AI in Swahili

แชร์
ฝัง

ความคิดเห็น • 7

  • @rahimfaraji6916
    @rahimfaraji6916 6 หลายเดือนก่อน

    Kubadilisha maneno au majina kwenye technology si sahihi ni Bora yatamkwe kwa lugha yake ya asili,

    • @afrikaimara
      @afrikaimara  6 หลายเดือนก่อน +1

      Asante @rahimfaraji6916 kwa maoni yako. Umuhimu wa kutafsiri ni kusaidia mtu ambaye haelewi kitu kinachozungumziwa kwa lugha fulani aweze kuielewa kutumia lugha ambayo anijua na kuizungumza. Zaidi ya hayo, lugha ndio njia tunayotumia kuzungumza na kuelewana. Hivyo basi, kutafsiri majina ya kiteknolojia ni kwa hiyari yetu kwani itatusaidia katika mazungumzo na mijadala. Lugha ya kiswahili ni yetu na ni wajibu wetu kuiboresha na kuitajirisha. Hamna hatia yoyote ya kutafsiri majina ya kiteknolojia kutoka kwa lugha ya kimombo kuja kwa kiswahili. Pia wazungu hutafsiri majina hayo hayo kutoka lugha zingine kama vile kijerumani au kifaransa. Je, unajua Albert Einstein alikua mjerumani? Mbona hatusomi vumbuzi zake kwa lugha ya kijerumani? Tafakari.

    • @rahimfaraji6916
      @rahimfaraji6916 6 หลายเดือนก่อน

      @@afrikaimara kutafsiri ni kitu tofauti na kubadilisha jina la kitu, (mf. Laptop = kompyuta mpakato) hii si tafsiri ni kubadilisha jina la kitu, haya majina mengine ni kifupi Cha maneno flani hivyo kubadilisha jina utaondoa maana halisi ya mfululizo wa ubunifu wa hilo jina, hivyo tafsiri itolewe kwa lugha yetu na tafsiri kieleza maana ya kitu na kazi zake hii ndio tafsiri, (mf. Computer hii neno Kila herufi ina kirefu chake kubadilisha jina ama namba ya uandishi utaliondoa kwenye uhalisia wake) ndio maana Kuna kitu kinaitwa kutohoa,

    • @rahimfaraji6916
      @rahimfaraji6916 6 หลายเดือนก่อน

      @@afrikaimara Asili ya majina kwenye technology ni kifupi cha maneno flani mf. computer ni kifupi cha maneno hinyo kubadilisha jina liwe kwa lugha nyingine au kuandika maandishi tofauti na asili yake ni kupoteza maana ya kitu husika, ndio maana kuna neno kutohoa, kinachohitajika ni kutafsiri maana, kazi yake na malengo ya kitu husika.

    • @afrikaimara
      @afrikaimara  6 หลายเดือนก่อน

      @@rahimfaraji6916 Natumai nimeelewa unachokizungumzia, lakini nadhania mtazamo wako unwezanyima nafasi watu ambao hawajui lugha nyingine kuelewa kinchozungumziwa na wenye hio lugha. Pia ni wazo langu kua ni juhudi ya kila watumizi wa lugha kujaribu kutafuta njia za kurahisisha mawasiliano kati yao. Unapofanya tafsiri, si vyema kutopoteza maana ya neno linalotafsiriwa, lakini mara nyingi hatuwezi kukua wakamilifu. Majina ya vumbuzi za kitecknolojia ni majina mageni na mara mingi ni majina yanyo tokana na majina mengine tofauti. Mfano ulionipa ni ule wa 'computer' ambayo inapata jina lake kutoka kwa jina 'compute'. Ikiwa tunaweza tafsiri neno 'compute', mbona tusitafsiri pia computer? Natumai unaona hakuna kasoro inatokana na kufanya tafsiri ya majina ya kiteknolojia.

    • @rahimfaraji6916
      @rahimfaraji6916 6 หลายเดือนก่อน

      @@afrikaimara COMPUTER Full Form: COMPUTER Stands for Common Operating Machine Purposely Used for Technological and Educational
      Hata hili neno lina mfululizo katika uvumbuzi,
      NB. kitendo cha kubadilisha majina ya gun
      duzi katika technology kunasababisha fani kuwa ngumu kueleweka, sababu mtu saa ingine atalazimika kukariri majina tofauti ya kitu kimoja,
      Elewa hata sisi tukigundua tutakiita kwa lugha yetu pendwa aka KISWAHILI