Mashishanga atimiza 90 akikumbuka migogoro ya ardhi Moro

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 6 ก.ย. 2024
  • Steven Mashishanga ni kati ya wanasisasa wakongwe nchini ambao watakumbukwa kwa mchango wao katika utumishi wa umma, hasa katika nafasi ya mkuu wa mkoa aliyoitumikia wakati wa Serikali ya awamu ya tatu chini ya Hayati Benjamin Mkapa.
    Amefanya kazi kama mkuu wa mkoa kwenye mikoa tofauti, ikiwamo ya Tabora (1995 - 1999), Mwanza (1999 - 2003) na Morogoro (2003 - 2006) kabla ya kustaafu utumishi wa umma akiwa na umri wa miaka 72.
    Mwanasiasa huyo mkongwe alipata umaarufu zaidi akiwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.
    Licha ya kuwa mzaliwa wa Shinyanga, aliamua kuweka makazi yake Morogoro kwa kuwa aliupenda mkoa huo kwa maelezo yake.
    Mwananchi imefanya mahojiano maalumu na Mashishanga ambaye Julai 27, mwaka huu anatimiza miaka 90, na katika mahojiano hayo, amezungumzia mambo mbalimbali, ikiwamo namna alivyopambana na migogoro baina ya wakulima na wafugaji mkoani Morogoro.
    Morogoro ni moja ya mikoa inayoongoza nchini kwa migogoro ya ardhi, ambayo kwa sehemu kubwa inahusisha wakulima na wafugaji ambao wamekuwa wakigombana hadi kuuana kwa sababu ya ardhi.
    Mashishanga anaeleza kwamba alipelekwa Mkoa wa Morogoro na Rais Mkapa kwa mambo makuu mawili; migogoro ya wakulima na wafugaji pamoja na elimu ambayo wakati huo Morogoro haikuwa vizuri.

ความคิดเห็น • 1

  • @eliasnganira7661
    @eliasnganira7661 หลายเดือนก่อน

    Kumbe bado yuko ? Amewahi kuwa mgeni rasmi mahafali yetu Kirumba TTC