KIAZI LISHE ''MKATE WA GAIRO''

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 19 พ.ค. 2018
  • Mkate wa Gairo ni jina maarufu ambalo jamii iliamua kukipatia kiazi kutokana na kuliwa na watu wengi kama kitafunwa cha Chai kwa kukifananisha na Mkate ambao huliwa na watu wengi nchini na duniani.
    Kuuta mkate wa Gairo kumetokana na wilaya hiyo ya Gairo kuwa kinara katika uzalishaji wa viazi nchini kwani viazi hivyo hutoka Wilayani Gairo na kusafirishwa kwenda maeneo mengine nchini.
    Zao la kiazi ndio zao kuu la biashara la wakazi wa wilaya hiyo ya Gairo.
    Katika kuhakikisha Viazi lishe vinalimwa kwa wingi na kusambazwa kuliwa Tanzania nzima watafiti kutoka Chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA wakaamua kuja na mbinu ya kusambaza mbegu hizo kwenye familia na vijiji vyote vya wilaya hiyo kwa kutumia watoto a shule.
    Hii inatokana na Viazi lishe kuwa na faida kubwa katika mwili wa binadamu lakini pia soko lake kuwa kubwa tofauti na viazi vingine vya kawaida.
    Fuatilia makala hii ili uweze kujifunza zaidi.
  • วิทยาศาสตร์และเทคโนโลยี

ความคิดเห็น •