REV. DR. ELIONA KIMARO: SADAKA NA NADHIRI, KUZUILIA

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 6 ต.ค. 2024
  • KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH : IBADA YA JUMAPILI (KUSIFU NA KUABUDU) - 05 NOV 2023.
    KICHWA CHA SOMO : SADAKA & NADHIRI
    (KUZUILIA)
    Mithali 11 : 24
    Matendo ya mitume 5 : 1 - 11
    Mwanzo 22 : 11 - 18

    Mithali 11 : 24
    24 Kuna atawanyaye, lakini huongezewa zaidi; Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji.
    Matendo ya mitume 5 : 1 - 11
    1 Lakini mtu mmoja jina lake Anania, pamoja na Safira mkewe, aliuza mali,
    2 akazuia kwa siri sehemu ya thamani yake, mkewe naye akijua haya, akaleta fungu moja akaliweka miguuni pa mitume.
    3 Petro akasema, Anania, kwa nini Shetani amekujaza moyo wako kumwambia uongo Roho Mtakatifu, na kuzuia kwa siri sehemu ya thamani ya kiwanja?
    4 Kilipokuwa kwako, hakikuwa mali yako? Na kilipokuwa kimekwisha kuuzwa, thamani yake haikuwa katika uwezo wako? Ilikuwaje hata ukaweka neno hili moyoni mwako? Hukumwambia uongo mwanadamu, bali Mungu.
    5 Anania aliposikia maneno haya akaanguka, akafa. Hofu nyingi ikawapata watu wote walioyasikia haya.
    6 Vijana wakaondoka, wakamtia katika sanda, wakamchukua nje, wakamzika.
    7 Hata muda wa saa tatu baadaye mkewe akaingia, naye hana habari ya hayo yaliyotokea.
    8 Petro akamjibu, Niambie, Mlikiuza kiwanja kwa thamani hiyo? Akasema, Ndiyo, kwa thamani hiyo.
    9 Petro akamwambia, Imekuwaje hata mkapatana kumjaribu Roho wa Bwana? Angalia, miguu yao waliomzika mumeo ipo mlangoni, nao watakuchukua nje wewe nawe.
    10 Mara akaanguka miguuni pake akafa; wale vijana wakaingia wakamkuta amekufa, wakamchukua nje, wakamzika pamoja na mumewe.
    11 Hofu nyingi ikawapata kanisa lote na watu wote walioyasikia haya.
    Mwanzo 22 : 11 - 18
    11 Ndipo malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akasema, Ibrahimu! Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa.
    12 Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee.
    13 Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.
    14 Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire,d kama watu wasemavyo hata leo, Katika mlima wa Bwana itapatikana.
    15 Malaika wa Bwana akamwita Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni
    16 akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema Bwana, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,
    17 katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao;
    18 na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu.

    Mhubiri : Rev. Dr. Eliona Kimaro
    Kwa maoni na ushauri:
    Mch. kiongozi: Dr. Eliona Kimaro
    Simu: +255 655 516 053, +255 754 516 053

ความคิดเห็น • 12

  • @bethwinfred4400
    @bethwinfred4400 3 หลายเดือนก่อน +1

    Amen ahsante

  • @BeatriceMunyua-v2z
    @BeatriceMunyua-v2z หลายเดือนก่อน

    Good teachings pastor Ur encouraging us

  • @JoyceMwandu-eu1vj
    @JoyceMwandu-eu1vj 3 หลายเดือนก่อน +1

    Mungu anisaidie nisizuilie sadaka.Nimebarikiwa Sana na ujumbe huu.Mungu akubariki mtumishi.

  • @ombenkallenge1924
    @ombenkallenge1924 10 หลายเดือนก่อน +1

    Nabarikiwa Sana na mafundisho Yako Sana

  • @miriamalute1540
    @miriamalute1540 5 หลายเดือนก่อน +1

    Mungu akubariki sana baba

  • @furahamtweve4222
    @furahamtweve4222 11 หลายเดือนก่อน +2

    Amen nmebarikiwa kuanzia Leo sitazuiria kutoa sadaka

  • @rahyanadam8328
    @rahyanadam8328 3 หลายเดือนก่อน

    Nimebarikiwa sana🙏

  • @IreneSambala
    @IreneSambala 4 หลายเดือนก่อน

    Aminaa

  • @KanadeMrangu
    @KanadeMrangu 11 หลายเดือนก่อน +1

    AMEN ❤❤❤❤

  • @rahimajuma5306
    @rahimajuma5306 9 หลายเดือนก่อน +1

    Mungu akubariki