HATIMAE ILE BANDARI YA 'WATER TAXI BOAT' RAMANI IMETOKA RASMI LEO, SMZ YATILIANA SAINI
ฝัง
- เผยแพร่เมื่อ 8 ม.ค. 2024
- RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali
Mwinyi, amesema serikali ina kila sababu ya kufanya mabadiliko makubwa katika sekta ya baharini ili kuweka mazingira mazuri ya usafiri wa bahari kwa wananchi wa Zanzibar na wageni wanaoingia nchini .
Dk. Mwinyi alieleza hayo mara baada ya kushuhudia hafla ya utiaji saini
mkataba wa ujenzi bandari ya abiria Mpigaduri Maruhubi baina ya wizara
ya Mawasiliano na Uchukuzi chini ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Khadija
CHINI YA na kampuni ya Zanzibar for a Brighter Future ZF Devco Ikulu
Mjini Zanzibar.
Alisema serikali imeamua kujenga bandari ya mpiga duri kutokana na
bandari ya Malindi ya abiria kuzidiwa,kuleta msongamano mkubwa na hata usalama wake kuwa mdogo.
Aidha alisema mradi huo itakuwa mfano mkubwa wa ushirikiano wa sera
ya serikali na sekta binafsi ya PPP katika kufikia malengo ya utekelezaji wa miradi mbalimbali nchini.
Alibainisha kuwa serikali haikuweza kuivunja bandari ya Malindi bali
imeamua kujenga eneo jengine la mpiga duri ambayo itahusisha maeneo
tofauti ikiwemo eneo la abiria la kisasa.
Dk. Mwinyi alibainisha kuwa mradi huo utakapokamilika ni ni fursa kubwa
ya biashara na wameamua kuingia makubaliano ili nchi iweze kufaidika
kiuchumi na kuondosha changamoto ya usafiri kwa wananchi wa Zanzibar
hasa kwa wasafiri wanaotoka kisiwani Pemba na Dar- es salam.
“Abiria waopita hapo ni kati ya 5000 mpaka 12,000 kwa siku hiyo ni fursa
kubwa ya biashara, wenzetu tumezungumza nao na tumeshirikiana na leo
tumeamua kwa pamoja kuingia mashirikiano ili kuweza kufaidika
kibiashara, kiuchumi na pia kutoa huduma bora kwa wananchi wetu,”
alibainisha.
Rais Mwinyi alibainisha kuwa serikali imejipanga kuwa na usafiri wa aina
mbalimbali ikiwemo usafiri wa barabara kwa kuwa na mabasi ya gesi na
umeme ,treni na usafiri wa majini kwa kutumia water tax.
.....................................................................................................
Angalia Video Hii Mwanzo mwisho , Kisha Subscribe ili uendelee Kupata Habari Zote.
Follow Ktv Tz Online
Facebook | KTV TZ ONLINE
INSTAGRAM |@ktv_tz_online
Wasiliana nasi kupitia number
+255 717 619 834
Ktv Tz Online Journalists
cc: Sadia Rashid
cc: Sauti Byego
Camera Department"
Dadi Ali
Omar (OJ)
Nassor Shaibu
Abdallah Juma
Editors:
Juma Maulid
Dadi Ali
Video Zingine:
Angalia hapa - Diamond Platnumz Alivyolisha watoto yatima
- Ali Kiba akiwa Oman
• ALICHOKIFANYA DIAMOND ...
• NI KWELI ALI KIBA AMNU...
Wewe ndo rais wa kweli kura yangu ipo kwako baba usijali inshaallah
Excellent
Hapa Zanzibar tumepata Rais ❤❤❤❤
mashallah,hekko Dkt.Mwinyi Kwa kupig hatua kubw na kukaza mkanda na Buti to our modern znzbr,,,so good strong foundation to znzbr.
Mheshimiwa hata akimaliza Muda wake wa uongozi itakuwa ameifumuwa zanzibar
Nzuri mashallah mmungu akueke doctor mwinyi watu watapata kazi
Mungu akulinde Rais wetu akukinge na maadui bado tunakuhutaji saana kwenye kisiwa chetu yajayo ni neema 💪
Rudi Tanganyica Mwinyi tumrudishe Mama yao ww ni mfano wa Magufuli unapiga kazi sana Hongera
Imekaa sawa tulikukubali kabla hujawa rais
Mh kwakwl unazidi kuiheshimisha Zanzibar
C mlisema mbara arudi kwao Njooni mumchukue Mama enu Turudishieni Mwinyi wetu
Naona kama dkt mwinyi hajatoka ccm
VIZURI SANA
Na zile sain za mpiga duri vp zile chelezo viwqnda vyuo
kilichofanyika leo ni utiaji saini mkataba wa ujenzi bandari ya abiria Mpigaduri Maruhubi,
khaswaaa, kuna mpga duri ya meli za makontena ilitiwa sain toka dk mwinyi alipoingia tu madarakani, kuna ya maruhubi ya kusarifu na kuhifadhi samaki ilitiwa saini tayar. au labda zitaanza zote kwa pamoja.
@@Allybinamourilikua ni feasibility study sio ujenzi
Na ule mradi wa kujenga mji wa malindi umeishia wapi au ndio kila sku kutia saini tu
Ukiskiliza vzur ule mradi wa malindi wala hutauliza maana mbaka ihame bandari ya malindi au hukusikia vzr
@@MohamedAhmada-ie7ke tusubiri tuone ayo yalotiwa sauni leo then njoo tena hapa baada ya miaka 7 unipe mrejesho
@@mohdseif2459 Tukijalwa uhai na uzima In Shaa Allah
Mazonge tu !
Imekaa sawa tulikukubali kabla hujawa rais