Dizasta Vina - Utaliimba Jina Langu Ft G Nako

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 6 ก.พ. 2025
  • Official Video for Tanzanian Hip Hop Artist, Songwriter, and Record Producer Dizasta Vina, Performing a record 'Utaliimba Jina Langu' Off the Album 'A father Figure'
    Written by Dizasta Vina
    Music by Ringle Beatz, J'cob
    Drums by Double
    Vocals by Dizasta Vina, G Nako, Double
    Mixed and mastered by J'cob & Double
    Download/Stream Utaliimba jina langu now
    TH-cam - • Dizasta Vina - Utaliim...
    Mdundo - mdundo.com/son...
    Apple music - / utaliimba-jina-langu-f...
    Audiomack - audiomack.com/...
    DISCLAIMER: Images used in this work were for educational purposes, no harm ever intended
    Lyrics
    VERSE I
    Sitauona uzuri wa mataa
    Maua na uturi au usafi wa suti nitayoivaa
    Mtajadili kama nilifunzwa chuki na hii njaa
    Au msamaha niliomba baada ya kuivunja mioyo kadhaa
    Mikono yangu haitaishika sayari
    historia nitakuwa nimeimaliza tayari
    Naenda upande wa pili, asili itanipiga kabali
    Nitakuwa nimeimaliza safari
    Maombi hayatakidhi nisimame soja
    Nanyi mtaijua hadithi hii ya upande mmoja
    Pesa na ustaa hautanibeba
    Itaandikwa "mwisho wa kila shujaa ni jeneza"
    Siwezi kimbia udhuru hata nikibadili njia
    Nakuwa huru dhidi ya kufuru za hii dunia
    Mwangaza hautafika himaya yangu
    Je mtafurahi nikifa ama mtaliimba jina langu?
    Siku hii iwakumbushe kuwa kesho mbali
    Iwakumbushe havina maana pesa mjengo mkali
    Vyeo urembo na pesa nyingi
    Ni kiburi cha hii pumzi, pumzi ambayo ni temporary
    Sijui Nitamwachia nani mama yangu
    Ikiwa, nitaacha dini, itikadi ya chama changu
    Cheo changu hakitakuwa na maana tena
    Nitalala gizani japo mtajua nimelala pema
    CHORUS
    Kwakuwa niko mbali na ukweli na mimi ni dhaifu
    na kweli
    Kwakuwa niko mbali na ukweli na mimi ni dhaifu
    na kweli
    Dunia inashindwa kunilinda
    Dunia inashindwa kunilinda
    Dunia inashindwa kunilinda
    Dunia...
    VERSE II
    Nitalala sitahisia karaha zako
    Sitasikia matusi sitasikia msamaha wako
    Sitasikia kicheko au kilio cha unafiki
    Ubongo hautatafsiri mawimbi ya sauti yako
    Nini maana ya chuki yako kwangu ikiwa
    Siwezi amka hayafungukia macho yangu
    Nitakuwa mbali peke yangu futi sita
    Hata kivuli hakiwezi kuwepo kando yangu
    Ufedhuli ni kibari cha hii nguvu
    Ya nyama na mifupa ambayo ni mali ya wadudu
    Ipo siku utaimbiwa pambio na wadau
    Kisha Ndugu watagawana salio na kusahau
    So, nataka nikifa msinidai
    Msilie msherehekee niliyoyafanya nikiwa hai
    I wonder kama mwangaza usipotimba himaya yangu
    Je utafurahi nikifa ama utaliimba jina langu?
    Minara yangu imara itadondoka nayo
    Sauti yangu ya gharama nitaondoka nayo
    Masikini roho yangu mimi
    Itaenda wapi pindi mwili utakapogusa
    Udongo mkavu chini
    Mwangaza hautafika himaya yangu
    Je mtafurahi nikifa, ama mtaliimba jina langu?
    BRIDGE
    Kwakuwa niko mbali na ukweli na mimi ni dhaifu
    na kweli
    Kwakuwa niko mbali na ukweli na mimi...
    CHORUS
    Kwakuwa niko mbali na ukweli na mimi ni dhaifu
    na kweli
    Kwakuwa niko mbali na ukweli na mimi ni dhaifu
    na kweli
    Dunia inashindwa kunilinda
    Dunia inashindwa kunilinda
    Dunia inashindwa kunilinda
    Dunia...
    Kwakuwa niko mbali na ukweli na mimi
    (Dunia inashindwa kunilinda)
    Kwakuwa niko mbali na ukweli na mimi
    (ni dhaifu na kweli)
    Dunia inashindwa kunilinda
    Dunia inashindwa kunilinda
    Dunia inashindwa kunilinda
    Dunia...

ความคิดเห็น • 897

  • @soudyruge-fi9xv
    @soudyruge-fi9xv หลายเดือนก่อน +325

    Dah!! Kuna muda inabidi sisi tuliofanikiwa kuzaliwa kizazi kimoja na THE GREAT THINKER DIZASTA VINA tujivunie na tujipige kifuani hiki kichwa sijui kama kitakuja kupatikana tena Tanzania miaka ya hivi karibuni 🔥🔥🔥

    • @Empirecreator-k5j
      @Empirecreator-k5j 29 วันที่ผ่านมา +10

      TRUE

    • @josephmagele5547
      @josephmagele5547 29 วันที่ผ่านมา +9

      Ngumu sana kupatikana kama huyu kama ngwea tu akuna aliye patikana kama huyo jamaa huyu ndo akuna atakaye jaribu ata kuwa hivi

    • @decoderhealthusa
      @decoderhealthusa 29 วันที่ผ่านมา +8

      Nimenunua album ilipotoka tu, ila leo nilivyoiona hii lyrics video naiona ni kama mpya na idea yangu imeenda mbali zaidi.

    • @MussaDilalile
      @MussaDilalile 29 วันที่ผ่านมา +3

      True

    • @MussaDilalile
      @MussaDilalile 29 วันที่ผ่านมา +3

      True

  • @danieldavid4733
    @danieldavid4733 8 ชั่วโมงที่ผ่านมา +1

    Dah Nina bahati sana kuipenda HIP HOP huu mziki ni ibada jamani

  • @Togahighlights
    @Togahighlights 29 วันที่ผ่านมา +154

    Ambao tuliinunua hiii nyimbo toka mwaka jana na tumeishika tujuane kwa like ❤

    • @AgustinoKinyaga
      @AgustinoKinyaga 28 วันที่ผ่านมา

      Nanunuaje nyimbo zake Master dizasta

    • @RamadhanSeif-b7l
      @RamadhanSeif-b7l 28 วันที่ผ่านมา

      toka mwaka jana mpaka mwaka huu kuna wapo walionunua hii nyimbo na saivi wapo pekeyao ndani futi sita 💔💔JE TUNATAKMBA MAJINA YAO

    • @Magna_Black
      @Magna_Black 28 วันที่ผ่านมา +1

      Nasubiria Mwanasesere

  • @mdudamotorc9600
    @mdudamotorc9600 29 วันที่ผ่านมา +61

    Nmesoma comment zote,,kama sisi ni suppoters wa mziki mzuri toka kwa dizasta vinaa, why ngoma ipo nafasi ya 25 on trending 🕊️🕊️🕊️🕊️🕊️ok twende p1 tupeleke maua yke ngoma ifke No 1 trending

    • @Jrockscyber
      @Jrockscyber 15 วันที่ผ่านมา +1

      NAKUBALI BOY WANGU

  • @yusuphisack285
    @yusuphisack285 หลายเดือนก่อน +70

    Tulionunua ulbum tuliyapat madini haya tangu mwaka mmoja uliopita. Support kwa HIP HOP .. nunueni ulbum bado kuna vitu mnachelewa kuvipata

    • @WilliamKaseza-m5d
      @WilliamKaseza-m5d หลายเดือนก่อน +4

      Kweli kabisa albamu ndo habari ya mjini

    • @johnizoboy
      @johnizoboy 29 วันที่ผ่านมา +6

      @@yusuphisack285 Sure..ile ni zaidi ya Album Kaka

    • @mugadimon3563
      @mugadimon3563 29 วันที่ผ่านมา +1

      Naamu kule kuna madini ya kutosha

    • @omarymilulu
      @omarymilulu 29 วันที่ผ่านมา

      Maisha ya ukweli salute # ukweli salu T

    • @tzmagaladiah5680
      @tzmagaladiah5680 29 วันที่ผ่านมา

      Ilikuwa ina nikataa sana we umenunua alafu kuna jamaa anakuambia nitumie unatuma namba za dizast

  • @dwightkurtschrute3184
    @dwightkurtschrute3184 22 วันที่ผ่านมา +7

    Kama umetambua zaidi ya 90% ya sura zilizoonyeshwa basi you are most likely from the 90s and earlier.
    Na hii inamaanisha ushakuwa mtu mzima sasa na huu ndio muda sahihi wa kuhakikisha unaacha kumbukumbu nzuri kabla ya muda kukutupa mkono.
    Watambue watu muhimu maishani mwako na hakikisha wanajua kuwa unawapenda na kuwajali.
    Sijawahi kumsikiliza vya kutosha @DizastaVina lakini damn! This song just tore my heart to pieces.
    Binafsi nimepoteza watu wengi muhimu maishani mwangu over the last few years but i guess kuendelea kupambana kuwa the best version of myself na kuwakumbuka waliotangulia ndio njia sahihi.

  • @stephenfelix5158
    @stephenfelix5158 29 วันที่ผ่านมา +37

    R.I.P Philipo Tobias, mdogo wangu, alifariki 22.12.2024,

  • @deetz3181
    @deetz3181 29 วันที่ผ่านมา +44

    IFIKE STAGE VINA APEWE HESHIMA ANAYOSTAHILI. GOAT!

    • @Nickbrown127
      @Nickbrown127 29 วันที่ผ่านมา

      Ulishawahi kununua album yake hata moja?

    • @deetz3181
      @deetz3181 29 วันที่ผ่านมา +1

      @Nickbrown127 FATHER FIGURE

    • @mdasaboi
      @mdasaboi 29 วันที่ผ่านมา

      ...yes huwaa wanaongea tu wakat hata hajawah kuwa na album ya mchizi

    • @ekicrevo6890
      @ekicrevo6890 22 วันที่ผ่านมา

      Tutamtengenezea tunzo mashabiki

  • @nassoromelele7339
    @nassoromelele7339 28 วันที่ผ่านมา +17

    NO. 1 - VINA
    Muda wa kuona Ukubwa wake katika hii tasnia.
    Album Imeshiba sana hii📌

    • @IpEleven-h1e
      @IpEleven-h1e 26 วันที่ผ่านมา

      Kweli kaka, time ifike media za bongo zimpe airtime ya kutosha

  • @felixmselle7579
    @felixmselle7579 29 วันที่ผ่านมา +30

    Maana halisi ya HIP HOP ni hii kupeleka ujumbe kwa njia ya fasihi. Fanani (Dizasta) 💯

  • @sospetermarandu1349
    @sospetermarandu1349 24 วันที่ผ่านมา +2

    1:30 Huyu Mwamba ameandika sana Kwenye Hii Ngoma!
    Vyote tulivyonavyo hapa Duniani ni vyakupita tu. Tuwe Wanyenyekevu sana na haya Maisha.

    • @MaijeNgogomba
      @MaijeNgogomba 23 วันที่ผ่านมา

      Jamaa anaandika sana sio hapa tu

  • @ibni_H2TL6r
    @ibni_H2TL6r 29 วันที่ผ่านมา +42

    I'm here to speak with you 2050s generation today it's 8 Jan 2025 THIS DUDE WAS BADDEST & MUCH CREATOR in our 90s generation PLEASE MUST RESPECT HIM

  • @JamalMgsi
    @JamalMgsi 14 วันที่ผ่านมา +4

    Wadau tunaoziona jitihada za story teller tujitahidi kupush kazi za vina tujaribu kuzindua jamii

  • @ZakaZakazi-c5d
    @ZakaZakazi-c5d 28 วันที่ผ่านมา +3

    Hii ngoma najikuta najililia mwenye

    • @ZakaZakazi-c5d
      @ZakaZakazi-c5d 28 วันที่ผ่านมา

      R i p brother wangu kipenzi tizo ipo siku tutaonana😭😭😭😭

    • @Slechakanyi
      @Slechakanyi 27 วันที่ผ่านมา

      Pole sana

  • @frankkajoba8372
    @frankkajoba8372 20 วันที่ผ่านมา +9

    Sijutii kununua album ya huyu mwamba. The best hip hop kwa Tz kwa sasa.

  • @dakeeog585
    @dakeeog585 29 วันที่ผ่านมา +12

    Daah Dizasta ni mmoja tu sasa hapo watoto wa iringa mmekutana G NAKO kauwasha moto

    • @AmmielNzala-fu4xu
      @AmmielNzala-fu4xu 29 วันที่ผ่านมา

      Watoto w iringa kivipi kaka sijaelewa

    • @frankcharles3980
      @frankcharles3980 29 วันที่ผ่านมา

      ​@@AmmielNzala-fu4xuhata mm cjamuerewa

    • @emanuelsamkinda2893
      @emanuelsamkinda2893 29 วันที่ผ่านมา

      Kwhy G nako n wa iringa 😂😂😂, sorry lkn km nmekuelewa vibaya

    • @ShedrackKiwale
      @ShedrackKiwale 28 วันที่ผ่านมา

      Hii ya moto sana kaka 🔥🔥🔥🔥🔥

    • @mpjozzegalvanize4926
      @mpjozzegalvanize4926 27 วันที่ผ่านมา

      ​@@emanuelsamkinda2893 kiasili sema kazaliwa na kukulia chuga

  • @mollelezekiel4337
    @mollelezekiel4337 28 วันที่ผ่านมา +5

    Sina cha kusema aisee… kuna wasanii….. hakuna msanii kama huyu Tz nzima, swala sio kuimba, swala ni Tungo. “🫡🫡🫡🫡🫡

  • @yosown1778
    @yosown1778 29 วันที่ผ่านมา +13

    G NAKO CHORUS YAKO IPO SO EMOTIONAL ALAFU JINSI VINA ANAVYOFLOW UNAJIFEEL UPO DUNIA NYENGINE SPIRITUAL YOU GUYS ARE MY MENTORS TOO

    • @EmmanuelMvinga
      @EmmanuelMvinga 28 วันที่ผ่านมา +1

      Aisee unakuta UMETULIA ADI UNAOGOPA lakin ndio song 😂

  • @djdarmaga
    @djdarmaga 29 วันที่ผ่านมา +9

    YE, NAS, TRAVIS SCOT, KENDRICK LAMAR, J COLE hawa watu wanauandishi mzuri na wanafikilia sana TZ tujivunie kuwa na DIZASTA VINNA jamani 🎉🎉🎉🎉

    • @C.O.D7467
      @C.O.D7467 27 วันที่ผ่านมา

      Ila sio same flow kama vina wetu vina mkali ila awezi change Kama awo uliowataja

  • @_Sammy_BbOy_Bseven
    @_Sammy_BbOy_Bseven 19 วันที่ผ่านมา +6

    Nyimbo zako zimekuwazikinijenga sana kwamafunzo, hii nayo funzo tosha wakati tupo hai tuishi kwakuandaa mwisho wetu mwema tusiishi kwakujisahau dunia ni mapito na kila nafsi itaonja umauti, Asante sana D.vina kwakutukumbusha ilo ubarikiwe sana ❤
    😢 Dunia inashidwa kunilinda.

  • @godzillahlegacy4889
    @godzillahlegacy4889 26 วันที่ผ่านมา +6

    "Masikini roho yangu mimi, itaenda wapi pindi mwili utakapogusa udongo mkavu chini"💔

  • @charlesmarandu220
    @charlesmarandu220 10 วันที่ผ่านมา +2

    Dizastaa

  • @PhillyAmbilikile
    @PhillyAmbilikile 29 วันที่ผ่านมา +21

    Ni kweli Kila mtu ana rapa wake Bora kulingana na vigezo vyake kwanguuu Mimi dizasta vina ni kinara wao

  • @YunusYahya-gr6ks
    @YunusYahya-gr6ks 22 วันที่ผ่านมา +3

    Dhida ni mojaa tu mwamba anakaziwa sana ilaa poaa tuu one day yes you will be up than them master thinker but now no 1 to 9 best rapper is dizasta only anaweza akaapiga kibao kikali mpaka FID Q Nkamuona SAJNA tu

  • @emilyrenatus9374
    @emilyrenatus9374 24 วันที่ผ่านมา +4

    Ni time taasisi za elimu ya juu kumualika vinna kutoa elimu ya fasihi kwa wanafunzi wa elimu ya juu…. His lyrical will live forever …. Ni muziki wa guidance kwa kutuweka katika kutunza misingi….. whenever I wanna meditate alone I just put dizasta vina songs on backgrounds …. Pure culture ✍🏿

  • @Dannytitoff254
    @Dannytitoff254 29 วันที่ผ่านมา +12

    Ifike muda sasa dizasta vina atoe hata riwaya ili kizazi kichacho kikuje kufaidi vyote viwili yani kitabu na hizi ngoma zake
    MUCH RESPECT

    • @RajabNgome-b3z
      @RajabNgome-b3z 29 วันที่ผ่านมา

      Au maktaba za serikal zihifadh kumbukumbu za kazi za huyu jamaa ili kuja kuwapa madini kizazi kinachokuja

  • @kejomaster6161
    @kejomaster6161 23 วันที่ผ่านมา +6

    Uwezo mkubwa wa kufikiri peni haiwezi kugoma kwenye karatasi, hii nimeikubali sana always salute to "VINA"

  • @collinwalter8965
    @collinwalter8965 29 วันที่ผ่านมา +8

    Inapoweza Kuibua husia FULANI ndani yako ,Hiyo ndiyo sanaa .."THIS IS ART"

  • @MengiMeng-fd7sq
    @MengiMeng-fd7sq 25 วันที่ผ่านมา +10

    tujuane basi wanangu wa ngumu kumeza kama hizi zenye ujumbe mzuri ndani❤❤❤❤❤

  • @PhillyAmbilikile
    @PhillyAmbilikile 29 วันที่ผ่านมา +10

    Rapper Bora halindwi mungu ametupa mchizi kama darasa la kujifunza mengi mda mwingine ni kama dini tuu

  • @abdulshakoursalumsaid7125
    @abdulshakoursalumsaid7125 19 วันที่ผ่านมา +2

    Itaandikwa mwisho wa kila shujaa ni jeneza, nipo hapa tena, nilifaidi sana hii ngoma baada ya kununua album January 9th 2024 pamoja na conf of mad father, mwanasesere na ile last confession, ilikuw hunielez kitu kuhus hiz ngoma.

  • @Isaka05
    @Isaka05 27 วันที่ผ่านมา +12

    (sad😢) nimewakumbuka ndugu zangu......!
    Ukiona comment hii we like ili inirudishe kuisikiliza tena hii ngoma ya mtaalam Dizasta vina

  • @ChrissJoel-t1c
    @ChrissJoel-t1c 29 วันที่ผ่านมา +34

    Video 100%
    Lyrics 100%
    Audio 100%
    Beat 100%
    Idea
    100%
    DIZASTA vina 100%. Moja ya zawadi kubwa kwa kizazi hiki ni kumshuhudia DIZASTA VINA

    • @DavidMohamed-r5q
      @DavidMohamed-r5q 28 วันที่ผ่านมา

      Really interested music

    • @Ashibutz
      @Ashibutz 26 วันที่ผ่านมา

      Real

  • @lukundoGrace
    @lukundoGrace 29 วันที่ผ่านมา +12

    Ila g nako popote kambi🙌

  • @salumukatani03-u8b
    @salumukatani03-u8b 29 วันที่ผ่านมา +11

    Genius Dizasta vina umetukumbusha Jambo la muhimu sana kifo,,, Mwenyezimungu atujaalie mwisho mwema🙏

  • @emanuellawrence7462
    @emanuellawrence7462 27 วันที่ผ่านมา +5

    Tuko nonde apa kilimani tuna choma uchafu kusafisha akili respect tkoea mbeya .... One love fam

  • @rogerslwitiko3915
    @rogerslwitiko3915 25 วันที่ผ่านมา +3

    Underground Hip Hop ndiyo ujumbe halisi wa Jamii ulipo Dizasta Vina+G nako mmewakilisha vyema ile maana halisi ya Msanii kioo cha Jamii

  • @avivtelcomms
    @avivtelcomms 29 วันที่ผ่านมา +6

    13hrs with more than 18k views, big up dizasta...i know the hustle, seeing you making these heights am humbled....shawn midundo apa nina mizigo yako apa kaka

  • @daudisimwinga1324
    @daudisimwinga1324 29 วันที่ผ่านมา +7

    Dizasta has reminded us to know that we are all about to depart this world

  • @legawayz6093
    @legawayz6093 29 วันที่ผ่านมา +14

    UWEZO MKUBWA WA KUFIKIRI 👏
    G nako iyo chorus kauwa aise du!
    Storyteller mmoja tu DIZASTA VINA
    MTALIIMBA JINA LANGU 💪
    Take 👊 vina

    • @AbdallaYahya-bc9zb
      @AbdallaYahya-bc9zb 12 วันที่ผ่านมา

      Hio chorus nlimpaa mwenyewe Wara Wara

  • @awardandrew973
    @awardandrew973 29 วันที่ผ่านมา +3

    Great Work

    • @dizastavina
      @dizastavina  29 วันที่ผ่านมา

      Thank you! Cheers!

  • @Slechakanyi
    @Slechakanyi 29 วันที่ผ่านมา +143

    0.39 R.I.P Sajuki
    0.51 R.I.P Yusuph Manji
    0.53 R.I.P J.K. Nyerere
    1.02 R.I.P Godzillah
    1.11 R.I.P Albert Mangwea
    1.11 R.I.P Geez Mabovu
    1.18 R.I.P Kanumba
    1.23 R.I.P Amina Chifupa
    1.36 R.I.P Agnes Masogange
    1.44 R.I.P Augustino Mrema
    1.45 R.I.P Benjamin Mkapa
    1.52 R.I.P Salutaba (Salu Tee)
    1.57 R.I.P Abeid Karume
    2.03 R.I.P Vivian Tilia (Vivi)
    2.03 R.I.P Saimon Sayi (Complex)
    2.06 R.I.P Langa Kileo
    2.17 R.I.P Loshilaa Motika (Mr Ebbo)
    2.23 R.I.P Samuel Sitta
    2.30 R.I.P Cpwaa
    2.35 R.I.P Amina Ngaluma
    2.43 R.I.P Mandojo
    2.47 R.I.P King Majuto
    3.01 R.I.P Asimwe
    3.09 R.I.P Magufuli
    3.14 R.I.P Lowassa
    3.21 R.I.P Idi Amini Dada Oumee
    3.26 R.I.P Regnald Mengi
    3.42 R.I.P James Dandu
    3.48 R.I.P Fatuma Binti Baraka (Bi Kidude)
    3.56 R.I.P Nasma Khamis Kidogo
    4.00 R.I.P Akwelina
    4.05 R.I.P Banza Stone
    4 16 R.I.P Nisher
    4.39 R.I.P Bi Hindu
    4.43 R.I.P Kingunge Ngombale Mwiru
    4.52 R.I.P Hussein Jumbe
    4.57 R.I.P Ephraim Kibonde
    4.57 R.I.P Gadner G. Habash
    5.02 R.I.P Mohamed Fungafunga (Jengua)
    5.07 R.I.P Yusuph Kaimu (Pembe)
    5.12 R.I.P Dida Shaibu
    5.30 R.I.P Mwalimu Kashasha
    5.36 R.I.P Hamza
    5.41 R.I.P Ruge Mutahaba
    5.46 R.I.P Sharo Milionea
    5.55 R.I.P Malcom Masoud Kipanya

    • @allymbondo111
      @allymbondo111 29 วันที่ผ่านมา +6

      Kuna Aquelina, na nisher

    • @dizastavinafanaccount
      @dizastavinafanaccount 29 วันที่ผ่านมา +7

      Add
      Amina Ngaruma
      Bi Hindu
      Pembe
      C pwaa

    • @Slechakanyi
      @Slechakanyi 29 วันที่ผ่านมา +4

      @@dizastavinafanaccount Cpwaa yupo dakika ya ngapi??

    • @Slechakanyi
      @Slechakanyi 29 วันที่ผ่านมา +1

      @@allymbondo111 Nisher kaonekana dakika ya ngapi

    • @Ashibutz
      @Ashibutz 29 วันที่ผ่านมา +1

      @@dizastavinafanaccount cpwaa

  • @MartinJ.D.Msigwa
    @MartinJ.D.Msigwa 4 วันที่ผ่านมา +3

    Vina stay blessed always, nimeamka na kuomba tunaishi tunaishia 🙏🏾🙏🏾

  • @kingshaat1101
    @kingshaat1101 29 วันที่ผ่านมา +11

    Sasa huu ndio mziki!
    Unasikiliza na akili, moyo, na roho.

  • @Movie_point128
    @Movie_point128 22 วันที่ผ่านมา +1

    Sidhani Kam kuna mtu ana mind Kama ya BOE VINA

  • @friendstobias1551
    @friendstobias1551 29 วันที่ผ่านมา +6

    Utatembea lini Kenya black Maradona tunakukubali sana huku. Consiuos music nearly Godly.

  • @onlinewinner8891
    @onlinewinner8891 28 วันที่ผ่านมา +14

    Utalala gizani, japo watasema umelala pema😢

  • @officer1208
    @officer1208 29 วันที่ผ่านมา +14

    Dizasta Vina ni Dizasta kweli,hili ni toleo la mwisho la viumbe wa aina yake.

  • @Ashibutz
    @Ashibutz 26 วันที่ผ่านมา +6

    Twendeni hii ngoma binafsi natamani itfike ata kwenye 10-9-8 trending lakini dah em tukaze wanangu tupite kila platform kuisapoti

  • @AbdulwahidNassir
    @AbdulwahidNassir 25 วันที่ผ่านมา +2

    Muda ndio huu wakuonyesha upendo kwa dizasta vina inakadiria vichwa miamoja kuja na hii idea @Dizasta ni highthinker

  • @paulonjozi1638
    @paulonjozi1638 29 วันที่ผ่านมา +7

    dizasta vina kaondoka nahisia zawengisana kupitia hii❣️🇹🇿🇹🇿🇹🇿

  • @denishaule6314
    @denishaule6314 29 วันที่ผ่านมา +14

    Na comment ili dunia ikinimeza wajue hii ngoma kuna marehemu ali comment…..fire this song is

  • @SteveTegemea-fj6de
    @SteveTegemea-fj6de 21 วันที่ผ่านมา +3

    Dizasta Huwa Ana fikra Chanya Sana.....

  • @johnizoboy
    @johnizoboy หลายเดือนก่อน +26

    This Guy is truly a Genius. Huu uwasilishaji uliojaa Vina lukuki na Moangilio wa Dhima ya kuliimba jina langu ni wa kipekee sana...Dizasta Vina ni kama mtaala tu kwa Sasa kwenye hichi kizazi cha Young rappers...Beat kali sanaa, Mixing🔥🔥🔥🔥...Animations zimetulia sana...Chorus kali sanaaa...Hip hop at its finest level and Dizasta is the Man of the Moment🔥🔥🔥

    • @kingshaat1101
      @kingshaat1101 29 วันที่ผ่านมา +1

      Man this is golden!

  • @MabrouckMussa
    @MabrouckMussa 29 วันที่ผ่านมา +12

    Ukinunuaa albam ya dizasta vina!! Hutojutia pesa yako... Vina katika kilele cha ubora!!

    • @dismacking8421
      @dismacking8421 26 วันที่ผ่านมา

      Album unanunuaje

    • @MabrouckMussa
      @MabrouckMussa 26 วันที่ผ่านมา

      @dismacking8421 ingia kwenye page za dizasta kuna namba ake unatuma hela anakuwekea kwenye email au kama unataka wasap

  • @HamisiMatandaya-xs3lz
    @HamisiMatandaya-xs3lz 29 วันที่ผ่านมา +14

    Ngoma ina fact nyingi, tz kuna wasanii wengi ila dizasta ni mmoja tu...✍️

  • @nuruhegera3760
    @nuruhegera3760 29 วันที่ผ่านมา +15

    Kama umemshuhudia Messi , Umemshuhudia Dizasta Vina , Umemshuhudia na lisu basi Umemshuhudia kila kitu

  • @MoDesigner-z4j
    @MoDesigner-z4j 29 วันที่ผ่านมา +8

    Tujitahidini kushare kila pande ngoma kali hii iwafikie wana hip hop na wasioelewa wajitambue

  • @AmaniLangsoni-k9f
    @AmaniLangsoni-k9f 23 วันที่ผ่านมา +5

    Dizasta Vina ulishasema we so malaika we ni Mungu wa rapu

  • @Manfesto001
    @Manfesto001 21 วันที่ผ่านมา +4

    Nidhaifu na kweli dunia inashindwa kunilinda,,

  • @kicheko4980
    @kicheko4980 24 วันที่ผ่านมา +7

    Ambacho hamjui hapa ni kwamba kila mtu anatokea kwenye mstari mahususi, hajawekwa tu

  • @DavidmyJohnDavidmyJohn
    @DavidmyJohnDavidmyJohn 29 วันที่ผ่านมา +10

    Wimbo wa Dunia vizazi na vizazi respect brother dizavina vs g Nako ❤❤❤❤❤🎉🎉🎉🎉🎉

  • @erastomichael9840
    @erastomichael9840 29 วันที่ผ่านมา +5

    Sauti yangu ya gharama nitaondoka nayo..!
    Huu msitari umenifanya nijisikie vibaya sana😢..!
    Mungu aendelee kukuweka kaka.!🙏

  • @emmanuelchilimo
    @emmanuelchilimo 14 วันที่ผ่านมา +2

    Dizasta Mavina

  • @abhralyrics9816
    @abhralyrics9816 29 วันที่ผ่านมา +13

    Oya huu ni mgodi ambao hauishiw na madin shabik namb 1 hapa wa dizasta vina

  • @alhadymoratal5055
    @alhadymoratal5055 28 วันที่ผ่านมา +6

    Hii ni mara ya 50 narudia ila bado xjaridhika kbisaaa maana inagusa uhalisia 😢😢😢 UPO KWA AJILI YA JAMII YETU 😢😢MUNGU NDIE ANAJUA UKUBWA WAKO🙏🙏

  • @ramadhanimwajuma4701
    @ramadhanimwajuma4701 29 วันที่ผ่านมา +6

    Hubembelezi warembo we sio marioo,

  • @sirilykiwory1911
    @sirilykiwory1911 หลายเดือนก่อน +10

    In loving memory of Malcom Masoud Kipanya 👏🏽

  • @wizboyfriend
    @wizboyfriend 29 วันที่ผ่านมา +6

    Kama Siku ya kwanza ya dunia ipo hata siku ya mwisho ipo pia....Dini ni njia 😢So fatilia dini yako mambo mangapi inakuficha DUNIA HAIWEZI KUWA MILELE DON'T 4GET FAMILIAR

  • @kingsheky2344
    @kingsheky2344 27 วันที่ผ่านมา +5

    If u get to be a dizasta fun ur blessed ...DIZASTA ON TOP

  • @danceworld255
    @danceworld255 24 วันที่ผ่านมา +4

    Dizasta wewe ni rappa namba 1+
    Na ninavyo ona hakuna anae kukaribia maana namba 2, 3 4 na 5 zote zipo wazi, hazija mpata angalau anae kufanania.
    Wao wameanza namba 6,7,8...
    Na wana struggle kuwa kama wewe ila kalamu inawakataa maana mashairi yao sio stong kwenye masikio
    🙌

  • @yustinajoseph5819
    @yustinajoseph5819 19 วันที่ผ่านมา +2

    Great of all time dizasta🇹🇿🇹🇿

  • @Mnyakyuboy
    @Mnyakyuboy 29 วันที่ผ่านมา +10

    Dah brother 😢😢 akika mungu kakujalia uwezo m najivunia saaan kuskiliza ukiimba napata elimu dunia napata hekima napata vingi saaan brother 😢😢 mungu tu akujalie miaka mingi 🎻

  • @JohnRango-s1d
    @JohnRango-s1d 23 วันที่ผ่านมา +3

    Kila nikifikiria fikra zangu najiuliza naweza fikiri kama D,kaka anajua sanaa sayansi yake yake ubungo ipo juu sana ❤

  • @MeshackKabuje
    @MeshackKabuje 26 วันที่ผ่านมา +4

    Aise atakae tazama hii video usilie tumu like dizasta vina kwanza ananitoa chozi la uchungu

  • @rashidsaidy4647
    @rashidsaidy4647 27 วันที่ผ่านมา +7

    huusio wimbo tu Bali ni mawaidha pia 🙏

  • @Ashibutz
    @Ashibutz 25 วันที่ผ่านมา +2

    From yesterday 1️⃣ step forward 13-10-09-

  • @Ashibutz
    @Ashibutz 22 วันที่ผ่านมา +1

    Seven days means one week tupo pale 13 na fresh

  • @TitoKabwe
    @TitoKabwe 25 วันที่ผ่านมา +3

    Dizasta

  • @abdulrazakimpunda8235
    @abdulrazakimpunda8235 29 วันที่ผ่านมา +8

    Disaster NI zaid ya module za chuo 🙌
    Kama unaubongo mdogo WA kufikiria huwez muelewa nilazima atakuacha at the beginning 🙌

  • @yuzzomanboy
    @yuzzomanboy 27 วันที่ผ่านมา +3

    Watoto wadogo hawawezi kuelewa vinywa vinavyotema madini acha wendelee na wasanii wao 🙏🏾🙏🏾

  • @SaidouSarr29
    @SaidouSarr29 28 วันที่ผ่านมา +3

    "Sauti yangu ya gharama nitaondoka nayo" RIP Bi Kidude💔

  • @ImaniMalebeto-l1s
    @ImaniMalebeto-l1s 24 วันที่ผ่านมา +2

    R.S.P Dadaangu kipenz,, Najua Mbele yko nyuma yetu tutaja onana tena.

  • @griezmannmhalaka4338
    @griezmannmhalaka4338 29 วันที่ผ่านมา +9

    Dizasta ni mmoja tu, Rigo beat ni mmoja tu na G nako ni mmoja tu....
    Ngoma imesimama hii. Kuanzia Beat, Vocal, Lyrics, Sound, chorus na verse zote.
    Vyote vipo emotionally kama dhima ya ngoma.
    Sema sauti ya Vina ni ya Gharama kweli kweli

  • @RichadIsaya
    @RichadIsaya 22 วันที่ผ่านมา +4

    Oyaaaaa mwamba anazingatia sana pen tuache unafiki tukae kwenye ukweli

  • @CamweziKarashnekov
    @CamweziKarashnekov 18 วันที่ผ่านมา +3

    Dizasta aeshimike sana, yy ndiye tafsiri ya kio cha jami, ❤ from Burundi 🇧🇮

  • @charleskitoki4648
    @charleskitoki4648 28 วันที่ผ่านมา +8

    Ishi sana mwamba sauti yako hakika yagharama sana.

  • @jacksonyusuph606
    @jacksonyusuph606 26 วันที่ผ่านมา +3

    Hii ngoma noma sana.
    kimaana, Tungo ziko sambamba na picha za marehemu

  • @JumaJingiynho-is9ts
    @JumaJingiynho-is9ts 28 วันที่ผ่านมา +4

    Kila siku lazima niangalie kama jamaa ameachia jiwe hatimaye la kuanzia mwaka hili hapaa❤❤

  • @chechetv9668
    @chechetv9668 24 วันที่ผ่านมา +4

    Ma meeeeen DIZASTA

  • @BonMaro
    @BonMaro 29 วันที่ผ่านมา +8

    Dizasta vina ,bro unajua adibasi maana unatupa darasa kua hiii memory yandgu zetu walio tangulia mbele ya haki wote walikuepo nasi lakni atukuwaikupa sifa napongez zao kwayote waliyo fanya wakiwa hai tuasubiri wapotee kwenye usowaduni ndotuanze kusema ooh alkua bora ooh ailkuIv hapana ,for me thanks u bro unajua kutupa mashabiki zako what we need mmh coz umeimba maisha yakweli kwass tuliopo tujitafakari snaaa 🎶🇹🇿🙏 God bless you and long life to you Eendelea kutupa vitu vzrii

  • @JohnChibanhila-ld6vv
    @JohnChibanhila-ld6vv 24 วันที่ผ่านมา +2

    Safi

  • @taisonbd1844
    @taisonbd1844 29 วันที่ผ่านมา +10

    Toka Congo pokeya zangu respect 🤗

  • @jacksonedward2190
    @jacksonedward2190 29 วันที่ผ่านมา +6

    Mara ya kumi hii narudia kuusikiliza huu wimbo daah✊️🙌

  • @113chamber
    @113chamber 29 วันที่ผ่านมา +9

    Kwenye kazi zake dizasta amekua akitukumbusha tusisahau kuwa hapa Duniani we just passing through ✊

  • @HosianaKulanga
    @HosianaKulanga 29 วันที่ผ่านมา +12

    Npo kwenye taifa ambalo dizasta yupo❤❤❤❤❤❤

  • @HygieneKapachino
    @HygieneKapachino 24 วันที่ผ่านมา +2

    Daaah mwamba alex kashashaaa

  • @LuqmaanAthuman-n2e
    @LuqmaanAthuman-n2e หลายเดือนก่อน +10

    Mungu akuweke mshikaji kuna vitu tunajifunza sana kwako

  • @ibni_H2TL6r
    @ibni_H2TL6r 28 วันที่ผ่านมา +10

    Huyu ni kama darasa ama din tunajifunza na kueleimika kupitia Talent aliyobarikiwa na mungu..... Eeh M/Mungu Ampe umri mrefu Dizasta kwa AJILI YA kuokoa kizazi chetu kupitia kipaji CHAKO kinatukumbusha kuhus hii TEMPORARY AIR TUNASHUKURU BRO WEWE NDIO UKUMBUSHO WA HIKI KIZAZI CHETU WE LOVE YOU❤❤

  • @swaggergboy6478
    @swaggergboy6478 24 วันที่ผ่านมา +3

    Hip hop for my life