RAIS DKT. MAGUFULI AWASIMAMISHA TBA KUJENGA NYUMBA ZA MAGEREZA UKONGA

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 15 มี.ค. 2019
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 16 Machi, 2019 amefanya ziara ya kushtukiza katika mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya Askari Magereza wa gereza la Ukonga Jijini Dar es Salaam na kuagiza mradi huo ukabidhiwe kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ).
    Mhe. Rais Magufuli ametoa maagizo hayo baada ya kubaini kuwa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) imeshindwa kutekeleza mradi huo kwa wakati, licha ya Serikali kutoa shilingi Bilioni 10 za ujenzi.
    Ametaka wataalamu wa TBA waliokuwa wakisimamia mradi huo pamoja na Askari Magereza waondoke na kuwapisha JWTZ.
    “Kwa hiyo hapa nisimuone mtu wa TBA, nisimuone mtu wa Magereza kuja kusimamia, muwaache Jeshi la Wananchi wafanye kazi zao, siku watakapokuja kunikabidhi na mimi nitawakabidhi Magereza, kwa hiyo watu wa TBA kuanzia leo nimewafukuza hapa” amesema Mhe. Rais Magufuli.
    Mhe. Rais Magufuli ameelezea kutoridhishwa na utendaji kazi wa TBA katika mradio huo ambao ulianza zaidi ya miaka 2 iliyopita kwa kushirikisha Jeshi la Magereza ambalo lilikuwa linaisadia TBA katika kazi za ujenzi, na ametaka TBA na Jeshi la Magereza wabadilike katika utekelezaji wa majukumu yao.
    “Nataka kila mlipo watu wa Magereza mfanye kazi, msimamie watu, kama ni ng’ombe muwafuge vizuri wazalishe vizuri hadi muuze mazao nje, kama ni kilimo mlime kwelikweli, muwe ni jeshi la kuzalisha, hii ni aibu kuleta jeshi jingine la wananchi kuja kuwajengea nyumba nyinyi, wakati nyumba mnakaa nyinyi, mlitakiwa muwe mmeshapanga mkakati kwamba TBA wamesuasua, ngoja tufyatue matofari, tuanze kujenga” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.
    Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Kanali Charles Mbuge amesema JKT itakamilisha ujenzi huo ndani ya kipindi cha miezi 2 na nusu kuanzia kesho na kwamba kazi zitafanywa usiku na mchana.
    Aidha, Mhe. Rais Magufuli ameitaka TBA kutoa maelezo ya namna fedha zilizotolewa na Serikali kiasi cha shilingi Bilioni 10 zilivyotumika, na ameonya kuwa endapo itabainika matumizi ya fedha hizo hayaendani na kazi zilizofanyika hatua kali zitachukuliwa.
    Katika mradi huo, ujenzi wa majengo 12 ya makazi ya Askari Magereza yaliyopangwa kuwa na ghorofa 4 kila moja ulioanza Desemba 2016 umefikia asilimia 45 tu na unaendelea kwa kusuasua.

ความคิดเห็น • 80

  • @abduladhimually3542
    @abduladhimually3542 5 ปีที่แล้ว +15

    Jembeeee#watakubalitu..........your a good leader never met before

  • @amos878
    @amos878 5 ปีที่แล้ว +13

    Outstanding mkuu na waje walale na wafungwa wao 😂😂😂😂

  • @allyfutto8763
    @allyfutto8763 5 ปีที่แล้ว +11

    Faraja iliyoje kubahatika amirijeshi anayeona mbalisana watanzania ni jambo la kujivunia sana ni mipango ya mungu Tumeteseka sana Tubadirike twende na wakati.

  • @zefamange7281
    @zefamange7281 5 ปีที่แล้ว +7

    KMBIZA HAO COMMANDO WANGUUU, WAMEZOEA UJINGA UJINGA HAO

  • @nyanda427
    @nyanda427 5 ปีที่แล้ว +7

    Waoh. Love you Mr. President Dr. John Pombe Magufuli

  • @sk-wj9or
    @sk-wj9or 5 ปีที่แล้ว +10

    I salute you Mr president!

  • @bundalamlolasa3774
    @bundalamlolasa3774 5 ปีที่แล้ว +12

    Safe Sana mheshimia Rais Kaz yako inaonekana.

  • @aloycekiwia8613
    @aloycekiwia8613 5 ปีที่แล้ว +16

    Hata Umchukie vipi Uncle Magu, Kuna mambo mengine lazima umkubali tu! labda uwe Chizi.!? Hizi nyumba nazikumbuka ni miaka mingi kweli. Kumbe walishapewa na Pesa zote.!!??

    • @kwandukanunda4351
      @kwandukanunda4351 5 ปีที่แล้ว +1

      Watapike

    • @shabanmlekwa9513
      @shabanmlekwa9513 5 ปีที่แล้ว +1

      Na Tanzania ndo ilishafikia hapo. Alitakiwa aje mtu ka Magufuli.

  • @ramadhanimmana3829
    @ramadhanimmana3829 5 ปีที่แล้ว +7

    Safi saan mkuu

  • @freddymello3227
    @freddymello3227 5 ปีที่แล้ว +5

    Sifa ya kiongozi bora ni kuchukua hatua katika muda mwafaka.
    hongera J.P.M kwa hatua hii uliyochukua.hakika wewe ni mfano wa kuigwa kwa vizazi vijavyo.
    aina ya uongozi wako ni wito na kujitoa kweli kweli.nchi yetu inauozo kila sehemu.
    Viva C.C.M,viva J.P.M

  • @neemajoshuaer9562
    @neemajoshuaer9562 5 ปีที่แล้ว +8

    Saf Sana mhe Rais

    • @freddymello3227
      @freddymello3227 5 ปีที่แล้ว

      Neema Joshuaer ,mambo!!uko poa neema wng

  • @jacksonjombo7221
    @jacksonjombo7221 5 หลายเดือนก่อน +2

    God give me a vision like this Father, Ee Mungu nipe maono kama uyu Baba

    • @j.bjacobbasubi2187
      @j.bjacobbasubi2187 4 หลายเดือนก่อน

      I'm a congolaise but 😢😢😢

    • @amirimbago8325
      @amirimbago8325 4 หลายเดือนก่อน

      Nikikupa maono watakuua mapema...pambanatuu na hali yako kwa maendeleo ya ukoo wenu.

  • @JoasDioniz
    @JoasDioniz 5 ปีที่แล้ว +7

    Haaaaahaaaaa lazima wazitapike #JeshiHalishindwi #TanzaniaMpyaYaJPM

  • @user-pe1ze9sw4f
    @user-pe1ze9sw4f 9 หลายเดือนก่อน +2

    Uko ulipo Mungu azidi kukulinda

  • @magilemabula5755
    @magilemabula5755 5 ปีที่แล้ว +5

    Tanzania kwanza

  • @victustemba
    @victustemba 5 ปีที่แล้ว +5

    Hapa kazi tu, 10% watazitapika..!😀

    • @gooddeeds162
      @gooddeeds162 5 ปีที่แล้ว

      Victus temba Shemeji Nafurahi sana hatua anazochukua Mh Rais zinatia sana Faraja, Lakini Kuna wachache wanataka kuzingua tu .
      Watashindwa tu

  • @agneomasonda2462
    @agneomasonda2462 5 ปีที่แล้ว +4

    Piga kazi baba

  • @masigomhoja5182
    @masigomhoja5182 5 ปีที่แล้ว +2

    Safi sana duh kura yangu mimi ni yakoo mjombaa

  • @shukurumwangosi1537
    @shukurumwangosi1537 5 ปีที่แล้ว +3

    Wooh

  • @shayoyahaya3736
    @shayoyahaya3736 5 ปีที่แล้ว +2

    Sipata ona...!!
    Huyu ni zaidi ya Rais.
    Washa moto haya ndio mabadiliko ...
    Walishazoea ubwenyenye....

  • @zawadix9574
    @zawadix9574 5 ปีที่แล้ว +3

    Jembe

  • @tufyambefredrick4340
    @tufyambefredrick4340 5 ปีที่แล้ว +1

    Ukimuona mh Raisi amevaa hiyo kofia na yuko kwe ziara ujue kuna jambo litatokea nani anakubali hii

  • @kahmardintebe9266
    @kahmardintebe9266 7 หลายเดือนก่อน +1

    Chuma hakika mungu alituzawadia Ila hatukuona umuhimu wake pumzika kwa amani jpm

  • @h2kizzyboymsafi832
    @h2kizzyboymsafi832 5 ปีที่แล้ว +1

    Safi sana jembe

  • @tanzania2559
    @tanzania2559 5 ปีที่แล้ว +2

    🙌🏾🙌🏾🙌🏾👏🏾👏🏾👏🏾👏🏾👏🏾

  • @Lusekelo98
    @Lusekelo98 21 วันที่ผ่านมา

    Real life

  • @thomasmollel9465
    @thomasmollel9465 3 หลายเดือนก่อน

    Rest in peace kipenzi cha watanzania

  • @benbranco3688
    @benbranco3688 3 ปีที่แล้ว +1

    R.I.P MKUU DAHH

  • @RedpilledPhoenix
    @RedpilledPhoenix 5 ปีที่แล้ว

    Mungu mlinde Rais wa 🇹🇿 namwombea afya nzuri

  • @gabrieladam491
    @gabrieladam491 5 ปีที่แล้ว +1

    Huwa nakuelewaga Sana naomba Mungu anipe nifanye kama wewe President

  • @matingo-bk1248
    @matingo-bk1248 5 ปีที่แล้ว +1

    Hii ndio maana halisi kiongozi, kuwa na maamuzi magumu mambo yanapoenda sivyo

  • @ismailyusuph740
    @ismailyusuph740 5 ปีที่แล้ว

    ....NA WATAITAPIKA...!
    JESHI halishindwi Mh Rais...!

  • @manyotaskipper5765
    @manyotaskipper5765 5 ปีที่แล้ว +1

    Ukinuna UWE NA SABABU MJOMBA MAGU BADO WANAJUSAHAU TBA WANALALA TU

  • @joesimba
    @joesimba 2 ปีที่แล้ว +1

    2:50

  • @raphaelkessy7360
    @raphaelkessy7360 3 หลายเดือนก่อน

    Pumzika kwa amani na baraka Kamanda mkuu JPM

  • @user-mf8iu1qp3n
    @user-mf8iu1qp3n 4 หลายเดือนก่อน

    Hahahaha et ntawakabidhi 😂😂 walale na magereza wao😂😂 Rest in peace 🕊️ rais wetu

  • @ismailmasoud6001
    @ismailmasoud6001 หลายเดือนก่อน

    Aisee huyu jamaa alikua ni MWAMBA kabisa..!

  • @mussamkali9926
    @mussamkali9926 7 หลายเดือนก่อน

    Magu kazini

  • @mupagedragon1972
    @mupagedragon1972 3 ปีที่แล้ว

    Vizur sana baba etu magu

  • @nassoromzenga866
    @nassoromzenga866 5 ปีที่แล้ว

    Napenda sana mamuz ya rais anataka wachapa kaz

  • @allythabit5175
    @allythabit5175 5 ปีที่แล้ว

    raha sana

  • @utukufueliya5279
    @utukufueliya5279 5 ปีที่แล้ว

    kwa kauli hii kuna watu wanaenda kufungwa.....

  • @SaleheMkomwa
    @SaleheMkomwa หลายเดือนก่อน

    Fukuza tu

  • @ulemse6067
    @ulemse6067 5 ปีที่แล้ว

    Twahitaji kiongozi Kama huyu huku Kenya.

  • @charlesmakuri792
    @charlesmakuri792 5 ปีที่แล้ว

    Hawa wanajikosha kwa kina mbowe eti serikali iwape magodolo wafungwa,hivi uende gerezani utoke hujakelwa sasa hereza au umeenda kutalii ,jengeni makazi yenu

  • @godfreymwacha8711
    @godfreymwacha8711 5 ปีที่แล้ว

    That my president I salute you

  • @kolinsimahanga9845
    @kolinsimahanga9845 5 ปีที่แล้ว

    jwtz safi

  • @vincentmasanja789
    @vincentmasanja789 5 ปีที่แล้ว +3

    Inawezekana Raisi wa awamu hii akaweka historia ya pekee ,kwa kuwa nchini bila kwenda ughaibuni kwa miaka minne.

    • @fathermore9772
      @fathermore9772 5 ปีที่แล้ว +1

      Vincent Masanja tuseme asante kwakua nakiongozi mwenye mtizamo chanya namsimamo kama uncle

    • @vincentmasanja789
      @vincentmasanja789 5 ปีที่แล้ว

      Hakika Fadher More.

  • @tevintevin1884
    @tevintevin1884 5 ปีที่แล้ว

    Hadi raha ...bravo Mr President... Hao wa kuzitapika itabidi watapike mpaka nyongo

  • @user-me2nk2me9d
    @user-me2nk2me9d 5 หลายเดือนก่อน

    Jaman ludi kigambon uvukaji feery tunateseka panton kla sku zinaalibika tunateseka

  • @utukufueliya5279
    @utukufueliya5279 5 ปีที่แล้ว

    Kazi usiku na mchana.... 😀😀😀😀😀😀

  • @barakamashinga463
    @barakamashinga463 5 ปีที่แล้ว

    A cleansheet president!

  • @athumanomary1438
    @athumanomary1438 5 ปีที่แล้ว

    Ewe mwenyez MUNGU ewe mwenyez MUNGU tunakuomba na tunazidi kukuomba enderea kumuongoz kumsimamia kumrinda na kuzidi kuimarisha afya yake raisi wetu ewe mwenyez MUNGU mkuu

  • @mickwealthy500
    @mickwealthy500 ปีที่แล้ว

    RIP

  • @Mwinamila-3
    @Mwinamila-3 6 หลายเดือนก่อน

    N viongoz wachache wanaoweza kichukua maamuzi kama haya

  • @samsonmagesa3959
    @samsonmagesa3959 5 ปีที่แล้ว

    Hapo ndipo waga Nasema 2020 Kura yangu Kwakoooooo

    • @samsonmagesa3959
      @samsonmagesa3959 5 ปีที่แล้ว

      Jeshi halishindwi huko Vizuri Kanali

  • @genimaige6023
    @genimaige6023 5 ปีที่แล้ว

    kusema ukweli toka moyoni jeshi la magereza lijitathinini upya yani ni sawa na baba tkt nyumba anatoa maagizo ktk familia yake na hayatekelezeki kwa wakati, hata mm nimechukia hii ni aibu, kama pesa zipo tatizo ni nn?? 😄😄😄😄😄😄

  • @mashimbadeograthiasmathias8583
    @mashimbadeograthiasmathias8583 5 ปีที่แล้ว

    Canal jenga Bila shida Ila hao MAGEREZA watapike hela hizo

  • @thabitngangila8562
    @thabitngangila8562 5 ปีที่แล้ว

    chuma cha pua ukizingua anakuumbua

  • @florencebudoya3814
    @florencebudoya3814 5 ปีที่แล้ว +1

    Elelo yeye.

    • @lengaiolesabaya8209
      @lengaiolesabaya8209 5 ปีที่แล้ว +1

      Mungu unatisha.Unajua kuwaleta watu wako kwa saa zako, kuliponya taifa lako.

    • @samuelmwaikambo5691
      @samuelmwaikambo5691 5 ปีที่แล้ว

      President JPM nadhani bado hawajakuelewa hao wanafanya wajuavyo ni pingu tu huko ni kuhujumu mali ya watanzania walipa kodi usiku na mchana.

    • @abdilahijuma2852
      @abdilahijuma2852 5 ปีที่แล้ว

      Dr magufuli safi sana

  • @eliyawilliammagesamarwa8413
    @eliyawilliammagesamarwa8413 5 ปีที่แล้ว

    Kura yangu

  • @mussaramadhani-in1ci
    @mussaramadhani-in1ci ปีที่แล้ว

    Zmzm