KILIMO CHA NYANYA:Jifunze Hasara za kutumia mbegu za kukamua na sio mbegu chotara za nyanya.

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 15 ก.ย. 2024
  • KILIMO BORA CHA NYANYA NA SOKO LAKE
    mtaji wa kilimo cha nyanya
    gharama za kilimo cha nyanya
    utajiri wa kilimo cha nyanya
    kilimo cha nyanya kiangazi pdf
    kilimo cha nyanya wakati wa mvua
    kilimo cha nyanya 2020
    kilimo cha nyanya ndefu
    kilimo cha nyanya masika
    1.0 UTANGULIZI
    Nchini Tanzania zao la nyanya hulimwa karibu katika mikoa yote hasa ya Arusha, Kilimanjaro, Morogoro, Iringa, Mwanza, Dodoma, Tanga, Pwani na Mbeya.
    Nyanya ni zao la chakula na
    biashara.
    Kilimo cha zao hili hufanyika majira yote (masika na kiangazi), na faida hupatikana
    haraka na ni ya kuridhisha ikilinganishwa na mazao mengine.
    Pamoja na umuhimu wa zao hili, wadudu waharibifu na magonjwa huathiri uzalishaji na ubora wa matunda.
    Ili mkulima aweze
    kupata faida na kuongeza pato la kaya yake ni vema kuzingatia kanuni bora za kilimo pamoja na
    udhibiti wa magonjwa na wadudu wa zao hili.
    Kwa manispaa ya Musoma zao la nyanya hulimwa na wakulima hulitegemea zao hili kama zao
    la biashara kwa kuwa huwapatia faida kubwa ukilinganisha na mazao mengine ya mbogamboga.
    .1.1 FAIDA YA NYANYA
    -Nyanya hutupatia vitamini A, B, na C. pia zina madini aina ya chuma na chokaa. -Nyanya hutumika zaidi kama kiungo na ni chakula. -Nyanya hutupatia pesa (Ni zao zuri kwa biashara)
    1.2 MATUMIZI:
    Nyanya hutumika kama kiungo cha kupikia. Huweza kuliwa mbichi kama kachumbari au zikiwa
    zimekaangwa pamoja na nyama au mboga yoyote.
    Nyanya pia zinaweza kutengenezwa supu, vinywaji, achari, jemu, sosi na pesti.
    Vilevile zinaweza kukatwa katwa vipande na kuhifadhiwa
    kwenye makopo.
    Mabaki ya mimea hutumika kama mbolea na chakula cha wanyama.
    1.3 MAZINGIRA:
    · Udongo
    Nyanya hustawi kwenye aina zote za udongo kuanzia udongo wa kichanga, mwepesi na
    tifutifu hadi udongo wa mfinyanzi, ili mradi uwe na mboji ya kutosha.
    Udongo unaofaa
    zaidi ni ule wa kitifutifu na wenye mboji nyingi.
    Hali kadhalika udongo wenye uchachu
    wa wastani yaani pH 6.0 - 7.0 ni mzuri kwa kilimo cha zao hili.
    · Hali ya Hewa
    Nyanya hustawi vizuri zaidi kwenye mazingira ya joto la wastani kuanzia nyuzi joto 18-30
    sentigreti.
    Mvua nyingi husababisha mlipuko wa magonjwa ya ukungu kama vile Baka jani
    chelewa n.k.) Joto likizidi husababisha matawi ya matunda kuwa machache.
    Vilevile joto
    jingi, mwanga kidogo, pamoja na hali ya unyevunyevu husababisha magonjwa mengi
    kuenea na mmea kuwa na majani mengi na matunda kidogo.
    Joto kidogo hufanya mimea
    kutoa matawi mengi na matunda madogo ambayo huchelewa kukomaa.
    Zao hili hupendelea mvua za wastani pamoja na kipindi kirefu chajua.
    Hali ya mvua nyingi pamoja
    na baridi kali husababisha kuenea kwa magonjwa na wadudu waharibifu.
    2.0 AINA ZA NYANYA:
    Aina nzuri za nyanya ni zile zinazotoa mavuno mengi na bora; zinazostahimili magonjwa, zinazokomaa mapema, zenye ladha nzuri na umbo la kuvutia,.
    Zifuatazo ni aina bora za nyanya
    zinazolimwa hapa nchini; Aina hizi zimegawanyika katika makundi makuu mawili kutegemea
    ukuaji wake.
    2.1 Kutokana na tabia ya ukuaji, nyanya zinagawanyika katika makundi
    mawili:
    1.Aina ndefu ( intermediate) kwa mfano ANNA F1, Tengeru 97. Money Maker, Marglobe, Beef
    Master, Lot No 2009, Mandel na Tanya.
    Aina hizi hufanya vizuri zaidi zinapopandwa ndani ya
    greenhouse. Uvunaji wake ni wa muda mrefu, zipo ambazo zinavunwa hata zaidi ya miezi 6, yaani hiyo miezi 6 ni ya uvunaji.
    2. Aina fupi (determinate) kwa mfano Tanya, Cal J, Mwanga, Onyx, Roma VF (nyanya
    mshumaa), Dwarf germ, Amateur, Red Cloud, Reza na Columbian.
    2.2 Kutokana na uchavushaji, nyanya zinagawanyika makundi mawili:
    1. OPV (Open Pollinated Variety) - Aina za kawaida
    2. Hybrid - Chotara:
    Hizi ni aina zenye mavuno mengi, kati ya hizo zipo aina fupi na ndefu. Katika karne hii ya 21, nyanya zinazopendelewa kulimwa zaidi na wakulima, ni zile zinazoweza
    kuvumilia magonjwa, zinazo zaa sana, na zenye ganda gumu ili kufanikisha usafirishaji, na
    kuhifadhika kwa siku nyingi bila kuharibika mapema.
    3.0 Kuandaa Kitalu cha Nyanya
    3.1 Mambo muhimu ya kuzingatia
    • Kitalu kiwe karibu na maji ya kutosha na ya kudumu
    • Kiwe sehemu iliyowazi na yenye udongo ulio na rutuba ya kutosha
    • Eneo la kitalu kama ni kubwa liwe tambarare au na mwiinuko kidogo ili kuepuka maji
    yasituame kwenye kitalu,
    mtelemko ukiwa mkali sana nao sio mzuri kwani husababisha
    mmomonyoko wa udongo.
    • Kitalu kiwe sehemu ambayo haikuwa na zao la nyanya au viazi mviringo (au mazao ya jamii
    ya nyanya k.m. mnavu, biringanya n.k.)
    • Kiwe sehemu ambayo ni rahisi kupata huduma zote muhimu kwa urahisi, ikiwa ni pamoja na
    uhamishaji wa miche kwenda sehemu nyingine. Pia kurahisisha usambazaji wa miche kwenda
    sehemu nyingine.
    Dawa zinazopendekezwa ni
    Ridomil, Dithane 45, Bravo, Funguran, milraz, Topsin M 70, Cupric Hydroxide
    (Champion) na Copper Oxychloride (Cupro).
    #mkulimasmart
    #shambadarasa

ความคิดเห็น • 14