#UVUVI

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 15 ต.ค. 2024
  • TANGA
    Jiji la Tanga ni mji mkuu wa Mkoa wa Tanga uliyoko ufukoni mwa Bahari ya Hindi wenye Postikodi namba 21100. Tanga ina bandari kubwa kabisa katika sehemu ya kaskazini mwa Tanzania. Njia ya reli kwenda mji wa Moshi inaanzia hapo.
    Jina la mji wa Tanga linaaminiwa kutokana na lugha ya Kibondei yaani Shamba, kwa sababu wenyeji ambao walikuwa Wabondei waliishi kisiwa cha Toten lakini shughuli zao za kilimo walizifanyia eneo ambalo kwa sasa linajulikana kama mji wa Tanga.
    UVUVI
    Uzalishaji Samaki Samaki waliozalishwa katika jiji la Tanga kwa mwaka huu ni kg 1,626,768 (tani 1626.77) ikilinganishwa na kg 2,000,000 (tani 2000) za samaki waliokadiriwa kuzalishwa sawa na 81% ya samaki waliokadiriwa kuzalishwa. Samaki hawa ni kutoka katika vituo vya Kasera, Deep sea na Tongoni.
    Hali ya Ufugaji Samaki Katika jiji la Tanga, uhamasishaji wa kilimo cha viumbe wa majini na kilimo cha mwani unaendelea ingawa bado mwitikio ni mdogo .Kuna mabwawa 34 ya maji na malambo 4 na kati ya hayo ni mabwawa 19 tu ndio yaliyopandikizwa samaki. Doria za kubaini uvuvi haramu zinaendelea katika maeneo ya ukanda wa bahari.
    MAFANIKIO YA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI
    Kuongezeka kwa mifugo iliyoboreshwa inaofugwa kwa mfumo wa zero grazing ili kuondokana na ufugaji wa mifugo mingi na isiyo na tija. Kuboreshwa kwa huduma ya uhamilishaji na kuongezeka kwa watumiaji wa huduma hiyo.
    Doria za kupambana na uvuvi haramu zinaendelea kufanyika katika maeneo mbalimbali ya bahari na masoko ya samaki. Ufuatiliaji umeendelea kyufanyika ili kubaini vyombo vya uvuvi ambavyo havina leseni na kuchukua hatua. Kupatiwa Pikipiki 2 kwa ajili ya shughuli za ukusanyaji wa mapato ya Uvuvi

ความคิดเห็น • 1