Dizasta Vina - Hatia VI

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 9 ก.พ. 2025
  • Official lyric video of Dizasta Vina perfoming Hatia VI, Marking a 3rd release Off the album A father figure
    Stream/download Hatia VI
    Mdundo - mdundo.com/son...
    Boomplay - www.boomplay.c...
    Apple Music - / hatia-vi-single
    Audiomack - audiomack.com/...
    Spotify - open.spotify.c...
    Dizasta Vina on socials
    Instagram - / dizastavina
    Twitter - / dizastavina
    Facebook - / dizastavina07
    Lyrics
    Salamu baba mi mwanao
    Naandika waraka kwa maana hutaki vikao
    Nahitaji majibu nikihisi ni haki yangu
    Najisikia vibaya kusikia unaishi na sina ngao
    Nimeshika kalamu haya maandiko
    Yametoka mahala timamu palipo wito
    Sijatumwa na wenzangu hii ni akili yangu mwenyewe
    Waraka huu ni salamu zangu za mwisho
    Nina akili najua mambo yanapokuwa mrama
    Natambua uhalisia nazitambua njama
    Pengine nitachokisema kitazua laana
    Nitaibeba lawama kwa kujifanya najua sana
    Ndugu zangu wanachosema sisawiri
    Mpaka wanahisi nimeanza kuchezwa na akili
    Hata wakitaka kunitenga sibadili
    Ulinitenga jana siogopi kutengwa mara mbili baba
    Majirani wanatamba kukuongelea
    Wakisema sina baba na kazi ya kukusemea
    Na ukweli ni kwamba ni utata sana kukutetea
    Maana shida ilinibana na baba haukutokea je
    Utachukia nikiegemea penye power
    Au utanipa hatia mikono michafu niende nawa
    Nipo mbele yako kamwe siigizi uwepo kama wewe
    Basi jibu kero zangu twende sawa
    Juzi nilikuhonga maua, Jana nikakuhonga na tena
    Subira gani isiyo na heri shaabash
    Nimechoka kuchomwa na jua
    Jionyeshe leo nimechoka barua
    Nimechoka barua
    Barua zako zinahubiri ushindi
    Kutangaza vita wakati mtutu tu haushiki
    Na cha ajabu maadui ni wa kurithi
    Chanzo ni kitendawili nilichokisoma kwenye hadithi
    Njoo ulee wagonjwa ndo' uongee kuhusu upendo
    Tuvae bendera moja ndio uongee kuhusu uzalendo
    Msamehe aliyekufanya uondoke ndo' uendeelee
    Kuhubiri kutubu kuhifadhi na kusamehe
    Jenga daraja baba mahusiano yanavunjika
    Hamna faraja huoni wanao wamekaza ndita
    Jenga imani tena kwa wote waliogadhibika
    Jenga kama ambavyo uliijenga hii nyumba kwa siku sita
    Haukuja tulipopita kwenye
    Miaka 400 ya utumwa njaa maradhi vita giza nene
    Nipe sababu moja vipi nikujali vipi nikupende
    Sababu moja tu kukusikiliza wewe
    Nyumba uliyotupa ina twiga ina ndovu
    Majirani warembo wenye figa na vitovu
    Vinavutia, kuna dhahabu kadhalika
    Zinatutajirisha ila zinafanya tuwe waovu
    Huu uchafu atatetea wakili gani
    Siri ipi na asili zetu hazilingani
    Japo akili mali sio siri asili ghali
    Tunamwagana damu kugombea rasilimali
    Tunaisha kwa wivu wetu
    Tunasita kwa uvivu wetu
    Tunazikwa na mbinu zetu
    Tunapikwa na kinu chetu
    Tunasita kushika insha
    Tunapitwa na wapita njia
    Umoja unavunjika huku
    Tumeshikwa na simu zetu
    Sina tofauti nna watoto kama wewe
    Napata changamoto kama wewe
    Kama soja kwa ajili yao napambana naposhindwa
    Tunateseka pamoja Kwani sina roho ndogo kama wewe
    Asante kwa ulezi dhanifu
    Asante kwa kuniandikia sheria za kishenzi
    Kwenye pegi nadhifu asante kwa kuniacha stendi
    Nikisubiri mapenzi ya ahadi nakesha nikienzi wasifu
    Asante kwakuwa mbali nami
    Kiasi nina shaka kuwa haujui nina hali gani
    Umeacha barua ndefu ambayo sijui kama yako
    Au ya kufoji na bado inahitaji mkalimani
    Ona Napanga mipango ya kijinga
    Ona naghafirika nafanya uliyopinga
    Ona napinda napika chuki wenzangu
    Wenye nyumba ndinga maana mimi ngano tu inanishinda
    Huko mbali umejitenga nashanga
    Haujui kinachosemwa na jamaa
    Haujui usafi ni ndoto, ndoto iliyotengwa na ridhaa
    Haujui ni ngumu sana kuwa mwema ukiwa na njaa
    Haujui kuhusu adha za dunia
    Haujui kero maana maudhi yalipokupata ukakimbia
    Haujui kuhusu kifo na magonjwa haujui kuhusu
    Insha na maandiko haziwezi tibu hivi vidonda
    Ndugu zangu umewajenga kwa vpaji
    Wapo kadhaa umewapa pesa za mitaji
    Wengine warembo wenye vyeo wenye hadhi
    Sisi tusio na hali tulalamike kunyimwa haki
    Imechafuka taswira inaenda slow focus
    Pengine its all bogus
    Pengine I'm mad
    And I'm talking to my own conscious
    Labda haupo ni hadithi tu
    Na kama ulifikia kifo ufalme umefika mwisho
    Haurudi tena so nawaza
    Lini utakuwa mwisho wa uhanithi huu
    Uzazi sio simple but I still care
    Nina watoto shida zipo and I'm still here
    Matatizo yanapokaba kwenye shingo sikimbii
    Napambana mpaka mwisho like a real man
    Sio kosa langu kutokuwa na uhakika upo
    SikujuI sura maana hauna picha Google
    Nipe ishara kuwa unaishi hata nikituma
    bakshishi niwe ninajua kuwa zinafika huko
    Wenye majoho rangi nyeupe na dhahabu
    Wana barua zako za tafsiri za kiarabu
    Wanasema wanakujua kuliko ninavyokujua
    Nikiwatilia shaka wananiita mwanaharamu
    Je ni kweli uliwapa uwakilishi
    Ni ngumu kuwasadiki hasa ukiwadadisi
    Kama wanaongea uhalisi au wanachonga sera
    Sometimes hawafundishi wananiomba hela
    Thibitisha hizi hifadhi si uwongo
    Uliowaacha wana nishani za,,,,
    read full lyrics - genius.com/Diz...

ความคิดเห็น • 632