DC MWANSASU "TUSIKAE NA FEDHA KWA KUZIFUKIA NDANI/NMB WAMEUPIGA MWINGI WAPO KWETU UYUI"

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 28 ส.ค. 2024
  • Mkuu wa wilaya ya Uyui mkoani Tabora ZAKARIA MWANSASU amewaonya Wananchi wa wilaya hiyo kuacha tabia ya kutunza fedha ndani ya nyumba zao na badala yake wazitunze kwenye taasisi za kifedha kwa usalama.
    Mwansasu ametoa rai hiyo wakati akizindua Benki ya NMB tawi la Uyui ambalo ni la kwanza kuanza kutoa huduma za kifedha tangu kuanzishwa kwa wilaya hiyo zaidi ya miaka kumi iliyopita.
    Mkuu huyo wa wilaya amesema kuanzishwa kwa huduma za kibenki kutachochea na kuharakisha maendeleo ya Wakazi wa wilaya ya Uyui, wilaya jirani na kutoa wito kwa Wafanyabiashara kuwekeza katika wilaya hiyo.
    Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Uyui SAID NTAHONDI ameagiza huduma zote za kifedha za Halmashauri zihamishiwe katika tawi hilo na kueleza kuwa miamala ya wilaya hiyo inafikia Bilioni 90 kwa mwaka.
    Katika taarifa yake, Meneja wa NMB tawi la Mihayo GEORGE FUNDI akimwakilisha Meneja wa Kanda ya Magharibi, amesema tawi la Uyui linaweza kutoa huduma zote za kibenki kama ilivyo kwa matawi mengine.
    Naye Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi wilaya ya Uyui LUBASHA MAKOBA amesema zimefanyika jitihada kubwa kupata huduma za kibenki katika wilaya hiyo.
    Kuanzishwa kwa NMB tawi la Uyui kunafanya Benki hiyo kuwa na huduma za kibenki katika wilaya zote saba za mkoa wa Tabora.
    #nmb #uyui #Tabora

ความคิดเห็น •