Wizara ya Kilimo kununua Ndege 2024/25, Mashamba kunyunyizia dawa kwa Drone Songwe

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 28 ส.ค. 2024
  • Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), Profesa Joseph Ndunguru amesema kuwa mamlaka hiyo imeanza matumizi ya akkilibandia hasa matumizi ya ndegenyuki (Drones) kwenye unyunyiziaji wa dawa kwenye mashamba ya wakulima nchini.
    Ndunguru ameyasema hayo wakati akizungumza nasi kwenye maonesho ya Wizara ya Kilimo Bungeni jijini Dodoma yanayoendelea wakati Bunge likiendelea kujadili bajeti ya wizara hiyo iliyowasilishwa jana Alhamis, Mei 2, 2024 bungeni, ambapo ameeleza kuwa tayari wameanza matumizi ya ndegenyuki kunyunyizia dawa kwenye mashamba ya wakulima.
    Aidha kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya TPHPA, Profesa Andrew Temu amesema bajeti ya Wizara ya Kilimo kwa mwaka 2024/25 inakwenda kuifanya taasisi hiyo kuwa ya kkiteknolojia ambayo itaiwezesha taasisi hiyo kununua ndege ya kunyunyizia dawa kwa mwaka 2024/25.

ความคิดเห็น •