Sizonje - Mrisho Mpoto ft Banana Zorro (Official Video)

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 7 ก.พ. 2025
  • Nyimbo Mpya ya Mwaka 2016, Sizonje.
    [Kibwagizo - Banana Zorro]
    Sizonje hii ndio nyumba yetu
    Milango ipo wanapita madirishani
    Sizonje ndio nyumba yetu
    Milango ipo wanapita madirishani
    Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
    Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
    [Bridge - Banana Zorro]
    Tulikaa barazani, tukasikia kelele
    Kelele toka ndani, mtu anaruka dirishani
    Sizonje, karibu nyumbani kwetu
    Uone maajabu ya nyumba yetu
    [Verse 1 - Mrisho Mpoto]
    Karibu sana Sizonje, hii ndo nyumba yetu,
    Tulipoficha mundu za kupondea wezi,
    Kwani, makaburi yaliofukuliwa lazima yazikwe upya?
    Nyumba hii Sizonje ina vyumba vinne,
    Vitatu havifunguki, kimoja hakina mlango,
    Japo kuwa kina watu ndani, na hawaongei kiswahili,
    Wenyeji wanalala sebleni na walishazoea,
    Sizonje kule tulipotoka panaitwa jikoni,
    Huna haja ya kwenda kule, kumejaa mafundi wa kupika
    Sasa hivi wanakupikia wewe ili ule ulale
    Ukiamka muongee nini hasa ujio na dhima ya safari yako
    Wanashangaa mbona ghafla
    Samahani sana mgeni
    Wapishi wameniomba kwamba
    Nikuulize tena kwa kukuomba kwamba
    Eti unapenda vya mafuta au vya nazi?
    Wanataka kukuonyesha madoido katika mapishi yao Sizonje
    Sizonje chumba hiki naomba usiingie
    Ukimaliza nitakwambia kwanini
    Kuna sauti inajirudia mara kwa mara
    Na hapa mlangoni kulikuwa na picha mbili kubwa
    Moja picha, nyingine mchoro wa picha wa kwanza
    Ninachokumbuka iliwahi kuandikwa
    “USIYEMTAKA KAJA”
    Hatukuwahi kuelewa maana yake
    Labda kwa sababu ya ujio wako unaweza kutusaidia
    [Chorus - Banana Zorro]
    Sizonje hii ndio nyumba yetu
    Milango ipo wanapita madirishani
    Sizonje hii ndio nyumba yetu
    Milango ipo wanapita madirishani
    Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
    Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
    [Verse 2 - Mrisho Mpoto]
    Najua, wimbo mbaya haufai kubembelezea mtoto
    Na kamwe mtoto hawezi kuungua
    Kwa kiazi kilichokuwa kwenye kiganja cha mama yake mzazi
    Njoo huku uone Sizonje
    Si unajua, harufu ya uzazi haiishi mpaka mtoto akue?
    Sawa, Sizonje, huu hapa ni ua
    Lile pale ni shimo la taka
    Na kile pale ni choo
    Kinachotutisha na kutuogopesha zaidi
    Wanaoishi humu ndani hawajawahi kutupa taka
    Wala kwenda chooni
    Kama ukiwa makini
    Kwa nje utasikia sauti za makundi ya watu
    Wengi ni vijana, wana bahasha za khaki mikononi
    “KAMA HAMTUPI TAKA SHIMO HILI MLICHIMBA LA NINI?”
    Lakini pia kwenye sauti zao, Sizonje
    Kuna watoto, wazee na kina mama
    Ukiunganisha sauti zao ndio unapata hizo kelele
    Ninavyosikia, ila sina uhakika
    Waliambiwa kihistoria nyumba hii ni ya kwao
    Na wana haki ya kutupa taka na kutumia choo hiki
    Sasa, njoo nikuonyeshe huku uchochoroni
    Uone maajabu mengine ya nyumba hii
    Sizonje, ukiona tembo anaringa
    Ujue mvua zinakaribia
    [Chorus - Banana Zorro]
    Sizonje hii ndio nyumba yetu
    Milango ipo wanapita madirishani
    Sizonje ndio nyumba yetu
    Milango ipo wanapita madirishani
    Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
    Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
    Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
    Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu

ความคิดเห็น • 422

  • @davisnyandindi4917
    @davisnyandindi4917 หลายเดือนก่อน +4

    2025 huu mwaka tunategemea sana nyimbo zako,,, ganga like nying km mpo pamoja na mimi

  • @stephanokigosi656
    @stephanokigosi656 3 ปีที่แล้ว +31

    huu wimbo ulikuwa special to MAGUFULI..Rest in paradise our icon 🕯🕯😭😭

  • @kombakomba7922
    @kombakomba7922 3 ปีที่แล้ว +65

    Nyumba ni nchi,kwa nje inatafsirika na kuonekana ni maskini ila ndani ina utajiri mkubwaa,ila inaibiwa na manyemera wanaopita njia za panya kuiba rasilimali zetu, pia undugunization kwenye ajira ni tatizo,afya za kina mama na watoto,uchumi,rushwa na uwajibikaji ila sizonje ushafika umekomesha hayo yote. Hongera sana sana Mrisho na hongera kwa Sizonje.

    • @Richplumbing11
      @Richplumbing11 3 ปีที่แล้ว +5

      Leo ndio nimeielewa atari sana uyu jamaa

    • @tengezashemisea1787
      @tengezashemisea1787 2 ปีที่แล้ว

      Hongera mrisho, ila bado mwendo hujaumaliza endelea kuwa kumbusha wenye dhamana , hakika bado tunakuhitaji.

    • @alvinmuthui
      @alvinmuthui 2 ปีที่แล้ว

      Elenzea zaidi tafadhali

    • @المهلهلالحراصي
      @المهلهلالحراصي 2 ปีที่แล้ว

      duuuuuuh kumbe ndo nimejua leo hii maana ya wimbo huu

    • @bonfacemark9048
      @bonfacemark9048 2 ปีที่แล้ว

      Asante kwa tafsiri yako ndugu from 🇰🇪 🙏

  • @mariammalendeja370
    @mariammalendeja370 ปีที่แล้ว +6

    nyimbo hii ulimuimbia maghufuli nae akaskia sauti yako akawaadhibu wadhalimu hadi wakaanza kupitia mlangoni r.i.p maghufuli tutakukumbuka milele

  • @VictorMligo-t9c
    @VictorMligo-t9c 11 หลายเดือนก่อน +7

    Ila mpoto I nyimbo nimekuja kuelewa leo trh 5-3-2024😂😂😂

    • @Gbril45
      @Gbril45 11 หลายเดือนก่อน

      Inamaanishi nini kwani? Mimi bado naangaika

    • @SalvatoryKayinga
      @SalvatoryKayinga หลายเดือนก่อน

      Hongera kijana

    • @FanuelJoel
      @FanuelJoel 26 วันที่ผ่านมา

      Mm cjaelewa bado

  • @allyhussein516
    @allyhussein516 5 ปีที่แล้ว +4

    Bila akili ya ziada kwa mrisho mpoto hutoki na kitu njooni tuungane jaman gonga like hapa kama umeikubali hii

  • @solangeramadhani4038
    @solangeramadhani4038 ปีที่แล้ว +1

    Duuuh miaka nenda miaka rudi leo ssa ndonimeelewa maan ya huu winbo

  • @jodasonudavis1131
    @jodasonudavis1131 8 ปีที่แล้ว +138

    MLANGO UPO WANAPITA MADIRISHANI.... ..kwamba Kuna utaratibu wa kufikia jambo fulani Ila watu hutumia njia za mkato(rushwa) kupata jambo hilo.....SHIMO HALITUPWI TAKA WALA HAWAENDI CHOO... maana yake Kuna mfumo wa watu kustaafu Lakini Kuna watu hawaachii nyazifa na pia kuna kazi fulani hivi zimekuwa za koo fulani wanarithishana kutoka kwa baba then mtoto hatimae mjukuu mfano(benki kuu) na hivyo kusababisha vilio vya vijana wengi wasomi kuzunguka na bahasha kwa kutafuta ajira na ajira hamna.......This is the best literature song I ever meet. Good work for this guy

    • @martinnsuhuje4391
      @martinnsuhuje4391 8 ปีที่แล้ว +1

      Asante kwa kufafanua kidogo nadhan umesoma kiswahili vzr

    • @jodasonudavis1131
      @jodasonudavis1131 8 ปีที่แล้ว +3

      Sikuachwa nyuma sana katika fasihi

    • @davidomemu471
      @davidomemu471 8 ปีที่แล้ว +2

      Nakubaliana nawe Jodasonu kabisa, the best oral lit, of modern time, big up MPOTO.

    • @khadijambuta4360
      @khadijambuta4360 7 ปีที่แล้ว

      Jodasonu Davis yani huko benk kuu ndio ucseme watu wapitishana tu msemo wao hpa kaz tu

    • @doreenmalesi6039
      @doreenmalesi6039 6 ปีที่แล้ว +1

      Asante kwa kunifafanulia

  • @jimmyfredmwanswaswa4562
    @jimmyfredmwanswaswa4562 3 ปีที่แล้ว +6

    Tutolee nyimbo nyingine nzuri kama hii Mrisho! Asante kwa kutufundisha Kiswahili na utunzi!
    Mashairi Yako natamani watoto wetu wayasome shuleni!

  • @patrinraura1397
    @patrinraura1397 3 หลายเดือนก่อน +1

    Hakika huyu ni Artist❤ mbobevu na gwiji la Mashahiri yaliyosheheni Ujumbe mzito kwa Jamii Ni style ya Wimbo usio na Vionjo vya Tamaduni za nje Wimbo huu umebeba maisha yetu kupitia mila,desturi na Tamaduni zetu Hongera Msanii Mwamba Mrisho Mpoto

  • @upendorealestateagentintan190
    @upendorealestateagentintan190 ปีที่แล้ว +9

    Mjomba Tanzania imekumiss sana. Tunaamini bado unatupenda yapo mengi tunahitaji utusemee hasa ktk wakati huu.

    • @SalvatoryKayinga
      @SalvatoryKayinga หลายเดือนก่อน +2

      Tangu apewe kipande cha keki saut haitoki tena

  • @phillies846
    @phillies846 8 ปีที่แล้ว +59

    Mrisho mwalimu wako wa kiswahili alikuwa anapata shida saana kwa kukosolewa na wewe 🙏🏽 amen

    • @merryn4891
      @merryn4891 6 ปีที่แล้ว +1

      😀😀😀😀

    • @ssur5797
      @ssur5797 6 ปีที่แล้ว +2

      Nampnda mpka bac huyu kaka mola ampe umri mrefu wenye kheri ishllh

    • @catenzeki678
      @catenzeki678 5 ปีที่แล้ว

      @S Sur AMINA

  • @kenneth.m.siwale9699
    @kenneth.m.siwale9699 6 ปีที่แล้ว +6

    Pamoja na hayo mjomba Mpoto,leo hii nikiwa natokea kwenye kilele cha sherehe ya kilele cha miaka mia moja ya vita kuu ya Dunia ya kwanza! Mjomba Mpoto nimelazimika kutumia au kuiba jumbe zako hizi kwa mapenzi na ujumbe sahihi kwa wakati mwafaka hasa hapa kwetu Zambia!

  • @kenneth.m.siwale9699
    @kenneth.m.siwale9699 6 ปีที่แล้ว +1

    Mjomba Mpoto utaniwia radhi kwakweki mjomba uliwahi kuniliza enzi za awamu ya nne ya Mzee wetu Dr. wa Ukweli wa Msoga, niliwahi kulia na kucheza sana pala LUGOBA!ulikuwa wimbo Adela,na Sasa hivi SIZONJE huu si tu ni wimbo ni FASIHI KALI!!!!. Wewe kweli ni aina ya akina Shaban Robart

  • @josephseleman7780
    @josephseleman7780 4 ปีที่แล้ว +19

    Kama unamkubari mrisho mpoto gonga like hapa

  • @mhonamisaomar7011
    @mhonamisaomar7011 8 ปีที่แล้ว +1

    ukiisikiliza mankini itailewa 2..hongera. mjomba coz umenifanya ninitulie xanaa kukusikiliza Na kufafanua..wakuache jomba..nakusikiliza. mwana Kenya nikiwa saudia nimetua mankini..

  • @msafirisalehe563
    @msafirisalehe563 8 ปีที่แล้ว +9

    Kama umesoma sana vitabu vya Hayati Shabani Robert,hakika hutokuwa na kazi kubwa ya kumuelewa Mpoto.

  • @thedoctor8301
    @thedoctor8301 8 ปีที่แล้ว +1

    SIKU ZOTE MWENYE HEKIMA HANUKI MDOMO NA MWENYE AKILI HASEMI NDANI YA MAJI.... HESHIMA KWAKO MR MPOTO NATAMANI NIJIFUNZE ZAIDI TOKA KWAKO.

  • @abukiczan6600
    @abukiczan6600 8 ปีที่แล้ว +7

    Mwenye akili ndogo hawezi elewa nyimbo zako but wewe ni zaidi ya msaniu hapa afrika na natamani siku nikukumbatie kwa furaha. U are the best mjomba

  • @eusebiusjmikongoti6625
    @eusebiusjmikongoti6625 8 ปีที่แล้ว +13

    Nakukukubali sana mtaalamu Mjomba, kazi zako huwa zina nipa shida kuzielewa lakini huwa nakuelewa taratibu. Ninahisi hakuna kazi niliyowahi kukuelewa kwa 100% maana kila nikirudia kusikia wimbo fulani huwa naongeza kitu fulani kutoka humo! Wewe ni Shaaban Robert wa pili kwakweli, yapasa nawe uandike kitabu cha KUSADIKIKA kama mzee Shaaban, sijui utakiita SIZONJE....., au NYUMBA YETU!

  • @rosenamilia4140
    @rosenamilia4140 2 ปีที่แล้ว +1

    Sizonje ni jina la HAYATI JOHN POMBE MAGUFULI,alilopewa na Ndugu yetu msanii Mrisho Mpoto.Nyumba ktk wimbo huu ni IKULU YA RAIS MAGOGONI Dar es Salaam.

    • @JoshuaLyalukilo
      @JoshuaLyalukilo หลายเดือนก่อน

      Wimbo huo ni wazamani mno hata kabla ya huyo magufuli hajajitambua kabisa

    • @Yana_queen1
      @Yana_queen1 หลายเดือนก่อน

      @@JoshuaLyalukiloAliutoa wakati magufuli ndo kaingia madarakani…nyumba ina vyumba 4 means awamu nne
      Usiyemtaka kaja (Magu km Magu)

  • @nyabisemaro2095
    @nyabisemaro2095 7 ปีที่แล้ว +1

    Mrisho Unajitahidi sanaaaa kusema kweli nazipenda nyimbo zakooo hasa Sizonje,kitendawili,nikipata nauli,Waiteee nk

  • @silassambia876
    @silassambia876 4 ปีที่แล้ว +10

    My all time Tanzanian Artist..love from🇰🇪

  • @mwangacharles8474
    @mwangacharles8474 8 ปีที่แล้ว +1

    Kaka hongera sana kaka, nimeielewa sana nyimbo hiii, hasa choo kipo lakini hakitumikiiii. Unatisha kaka.

  • @bakarikimea4711
    @bakarikimea4711 2 หลายเดือนก่อน

    Ila huyu mzee phana nasikilizaga nyimbozake lakn hii mh katumia methali tupu aisee safisana

  • @ernestshaha1932
    @ernestshaha1932 5 ปีที่แล้ว +1

    Huu wimbo nimeusikiza Mara 7 sai
    Mjomba juu wimbo unamafundisho saana

  • @johnambrose7223
    @johnambrose7223 ปีที่แล้ว

    Siku hizi mrisho mpoto haimbi tena

  • @saidbarawa9096
    @saidbarawa9096 5 หลายเดือนก่อน

    Mrisho shujaa shujaa shujaa,saluti kwako,mimi ni mkenya anaefurahia kazi yako nzuri mungu akubariki

  • @DoubleDlyrics-v7k
    @DoubleDlyrics-v7k ปีที่แล้ว

    Dah!!na mkubali sana mrisho miaka 7 imepita nasikia wimbo huu ila leo ndo mmeelewa sahihi ya wimbo huu

  • @JosephatJuma-dj5tq
    @JosephatJuma-dj5tq 8 หลายเดือนก่อน +1

    Mjomba hapa Kenya unapendwa kakangu

  • @abbouramsey154
    @abbouramsey154 9 ปีที่แล้ว +1

    Apo Godfather au nenene? bonge la kichupa straight to Urban top Ten

  • @IrineKimaro
    @IrineKimaro 8 หลายเดือนก่อน

    Mjomba tumemiss mashairi yako, come back legend

  • @salumkanju1732
    @salumkanju1732 8 ปีที่แล้ว +2

    daah kwa sisi tuliosoma arts aisee mzee mpoto unatisha baba angu.....nakutamani san katik matumizi ya lugha na hasa lugha ya picha kikubwa zaidi ni hiyo nyumba yaudongo lakin ndani noouma!! bila shaka watanzania waliotazama video hii wamejifunza kitu, binafsi sanaa yako sio tu kiburudisho kwangu maana najifunza mengi san na ni miongoni mwa mhimili wa utamaduni wa nchi yetu! unaimba kwa kusoma upepo unavyovuma ila ulituomba nauli ili uwende kwa mjomba na je sizonje ni naniiiiiii?

  • @barackolgeno1076
    @barackolgeno1076 8 ปีที่แล้ว +34

    this guy is marvellous... your Tanzanian fan from Australia

  • @lightnessmruma9740
    @lightnessmruma9740 9 ปีที่แล้ว +5

    nmeelewa kidogo,anamkaribisha maguful ikulu(nchi yetu)....asiye mtaka kaja hahaha I like this ....japo mafumbo n mnge

  • @FredySokolo
    @FredySokolo 8 หลายเดือนก่อน

    Kiongozzzz unajua sana ,sasa sijajua umesoma kiswahili sana au mimi ndio btplms

  • @ezrambilinyi6788
    @ezrambilinyi6788 3 ปีที่แล้ว +1

    Mhhh ngoja niseme ukweli tuuu. Ni miaka 3 now nasikiliza nyimbo za huyu jamaaa cjawai elewa anae elewa anielekezeee

    • @Catherinemichael1995
      @Catherinemichael1995 3 ปีที่แล้ว

      Amemaanisha kuwa nchi inaonekana masikin wakati ndani yake inautajir tena amemaanisha sheria ipo lkn watu wanatumia njia ya mkato ameelezea mambo mengi

  • @davidomemu471
    @davidomemu471 8 ปีที่แล้ว +2

    Mjomba, kwa kweli nyumba za Africa mashariki zina mambo na maajabu, zaidi hapa Kenya.

  • @rumbikamachumu3292
    @rumbikamachumu3292 9 ปีที่แล้ว +3

    one of the best video and nice message to Tanzanian. kazi nzuri Mjomba endelea kuelimisha ,kufundisha na kukosoa jamii

  • @fatmafetty4117
    @fatmafetty4117 5 ปีที่แล้ว +4

    Sizonje naipenda mnoo sichoki kuiangalia wallah love u bro mrisho ❤️❤️❤️❤️❤️ kazi nzur sanaaaa👌👌👌👌👌👌

  • @zulferabour607
    @zulferabour607 5 ปีที่แล้ว

    Wakati leo nasom kiswahil ....mwalim wanv kantolea mfano wa mwanafasihi anaetumja lugh y fasihi kufikish ujumb ktm jamii....ndipo akntajia huu wimbo ....hap nmeelewa kwann mrisho umeamua kutmia lugha hii....hongera sana

  • @mwitaadah3649
    @mwitaadah3649 4 ปีที่แล้ว +1

    Mjomba umetulia Sana. Tupe mashairi baba🔥

  • @Franko-zd6hc
    @Franko-zd6hc 3 ปีที่แล้ว

    Huu ni usanii wa hali ya juu.Utumiaji wa kejeli ilikupeana ujumbe flani.

  • @bwakilamychanel5951
    @bwakilamychanel5951 5 ปีที่แล้ว

    sizonje hii ndiyo nyumba yetu ingia uyaone hapa anaizungumzia tz yetu jinsi watu wanavyopenda rushwa na kurisishana madaraka na wakat kila mtu ana haki

  • @kihanda2554
    @kihanda2554 9 ปีที่แล้ว +5

    Long live Mrisho mpoto. Nimekuelewa vzr mnooo. Mfumbie mtoto mkubwa ang'amue

  • @SostenesMasawa-ls1eo
    @SostenesMasawa-ls1eo 4 หลายเดือนก่อน

    2024 eeeeeh 🔥 "MASTERPIECE"

  • @augustinomkongwa5444
    @augustinomkongwa5444 5 ปีที่แล้ว +1

    Usiyemtaka kaja, sizonje huyu huenda akawa ni JPM aka Jembe aka Chuma cha Pua, siyo lazima niwe sahihi kumtambua Sizonje kwenye ghani hii ya Mrisho

  • @eliatalented7592
    @eliatalented7592 5 ปีที่แล้ว +13

    Who else is still here in 2019

  • @ivanmutwol
    @ivanmutwol 4 หลายเดือนก่อน

    A true Patriot, maisha marefu

  • @aminagoliama8668
    @aminagoliama8668 9 ปีที่แล้ว +3

    Weng ni vijan na wanabahasha za kaki mikonon daaaaah nimeelewa sana nakupend sasa mpot ii ndo nyumb yetu TZ ingia uyaone
    Kile ni choo wanaoish hawajawai kukitumia mean hospital zipo ila wanaenda nje hahahahahahaha
    😍💞💕😘💜👏👏👏

  • @emmanuelmsambya5293
    @emmanuelmsambya5293 9 หลายเดือนก่อน

    Hii nyimbo iliimbwa na watu wenye IQ kubwa

  • @Tutankhamun-s3n
    @Tutankhamun-s3n ปีที่แล้ว

    Nyimbo ngumu sana kuielewa inahitaji utulivu wa kutosha

  • @anitaphilip2070
    @anitaphilip2070 9 ปีที่แล้ว +10

    upenda Wangu nimependa kilakitu wanao sema sinzuri wajaribu nawao tuona zao zitakuaje

  • @sirajiabdallah6824
    @sirajiabdallah6824 ปีที่แล้ว

    Wale WA 2023 tuktane

  • @enockjohn332
    @enockjohn332 9 ปีที่แล้ว

    mtoto hawezi kubembelezwa kwa wimbo mbaya,na mtoto aungui na kiazi kilchopo kwenye kiganja cha mama yake,nimekusoma mjomba

  • @ezekielbituro7969
    @ezekielbituro7969 9 ปีที่แล้ว +1

    nimeilewa asee...mashairi yanaeleweka kiasi! HII NDO TANZANIA

  • @mohdkhalifa8828
    @mohdkhalifa8828 5 หลายเดือนก่อน

    Hekima kaka safi sana

  • @ibrahimzuberi1029
    @ibrahimzuberi1029 8 ปีที่แล้ว

    yan nimeskiliza zaid ya 10 tym sijaeleza zaid ya bahasha za kaki2...daaah shkaaaaamooooo burazaaaaa

  • @amosnguvumali7869
    @amosnguvumali7869 8 ปีที่แล้ว

    hahaha kwel mtoto hawez kuungua kwa kiaz kilichopo kwenye kiganja cha mama yake ahsante sana

  • @juniorlangen2648
    @juniorlangen2648 3 ปีที่แล้ว

    Wewe ni mwalimu , kazi zote zako hujawahi kosea

  • @saknamtaki8168
    @saknamtaki8168 8 ปีที่แล้ว +1

    Nyimbo nzuli kweli uko posh kak kimziki nakupa respect

  • @abusheheyusufu3586
    @abusheheyusufu3586 8 ปีที่แล้ว

    uliye post coment hapo juuu kuwa hujaelewa nyimbo .hujui nyimbo..
    unavamiavamia tuuh ..imba wwe bac ueleweke

  • @kedmondkepha7707
    @kedmondkepha7707 6 ปีที่แล้ว

    Daaaaaaah mjomba ulisomea wapi kiswahili chako maana hayo mashairi yako hakuna anaeyaweza duuu big up sana mziki wako ni wa kibantu zaid

  • @hermanngaiza9327
    @hermanngaiza9327 9 ปีที่แล้ว +1

    Kiukweli wimbo umetulia una ujumbe wa maana sana.ukionesha kwamba tuwe na nguvu na kupambana
    ahsante brother Mpoto

  • @barick
    @barick 8 ปีที่แล้ว

    Huyo mzee anavyo Lia na mimi nimelia mmh!sizonje

  • @neykapoor5871
    @neykapoor5871 2 ปีที่แล้ว +1

    Artist is more beautiful because one thing can bring different meaning and understanding as what it is in this song of. Sizonje salute mrisho mpoto

  • @wilhardjohn8287
    @wilhardjohn8287 9 ปีที่แล้ว

    huyu hanscana ni director anayejielew pengine kuliko wote kwa sasa young but a real inspiration in music industry

  • @dorcasgitari8278
    @dorcasgitari8278 8 ปีที่แล้ว +2

    Nimeingia nami nimeyaona maaaajabu ya nyumba yenu I say...great poetical pieces. Wengi waaalewa maaana ila kwa vile ina wachoma basi wanajifanya kutoelewa I say. He heeeeee.

  • @nyabisemaro2095
    @nyabisemaro2095 7 ปีที่แล้ว

    Wana fasihi tupo tunakuewaga sanaaaa Asante MWL wanguu wa kiswahili MWL MACHUMU, MWL Alexander na PRISCA Bila nyie mm nisingejuaaa ujumbe wa mpoto Mbarikiwe sanaaa

  • @tiaschris7070
    @tiaschris7070 8 ปีที่แล้ว

    aisehhh hii nyimbo ni hatari, xijui km ntakuja kuisikia nyimbo km hii tena

  • @clementsanga
    @clementsanga 9 ปีที่แล้ว

    bonge la kazi kaka na kwa upande wa video ipo poa ile mbaya.

  • @ibrahimjuma8577
    @ibrahimjuma8577 9 ปีที่แล้ว

    hongera Mjomba mi huwa nakuelewa sanaa nice song babaa

  • @christopherkipeke7547
    @christopherkipeke7547 8 ปีที่แล้ว

    Mlisho kwangu hata usipoimba, kitendo cha kukuona nahisi nguli na gwiji la sanaa anajambo analitoa

  • @iamjimba9775
    @iamjimba9775 9 ปีที่แล้ว +1

    duuh! maishairiii nondo sana

  • @masirian06
    @masirian06 3 ปีที่แล้ว

    nazipenda kazi zenu safi sana wanaTanzania... mwatufunza maadili mema ya upendo sis kama wakenya
    lakini wote tu waafrika na hivyo nafurahia kazi zetu,, hongera sana

  • @isackyakobo7829
    @isackyakobo7829 4 ปีที่แล้ว

    Asante sizonje, Kwa sasa wenye nyumba tunalala vyumban piah, Magufuli Oyeeee! Bahasha za kaki tu ndo bado ila karbu tena 2020, ulitatue na hlo! Kwa sasa hawapt madrishan tena,

  • @shamsally6277
    @shamsally6277 3 ปีที่แล้ว +1

    Genious sijawahi pata ona

  • @mwalimmaroaibrah8051
    @mwalimmaroaibrah8051 8 ปีที่แล้ว

    Dah! Kwakweli mashairi yamesimama sana. Hongera Mrisho kwa mashairi haya

  • @jovituskamugisha
    @jovituskamugisha 9 ปีที่แล้ว

    Maudhui, mashairi, rekodi,... Nimeipenda. Ahsante sana Baba Mrisho Mpoto.

  • @ephraimkagungu6050
    @ephraimkagungu6050 9 ปีที่แล้ว

    Oooh Woookey Burhoney Wa Mponda Ha Hha Somehow Umenipa Idea

  • @hadijapazia8255
    @hadijapazia8255 4 ปีที่แล้ว +1

    Naikubali xn hii ngoma🔥🔥🔥🔥👌🏻👌🏻👌🏻👌🏻

  • @wazirikonzo7529
    @wazirikonzo7529 9 ปีที่แล้ว

    nakukubari sana mpoto aka MJOMBA mngu akubariki endelea kuwambia wana sizonje

  • @Nairobipicturesstudios
    @Nairobipicturesstudios 3 ปีที่แล้ว

    Alaaah! Mrisho wanidekua kwa mishororo na ushairi wako kila tungo lanijenga ajabu. mie nasoma sana fan wako mpya hapa toka Kenya.

    • @mabudaissere2295
      @mabudaissere2295 11 หลายเดือนก่อน

      Ana kiazi cha moto mdomoni ataimbaje sasa

  • @MishenOnMission
    @MishenOnMission 2 ปีที่แล้ว

    Mbona mrisho haimbi tena..

  • @piusthomas5713
    @piusthomas5713 2 ปีที่แล้ว

    PongeZi pia kwa director aise ameitendea haki hii ngoma

  • @nelsonkimutai5526
    @nelsonkimutai5526 5 ปีที่แล้ว +7

    I love the patriotism in this guys music,

  • @muddysimba887
    @muddysimba887 5 ปีที่แล้ว +6

    Yuliopo hapa 2020 tupia like

  • @ShariphSeleman-ym6ie
    @ShariphSeleman-ym6ie ปีที่แล้ว

    African have to proud of our culture.we are top

  • @singidaboy1586
    @singidaboy1586 5 ปีที่แล้ว

    nakubali Sana'a Kaz za mjomba nyimbo ujumbe Kwa waelewa

  • @williammwajeka3347
    @williammwajeka3347 9 ปีที่แล้ว

    "Najua, wimbo mbaya haufai kumbelezea mtoto,
    Na kamwe mtt hawez kuungua kwa kiaz kilichokua kweny kiganja cha mama yake mzazi,
    Njoo huk uone sizonje
    Siunajua, harufu ya uzaz haiish mpk mtt akue?
    Haa haa haa daahh mpoto unaandk xn, hongr xn kwa uandsh Mzur, nazkubal xn nyimbo zko
    ✋✋✋✋

  • @alfredally1955
    @alfredally1955 4 ปีที่แล้ว

    Tanzania inaonekana masikini ndani nitajiri hyo ndio jambo nimeona

  • @jameskamau9026
    @jameskamau9026 8 ปีที่แล้ว +1

    mrisho mpoto kwa hakika nyimo zako za burudisha hasa katika matumizi la lugha yetu teule kiswahili

  • @kingimiwani3440
    @kingimiwani3440 4 ปีที่แล้ว

    kiukweli hii nyimbo huwa ninaipenda . sana

  • @johannesshornest4916
    @johannesshornest4916 9 ปีที่แล้ว +1

    we unayesema amealibu au angemuonesha sizonje auna uelewa kumbuka wimbo uu ni fumbo akikuonyesha sizonje utaelewa yeye mpoto anatupa mtiani tumjue sizonje ni nani kua mwelewa sio unakulupuka kuongea tu au unadhani mpoto ni sawa na wale wa mpenzi nakupenda

    • @bitaetenge3989
      @bitaetenge3989 8 ปีที่แล้ว +1

      Johanness Hornest
      Mbona hote mnabaki jujuhu majela yamejengwa lakini wafisadi wakubwa ambao wangefaha watupwe na kuozea huko kama kinyesi kinavyo hozea chohoni awatupwi huko.
      Wasomi wanaho maliza awapewi kazi wanashinda waki zunguka mahogisini lakini awapati milango.
      Sizonje niserekali na nyumba ni inchi.
      Sio Tanzania tu Africa yote.

  • @rich.kizza10
    @rich.kizza10 3 ปีที่แล้ว

    hii ngoma bhana ni balaa

  • @rashidhassankadege1455
    @rashidhassankadege1455 4 ปีที่แล้ว

    Yaani nyumba yetu kwa nje ni mbaya sana nayakizamani mno ila ukiingia ndani ndo utajua uzuri wake najinsi ilivonakshiwa kwa mapambo ya gharama na ustaarabu uliotukuka

    • @ramadhanboi6485
      @ramadhanboi6485 4 ปีที่แล้ว

      Imemaaanisha mbuga za wajama na dhahabu tulizonazo na maziwa

    • @ramadhanboi6485
      @ramadhanboi6485 4 ปีที่แล้ว

      Imemaaanisha mbuga za wajama na dhahabu tulizonazo na maziwa

  • @josephseverin5973
    @josephseverin5973 8 ปีที่แล้ว

    Nkukubali sana mkubwa hongera huna spair

  • @leonardcharles3169
    @leonardcharles3169 9 ปีที่แล้ว +2

    video ni nzuri, tuendelee kumpigia kura tuzo ya kola! wonderful video,

  • @jeneralAthanoel
    @jeneralAthanoel 8 ปีที่แล้ว +1

    Mjombaaa, Banana kazi nzuri sana, ni pekeee

  • @winstonkwoba1994
    @winstonkwoba1994 4 ปีที่แล้ว +2

    madhumuni nimeyapata