#TBCDIGITAL

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 21 ส.ค. 2024
  • Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amesema serikali inaendelea kutilia mkazo marejesho ya mikopo kwa wanufaika waliopata ajira kuhakikisha wanarudisha fedha kwa ajili ya wengine nao kunufaika kama walivyonufaika wao.
    Akizungumza Bungeni Dodoma leo Aprili 15, 2024, Mkenda amewaambia wabunge, hata hivyo, kwamba Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inaendelea na mkakati maalumu wa kuhakikisha ongezeko la marejesho linakuwa kubwa.
    Katika hatua nyingine Waziri ameiagiza Bodi hiyo ya Mikopo kuhakikisha wanaweka wazi vigezo vya waombaji wa mikopo ili kuondoa aina yoyote ya upenyo usio halali wa mwanafunzi kupata mkopo wakati hastahili.
    ✍🏾 @clementsilla
    #BungelaBajeti #Bungeni #TBCdigital #TBCupdates

ความคิดเห็น •