Watatu wafariki kwa ajali Lindi, wapo mapadri wawili
ฝัง
- เผยแพร่เมื่อ 11 ก.ค. 2024
- Watu watatu wamefariki dunia wakiwemo mapadri wawili na wengine wawili kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wamepanda kupata ajali katika eneo la Mtama mkoani Lindi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi ACP, John Imori akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo Ijumaa Julai12, 2024 amesema kuwa ajali hiyo imetokea saa12.00 asubuhi katika eneo la Mtualonga Barabara ya Masasi -Mnazi Mmoja katika Halmashauri ya Mtamaa mkoani Lindi.
Amesema gari aina ya Mitsubishi Outlander iliyokuwa ikitokea Ndanda kuelekea jijini Dar es Salam ililipiga shimo na kupoteza mwelekeo na kuacha njia kisha kutumbukia kwenye shimo la karavati na kusababisha vifo na majeruhi wawili.
Kamanda Imori amewataja waliofariki kuwa ni Cornelius Modoe (55), Padri wa Kanisa Katoliki wa jijini Dar es Salaam, Pius Boa (51) na Padri wa Kanisa Katoliki na mkazi wa Tanga Haphymark Mkenda (51).
Imeandikwa na Bahati Mwatesa
Mungu awapokee kwake watumishi wake na majeruhi wapate matibabu na wapone haraka. Pole kwa kanisa Katoliki kwa kuondokewa na watenda kazi wake
Polen Sana mapadre wetu kwa kuondokewa na watumidhi mungu azilaze roho za marehemu mahala pema pepon Amina😭😭😭
DAH AISEE R.I.P MAPADRI WETU 😭😭😭😭😭
Eeh Mungu turehemu, Wapumzishe Roho za marehemu salama na uwapunguzie adhabu ya kaburi.Poleni sana ndugu wa marehemu Mungu awatie nguvu kwa kipindi hiki kigumu mnachopitia.
Inalilaahi wainalilah rajighun polen jaman wanafamilia pamoja na jamaa zenu wote walio fariki😢😢😢
Sisi sote ni wa mwenyezi Mungu na kwake tutarejea ubarikiwe sana kwa pole yako 😭😭😭
Wapumzike Kwa aman
Yesuuu wangu wabariki wote
Jamani da siamin macho yangu
Pumzikeni kwa Amani ndugu zetu
Jamani dah paroko zangu 😢😢😢😢😢😢😢😢😢😢
RIP Wapendwa wetu
Mwaka wa mapadre huu