AHSANTE LYRICS - MERCY MASIKA & PAUL CLEMENT
ฝัง
- เผยแพร่เมื่อ 10 ต.ค. 2024
- 1 Wakorintho 1:9
Mungu ni mwaminifu ambaye mliitwa na yeye mwingie katika ushirika wa Mwanawe, Yesu Kristo Bwana wetu.
2 Wathesalonike 3:3
Lakini Bwana ni mwaminifu, atakayewafanya imara na kuwalinda na yule mwovu.
*Mercy Masika & Paul Clement - Ahsante Lyrics
*Lyrics By Partialyrics
SWAHILI LYRICS
Nauona uaminifu wako
Katika kila jambo
Kwa vile unavyotenda mema
Nauona uaminifu wako
Katika upendo wako
Kwa vile unavyopenda
Nauona uaminifu wako
Katika damu yako
Kwa vile unavyonena mema
Naiona neema yako
katika maisha yangu
kwa vile umeniweka vyema
Amani yako yatiririka
Ndiwe unijaliaye
kukaa vyema
Uaminifu wako watiririkia
Umenitia furaha moyoni mwangu
Umeniponya magonjwa
yangu yote
Ewe Yesu
Ukaukomboa uhai wangu
na kaburi
Ewe Yesu
Nashukuru
Asante kwa yaliyopita
na ya sasa umeyatimiza
wewe ni mwaminifu
Asante kwa yanayokuja
Naamini utayatimiza
wewe u mwaminifu
Nikitazama fadhili zako
Ninaona fikra zako
kwa namna unavyoniwazia
Na nikisema hunipendi
najidanganya mwenyewe
Na sijaona thamani ya
upendo wako
Uaminifu wako watimilika
Sababu jina lako ni mwaminifu
Mwaminifu ni Mungu
Mungu ni Mwaminifu
Uaminifu wako ni wa milele
Uaminifu wako haupimiki
kwa njia ya matendo yangu
Hata nikikosea haupimiki
kwa njia ya makosa yangu
Hata nikipatia haupimiki
kwa njia ya kuweza kwangu
Uaminifu wako unabaki
(Palepale palepale palepale)
Kwenye kiwango cha
uaminifu wako
Hee unabaki
(Palepale palepale palepale)
Asante kwa yaliyopita
na ya sasa umeyatimiza
wewe ni mwaminifu
Asante kwa yanayokuja
Naamini utayatimiza
wewe u mwaminifu
Uaminifu wako
Ee Bwana
Wadumu milele hata milele
#paulclement
#mercymasika
@Ambmercymasika
@paulclement_
@partialyrics
❤❤❤
Thank you!
Be blessed
Can't get enough of this song
Be blessed as we thank God for everything
🥳🥳🥳🥳🥳🥳🥳🥳🥳🥳🥳
❤❤❤. Nice song.
❤️❤️❤️❤️