Shairi Fundi wa kukuna nazi
ฝัง
- เผยแพร่เมื่อ 28 มิ.ย. 2018
- **Fundi wa kukuna nazi**
Jamani kila shetani, huwa na mbuyu wake
Litieni akilini, wangwana msishituke
Nami nabwaga makini, kisha chini niandike
Ameimiliki mbuzi, fundi wa kukuna nazi.
Mbuzi akishaishika, kifuvu hutetemeka
Kwenye mbuzi huchomeka, kijasho kikimtoka
Fundi amekamilika, kwao anaheshimika
Ameimiliki mbuzi, fundi wa kukuna nazi.
Nazi hukuniwa ndani, huku jungu latokota
Hakunii hadharani, watu wakamwita ita
Jasho kimwaga mwili, mkuna nazi hufuta
Ameimiliki mbuzi, fundi wa kukuna nazi.
Huikuna kwa ujuzi, huku akiimba imba
Anaijulia kazi, namba wani anatamba
Na hakuni kwa ufyozi, si mtu wa kujigamba
Ameimiliki mbuzi, fundi wa kukuna nazi.
Kifuvu hukitingisha, kikunwe kila upande
Bila nazi kubakisha, na panza hata kipande
Fundi huyu hunikosha, akunavyo chonde chonde
Ameimiliki mbuzi, fundi wa kukuna nazi.
Hakuni kwa kubambanya, ni jasiri kama chui
Miguu huitawanya, mbuzi haimsumbui
Akuna akiifinya, hadi inamwaga tui
Ameimiliki mbuzi, fundi wa kukuna nazi.
Nasita mwana wa mama, ama kungwi wa kiume
Kama una la kusema, litapike uliseme
Kukujibu sitogoma, najiamini kidume
Ameimiliki mbuzi, fundi wa kukuna nazi.
Ni yule yule
Malenga Msema Kweli
Abdulkarim Kuchengwa
Mwana wa Mama
Kungwi wa Kiume
County 002, Coast Ke.
©2017
#KungwiWaKiume #kuchengwa
Ma Shaa Allah MUNGU azdi kukuza kipaji chako ABDULL KAREEM
Asantaaa Kk abdu sauti na paali pake ...hongera kwa kipaji chako tuko pamoja.
akuna kwa kuifainya hadi inamwaga tui, hahahaha, hapo ndio paliponibamba mie, ila anaweza ikuna ila akashindwa kuthuja,🤣🤣🤣🤣🤣
Uwe bwana unamanya 👏🙌
Nakupendea hivyo mwana wamama🤣🤣🤣👏👏👏👏
Mashaallah shairi tamu sana
Hii tenzi itabaki Kua tenzi Bora kwangu katika tenzi zako zote,Yani siwachi kuisikiza congrats kungwi wa kiume
Masha Allah, mwanangu your Aunty lady R Hamsini
Mashallah kk 😊😊😊kpaji kipo
Hongera sana Kungwi wa Kiume.
Duuuh shairy limenimaliza ,,mie mtoto wakidigo yani kila viungo vimeachia. Mashallah Mungu akuzidishie ishaallah
Tabarakallah... Yarabiii.. 😂
Hyo bet ya pili mwisho 😂😂😂
Fasihi kiwango cha juu
Hahahaaaaaa hapoooooo mi naona ilo kasmeli tui LA mwanzo tu
Kipawa hicho
MashaAllah
💪💪💪u represent us good brother....kidigo to the world💥💥
MashaaAllah😊
Waeza nitumia hilo shairi mashaallah nimelipenda from Qatar
Naam naweza
@@abdulkarimkuchengwa4900 +254785221321
mbuzi inamwaga Tui hahahahahahahaha
Hili shairi ni zuri sana
Maa shaa Allah
Wow santaa sana kuchengwa
Mashaallah
First to comment.this is Laylathu swaleh at facebook. Com
Matus hayo ujue hahahaha
Safi sana maa shaa Allah
Safi sana
Sina lakusema kaka😂🤣
Hongera
Swadakta
Aya weee fundi mkwezi wa minaz kkkkkkk
Mime kuona baby👍 by Addam rehema
Safi kuchengwa,heko
Maashallah
Patam apo😍
mafumbo yalosheheni,,napenda mashairi yako
Upo vizur
mmmmh patamu hapa findi wa kukuna mazi mjuzi sana
Mashairi mazuri wekn sauti vipmbona haiendi Sawa?
Kuchengwa Yule dogo anajua jikaze bro
Aejjab
MashaAllah
Hahahaha jamani hiyo Nazi sasa Aya bhana
Mashaallah