Dizasta Vina - Almasi (Feat Tk Nendeze)
ฝัง
- เผยแพร่เมื่อ 15 มิ.ย. 2023
- A video lyrics of Dizasta Vina perfoming Almasi from the Album The Verteller
Stream and Download Almasi
Boomplay - www.boomplay.com/songs/63553588
Audiomack - audiomack.com/dizastavina/son...
Mdundo - mdundo.com/song/2081301
Spotify - open.spotify.com/track/3Kl6Y9...
Apple Music - music.apple.com/us/album/alma...
Other contents
Audiomack - audiomack.com/dizastavina
Boom play - www.boomplay.com/artists/3288611
Mdundo - mdundo.com/a/2263
Spotify - open.spotify.com/artist/1IC2b...
Apple music - / dizasta-vina
Connect with Dizasta Vina on social medias
Instagram - / dizastavina
Twitter - / dizastavina
Facebook - / dizastavina07
sw.wikipedia.org/wiki/Dizasta...
Business: Pan.authentik@yahoo.com
Website - bio.link/dizastavina
Lyrics
Nilikutana mtaani na Mzee mmoja
Tukaketi chini akanipa soga
Mimi sitamsahau
Alisema wangapi walikuwepo namba moja
Sasa wamerudi chini ni vioja
Watu wamewasahau
Utavamia kwenye tamasha la muziki
Usoni bashasha huku rohoni umeikumbata dhiki
Sanaa imesanda na sasa tena hauna kiki
Utaigiza furaha kwa kunywa bia za mashabiki
Zitaongea nguo ulizoazima kwa msela
Hazitatosha kuficha ukweli kwamba hauna hela
Hautakumbukwa kama mwanzo wakati unatisha
Paparazi hawatakujua so hautapigwa hata picha
hakuna atakayekuangalia usoni
Tamasha utaingia kwa kuzidandia kuponi
Mchumba uliyemmwaga atang'ang'aniwa kiunoni
Utatabasamu huku hasira umeifungia moyoni
Utapotaka kujichanganya utahisi haya
Lipsi denda zitachakaa kusizi kaya
Watasikika wadadisi wakiongea kwa kudisi
Kamera zote zitamfata msanii uliyemu-Inspire
Hayatakuwepo majumba magari na mapochi nene
Milo ya hoteli za kifahari na ma-roast kede
Zitasahaulika idadi ya tuzo ulizohodhi kwenye majukwaa
Huku magazeti yakiku-Post mbele
Hautatembeza tena rungu ka' Kipepe
Hautavutia Wachuchu maana nyota haina nguvu
Hautafatwa tena na Mashushushu kwa maseke
Utakumbuka ulivyozungukwa na grupu la Vicheche
Michuzi itakauka utapiga hodi ukame
Hautawekwa kwenye ma-board ka' Van Dame
Hautashawishi magari road yapangane
Na utakuwa peke yako bila ya ma-Bodyguard nane
Kipindi ambacho taswira yako ipo gado
Ndo' kipindi cha kulikata shauri lako
Kutambua nafasi na thamani ya sauti yako
Kutambua dhamana mapema kabla ya mauti yako
Dhamana yako ni zaidi ya kula na kupiga pamba kali
Kununua Bupa na chupa ukizilaza chali
Jina kubwa likikufumba ushindwe tafakari
Utakufa masikini ukizubaa kuzichanga mali
Usijesahau maisha yako halisi
Yanayolingana na kipato chako thabiti
Usijekufa kipindi ambacho michango haikidhi
Haitoshi hata kujenga nyumba ya mama'ako Kibiti
Uko wakati wa kumiliki idhini ya uwongo wako
Wenzako wamedondoka, Je utajifunza?
Unasifika mjini kwa wingi wa longo zako
Ukifa tutasimulia nini watoto wako
Tutasimulia idadi totoz ulizonusa
Au gambe idadi ya Kopo ulizoruka
Idadi ya mahusiano au idadi ya mioyo uliyoivunja
Au idadi ya wasichana wadogo uliowavuruga
Najua mwisho mwanangu hamna njia
Utatokewa na kila hadithi uliyoisikia
Sicho kitu ninachokihofia
Hofu yangu kama umeshaiandaa saikolojia
Ukija wakati pazia halifunguki
Wadananda uliowadandia hawakukumbuki
Najua itafanya akili ichoke utapagawa
tafadhali usijegeukia pombe na madawa
Kipandacho hushuka ulishawaza
Si muiujiza ni asili inayoshangaza
Wasahaulifu Walimwengu ilitangazwa
Watataja mashujaa na jina lako halitatajwa
Wanafki, Walafi na Mabishoo zako
Wangapi watakuwepo kiu ikidaka koo lako
Muda wa kuwasoma wote waliopo kando yako
Maana hata pesa haitatibu jelaha la roho yako
Maagano ya siri yatakuwinda
Vyote walivyotabiri vitafika
Maisha ya ndoto yataisha
Utairudia kawaida utagundua kuwa haukuwa malaika
Kiasi utajua dini
Utajua harufu ya sakafu kwa maana utakuwa chini
Hata maana ya maisha itapotea
Sumu, Kisu na vitanzi vitasogea
Sikutishi ila utakufa peke yako
Jeneza lako halitabebwa na hao vicheche wako
Sishangai wenge lako, Ng'ombe
Nashangaa unapoyumba kwa kuzidiwa na ukubwa wa pembe lako
Ni heri kuwa mwewe
maana mwoga anajali kuwa uelewe
Kundi la watoto nyumba wanakupenda
Na wanaota siku moja waje kuwa kama wewe
G.O.A.T
Almasi inaweza kuwa lugha ya picha tu katika fasihi,ina maana katika hali ya maisha hasa ujana kuna wakati tunapata fedha nyingi,badala ya kuwekeza tunafuja kwa pombe na wanawake,hivyo almasi inaweza kuwa muda wa ujana na pindi almasi itakapoisha na wakati huo huna kitu ndipo kila mtu atakuwa kinyume nawe....Almasi sio tu Diamondi Platnumz ila ni fumbo na picha kubwa ya maisha ya ujana na uwekezaji kuhusu kesho yetu.
Watoto mnasikiliza hii ngoma mwaka 3000, huyu Jamaa zetu tulimfanya shule ngoma zake kadhaa tulitumia kutongozea mademu
Wakwanza naombeni like zangu Kam unamkubali black maradona
Hii ngma c kwa dis track kwa mond ila hii ngma inazungumzia maisha ya bnadam yoyote alie na nafuh ya maisha kwa mda furan na kushndwa kufanya v2 vya mana kma wakina mack muga
Yaan huyu mjumbe wetu angekua mtu wa mitandao ya kijamii basi hakuna msanii wa hip hop angekua anasikika,,huyu ni genius ,anakuandikia,anakuimbia na anakusimulia,dizasta vina👐
Ii Lesson inaenda kwa Mr Almass mwenyew ama?
Mashabiki wa diamond platnumz hamjambo😂
Mimi ni shabiki mkubwa wa dizasta na alichonifuraisha ni kwamba yupo one man army na huku akijua kuwa kwenye muzik industry ya Tanzania uwezi toboa bila kumhusisha diamond kwenye muzik wako kikubwa tutambue kuwa tumebarikiwa kupata rapper km dizasta lakini pia MUNGU amutupa zawadi kubwa sana kwa kumuumba diamond akiwa mtanzania ili kuwa msaada kwa vijana wa kitanzania kwa maana hii ngoma ya dizasta itakuwa kubwa kuliko zote kwakuwa diamond amehusishwa hapa MUNGU ibariki Tanzania mungu mbariki dizasta lakini MUNGU akubariki kwa ukubwa zaidi DIAMOND PLATNUMZ ili uendelee kuwa daraja kwa watanzania
Kwani hii ngoma ni special kwa Diamond Platnumz?!
Wasanii tumechanwa tuelimike
HII NGOMA NI MOJA KWA MOJA INAMLENGA DIAMOND PLUTNUMZ😂😂😂 AISEEE NOMAAA...
This guy is a genius🫡..
amemzungumzia diamond platnm ,,,,hakumtaja ila ameeka diamond
Rapcha mavi umesikia mistar kutoka kwa kichwa timamu yani haya maneno ni chakula cha ubongo %
Leo nakuwa viewer wa kwanza, piteni na kwangu🤐
hii ngoma inamuhusu diamond platnumz
Hakuna mayooyoo humu, n mawe tupu!! Dizasta Vina n Robot lakuandika, ama n Jini flani hv ambaye anatoka Dunia ya mbali huko ujinini kuja kutuelekeza duniani
Kaa ameambiwa chid kwa namna Fulani hivi
Ngoma yakitambo sana ila kama mpya asee siichokagi