Salama Na ROSE MUHANDO SE6 EP53 | NIPE UVUMILIVU PART 2 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460
ฝัง
- เผยแพร่เมื่อ 5 ก.พ. 2023
- #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Katika binadamu ambao walinipa wakati mgumu na kusubiri kwingi kabla ya kuja kukaa kwenye meza yetu ya kigae na kiti chakavu basi mmoja wao ni Rose huyu wa Muhando. Upatikanaji wake ni kama ukitaka kumuona SIMBA mbugani, lazima uamke asubuhi na mapema au uwe na bahati ya mtende kama ambayo sisi tumepata. Ingawa tulisubiri kwa masiku tele na miezi tele katikati ya mwaka huu tuliweza kumpata na kukaa nae chini ili tuweze kuzungumza nae.
Rose ni wa moto sana, kalenda yake imejaa safari tele za nje na ndani ya nchi, anazunguka mara kwa mara kwaajili ya kutoa elimu na burudani kwa watu wengi ambao nao pia wamekua wakimgojea kwa hamu na kwa masiku tele. Kipaji chake cha kipekee ndicho ambacho kimemfanya awe maalum miungoni mwa wasanii wanaofanya muziki wa Injili na uzuri wake mwengine ni kwamba amekua akitoa huduma hiyo kwa miaka mingi bila ya ‘kuchuja’.
Sasa nini hasa siri ya mafanikio hayo?! Ukiachana na panda shuka tele ambazo Rose amepitia toka akiwa na umri wa miaka 6, kukata tamaa ni jambo ambalo halipo kabisa katika mambo ambayo huwa anayawaza. Pengine kujiuliza kwanini na anatokaje kwenye hilo zito alilo nalo linaweza likawa ndo swali, ila kusema kwamba hatoweza au haiwezekani hilo jambo kwenye kitabu chake au kichwani chake huwa halipo kabisa.
Ukiskiliza kwa makini maneno ambayo yanatoka katika mdomo wake utagundua Rose ni mmoja kati ya wanawake jasiri sana ambao wamewahi kutokea katika kiwanda hiki cha Sanaa hapa Tanzania. Ukimuangalia macho yake, mikono yake ambayo imejaa makovu na nna uhakika pia kuna sehemu nyengine kwenye mwili wake pia zimejaa makovu lakini hatukuweza kuona unaweza ukapata tu idea ya makubwa na mazito ambayo amepitia na ambayo yameacha makovu makubwa tu si mwilini mwake tu bali hata kwenye moyo wake. Ananihadithia kwenye episode hii jinsi ambavyo watu walikua wanamuadhibu ki mwili na ki akili ikiwa ni pamoja na kupigwa, kuchomwa moto, kukatwa na kunyang’anywa mali zote ambazo amewahi kutengeneza tokea wakati anaanza muziki ila hayo yote hayajawahi kumkatisha tamaa wala kumrudisha nyuma.
Rose anaamini na aliamini kwamba ana uwezo wa kuvipata vyote ambavyo watu walimdhulumu kwenye kipindi flani kwenye maisha yake, aliamini hakuna ambaye anaweza kumnyang’anya kipaji ambacho Mwenyezi Mungu amempatia na kwa kupitia hiko kipaji na akiwa hai na mzima basi vyote ambavyo aliwahi kuwa navyo na vikapotea basi alikua na uwezo wa kuvirudisha na ni kweli, kuvirudisha ameweza na vimekuja maradufu yake.
Simulizi zake za safari yake toka siku ya kwanza alipokua mdogo nyumbani kwa Baba na Mama yake huko kwao Morogoro wakati anaumwa ni moja ya vitu vya kufikirisha sana ambavyo nimewahi kuvisikia toka tumeanza kukalia kiti chakavu, na yangu matumaini maongezi haya kwa kiasi kikubwa yatakupa ile vibe ambayo huwa naizungumzia kwenye intro ya kipindi chetu hiki.
Tafadhali enjoy.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
TH-cam Link bit.ly/TH-camSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz - บันเทิง
I like the fact that, Salama amesikiliza kila kitu na wakati wa kufunga amefunga kwa sauti ya taratibu kabisa kutokana na uzito wa story Rose aliyoitoa. You both are the best, Pole sana sister Rose
Aisee, this is purely gospel of Jesus Christ
Asante Rose Muhando. Umenifundisha sana na umenitia moyo sana ktk Imani. Hallelujah
Salama , she is talented. Ana uwezo mkubwa sana . Anamsikiliza bila kumwingilia. Keep it Salama
Saaana
Sanaaaaa Yani she is the Best achana na Hawa watangazaji Wengine ujamaliza kuongea ashakudakia
Santé mitume yakuta mm arfa umepa matumaini nimepitia magumu mm nimubeba maono napigwa Vita na wapendwa wenzangu
I really love her courage. She’s a inspiration to many people 🥰
Salama una utulivu wa akili huna mapepe,Sikuwai ku comment toka maguful afariki lkn leo nampa like yangu salama jabir good journalist yupo makin sana ata ktk kuhoji upo juu kama milard ayo!!na unampa nafasi mtu kujieleza na huna mapepe salama una utulivu wa akili.hongera sana sana sana.
Akili ikilishwa kazi itafanya kazi NIMEJIFUNZA KITU🙏🙏🦁
This testimony is a big encouragement to me today. Don’t look behind, move forward 🙏🏾❤️
Nazani kwangu hii ndio best interview kwangu na Rose anaongea vizuri sana ana akili kubwa sana
Saaana🔥🔥🔥
Ni kweli kabisa.
Rose muhando unazo alama za kumuonesha YESUKRISTO skuhyo kwaajili yake ole wetu sisi
Nakupenda sn kipenz changu Rose mhando Mungu azidi kufungua Milango yk ya Baraka milele yote na Afya njema Ameen 🙏😍
Hongera sana. Ni fundisho kubwa sana. Keep it up Rose.
Dada Rose Umenifundisha kuwa strong na kutokata Tamaa, Asante 🙏
Barikiwa Rose. Hakuna usiku usiokuwa na asubuhi.
Leo nmejua kujifunza kupitia Dada Rose...mungu azid kutusimamia....👏
Huwa naaapenda watu ambao wakiumizwa wanarudi kuelezea ili na wengine wapone na sio wanaokaa kimya
Pole sana rose kumbe hizi dini sio nzuri
Blessings Asante Kwa ushuhuda Mungu akakusimamie Rose 🌹
Rose muhando nakupenda sana wewe ndo ulinifanya nisikilize nyimbo za kwaya na wa pili ni gosbert
pole sana mama yangu, unayoyasimulia kwa mwingine angeweza kutokwa na machozi tena yawezakana asingemaliza kusimulia...ila umeonesha ukomavu, sijui ni kitu gani kingine kinaweza kuja kukupa stress kwenye maisha maana uliyoyapitia ni magumu mno, pole sana...story yako naifananisha kidogo na ile ya SAIDA KAROLI, wanawake mnapitia magumu sana Mungu awasaidie
Mtu yeyote Mwenye Roho Mtakatifu kuanguka huwa ni vigumu sana, ila Kuna kunakujikwaa na kuteleza lakini lazima usimame..Muombeni MUNGU Roho Mtakatifu.
😭😭Pole sana dada Rose pia hongera kwa ushujaa wako Mungu azidi kukubariki I LOVE YOU
Dk ya 19:38 KAONGEA fact 🙌🙌🙌 AKILI IKIFOCUS KWENY MAPENZIII INAENDA KWENYE MAPENZI, IKIFOCUS KWENYE KAZI INAFOCUS KWENYE KAZI. I GOT POINT
Nimeinjoy sana...nawapenda wote
Kupitia story hii hakika Mungu amegusa maisha yangu Leo hii. 1/4/2023 Mungu atukuzwe.
Kwa kweli Salama you are the best kwenye haya mambo.
Kuna kipande kimeruka hapo mwanzoni alipoanza kusimulia kilichomtokea mikononi. Nafikiri yalimhuzunisha sana Salama, unaweza kuona kupitia muonekano wake. Salama kauliza hardly maswali manne au matano tu.
Mungu akubariki na akuinue Rose! Amen!🙏🏾
Ushuhuda huu umenijenga , barikiwa
Mnoo
Nimepata funzo through you rose muhando
Salama hongera sana.
Leo umekuwa mpole sana.
May good Lord bless you.
Nashukuru Rose muhando ameonge vizuri ameniongeza kuwa na imani kubwa,na watu wawache kuongea uongo ati rose alikua luminat,
Rose.. We love you so much and the holly might God loves you too... Wish you all the best for your career
Kwakweli Rose wewe uliitwa na Mungu mwenyewe hata watu wafanyeje hawawezi kukuangusha. Ubarikiwe kwa Ushuhuda huu mkubwa.
Toka nilipokuona mara ya kwanza Rose, sijaacha kukupenda hadi sasa
Salama mashaallah leo umependeza sn you look beautiful 😍😍🔥🔥🔥
Kuna kitu gani Kiko Nyuma ya Pazia ..? VIPI Dada Rose usimtaje jina huyo Mtu aliyekutesa watu Turuke naye..?
All in all Pole sana Rose Muhando..Wewe ni Mteule wa Mungu..#WEWE NI MSINDI
Mungu akulinde maman wewenimshindi👍👍👍👍👍👍👍👍👍👍👍👍👍👍👍👍
Rose unaniispya sana nimejifunza kitu ubarikiwe 👏👏
Hakika Rosse ni shujaa nimebarikiwa mno 🙏
Love you Rose Mhando God bless you
Kuna watu ana nishangaa kwanini nipo single mda marefu na nawezaje hivi hee kumbe akili yangu haipo kwenye mapenzi da rose asantee 😢😢😢😢😢
I luv rose alwayssss...kabisaaa
Nathan Meneja wa kwanza wa Rose
Pole sana!Hadithi yako imenihuzunisha sana.
BIG UP SALAMA
Mama rose Salut 💪💪
Love u Rose❤️
Sounds like When Michael Jackson signed up with Sony and saw hell in paradise
Nmetamani kipindi kisiishe salama siku nyingine mwite anatuponya majeraha
Salama yani ukisikiliza stori ya ros unaweza kulia mungu amtie moyi
Rose ni amebarikiwa Kweli🙏
Hongera sana
Rose Muhando🔥💪🏾
Amen 🙏🙏🙏 mungu akusimamie
I love you Salama and Rose 🇨🇦🇨🇦
Dada Rose maisha yako na changamoto zako vimenigusa saaana nimefarijika umenipa fundisho kubwa katika maisha yangu.
Mama rose I love you
Love you Mom 😍😍
Rose anastahili udaktari wa heshima
😳😃
Rose Maisha ni hadidhi, umetufunza mengi uliyopitia na kukata tamaa ni mwiko, ushuhuda wako umenipa ukurasa mpya katika maisha yangu. Mungu aliye juu ya vyote azidi kukupa amani na furaha. Thanks Salama J, your the best interviewer currently in Tz. God bless you all n the team.
Allah nipe mwisho mwema.
Kwa kweli unaeza pitia Leo Kwa utukufu w kesho na mungu atabaki kuwa mungu
HII INTERVIEW DADA SALAMA NA DADA ROSE HAIKUW RAISI IMENIPA NGUVU KUBWA MBARIKIWE SAANA YAHKINGSTONE
Dunia ina mambo pole sana Rose
Salama Mungu akubariki Sana.
Hakuna kukata tamaa. Kushinda ni lazimaaaa
History yako mama ya mateso hunipa huzuni mno hujisikia vibaya mno lakn mungu anajivunia ww
😭😭😭😭
Wa kwanza leo
Pole sana😭😭😭
Ngangana Hilo Ndo Neno Kwa Siku wetu RoseMuhando:(
Anaongea Kwa uchungu.. jamanii..🙂
Ni kweli Dada Rose akili inacholishwa ndicho inachokifanya
MUNGU AKUTANGULIE SANA ROSE MUHANDO
Nami mi napenda sananyimbozako kamazote.🇧🇮🇧🇮🇧🇮🇧🇮🇧🇮👈👈👈
Salama kaishiwa maswali
Dunia👋🏻🙌🏻😭😭😭 sad story ikiwa mbaya ni mwanadam mwenzie Allah nipe mwisho mwema😭😭😭
Binadamu wabaya sana
☀️
Hakika Rose Amebarikiwa
Maana ya mwanadamu iyo, ukifanikiwa anakua adui yako, pole Dada ila yupo Mungu alie juu ya yote
Wooowww Rose muhando Shujaa wa waimbaji injili afrika
Mh mpe pole rozi
😁😁😁wakaenda walikoenda baba wa watoto.
😅😅😅😅
😁😁😁😆😆🤣🤣
Tuongeze kusubcribe kwa mtumishi huyu SHUJAA WA KRISTU. Tumsapoti kwa kusubcribe
Jmni uje ufundishe kwaya fpct nyagulugulu mwanza mahina
Leo salama maswali hayafiki atabkumi😌
Amemruhusu atiririke..ameamua kumtibu Rose 🌹.
Hakutaka kumuingilia amemuacha awe free 😍❤️❤️
ASANTE
Salama Una utulivu sana
Love u Rose
Tuilisheni akili zetu kwenye yenye manufaa🤸
Lete Mgunda
Adult conversation
That’s the most issues the successful people have they forget to build a security while they know there are lions out Side waiting for you
Dhuu hadi nimelia
🙏🏻😴
❤️🇹🇿🇩🇰
Kupidia mama rose nitashinda haya amina imani yako imenisimamisa amen
jamani mbona rose hajapata mahanjumati😚
Nyimbo zote Kwa mpigo
duh
Huyo mchungaji alikuwa ana jeuri gani ya kukutesa bila kuogopa?!
Huyo sio mchungaji... ni mtu aliye msponsor , japo ni wa kanisani. Na ni mtu maarufu anajulikana sana.
Duuuuuh