • @lashansoky1437
    @lashansoky1437 2 ปีที่แล้ว +3

    The humble and kind people don't last long 😭😭😭,, Tanzanians are so simple in the eyes of the Lord .
    Ewe Mungu nipe hii roho katika nchi taifa la Kenya.

  • @uwamaliyadidacienne6052
    @uwamaliyadidacienne6052 4 ปีที่แล้ว +1

    Nashukulu sana kwa Rais wa Tanzania na unyenyekevu wake Mungu amubaliki,mimi siyo mtanzania lakini napenda Watanzania na Rais wao sana!Mbalikiwe!

    • @missykalele5520
      @missykalele5520 2 ปีที่แล้ว

      Our president is no moree😭😭

  • @esaumahundi5076
    @esaumahundi5076 4 ปีที่แล้ว +1

    Mungu akubariki mtumishi wa mungu rais wetu kwa busara zko bwana akuzidishie uheri ukawe na hekima Kama mfalme seleman niwachache wanaofanya hayo tunashukuru baba unaenzi yote aliyotaka mwl tunakushukuru unatengeneza amani ya vizazi vijavyo hutatafuti vya Koko Bari vya Uma sante

  • @kabaranamaganga6646
    @kabaranamaganga6646 5 ปีที่แล้ว +5

    Ubarikiwe Mh Rais kwa kumkumbuka Madame Maria Nyerere

  • @saumusulaiman4742
    @saumusulaiman4742 9 หลายเดือนก่อน +1

    So sad 😢 dady magufuli wetu na ww tutakuenzi milele ameen😢🤲🤲tutakukumbuka sana dady mungu akupumzishe kwa amani😭😭😭😭😭😭

  • @kudranyome319
    @kudranyome319 5 ปีที่แล้ว +3

    Asante sana mheshimiwa kwa busara zako mungu akuongezee miaka mingi

  • @binurusm8886
    @binurusm8886 5 ปีที่แล้ว +45

    UnapoComent humu usiongee tu kwa chuki zako, Ni Lini Raisi Magufuli alikataa mfumo wa Vyama vingi, tuwe waungwana Na Uzalendo tuwe nao, huyu Baba anaweza Na Mungu atamlinda tu, acheni chuki binafsi.

    • @priscarchiragi5826
      @priscarchiragi5826 5 ปีที่แล้ว

      Binuru Sm hakuna anae mchukia ndugu yangu na pia ujuwe kuwa hata huyu anamapungufu yake na mema yake ila nilazima tuyaseme aache kuuwa wanyinge aache kuteka watu aache kukandamiza wanyonge mi ananikera tu hapo kubukeni hata shetani nae anajifanya mwema ila sio mwema ukicheza nae atakupeleka pa baya

    • @dinawankaba8205
      @dinawankaba8205 4 ปีที่แล้ว

      Binuru Sm mungu akubarika JP

  • @mahamoudabas8555
    @mahamoudabas8555 5 ปีที่แล้ว +1

    Pole mama Maria, badala ya baba wa Taifa Nyerere, waliofatia walikua ni rushwa tupu na tamaa kuiibia nchi na watanzania, lakin kwa bahati nzuri tumempata JPM rais wa ukweli mpiga kazi hata baba wa Taifa huko alipo ana mbariki. Jamani mama Nyerere aangaliwe sana atunzwe huyo mama. RIP baba wa Taifa.

  • @kaobamaabel5561
    @kaobamaabel5561 5 ปีที่แล้ว +16

    Jpm,asanteeeeee

  • @edsonlaurencemwagamasasi9074
    @edsonlaurencemwagamasasi9074 5 ปีที่แล้ว +3

    Asante Sana kwa Kazi nzuri juu ya kumbukizi ya hayati baba wa Taifa

  • @abelsabibi6192
    @abelsabibi6192 5 ปีที่แล้ว +13

    May God bless our nation,our president together with all Tamzanian's

  • @masanjawiza1734
    @masanjawiza1734 5 ปีที่แล้ว +1

    kwa kweli kazi unayoifanya mheshimiwa tunaiona wananchi wako hongera sana na mungu akuongoze vyema katika utendaji wako Wa kazi

    • @shebysheby607
      @shebysheby607 5 ปีที่แล้ว

      Kilambuz atakula kwaurefu wakamba yake ukiwa umetenda mema bs na mungu atakulipa mema kama ulitenda maovu ata tukuombee vp

  • @apolinashirima7424
    @apolinashirima7424 4 ปีที่แล้ว +6

    Mungu ni mwema kila wakati.

  • @Okwash1
    @Okwash1 4 ปีที่แล้ว +2

    Tanzanians are very respectful...I can't imagine Moi's or Kenyatta's grandchildren kneeling down for any future head of state.

    • @thebossman4875
      @thebossman4875 4 ปีที่แล้ว

      And this is why I love Tanzania more than any other African country, the respect the people have for each other and their president is extraordinary

  • @doramarcel1013
    @doramarcel1013 5 ปีที่แล้ว +11

    Huwa unabusara sana J.P.M umefanya jambo jema kbs

  • @timotheondimbo8322
    @timotheondimbo8322 5 ปีที่แล้ว +38

    hata kwenda kumtembelea Mama Maria bado mtu ana dislike, tujitafakari

    • @tegezdomin8363
      @tegezdomin8363 5 ปีที่แล้ว +2

      Hao ni wale waliobinywa wanahisi wapo kuzimu

    • @emmanuelsabuhoro3265
      @emmanuelsabuhoro3265 4 ปีที่แล้ว

      Matatizo ya mkojo man

    • @na0m1fes51
      @na0m1fes51 4 ปีที่แล้ว +1

      Hahahahahahaha yaan we acha tuuu 😆

    • @mohamedyhamis7598
      @mohamedyhamis7598 4 ปีที่แล้ว

      Saw kabisa

    • @allykazimoto8136
      @allykazimoto8136 3 ปีที่แล้ว

      Wengine mavidole makubwa yameenda Dislike lengo ni like

  • @doricatenga4096
    @doricatenga4096 5 ปีที่แล้ว +14

    Mama wa kwanza wa Tanzania mama Maria.Magufuli wewe ni mstaarabu mnooooo.big up.

    • @fezahagumi924
      @fezahagumi924 4 ปีที่แล้ว

      Sinazaidi yakusema mungu akulinde mimi ni Mukongo mani goma

  • @saumuhassan6365
    @saumuhassan6365 3 ปีที่แล้ว +3

    Rest In peace Rais John Pombe Maguful 17/3/2021, DAIMA nawe TUTAKUKUMBUKA, hakika wewe Magufuli ndio Baba wa TAIFA. 😭😭😭🙏

  • @keithochieng8805
    @keithochieng8805 3 ปีที่แล้ว +7

    Rest well Daddy 💕💕

  • @pikipikiusedtanzaniacoltd4596
    @pikipikiusedtanzaniacoltd4596 5 ปีที่แล้ว +10

    Rais superstar jpm. Mpenda watu na rais unaependwa na wanyonge koteeee inch ata km ukichukiwa basi wachache ila ww km nyerere

  • @wisdomuta1039
    @wisdomuta1039 5 ปีที่แล้ว +6

    Mungu akubariki jpm

  • @georgemhalla3515
    @georgemhalla3515 4 ปีที่แล้ว +5

    I have nothing to comment ,but Machozi ya furaha yananitoka!

  • @saudaligomba600
    @saudaligomba600 5 ปีที่แล้ว +10

    Rais uyu uyu anatutosha tumuombeen kwa mungu uyu rais wa watu wote

    • @elizabetymushi2500
      @elizabetymushi2500 4 ปีที่แล้ว

      Mungu peke yake amlinde rais wetu nasi tuzidi kumwombea

  • @princesarykhan4761
    @princesarykhan4761 4 ปีที่แล้ว +1

    Mungu akuongoze na akubariki katika kulijenga Taifa letu Ameen

  • @saimonmanyerezi7169
    @saimonmanyerezi7169 4 ปีที่แล้ว

    Napenda the way ulivyomnyenyekev kwa wananchi wa Tanzania na pia mjeuri kwa watu wanaoenda ndivyo sivyo ,big up sana mh.

  • @gladyssembojas5308
    @gladyssembojas5308 5 ปีที่แล้ว +12

    Yeah first Lady original

  • @veronicadaniel1122
    @veronicadaniel1122 4 ปีที่แล้ว +3

    Nimependa Nimelia Kwa furaha kumuona bibi maria ana furaha mwenyezi mungu tulindie bibietu WA Taifa 🙏🙏🙏🙏

  • @gracejohn886
    @gracejohn886 4 ปีที่แล้ว +2

    Asante Rais wetu kwa kwenda kumtembelea Bibi yetu amejisikia vizuri

  • @mugishaherve6854
    @mugishaherve6854 5 ปีที่แล้ว +4

    Good president for Tanzania

  • @neemapatrick8293
    @neemapatrick8293 4 ปีที่แล้ว +2

    Huyu ndie raisi anajuwa kuongea kwa unyeyekevu sana na anaofu ya mungu sana mungu akufikishe bali baba

  • @cassiusniyimpagaritse5347
    @cassiusniyimpagaritse5347 4 ปีที่แล้ว +4

    Raisi Jpm nakosa cakusema ,so mungu akubariki sana

  • @anifaally1179
    @anifaally1179 5 ปีที่แล้ว +2

    Mungu azidi kukupa afya njema nakupenda sana rais wetu

  • @eliuskalangaeliuskalanga104
    @eliuskalangaeliuskalanga104 10 หลายเดือนก่อน

    Duuuu i love you magufuli jembe wa watanzani nilikuwa na mengi sana ya kusema lakini nitayazuia kwa sababu sina mwingine wa kumwambia lakini nitakuombea kwa mungu baba akulalishe mahali salama ❤❤❤ nakupenda sana sana sana sana tena sio kidogo mungu alinde na familia yako yote kwa ujumla milele na milele amen ❤❤❤

  • @user-mn7ic6wt6j
    @user-mn7ic6wt6j 9 หลายเดือนก่อน

    Ubarikiwe sanaaaaaa na magufuli ubarikiwe kwa kuwakumbuka wajane hawa

  • @MariamMandi-io5sq
    @MariamMandi-io5sq 5 หลายเดือนก่อน

    Mungu akubariki baba yetu Magufuli popote ulipo.

  • @user-ik6jo6zy2v
    @user-ik6jo6zy2v 6 หลายเดือนก่อน

    Roho inaniuma sana nikikumbuka❤❤❤

  • @shijaathanas1897
    @shijaathanas1897 3 ปีที่แล้ว +3

    Hakika ulikuwa rais bora tutazidi kkumbuka daima 😭😭

  • @nyangimarwa3448
    @nyangimarwa3448 3 ปีที่แล้ว +1

    Dah 😭😭😭 Kweli kabisa Rais wetu umetuacha 😭😭

  • @muchunofrank1326
    @muchunofrank1326 5 ปีที่แล้ว +7

    Vizuri sana mheshimiwa

  • @korongoibrahim3524
    @korongoibrahim3524 4 ปีที่แล้ว

    Dk jpm verr good baba yangu Nirahis wa mfano umeletwa na mungu Asante tunakuombea babayetu

  • @priscabuzoya3087
    @priscabuzoya3087 8 หลายเดือนก่อน

    Ulale salama mzee, tutaku enzi pia ,milele

  • @mudingogo6573
    @mudingogo6573 5 ปีที่แล้ว +5

    mm hua napenda unyenyekevu wako tu mungu akurinde jemedari wangu

  • @christophercheruiyot5755
    @christophercheruiyot5755 5 ปีที่แล้ว +5

    I like this president oo

  • @marrysaimon4330
    @marrysaimon4330 3 ปีที่แล้ว +1

    R.I.P Rais wetu twakuombea Mungu akupe pumzika la milele

  • @nyanchokachacha6975
    @nyanchokachacha6975 5 ปีที่แล้ว +7

    Ni RAIS WANGU ambae nikifuatilia vizuri anaefata Nyayo za Baba wataifa kwan katika kupitia nyaraka mbalimbali nagundua kumbe hadi Stgiler mwalimu aliwaza kuijenga.

  • @hamiafasta
    @hamiafasta 5 ปีที่แล้ว +2

    you are my President and always you bless me on what you are doing,,keep it up

  • @edmondkataya5723
    @edmondkataya5723 ปีที่แล้ว

    Kila Leo nataka kuona picha za Magufuli, ni rais kwelikweli. Mungu amulaze mahala pema peponi.

  • @SamuelOjiambo-p6w
    @SamuelOjiambo-p6w 10 หลายเดือนก่อน

    Nothing and nothing forever but we shall remember him no where tu see him but too painful for his absence

  • @swalehabdallah502
    @swalehabdallah502 4 ปีที่แล้ว +3

    Kwa kweli hakuna rais kama ww magufuli kwa Africa nzima kwa uongozi bora na mwenye hekima hongera na mola akuhifadhi kwa Shari katika uongozi wako, mm nikutoka Kenya

  • @geofreyruta1723
    @geofreyruta1723 2 ปีที่แล้ว

    Inauma sana hata siamini kama hayupo kweli Dunia tunapita

  • @jacklinmasawe2697
    @jacklinmasawe2697 2 ปีที่แล้ว +1

    Baba yetu umatuacha tutakukumbuka daima milele

  • @bobm4381
    @bobm4381 5 ปีที่แล้ว +4

    Umefanya vizuri Rais

  • @oddahoward4902
    @oddahoward4902 4 ปีที่แล้ว +1

    The best African President.
    May God continue to bless him.

  • @isayakimbe9610
    @isayakimbe9610 4 ปีที่แล้ว +4

    Mama amefanana na nyerere

  • @khalfanmustafa6615
    @khalfanmustafa6615 ปีที่แล้ว

    Mugufuli mungu akulaze mahala pema umetuacha tuna pigwa vibaya

  • @angemaguru780
    @angemaguru780 4 ปีที่แล้ว +2

    Asante magufuri ndiye wewe nyerere wapiri Dinia muzima na Afurika .

  • @samnsadhameyer458
    @samnsadhameyer458 4 ปีที่แล้ว +2

    This is Awesome!
    Wow!!

  • @edwinc9421
    @edwinc9421 6 ปีที่แล้ว +5

    Ubarikiwe , umetuwakilisha wananchi wote

  • @rudakemwafelicien7776
    @rudakemwafelicien7776 5 ปีที่แล้ว +4

    Nawashukuru sana wa Tanzania nyinyi muko mufano wawa frica wote

  • @shabinahashiri8365
    @shabinahashiri8365 3 ปีที่แล้ว +1

    Kila jambo anastahiki mungu

  • @musamagot6013
    @musamagot6013 4 ปีที่แล้ว +1

    Jpm safii sana ktk marais wote Ww tu nakukubali akitoka nyerere ni ww

  • @RepdcObama
    @RepdcObama 9 หลายเดือนก่อน

    Upumuzike kwa Amani baba MAGUFULI

  • @deokessy6288
    @deokessy6288 3 ปีที่แล้ว +2

    Daaaa!!! Duniani mapito

  • @danieljohn2741
    @danieljohn2741 4 ปีที่แล้ว

    Ubarikiwe na Mungu akuinue

  • @lucasalphonce7820
    @lucasalphonce7820 ปีที่แล้ว

    Rais Magufuli akumbukwe milele,pia yatupasa kumuombea rais wetu kipenzi mama Samia Mungu amulinde sana.ame.

  • @ignaspius
    @ignaspius 2 ปีที่แล้ว +1

    😭😭😭😭 masikin😭😭😭😭

  • @jumaibrahim7605
    @jumaibrahim7605 5 ปีที่แล้ว +6

    Mweshimiwa Mimi naitwa juma Ibrahim nipo mwanza naomba msaada wa geleji Mimi ni fundi Makenika we ndio mpenda watu na sisi ni watoto wako toka nimeanza kuona malaisi tz Basi akitoka baba wa taifa unakuja wewe hakuna mwingine

  • @ijamboryimana5687
    @ijamboryimana5687 4 ปีที่แล้ว

    From Rda , love you so much magufuri God bless you

  • @sheysarahnjeno5207
    @sheysarahnjeno5207 ปีที่แล้ว

    Endlea kupumzika BABA WA TAIFA..Pia Endlea kupumzika Hayati JOHN JOSEPH POMBE MAGUFULI,,,

  • @modestarubunda4250
    @modestarubunda4250 4 ปีที่แล้ว +1

    Nqtamani kuongea na huyo mama, najua ana busara za Mwl. Na za uongozi!

  • @mwinyisiwa-vl3gs
    @mwinyisiwa-vl3gs ปีที่แล้ว

    Tutakukumbuka Sana baba mungu akulinde uko ulipo

  • @lucialeonard6734
    @lucialeonard6734 3 ปีที่แล้ว

    Jambo zuri sana mh raisi umefanya mungu azidi kukupa heri raisi wetu

  • @julihanjosephyjs6361
    @julihanjosephyjs6361 4 ปีที่แล้ว +1

    Mama Maria azeeki msafi Bibi wangu ndio maisha mazuri lakini msafi , usafiri mzuri,Bibi wengine wanajitupa.

  • @mugetakasenyi821
    @mugetakasenyi821 2 ปีที่แล้ว

    Sasa mbona kina koloma Kama radio

  • @mfubwakilua5380
    @mfubwakilua5380 5 ปีที่แล้ว +2

    Mungu awabariki woote

  • @tinkadavis4757
    @tinkadavis4757 6 วันที่ผ่านมา

    True leader❤❤❤❤

  • @undulemwakibabala8119
    @undulemwakibabala8119 3 ปีที่แล้ว +1

    Hiyo ndo ilikuwa Ibada njema kuwaona wajane