Ambwene Mwasongwe - Nifundishe Kuomba (Official Music Video)

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 8 ก.ย. 2024
  • Ambwene Mwasongwe Presents the Music Video for "Nifundushe Kuomba"
    Maelezo ya wimbo wa Nifundishe Kuomba:
    Nifundishe kuomba ni neno lenye uhitaji wa mtu aliyeguswa na Roho Mtakatifu na akagundua kuna namna mambo hayaendi sawa kwa sababu mbalimbali.
    Unaweza kuwa unaomba lakini swali ni unaombaje? na ukigundua unaomba vibaya lazima urudi na umuombe akufundishe kuomba ili uombe sawasawa na mapenzi yake.
    Upande wangu niliomba nifundishwe kuomba nikiwa na mahusiano ya ndani sana na ya karibu ili kuomba kwangu kusizuiliwe.
    Ni wimbo wa baraka ambao natamani unaposikia upate neema ya kufundishwa kuomba pia.
    Watch All Music Videos by Ambwene Mwasongwe: • Ambwene Mwasongwe All ...
    Follow Ambwene Mwasongwe
    Instagram: / ambwenemwasongwe_
    Subscribe to Ambwene Mwasongwe: / @ambweneobadiamwasongwe
    Digital Branding & Marketing By:
    Black Ozen Entertainment Limited: / blackozenentertainment...
    Ambwene Mwasongwe - Nifundishe Kuomba (Lyrics)
    Jina lako messiah
    Hili ni ombi langu,
    Nifundishe kuomba
    Nifundishe kunena,
    Nifundishe kiasi
    Nifundishe imani ya
    Matendo, nipe moyo wa toba
    Nautaka uwepo unakoishi
    , Ambako wewe ni kichwa
    Cha kanisa.
    Nazitaka nguvu
    Ulizonazo wewe,
    Ninataka upako
    Maneno yangu, matendo
    Yangu, tabia yangu,
    Zifanane na hisia zako.
    Nikitembea nitembee
    Na wewe Yesu,
    Ninataka kushinda aaaiii
    Nami nakusalute
    Eeeh master
    Ninakuimbia wimbo,
    Ninapaza sauti
    Nami na kusifu,
    Kuhani wa ubora.
    Mmiliki halali kwa
    Agano la neem.
    Jina lako ni messiah
    Hili ni ombi langu,
    Nifundishe kuomba
    Nifundishe kunena,
    Nifundishe kiasi
    Nifundishe imani ya
    Matendo, nipe
    Moyo wa toba
    Ndani ya moyo
    Wangu, ninataka
    Uishi wewe bwana
    Wa wema
    Uewezae kuuzuia
    Ulimi wangu,
    Usinene sawasawa
    Na hasira zangu
    Uewezae kuituliza
    Akili yangu,
    Isichanganyikiwe
    Wakati wa raha
    Uwezae kunituliza
    Wakati wa shida na
    Matatizo.
    Wakati wengine
    Wakimbiapo, ukanipe
    Jibu la mbio zao.
    Nguvu yako ikanizuie
    Kwenda pale hakuna
    Awezae niona,
    Pale ambapo
    Hayupo awezae
    Sema acha, neno
    Lako likanizuie kufanya.
    Neema yako
    Ikanifanye kupakua
    Chakula tofautu
    Na njaa yangu.
    Kule nisikoweza
    Kwenda mchana,
    Nisaidie nisiende usiku.
    Yale nisiyoweza
    Sema hadharani,
    Nisiseme gizani.
    Nautaka uso wako
    Kama wa chuma
    Vinyamkela wasioweza
    Kuustahimili.
    Naitaka lugha ya
    Kimbingu, isiyoneneka
    Isiyonenwa na mtu.
    Natamani mbingu
    Za mbingu kwenye
    Neema, kule Paulo
    Alipoogelea nguvu zako.
    Nikitembea, nitembee
    Na wewe Yesu.
    Ninataka kushinda aaaaiiii
    Nitakanyaga mahali waoga hawapawezi.
    Nitafanya ubabe
    Kwenye ulimwengu
    Wa roho
    Nitapitisha mkong'oto
    Kwenye mikwamo.
    Nitaonyesha jeuri
    Kwa shetani
    Maana ufalme
    Nauteka oooo
    Unatekwa na wenye
    Nguvu aiiiii
    Nami nakusalute
    Ninakuimbia wimbo,
    Ninapaza sauti
    Nami nakusifu,
    Kuhani wa ubora
    Mmiliki halali wa
    Agano la neema
    Jina lako ni Messiah
    Hili ni ni ombi langu,
    Nifundishe kuomba
    Nifundishe kunena,
    Nifundishe kiasi
    Nifundishe imani
    Ya matendo, nipe
    Moyo wa toba.
    #AmbweneMwasongwe #NifundisheKuomba

ความคิดเห็น • 434