WAZIRI JERRY SILAA ASHTUKIZA OFISI ZA ARDHI JIJINI DODOMA, ATOA MAELEKEZO KWA NCHI NZIMA
ฝัง
- เผยแพร่เมื่อ 7 ก.ย. 2023
- Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya makazi, Jerry Silaa amefanya ziara ya kushtukuza katika ofisi za kitengo cha Ardhi za halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa ajili ya kujionea hali ya utendaji kazi ambapo amefika na kukuta baadhi ya watendaji hawajafika ofisini majira ya saa moja na nusu.
Waziri Jerry amewahimiza watumishi wa jiji la Dodoma na Tanzania kwa ujumla kuwa hasa watendaji wa ardhi kufika ofisini kwa muda uliopangwa na inapofika saa moja na nusu asubuhi huduma zianze kutolewa na si watu kuanza kuingia ofisini kwa wakati huo.
KAMA UNAMKUBALI JERRY SLAA TUJUANE✊✊
TUPO PAMOJA FYEKA FYEKA WAPUMBAVU WOTE...
Ziara za kushtukiza kama hizi ni nzuri sana, zinasaidia wafanyakazi kuwa active, Hongera sana Mh. Jerry Slaa. Mungu akuongoze.
Nzuri sana
Safi sana Mh Waziri Slaa njoo na Morogoro please ofisi ya ardhi Mvomero Morogoro ni hovyo kweli kweli hawafuatilii kazi wala kumaliza kila cku nenda rudi nenda rudi
“nikisema kuna mambo ya hovyo ni hovyo kweeri kwerii”! RIP Chuma
Yaani inasikitisha sana! Watu wako maofisini hawana akili ya kutatua changamoto zinazolikabili Taifa na watu wake, lakini wana vyeti vya madigrii na wamepewa vitengo, yaani wanatakiwa kutumia akili zao na kufikiri sawasawa kwa ajili ya kutatua changamoto zinazolikabili Taifa na watu wake na basically hawafanyi hivyo! Ajabu sana, halafu hatari sana!
Umeongea ukweli wote. Tatizo ni uwezo mdogo wa maafisa kutatua changamoto za ardhi.
Tunaelekea ni kubaya.Viongozi wetu hawana wasaidizi wazuri viongozi wazuri ila watendaji wa ovyo kbsaa.Marais wetu ni wazuri tuu Samia suluhu na Dr Hussein Mwinyi wote ni good leaders but baadhi ya watendaji wa ovyoo.Sisi tuna shida hapaa znz hayo hayo.
@@MrA24G Tena kama Rais Mwinyi ni mzuri mno. Poleni sana!
Safi kabisa chapa kazi Waziri. Maana wafanya kazi wazembe saa moja na nusu hakuna mtu mh...... HONGERA WAFANYA KAZI WA MHIMBILI MOI DRS AND NURSES WANAFIKA SAA 12 NA NUSU NA SAA HIZO KAZI ZINAANZA MMungu awabariki sana
Hata aibu hawana kazi kutapelii watu...na fidiaa udai ulipweee ..
KUMEKUCHA KAZI IENDELEE 🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿
Huu mfumo wa kushtukiza muda mwingine ni mzuri sana
Nakufuatilia kwa Makini sana kaka nakuamini piqa kazi
Good start Mr minister,,, ila tukuomba usibadilikie njian kuwa makapi. Idara ya ardhi inahitaji sana kufunga mkanda, usiweke njaa mbele, yaaan ukila tu Hela ya mtu ndo mwanzo wa haki haramu.
Safi sana apa ndo wana jionaga miungu watu yn apa ndo shidaa sana kwenye hati
Hawa watumishi ukiwapa Muda wa kujieleza ujue watakupoteza tu..yaani ni Wezi hatari...MH. SLAA PIGA KAZI BABA UNATISHA SANA MKUU..
Hongera sana mheshimiwa
GOOD, utumishi mzuri ni kutoka ofisini na kwenda kwa wananchi kwani kiongozi vitendea kazi yake ni wananchi na sio meza na mafaili tu
HONGERA HONGERA HONGERA MHESHIMIWA SLAA KAZA BUTI KWA PAMOJA TUTAFIKA
Shukran sana Waziriwetu wanyooshehao kaziyaonikuzulumu maskin aridh zao hawajuininimaana ya mtanzania.
Ndo kazi yao ao washezi sana na mimi takuja kwajili silaaa yupo mtetez takuja dodoma nishida wana ingia sanne ofisin
Waziri unafanya kazi nzuri najua hauna njaa kama ni maisha mwenyzi mungu amekbariki simamia haki wanainchi wanakukubali
Tumbua wazembe kazini na hapa mama hajakosea kumteua huyu mwamba piga kazi kaka
Kuna watu ndo kazi yao kuzungusha watu hivo. na kama huamini. mtume mtu asiseme katumwa na wewe uone atavozungushwa
Ofisi za ardhi kumegubikwa na majambazi sana, dodoma watu wananyanganywa viwanja hovyo tu,,,😢,,,Hongera sana mhe.
Mh umefanya Vzur sana,
Ungewashkisha adabu kdogo
Mungu awe pamoja nawe siku zote, Utaratibu huo utasaidia sana kutatua migogoro ambayo haina hata sababu ya kutotatuliwa.
ASANTE SANA BABA.
Hapo kinacho takiwa hazina watume list ya wateja wote hao 200 walio walipia na kila mmoja na amount yake aliyo lipia...mfano hata sisi bank wakitulipa wanalipa amount moja huwa tuna waomba list ya mchanganuo wanatuma then kila mteja tuna muingizia kiasi chake alicho lipiwa
Hawa watu wa ardhi ni wasumbufu sana, Mh. JERRY slaa mm pia hawajanipatia Hati yangu 2021
Kwa kweli Dodoma hasa Iyumbu kuna issue kubwa sana
Wawepe watu control number walipie viwanja vyao
Waliolipia mwanzo ndio wapewe haki sio janja janja
Tangu 2021.????? MHESHIMIWA chukua hatua....
Hicho kitengo cha Ardhi kinapaswa kuundwa upya hapo dodoma tena takukuru cjui wanang'ata wapi nao wachunguzwe hakuna process utafanikiwa hapo pasipo kutoa rushwa utarudi mara 30 hapo
Mkuu wa mkoa wa dodoma ni mzigo,
Kweli kabisa yaani
Wewe unaweza kuwa mfano Wa jembe ambalo lilitangulia mbele za haki mungu akupinganie
KWELI KABISA AWE NA MAISHA MAREFU, MUNGU AMJAALIE.....
Waziri hatari halali! Huyu Waziri APEWE TUZO YA WAZIRI BORA WA mda Wote
Safi sana kama Hayati JPM taratibu tutafika tuu.....
Waziri wangu mbunge wangu mimi kura yangu nimeitumia kihalali. Mungu aendelee kukutunza mwanangu
Safi sana waziri hiyo wizara inachangamoto sana ila nina imani teuzi ya mama imempata mtu sahihi kuna vimeo hususani baadhi ya watumishi,Mawaziri fanyeni ziara za kustukikiza wengi wa watumishi wanajisahau sana humo maofisini
Aiseei jerry mungu akutangulie hizii ni shida.
Duh Hadi aibu Baraka kujieleza kapata kigugumizi
Wanajifanya hawajui chochote kumbe wanajua Kila kitu.
❤ Mungu aendelee kukuinua
Km Magufuli hongera sana
Watu wa ardhi Wana matatizo sana uje na kongwa
Tunaanza upyaaaa hakikisha bando unalo
Mheshimiwa hata sisi tunazungushwa na eneo ni letu kila siku ni wasumbufu sana ao watu wajiji
Daah watu wanaishi watakavyo bila kufanya kazi 😢😢
Futa kazi Hao walaji tu hao
Mweshimiwa kama hili swala ukilifuatilia sana utakuta hao viongozi ndio sababu kuu ya migogoro na wana fahamu hizo propabanda zote mm pia ninayo changamoto kama ya huyo Mama kiwanja Ntyuka na sababu ni Mtendaji kata Mungu akusaidie katka hii wizara ina laana sana kwakuwa wamejaa wazulumaji
Kichaa amekabidhiwa rungu guys,kuweni makini ccm mtajikuta mpo uchi maana mungu huwa hachelewi wala hacheleweshwagi
Hawajibu barua hawa wafanyakazi wa ardhi kwa kweli mimi nina changamoto toka 2018 Morogoro
Dada yupo very smart nimependa anajua kufatilia jambo.
Mkuu hao huwa wanapenda kukwapua maeneo ya watu kisha wanajiweka majina ya ndugu zaa
Wanabahati sana JPM amepumzika!
Aibu sana
Safi kabisa
Hongera Mhe Rais kwakumteuwa huyu MTU
Waziri hapo ulikuwa unaongea na Wala rushwa hao ...Yani huyo mtumishi ardhi anajifanya hamtambui huyo Mama karatasi ni ngeni kwake wakati Huyo mama anasema alikuwa anachat nae ..
Mawaziri wengine waige mfano wa W AR Mhe. Jerry Silaa. Mtu mwenye malalamiko apate majibu ya moja kwa moja. Hii inaleta uwajibikaji
Hii nchi Mawaziri wana kazi ngumu mno.Kila mahali wanakuta uzembe na mazoea.
Ningeomba wazili anaehusika na NSSF sikumoja ashtukize atayaona mengi
Waziri umenikumbusha lukuvi uko vizuri
namba ya silaa ntaipataje jaman mm niko nashinda kwenye kiwanja changu
Tunaomba na waziri anaeshugulikia malipo ya mifuko ya ppf naye awe kama huyu pesa psssf hakuna na watu walikatwa private hawapeleki maboss
Hawa wanaoitwa watumishi wa serikari hata sielewi erimuyao hovyo kwa hovyo🤔🤔
Ziara kama hii nzuri sana ila imetoka bila uhakika wa dada kiwanja chake kipo au hakipo na inaonyesha atakaa miaka mingine 7 kisha Baibai hakuna kiwanja wala pesa kwani pesa indayo kwa mganga hairudi
Waziri uje na huku kwetu King'azi kata ya Kwembe. Kuna mgogoro wa mpaka kati ya Wilaya ya Ubungo vs Wilaya ya Kisarawe. Yaani wananchi hatupati huduma za kiserikali kwa muda mrefu sana mpaka barabara za mtaani hazipitiki, tumechanga mpaka tumechoka ili kutengeneza miundombinu hii.
Hapa kazi tuu
Naomba kupata contacts za ofisi ya waziri Jerry Silaa Dodoma
anapiga kazi anajitahidi 🙏
Hatuna kwa kukimbiria waziri wetu mtetezi
Kama huyo Mama kamwona Waziri na bado anakwama je sie tusiojua hata Mkuu wa wilaya anafananaje utaishia wapi?
Hapo sasa nani mtumishi mwenzao wa umma,mimi na wewe jee inakuwaje?
Matapeli wa ardhi wamejaa kwenye wizara ya ardhi hao wote wanaelewa huyo mama wanamsumbua tu ukiwaangalia usoni unaona tu walivyo waongo
Kupata hati ni kipengele duuu nilifuatilia ya kwangu toka mwaka2005 miaka mitatu nasumbuliwa njoo kesho week ijayo mpka nikaachana nayo mpka leo cna huo mda wa kupoteza
Tarime huku watu mpaka wanazeeka shida sana
Tarime sehemu gani ndugu me pia natokea Tarime
MH anauliza hujaiona muda mrefu😅😮
Njoo KATESH-HANANG' MANYARA.
Kidogo kama naanza kukuelewa wazili mana SS wanaichi tuna shida sana
Fukuza ayo mandunduka mhe.waziri
Hilo li baraka ndio sample ya maafisa ardhi matapeli....mbupu zako, haiwezekani mtendaji wa serikali ukawa mngese kiasi hicho km sio msomi
Au bhasi
Mtanuwe ofisi ziende kata zote Tanzania msongamano unanyanyasa raia na kumnyima haki yo umiliki nenda Rudi maendeleo yanaduma lakini kama Bado huu uozo tujipange kuiondoo madarakani ccm 2025
Hawa wako hawako sawa karibu nchi nzima kwenye ardhi na wengi siyo wasomi watu wako wa ardhi na halmashauri na watendaji wako
Waziri umeanza vizuri lakini utalambishwa asali na kuwa nguvu za soda. Nchi hii imejaa majangili ya ardhi. Hao ulionao wanamiliki viwanja kama pelemende kazi yao ni kutapeli wananchi.
Ofisa atapaje kigugumizi, si angempa maelezo kama ya kwako? Kwa nini azidi kumdanganya , subiri subira ya Tanzania 🇹🇿 inaumiza kwa kweli☹️☹️☹️☹️
Kuna kaimu mkurungezi anaitwa faziri na kamishina anaitwa hamisi wameshindwa kumariza mngogoro wa arizi mbezi kwa msunguri msingwa
Safi kuwatembelea mataperi wakubwa wajiji Sina hamu nao nimezunguka zaidi yamwaka moja sijapata mafanikio
Rushwa oyeeeee
Tatizo LA watumishi walioko kwenye ofisi za umma hawafanyii kazi barua Bali ni mpaka aliyeandika barua aende akatoe maelezo ya mdomo wakati barua inajieleza.Tatizo hili lipo. Serikali ione sasa mifumo ya ajira zake. Ajira za kujuana sio weledi.
kuna uozo sana kwenye hizi taasisi inawezekanaje toka 2021 mpaka leo mtu bado analalamika??
Haya mambo ya kushtukiza ndo mom hayataki, anataka mwendo wa danadana kama zama zileeee za unanijua mie nani?
Aiseee huyu ndiye jeri slaaa ana akili nyingi uwezi kumdanganya bado kijani tunamjua vizuri
HAO WACHAWI TUUUU😮😮😮
Shemeji njoo huku kivule napo kuna mgogoro wa aridhi
TANZANIA YETU NAMKUMBUKA MZEE MWENYEWE...
Mkuu baadhi ya watumishi ni mizigo endelea kufuatilia MUNGU anakuona
Daaah watu hawa fanyi KAZI aisee
Nilisimamia ununuzi wa kiwanja kikaja kuuzwa hapo ofisini tena mtu kapewa documents zote pasipo cc kujua huo ninaumia mno nikipita kwenye kile kiwanja
Hawafanyi kaz yao si unaona hawakai kazin
Njoo mhe na Dar es. Salaam watu wako wako tu ofisi za kata na kujimilikisha nafasi za ardhi za watu na kudai hii ni open space ukimwambia niandikie karatasi niende ardhi inakuwa kimya halafu wana kwambia nimesafiri au nipo kwenye kikao
Hivi ndio watanzania tunavyotaka
Mazoea ynakujisahau ndio hyo sasa.Huu ndio uongozi jmn.Sio unaandaliwa mahali kufika watu wanajipanga kwanza Ili uyajue Madudu yawatenda kazi wako nikushtukiza tu.hpo ndio shida.
Mh. Waziri chapa lkazi lakini Wizara ya Aridhi sawa na ''MFUPA ULIOMSHINDA FISI KUULA''. Mh. Waziri ongeza mmsisitizo wa uondoshaji wa matatizo yasababishwayo na watumishi wasio waaminifu la sivyo ukiondoka Uwe na dialog ya matatizo uliyoyapitia na wakupe mrejesho. Tunakutakia uwajibikaji mwema