REV. DR. ELIONA KIMARO: NIDHAMU BINAFSI

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 23 ต.ค. 2023
  • IBADA YA EVENING GLORY - THE SCHOOL OF HEALING - 23 OCT 2023.
    KICHWA CHA SOMO : KUENDELEA TOKA NGUVU HATA NGUVU.
    '' FROM STRENGTH TO STRENGTH ''
    Zaburi 84 : 7
    Zaburi 84 : 7
    7 Huendelea toka nguvu hata nguvu, Huonekana Sayuni kila mmoja mbele za Mungu.
    1.NIDHAMU BINAFSI ( SELF DISCIPLINE )
    1 Samweli 13 : 5 - 14
    1 Samweli 15 : 10 - 31
    2 Wafalme 5 : 20 - 27

    1 Samweli 13 : 5 - 14
    5 Nao Wafilisti wakakusanyana ili wapigane na Waisraeli, magari thelathini elfu, na wapanda farasi sita elfu, na watu kama mchanga ulio ufuoni mwa bahari kwa wingi wao; wakapanda juu, wakapiga kambi yao katika Mikmashi, upande wa mashariki wa Beth-aveni.
    6 Hata Waisraeli walipoona ya kuwa wa katika dhiki, (maana watu walifadhaishwa), ndipo hao watu wakajificha katika mapango, na katika vichaka, na katika miamba, na katika mashimo, na katika mabirika.
    7 Hata baadhi ya Waebrania walivuka Yordani, wakaingia nchi ya Gadi na Gileadi; lakini Sauli alikuwa akaliko huko Gilgali, nao watu wote wakamfuata wakitetemeka.
    8 Akangoja siku saba, kwa kadiri ya muhula uliowekwa na Samweli lakini Samweli hakuja Gilgali; na hao watu wakatawanyika mbali naye.
    9 Sauli akasema, Nileteeni hapa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani. Akaitoa sadaka ya kuteketezwa.
    10 Hata mara alipokwisha kuitoa hiyo sadaka ya kuteketezwa, kumbe! Samweli akatokea. Naye Sauli akatoka kwenda kumlaki na kumsalimu.
    11 Samweli akasema, Umefanya nini? Naye Sauli akasema, Ni kwa sababu naliona ya kuwa watu wanatawanyika mbali nami, na wewe hukuja siku zile zilizonenwa; nao Wafilisti wamekusanyika pamoja huko Mikmashi;
    12 basi nikasema, Wafilisti watanishukia sasa mpaka Gilgali, kabla sijaomba fadhili za Bwana; kwa hiyo nalijishurutisha, nikatoa sadaka ya kuteketezwa.
    13 Naye Samweli akamwambia Sauli, Umefanya upumbavu; hukuishika amri ya Bwana, Mungu wako, aliyokuamuru; kwa maana Bwana angaliufanya ufalme wako kuwa imara juu ya Israeli milele.
    14 Lakini sasa ufalme wako hautadumu; Bwana amejitafutia mtu aupendezaye moyo wake, naye Bwana amemwamuru yeye kuwa mkuu juu ya watu wake, kwa sababu wewe hukulishika neno lile Bwana alilokuamuru.
    1 Samweli 15 : 10 - 31
    10 Ndipo neno la Bwana likamjia Samweli, kusema,
    11 Najuta kwa sababu nimemtawaza Sauli awe mfalme; maana amerudi nyuma, asinifuate, wala hakufanya nilivyomwamuru. Samweli akasikitika, akamlilia Bwana usiku kucha.
    12 Samweli akaondoka asubuhi na mapema ili aonane na Sauli; Samweli akaambiwa ya kwamba, Sauli alifika Karmeli, na tazama, akajisimamishia ukumbusho, akageuka, akapita, akatelemkia Gilgali.
    13 Samweli akamwendea Sauli; naye Sauli akamwambia, Ubarikiwe na Bwana, nimeitimiza amri ya Bwana.
    2 Wafalme 5 : 20 - 27
    20 Lakini Gehazi, mtumishi wa Elisha mtu wa Mungu, akasema, Tazama, bwana wangu amemwachilia huyo Naamani Mshami, asivipokee mikononi mwake vile vitu alivyovileta; kama Bwana aishivyo, mimi nitamfuata mbio, nipokee kitu kwake.
    21 Basi Gehazi akamfuata Naamani. Naye Naamani, alipoona mtu apigaye mbio anakuja nyuma yake, alishuka garini amlaki, akasema, Je! Ni amani?
    Mhubiri : Rev.Dr. Eliona Kimaro
    Kwa maoni na ushauri:
    Mch. kiongozi: Dr. Eliona Kimaro
    Simu: +255 655 516 053, +255 754 516 053

ความคิดเห็น • 8

  • @Victoria-bv6xu
    @Victoria-bv6xu 2 วันที่ผ่านมา

    Ameni😘

  • @jasminejocta1734
    @jasminejocta1734 5 หลายเดือนก่อน

    Nabarikiwa Sana nawe mch kimaro

  • @vickyadrian1503
    @vickyadrian1503 9 หลายเดือนก่อน +1

    Ameeen

  • @abbymagospel6904
    @abbymagospel6904 9 หลายเดือนก่อน

    Ubarikiwe baba mtumish 🙏🏿

  • @felsonsanga8502
    @felsonsanga8502 9 หลายเดือนก่อน

    Ameeeeen

  • @felistermoshi5852
    @felistermoshi5852 8 หลายเดือนก่อน

    Amen Mtumishi Barikiwa

  • @josephlukumaya4223
    @josephlukumaya4223 9 หลายเดือนก่อน

    Amen

    • @user-kb1te1ze1b
      @user-kb1te1ze1b 9 หลายเดือนก่อน +1

      Ubalikiwe mtumishi maana mung amekupa kipawa Cha kuku balika mbele za watu