Historia Ya Kumbuka : Kuishia La 7 Mpaka Kuwa Mtangazaji Nguli | SALAMA NA DR KUMBUKA PT 1

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 3 ต.ค. 2024
  • #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
    Dr Kumbuka ni influencer mkubwa kwenye masuala ya mahusiano na maelewano inapokuja kwenye suala zima la ushauri na mashauri kwa watu wengi ambao wamekua wakimsikiliza na ambao wanamsikiliza kila siku za wiki anapokua kwenye kipindi cha Uhondo pale EFM. Na yeye kuwa pale hakufika kwa bahati mbaya. Ila pengine alipo anzia kazi yake pale Times FM ndo ilikua kama bahati kufika. Anakumbuka jinsi ambavyo alikua zake tu mtaani wakati mtangazaji wa Times FM wakati huo Bi Dida Shaibu alipokua mtaani akitafuta watu wenye kipaji cha ‘kuchamba’ watu wengine. Anasema wanawake ndo walikua wametawala jukwaa huku wakishusha maneno mengi ya karaha kwa wanaume, na hapo ndo yeye alipoona nafasi ya kupanda jukwaani na kuwawakilisha wanaume wenzie kuhusu ila na karaha ambazo na wao pia wamekua wakizipata kutoka kwa wanawake.
    Huo ndo ulikua mwanzo wa safari yake hii ya kuwa mmoja wa watangazaji hodari wa radio kwa muda huo anapokua hewani, EFM walivutiwa na kipaji chake na wao wakaona bora wamvute kwenye radio yao ili awatumikie wao na kipaji chake. Akiwa Baba wa watoto 5 sasa Dr anazungumzia kashfa na maneno mengi ambayo yamekua yakisemwa juu yake na muonekano wake na uzungumzaji wake. Anasema pia akiwa kama Baba na mtoto wake wa kwanza na wa pili nao wameshaanza kutumia mitandao ya kijamii na kuona comments ambazo watu wanaacha chini ya post zake huwa zinamtia unyonge wakati mwengine, hasa ile ambayo inahusu zaidi jinsia yake, mengine ya kwamba anajichubua huwa hayamsumbui asilani maana hiyo ndo rangi yake!
    Alilelewa zaidi na Mama yake mzazi ambaye katika umri mdogo kabisa Dr ilibidi naye amlee Marehemu Mama yake maana hakukua na mtu mwengine kwenye familia ambaye angeweza kufanya hivyo, kwa mtoto wa kiume kumuogesha, kumvalisha na kumfanyia mengine ya faragha Mama yake mzazi ilikua mtihani, ila kwa sehemu ambayo alikua wakati huo, hakukua na njia nyengine ya kufanya. Alikua akimaliza kumtaarisha Mama yake anamuacha kwa majirani na hapo ndo yeye anapata nafasi ya kwenda shuleni.
    Ni wengi wamepita na kushuhudia mengi wakiwa wanakua na mitihani na majukumu bila ya shaka hutofautiana, kwake yeye anaamini ni Baraka mara dufu kwa yeye kuweza kupata nafasi ya kufanya hayo yote kwa Mama yake kipenzi mpaka Mwenyezi Mungu alipo mchukua.
    Na Baba yake je alikua wapi wakati haya yote yanatokea? Na je alikua Mzee wa aina gani?
    Majibu ya hayo maswali yote Dr Kumbuka anatupatia katika episode hii ilojaa story nyingi za kukutaka utake kusikia zaidi.
    Kama Baba ambaye hakupata nafasi ya kuwa na Mzee wake wakati anakua, Dr Kumbuka anahakikisha watoto wake sasa anawalea mwenyewe na kuwapa asilimia 100 ya uangalizi wake, na hiyo haijalishi kama Mama wa mtoto bado yuko nae au la, kwa yeye kuwa pale ndo kitu ambacho kinamfanya yeye ajiskia vizuri zaidi.
    Yangu matumaini kutakua na mengi ya kujifunza kutoka kwenye episode yetu hii ya SABA ya msimu wetu huu mpya ambao tunahakikisha unapata kuwaskiliza watu wa aina mbalimbali ambao story zao zitakuvusha sehemu flani.
    Love,
    Salama.
    Support us through anchor.fm/yahs...
    SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
    Listen our Podcast on
    Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
    ‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
    GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
    Audiomack Link bit.ly/YahSton...
    ‪TH-cam Link bit.ly/TH-camS...
    Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
    Follow:
    Twitter: / yahstonetown
    Instagram: / yahstonetown
    Facebook: / yahstonetown
    Channel Administered by Slide Digital
    Instagram: slidedigitaltz

ความคิดเห็น • 129