CHALAMILA AWA MBOGO SAKATA LA WAFANYABIASHARA KARIAKOO, ATAKA MAJINA 891 YAFUTWE

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 11 ก.ค. 2024
  • Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Albert Chalamila ameagiza kuondolewa majina 891 ya wafanyabiashara yaliyowekwa kwenye mtandao wa Shirika la Masoko Kariakoo mpaka pale vyombo vya dola vitakapojiridhisha na majina hayo.
    Hatua hiyo inakuja baada ya wafanyabiashara zaidi ya 800 waliokuwepo sokoni hapo kabla ya soko kuungua Julai 2021 kuandamana jana Alhamisi, Julai 11, 2024 kwenda Ofisi za CCM Lumumba kupinga kutorejeshwa.
    Katika orodha hiyo, wafanyabiashara 891 kati ya 1,861 ndio walioelezwa kuwa na vigezo vya kurejea. Uamuzi huo uliwafanya kujitokeza katika viwanja vya Mnazi Moja kuhakikiwa na baada ya kutoridhishwa ndio wakaandamana.
    Chalamila ametoa maagizo hayo leo Ijumaa Julai 12, 2024, alipozungima na uongozi wa Shirika la Masoko Kariakoo katika Ofisi ya Shirika la Masoko Magogoni.

ความคิดเห็น • 14

  • @binsherbal6089
    @binsherbal6089 24 วันที่ผ่านมา +5

    Hebu nyoosha maneno, Rais amelipa!!!??? Hapo hapo unasema ni Kodi zetu walalahoi!!!??? Amelipa Rais au tumelipa sisi? Hii kauli inakera sana, Kila kitu Rais kafanya Rais kafanya Rais anatoa wapi pesa? Mbona mambo yakiharibika hamsemi kama Rais kaharibu? Kila kitu ni Uchawa tu siku hizi.

  • @hamidabarraball3162
    @hamidabarraball3162 24 วันที่ผ่านมา +3

    Yaani kila kiongozi akitoa hutuba lazima amtaje rais zaidi ya mara kumi, inatia aibu sana, tunaona nchi za wenzetu raisi hasifiwi kiasi hicho

  • @user-hi8le2vb7z
    @user-hi8le2vb7z 24 วันที่ผ่านมา +1

    leo ajastua leo😊

  • @gmdigitostore8550
    @gmdigitostore8550 24 วันที่ผ่านมา

    Hapo safi. Kibano hicho.

  • @hudhaifamsafiri8731
    @hudhaifamsafiri8731 24 วันที่ผ่านมา +1

    Kwan wakuu wetu hawawezi kufanya kazi bila kumuusisha Raisi

  • @maimunaathumani9121
    @maimunaathumani9121 24 วันที่ผ่านมา

    Kweli mkuu wengine pale kariakoo walisishana familia zima sisi twende wapi

  • @GeorgeSikazwe-mm7nn
    @GeorgeSikazwe-mm7nn 24 วันที่ผ่านมา

    😂 hii nchi bhn..serikali nd inalipa ww

  • @faustinluambano2958
    @faustinluambano2958 24 วันที่ผ่านมา

    Huyu naye.

  • @user-xk7vy4gb6g
    @user-xk7vy4gb6g 24 วันที่ผ่านมา

    Soko la ccm hilo

  • @user-tn7ic2ky3i
    @user-tn7ic2ky3i 24 วันที่ผ่านมา

    Aneye lipa ni Samiya ao ni serikali acha uchawa

  • @mbwanakiting7180
    @mbwanakiting7180 24 วันที่ผ่านมา

    Tuliambiwa pesa katoa maamaa na serikalli sasa shirika limeweka mtaji gani?

  • @evamacha4861
    @evamacha4861 24 วันที่ผ่านมา

    Mkuu wa mkoa nadhani unakumbuka soko la.mbagala zakgiem ulituuza sana kwa kutudanganya kuwa ukiona kuna mafisadi lakini ulitudanganya soko la zakhiem uliweka wafanyabiashara wapya badala ya wale waliopisha soko kujengwa.ulifanya dhambi kubwa sana bado tunalia machozi ya damu na mungu pekee ndio natafuta machozi yetu.

  • @hebronmwamwaja7660
    @hebronmwamwaja7660 24 วันที่ผ่านมา

    Siyo ameripa tumeripa acheni ayo mambo ya uchawa tumeripa

    • @edsonnelson4464
      @edsonnelson4464 24 วันที่ผ่านมา

      Amelipa tumelipa au tutalipa tusiharibiane kiswahili