REV. DR. ELIONA KIMARO: MANENO YA WATU

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 15 พ.ย. 2023
  • KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH - IBADA YA EVERNING GLORY - THE SCHOOL OF HEALING - 13/11/2023.
    KICHWA CHA SOMO: KUSUDI LA KUWEPO"
    "A SENSE OF PURPOSE"
    NENO KUU
    UNAFANYA NINI HAPA?
    WHAT ARE YOU DOING HERE?
    NYI - KYIKYI UWUTA IHA?
    1 Wafalme 19 : 9
    UNAFANYA NINI HAPA?
    SHAMBULIO LA KUSUDI LA KUWEPO KATIKA MAISHA YAKO
    (A SENSE OF PURPOSE ATTACK)
    ''MANENO YA WATU''
    ZUIO LA MAWAZO MAPYA NA SAHIHI
    Zaburi 69 : 20
    Hesabu 14 : 1 - 38
    Zaburi 69 : 20
    20 Laumu imenivunja moyo, Nami ninaugua sana. Nikangoja aje wa kunihurumia, wala hakuna; Na wa kunifariji, wala sikumwona mtu.
    Hesabu 14 : 1 - 38
    1 Mkutano wote wakapaza sauti zao wakalia; watu wakatoka machozi usiku ule.
    2 Kisha wana wa Israeli wote wakamnung'unikia Musa na Haruni; mkutano wote wakawaambia, Ingekuwa heri kama tungalikufa katika nchi ya Misri, au, ingekuwa heri kama tungalikufa katika jangwa hili.
    3 Mbona Bwana anatuleta mpaka nchi hii ili tuanguke kwa upanga? Wake zetu na watoto wetu watakuwa mateka; je! Si afadhali turudi Misri?
    4 Wakaambiana, Na tumweke mtu mmoja awe akida, tukarudi Misri.
    5 Ndipo Musa na Haruni wakaanguka kifudifudi mbele ya mkutano wa kusanyiko la wana wa Israeli.
    6 Na Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune, waliokuwa miongoni mwao walioipeleleza nchi, wakararua nguo zao;
    7 wakanena na mkutano wote wa wana wa Israeli wakasema, Nchi ile tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi njema mno ya ajabu.
    8 Ikiwa Bwana anatufurahia, atatuingiza katika nchi hii atupe iwe yetu, nayo ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali.
    9 Lakini msimwasi Bwana, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye Bwana yu pamoja nasi; msiwaogope.
    10 Lakini mkutano wote wakaamuru wapigwe kwa mawe. Ndipo utukufu wa Bwana ukaonekana katika hema ya kukutania, mbele ya wana wa Israeli wote.
    11 Bwana akamwuliza Musa, Je! Watu hawa watanidharau hata lini? Wasiniamini hata lini? Nijapokuwa nimefanya ishara hizo zote kati yao.
    12 Nitawapiga kwa tauni, na kuwaondolea urithi wao, nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, kisha yenye nguvu kuliko wao.
    13 Basi Musa akamwambia Bwana, Ndipo Wamisri watasikia habari hiyo; kwa kuwa wewe uliwaleta watu hawa kwa uweza wako, kutoka kati yao;
    14 kisha watawaambia wenyeji wa nchi hii; wamesikia wao ya kuwa wewe Bwana u kati ya watu hawa; maana, wewe Bwana waonekana uso kwa uso, na wingu lako lasimama juu yao, kisha wewe watangulia mbele yao, katika nguzo ya wingu mchana, na katika nguzo ya moto usiku.
    15 Basi kama wewe ukiwaua watu hawa mfano wa mtu mmoja, ndipo mataifa yaliyosikia habari za sifa zako watakaponena na kusema,
    16 Ni kwa sababu yeye Bwana hakuweza kuwaleta watu hao kuwatia katika nchi aliyowaapia, kwa ajili ya hayo amewaua nyikani.
    17 Basi sasa nakusihi sana, uweza wa Bwana wangu na uwe mkuu, kama ulivyonena, uliposema,
    18 Bwana ni mpole wa hasira, mwingi wa rehema, mwenye kusamehe uovu na makosa, naye hatamfanya mwenye hatia kuwa hana makosa kwa njia yo yote; mwenye kuwapatiliza wana kwa uovu wa baba zao, katika kizazi cha tatu na cha nne.
    19 Nakusihi, usamehe uovu wa watu hawa, kama ukuu wa rehema yako ulivyo, kama ulivyowasamehe watu hawa, tangu huko Misri hata hivi sasa.
    20 Bwana akasema, Mimi nimewasamehe kama neno lako lilivyokuwa;
    21 lakini hakika yangu, kama niishivyo, tena kama dunia hii nzima itakavyojawa na utukufu wa Bwana;
    22 kwa sababu watu hawa wote, ambao wameuona utukufu wangu na ishara zangu, nilizozitenda huko Misri, na huko jangwani, pamoja na haya wamenijaribu mara hizi kumi, wala hawakuisikiza sauti yangu;
    23 hakika yangu hawataiona hiyo nchi niliyowaapia baba zao, wala katika hao wote walionidharau hapana atakayeiona;
    24 lakini mtumishi wangu Kalebu, kwa kuwa alikuwa na roho nyingine ndani yake, naye ameniandama kwa moyo wote, nitamleta yeye mpaka nchi hiyo aliyoingia; na uzao wake wataimiliki.
    25 Basi Mwamaleki na Mkanaani wakaa katika bonde; kesho geukeni, mkaende jangwani kwa njia iendayo Bahari ya Shamu.

    Mhubiri : Rev. Dkt. Eliona Kimaro
    Kwa maombi na ushauri :
    Mch. Kiongozi: Dr. Eliona Kimaro
    Simu: +255 655 516 053, +255 754 516 053

ความคิดเห็น • 22

  • @vailethkisija5619
    @vailethkisija5619 หลายเดือนก่อน +2

    Ee Mungu unijalie kuchagua kutenda vyema Amina

  • @mankaobedi5969
    @mankaobedi5969 8 วันที่ผ่านมา +1

    Barikiwa sana...mtumishi, nabarikiwa saana ninaposikiliza mafundisho yako💯💯💯💯💯

  • @venasjastinvenasjastinedes9754
    @venasjastinvenasjastinedes9754 5 หลายเดือนก่อน +2

    Aminaaa mtumishi neno lako limenijenga sana nimebadilika kuanzia ssa

  • @user-yz5zn4tr6i
    @user-yz5zn4tr6i 14 วันที่ผ่านมา

    Eee Mungu unijalie mema na uniepushe na maneno mabaya

  • @PATRICIAMBIGIJA
    @PATRICIAMBIGIJA หลายเดือนก่อน

    Amina mtumishi

  • @GOZBERTMTASINGWA
    @GOZBERTMTASINGWA 4 หลายเดือนก่อน +1

    Nitafika Kwa jina la Bwana wetu YESU kristo

  • @mankaobedi5969
    @mankaobedi5969 8 วันที่ผ่านมา

    Sema mtumishi tuponeee

  • @theresiandunguru2717
    @theresiandunguru2717 8 หลายเดือนก่อน +1

    Ubarikiwe sana mchungaji

  • @marikwilliam9886
    @marikwilliam9886 7 หลายเดือนก่อน +1

    Be blessed always

  • @user-cg6oj2nn5v
    @user-cg6oj2nn5v 6 หลายเดือนก่อน

    Aminaa

  • @lovenessrichard
    @lovenessrichard 6 หลายเดือนก่อน

    Amen

  • @faridajoyce3181
    @faridajoyce3181 8 หลายเดือนก่อน

    Ameeen 🙏Asanteesana

  • @claudiamartin9607
    @claudiamartin9607 8 หลายเดือนก่อน

    Nabarikiwa sana

  • @amosziro7054
    @amosziro7054 7 หลายเดือนก่อน

    Limenijenga hilo neno

  • @user-th5xz1fg5t
    @user-th5xz1fg5t 8 หลายเดือนก่อน

    amen mung uwe nami

  • @veronicasarita8422
    @veronicasarita8422 8 หลายเดือนก่อน

    Amen hakika Mungu Yu pamoja nasi

  • @TeresastephanoTushabe-gj6ng
    @TeresastephanoTushabe-gj6ng 8 หลายเดือนก่อน

    Mungu akutienguvu milele ne uzidi kustawi sana

  • @josephlukumaya4223
    @josephlukumaya4223 8 หลายเดือนก่อน

    Amen kubwa

  • @amosziro7054
    @amosziro7054 8 หลายเดือนก่อน

    Waaaa...nimejengeka

  • @user-it5gj7ls8t
    @user-it5gj7ls8t 8 หลายเดือนก่อน

    Amen 🙏

  • @PATRICIAMBIGIJA
    @PATRICIAMBIGIJA หลายเดือนก่อน

    Amina mtumishi