AFRICA LIVE JUMATATU 28.O8.2O2O

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 16 ต.ค. 2024
  • RWANDA SCHOOLS REOPENING
    Serikali ya Rwanda imesema shule zote zitafunguliwa ifikapo mwezi Novemba mwaka huu.
    Kwa mujibu wa Waziri wa Elimu Valentine Uwamariya uamuzi wakufungua shule utaanza na Vyuo Vikuu.
    Uwamaria amesema kwamba shule zitafungua kwa awamu tofauti kuanzia ngazi ya Vyuo Vikuu ambavyo vitafungua milango mwezi ujao.
    Wizara ya Elimu inasema shule zitatakiwa kuzingatia masharti yaliyopo ya kujilinda na Covid -19 kama kuwa na sehemu ya kuosha mikono, kuvaa barakoa kwa kila mwanafunzi na kuacha nafasi ya mita moja kati ya wanafunzi.
    THESSANIKI
    Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Mike Pompeo, amefanya mazungumzo na mwenzake wa Ugiriki Nikos Dendias, wakati kuna mgogoro kati wa Ugiriki na Uturuki.
    Pompeo na Dendia wamekutana katika hoteli moja mjini Thessaniki, kaskazini mwa Ugiriki ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku mbili nchini humo.
    Anatarajiwa pia kufanya mazungumzo na waziri mkuu wa Ugiriki Kyriakos Mitsotakis.
    Taarifa iliyotolewa baada ya mkutano huo inataka migogoro ya mashariki mwa bahari ya Mediteranua, inastahili kusuluhishwa kwa njia ya amani kulingana kwa kuzingatia sheria ya kimataifa.
    HARARE
    Kundi la madaktari 10 kutoka China limewasili nchini Zimbabwe kusaidia nchi hiyo kupambana na janga la virusi vya .
    Madaktari hao watahudumu katika hospitali za Parirenyatwa kwa miezi 12 zijazo,kwa mujibu wa ripotiya gazeti la serikali la Herald.
    Mkuu wa madaktari hao, Dkt Luo Weiqiang, amenukuliwa akisema madaktari hao pia watanadi tiba asilia kutoka.
    London
    Kampuni ya uchukuzi ya Uber imeshinda kesi iliyokuwa imefunguliwa dhidi yake mjini London, Uingereza, kuhusu usalama wa huduma yake, na kuruhusiwa kuendelea na shuguli zake.
    Jaji aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo amesema kwamba kampuni hiyo haina matatizo yoyote na kwamba ni salama kwa usafiri.
    Mamlaka ya usafiri mjini London -TFL, ilikataa kutoa leseni kwa kampuni ya usafiri ya Uber, mwaka 2019 kutokana na kile kilitajwa kama kutokuwa salama, lakini Uber imesema kwamba imetatua wasiwasi uliokuwepo kuhusu bima na utambuzi wa dereva.
    NEW Delhi
    Maandamano ya wakulima yameongezeka katika sehemu kadhaa nchini India, kupinga sera ya serikali ya waziri mkuu Nrendra Modi kuhusu sekta ya kilimo, polisi wakiwakamata na kuwazuilia waandamanaji kadhaa katika mji mkuu wa New Delhi.
    Polisi wamekamata na kuwazuiliwa wanachama kadhaa wa chama cha upinzani cha kikomunisti waliokuwa wanashiriki maandamano hayo.
    Waandamanaji wamechoka trekta na sanamu za waziri mkuu Narendra Modi, wakipinga miswada inayowaruhusu wakulima kuuza mazao yao kwa mashirika makubwa na maduka ya jumla.
    Wanapinga miswada hiyo kwa msingi kwamba itapelekea Serikali kuacha kununua mazao yao huku mashirika binafsi yakiwa na mamlaka ya kununua kwa bei ya chini.

ความคิดเห็น •