NIMEKUTUMAINI WEWE BWANA - KWAYA YA FAMILIA TAKATIFU
ฝัง
- เผยแพร่เมื่อ 29 ส.ค. 2024
- Tumsifu Yesu Kristu,
Tunaendelea kuwakaribisha kujipatia album yetu mpya ya video inayoitwa HERI KUCHAGUA JINA JEMA. Wimbo huu unaoitwa NIMEKUTUMAINI WEWE BWANA na kuimbwa na KWAYA YA FAMILIA TAKATIFU KUTOKA KANISA KUU LA MTAKATIFU YOSEFU JIMBO KUU LA DAR ES SALAAM (SAINT JOSEPH'S CATHEDRAL) ni utunzi wake marehemu JOSEPH MAKOYE ambaye ni mmoja kati ya watunzi mahiri sana katika nyanja hizi za mziki Mtakatifu Tanzania, baadhi ya nyimbo zingine alizotunga ni kama Hiki ni chakula na Subira ya Mkulima.
Album hii imesheheni nyimbo kemkem ambazo ni
1. Mfanyieni Bwana Shangwe - P.F Mwarabu
2. Aliyeacha nyumba - Celestine Kapama
3. Aleluya Mshukuruni Bwana - Charles Saasita
4. Gloria - Antonio Vivald
5. Heri kuchagua jina jema - Richard Mloka
6. Ave Maria - Bach/Gounod
7. Tufuate Mfano - Fortunatus B. Mallya
8. Miaka 150 ya Ukristo Tanzania - David Benjamin Wasonga
9. Mwimbieni Bwana - Celestine Kapama
10. Nimekutumaini - Joseph Makoye
Kwa mahitaji ya album hii wasiliana nasi kwa simu namba +255755816669/0659557769
MANENO YA WIMBO (MUSIC LYRICS)
NIMEKUTUMAINI - J. MAKOYE
Nimekutumaini wewe e Bwana, nimekutumaini wewe ee Bwana
Nimesema wewe u Mungu wangu, siku zangu zimo mikononi mwako
1. Nimekukimbilia wewe ee Bwana
Nisiaibike milele, kwa haki yako yako uniponye
2. Wewe ndiwe genge langu na ngome yangu
kwa ajili ya jina lako, uniongoze unichunge
3. Wewe ni nuru yangu unimulike
wewe ndiwe wokovu wangu, uniokoe na adui
Kwakweli mmebarikiwa sana , Mungu awape nguvu zaidi!
Mmeimba vizuri sana
Nimekutumaini wewe Ee Bwana, nimesema wewe u Mungu wangu siku zangu zipo mikononi mwako dahh bonge la ujumbe
Mmeimba vizuri hata mtunzi kajitaidi ila pia watunzi wajitaidi kutunga kama john mgandu naona bado sijaona mtunzi kama yeye
Nimeupenda huu wimbo sana. lakini nota zake nimesitafuta bila kufanikiwa
Mpo vizuri Mungu wa mbinguni awabariki
Amina sana
Wimbo mzuri mbarikiwe
Amina
Hongereni sana mmeimba vizuri Mungu awabariki katika utume wenu
Amina
Hongereni sana hizo ndo nyimbo za kikatoliki ni kwaya ambazo zinaimbwa na kwaya chache
Amina
Tafakri nzuri sana katika wimbo huu
Wimbo mtamu Sana.
Hongera sana mmeimba mziki wa kikatoriki
Asante
Mbarikiwe sana, hizo ndio nyimbo za kikatoliki, sio hizi sebene za siku hizi, hongereni sana
Amina
Naomba jina la mtunzi nikautafite SMN
Joseph makoye
Makoye
👏👏👏👏👏👏
Amina
Kazi nzuri,hongeren
Asantee