KILIMO CHA NYANYA:Jifunze Hasara za kutumia mbegu za kukamua na sio mbegu chotara za nyanya.
ฝัง
- เผยแพร่เมื่อ 15 ก.ย. 2024
- KILIMO BORA CHA NYANYA NA SOKO LAKE
mtaji wa kilimo cha nyanya
gharama za kilimo cha nyanya
utajiri wa kilimo cha nyanya
kilimo cha nyanya kiangazi pdf
kilimo cha nyanya wakati wa mvua
kilimo cha nyanya 2020
kilimo cha nyanya ndefu
kilimo cha nyanya masika
1.0 UTANGULIZI
Nchini Tanzania zao la nyanya hulimwa karibu katika mikoa yote hasa ya Arusha, Kilimanjaro, Morogoro, Iringa, Mwanza, Dodoma, Tanga, Pwani na Mbeya.
Nyanya ni zao la chakula na
biashara.
Kilimo cha zao hili hufanyika majira yote (masika na kiangazi), na faida hupatikana
haraka na ni ya kuridhisha ikilinganishwa na mazao mengine.
Pamoja na umuhimu wa zao hili, wadudu waharibifu na magonjwa huathiri uzalishaji na ubora wa matunda.
Ili mkulima aweze
kupata faida na kuongeza pato la kaya yake ni vema kuzingatia kanuni bora za kilimo pamoja na
udhibiti wa magonjwa na wadudu wa zao hili.
Kwa manispaa ya Musoma zao la nyanya hulimwa na wakulima hulitegemea zao hili kama zao
la biashara kwa kuwa huwapatia faida kubwa ukilinganisha na mazao mengine ya mbogamboga.
.1.1 FAIDA YA NYANYA
-Nyanya hutupatia vitamini A, B, na C. pia zina madini aina ya chuma na chokaa. -Nyanya hutumika zaidi kama kiungo na ni chakula. -Nyanya hutupatia pesa (Ni zao zuri kwa biashara)
1.2 MATUMIZI:
Nyanya hutumika kama kiungo cha kupikia. Huweza kuliwa mbichi kama kachumbari au zikiwa
zimekaangwa pamoja na nyama au mboga yoyote.
Nyanya pia zinaweza kutengenezwa supu, vinywaji, achari, jemu, sosi na pesti.
Vilevile zinaweza kukatwa katwa vipande na kuhifadhiwa
kwenye makopo.
Mabaki ya mimea hutumika kama mbolea na chakula cha wanyama.
1.3 MAZINGIRA:
· Udongo
Nyanya hustawi kwenye aina zote za udongo kuanzia udongo wa kichanga, mwepesi na
tifutifu hadi udongo wa mfinyanzi, ili mradi uwe na mboji ya kutosha.
Udongo unaofaa
zaidi ni ule wa kitifutifu na wenye mboji nyingi.
Hali kadhalika udongo wenye uchachu
wa wastani yaani pH 6.0 - 7.0 ni mzuri kwa kilimo cha zao hili.
· Hali ya Hewa
Nyanya hustawi vizuri zaidi kwenye mazingira ya joto la wastani kuanzia nyuzi joto 18-30
sentigreti.
Mvua nyingi husababisha mlipuko wa magonjwa ya ukungu kama vile Baka jani
chelewa n.k.) Joto likizidi husababisha matawi ya matunda kuwa machache.
Vilevile joto
jingi, mwanga kidogo, pamoja na hali ya unyevunyevu husababisha magonjwa mengi
kuenea na mmea kuwa na majani mengi na matunda kidogo.
Joto kidogo hufanya mimea
kutoa matawi mengi na matunda madogo ambayo huchelewa kukomaa.
Zao hili hupendelea mvua za wastani pamoja na kipindi kirefu chajua.
Hali ya mvua nyingi pamoja
na baridi kali husababisha kuenea kwa magonjwa na wadudu waharibifu.
2.0 AINA ZA NYANYA:
Aina nzuri za nyanya ni zile zinazotoa mavuno mengi na bora; zinazostahimili magonjwa, zinazokomaa mapema, zenye ladha nzuri na umbo la kuvutia,.
Zifuatazo ni aina bora za nyanya
zinazolimwa hapa nchini; Aina hizi zimegawanyika katika makundi makuu mawili kutegemea
ukuaji wake.
2.1 Kutokana na tabia ya ukuaji, nyanya zinagawanyika katika makundi
mawili:
1.Aina ndefu ( intermediate) kwa mfano ANNA F1, Tengeru 97. Money Maker, Marglobe, Beef
Master, Lot No 2009, Mandel na Tanya.
Aina hizi hufanya vizuri zaidi zinapopandwa ndani ya
greenhouse. Uvunaji wake ni wa muda mrefu, zipo ambazo zinavunwa hata zaidi ya miezi 6, yaani hiyo miezi 6 ni ya uvunaji.
2. Aina fupi (determinate) kwa mfano Tanya, Cal J, Mwanga, Onyx, Roma VF (nyanya
mshumaa), Dwarf germ, Amateur, Red Cloud, Reza na Columbian.
2.2 Kutokana na uchavushaji, nyanya zinagawanyika makundi mawili:
1. OPV (Open Pollinated Variety) - Aina za kawaida
2. Hybrid - Chotara:
Hizi ni aina zenye mavuno mengi, kati ya hizo zipo aina fupi na ndefu. Katika karne hii ya 21, nyanya zinazopendelewa kulimwa zaidi na wakulima, ni zile zinazoweza
kuvumilia magonjwa, zinazo zaa sana, na zenye ganda gumu ili kufanikisha usafirishaji, na
kuhifadhika kwa siku nyingi bila kuharibika mapema.
3.0 Kuandaa Kitalu cha Nyanya
3.1 Mambo muhimu ya kuzingatia
• Kitalu kiwe karibu na maji ya kutosha na ya kudumu
• Kiwe sehemu iliyowazi na yenye udongo ulio na rutuba ya kutosha
• Eneo la kitalu kama ni kubwa liwe tambarare au na mwiinuko kidogo ili kuepuka maji
yasituame kwenye kitalu,
mtelemko ukiwa mkali sana nao sio mzuri kwani husababisha
mmomonyoko wa udongo.
• Kitalu kiwe sehemu ambayo haikuwa na zao la nyanya au viazi mviringo (au mazao ya jamii
ya nyanya k.m. mnavu, biringanya n.k.)
• Kiwe sehemu ambayo ni rahisi kupata huduma zote muhimu kwa urahisi, ikiwa ni pamoja na
uhamishaji wa miche kwenda sehemu nyingine. Pia kurahisisha usambazaji wa miche kwenda
sehemu nyingine.
Dawa zinazopendekezwa ni
Ridomil, Dithane 45, Bravo, Funguran, milraz, Topsin M 70, Cupric Hydroxide
(Champion) na Copper Oxychloride (Cupro).
#mkulimasmart
#shambadarasa
Shamba darasa idea nzuri
KARIBU
Naomba siku Moja muje mufike shambani kwangu nipo gairo
Good sana
good
sAFI SANA
Nimesubscribe najua nitapata mengi hapa...nataka kujifunza kilimo Cha nyanya ndipo nianze kulima..SIJUI CHOCHOTE
KARIBU SANA
UKO MKOA GANI
@@shambadarasaTV nipo Kigoma boss
@@teacherd karibu
Mbegu shingapi
unataka kiasi gani
@@shambadarasaTV zitakazo tosha kwenye shamba la eka moja