FAIDA ZA UHIFADHI ‖ MSITU WA ASILI CHENENE .

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 5 ก.ย. 2022
  • Msitu wa asili chenene unapatikana mkoani Dodoma na unaukubwa wa hekta 27,628. Awali ulitangazwa kuwa msitu wa hifadhi mwaka 1989.
    Wakazi wanaozunguka hifadhi za msitu huu wananufaika kwa kupata dawa za asili kutoka kwenye uoto wa miti mbalimabali kama mtalawanda kwaajili ya matatizo ya kifua, muagulula kwa matitizo ya tumbo na malaria,msokonoi, mhakachuma na mingine mingi ikiwa ni matokeo ya uhifadhi wa misitu ya asili.
    kabla ya usimamizi wa wakala wa huduma za misitu Tanzania (TFS) kwenye shamba hili kulikuwa na ukataji miti hovyo,ukame, njaa, miti midogo na madhara mengine mengi.
    Elimu iliyotolewa na wakala wa huduma za misitu Tanzania imewasaidia wakazi hawa kuutunza msitu huu na wamenufaika kwa kiasi kikubwa ikiwa ni pamoja na kuwa na mabadiliko ya hali ya hewa, mvua nyingi, uwepo wa chemchem za maji vilevile wameweza kujikita kwenye kilimo na ufugaji.
    Kutokana na shughuli za uhifadhi zinazofanyika katika shamba hili wawekezaji wanakaribishwa kutumia fursa hizi za kitalii ambazo haziathiri mazingira kama kuwekeza kwenye mahoteli na kambi za utalii hasa kwenye sehemu ambazo ni kame ili kuwavutia watalii kutembelea maeneo haya.

ความคิดเห็น •