WAFAMASIA JUMUIYA YA MADOLA WAJA NA MBINU HII KUMALIZA TATIZO LA USUGU WA VIMELEA NCHINI

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 18 ก.ย. 2024
  • Habel Chidawa- Dodoma
    TATIZO la usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa huenda ukapata ufumbuzi baada ya Wafamasia kutoka Jumuiya ya Madola kuanza kusambaza mafunzo ya kukabiliana na tatizo hilo.
    Mafunzo hayo yanalenga kuwafundisha wafamasia mahospitalini kuwa na ujuzi wa kutengenza vitakasa mikono kupitia Jumuiya ya Madola ya wafamasia, kwa kushirikiana na Tropical Health and Education Trust (THET).
    Akizungumza jana katika mafunzo hayo, mratibu wa mradi wa CwPAMS 2.0, Benard Makala alisema wanaendesha mafunzo ya kuzuia na kudhibiti maambukizi (IPC) kama sehemu ya kupambana na vimelea sugu vya magonjwa.
    Makala ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma alisema mafunzo hayo yalianza mwaka jana katika Hospitali mbalimbali za Mikoa ya Dodoma, Katavi, Kilimanjaro na Mbeya ambako wamepata matokeo mazuri.

ความคิดเห็น •