MRADI WA MAJI MIJI 28 MHE, DEO MWANYIKA ALIZUNGUMZA HAYA BUNGENI

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 22 ก.ย. 2024
  • Na Maiko Luoga Njombe
    Hatimae miji ya Njombe, Wanging’ombe na Makambako mkoani Njombe hivi karibuni inaenda kunufaika na huduma ya maji safi na salama kupitia mradi mkubwa wa maji katika miji 28 nchini.
    Mikataba ya ujenzi wa mradi wa maji katika miji hiyo ilisainiwa juni 06/2022 Ikulu Chamwino Jijini Dodoma kati ya Serikali na Wakandarasi watakaokamilisha kazi hiyo.
    Hafla ya utiaji saini mikataba ya ujenzi wa mradi mkubwa wa maji nchini, ili fanyika mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Samia Suluhu Hassan ambae amesema Serikali itaendelea kujenga miradi ya maji katika kila eneo la Tanzania.
    “Niseme Serikali itaendelea kujenga miradi ya maji katika kila eneo la nchi yetu ili kutimiza utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya kuhakikisha ifikapo mwaka 2025 huduma ya maji safi na salama inafikia asilimia 85 Vijijini na asilimia 95 mijini, tayari tuna dalili zote za kufanikiwa” Mhe, Samia Suluhu Hasan Rais wa Tanzania.
    Kufuatia hatua hiyo Mhe, Deo Mwanyika Mbunge wa jimbo la Njombe mjini amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea na jitihada za kutatua changamoto zinazo wakabili wananchi kote nchini.
    “Siku zote nilipopata nafasi ya kuchangia hoja Bungeni nimekuwa nikisema moja ya tatizo kubwa la watu wa Njombe ni uhaba wa maji, hatimae leo tunashuhudia mikataba ya ujenzi wa mradi wa maji katika miji 28 imesainiwa ikiwemo Njombe hii ni hatua kubwa kwetu”
    “Nampongeza Mhe, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake za kutafuta fedha na kuzipata kisha kupeleka huduma hii ya mradi mkubwa wa maji katika miji 28 nchini na sisi Njombe na mkoa kwa ujumla ni wanufaika” alieleza Mhe, Deo Mwanyika Mbunge wa jimbo la Njombe mjini.
    Katibu mkuu wizara ya maji Mhandisi Antony Sanga amesema, Utekelezaji wa mradi wa maji katika miji 28 nchini utakaogharimu fedha za kimarekani dola milioni miatano, unatekelezwa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia mkopo wenye masharti nafuu kutoka Serikali ya India kupitia Benki ya EXIM.

ความคิดเห็น •