Maisha Ya Zuchu Kabla Ya WCB : "Nilitaka Kuwa Mwanasheria" | SALAMA NA ZUCHU PART 1

แชร์
ฝัง
  • เผยแพร่เมื่อ 16 ต.ค. 2022
  • #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
    Kuna usemi mmoja unaenda kama hivi, kulea mimba si kazi ila kazi ni kulea mtoto, tafsiri yangu naamini mhenga hapo alikua anatuambia kazi pengine inaanza baada ya kupata kazi, tunaelewa jinsi gani ambavyo kupata kazi huwa ni kazi. Tena kazi yoyote, haijalishi kama ni ya upishi au ulinzi au ufundi au hata u daktari, mi nawajua madaktari kadhaa ambao nao pia wanapata shida kupata hizo kazi. Na baada ya kupata shida zote hizo wakati wa kutafuta kazi basi kazi halisi huanza pale unapoipata sasa hiyo kazi yenyewe.
    Kazi ya Zuchu ilianza kabla hajaipata hiyo kazi yenyewe na ilikua kazi haswa kuipata na Mama yake Bi Khadija Kopa ndo alikua kinara kwenye hiyo connection ambayo Binti yake alikua anaitaka ili aweze kuwa msanii wa Diamond, na hayo ndo yalikua maneno yake hasa, toka alivyorudi kutoka Nigeria kwenye mashindano ya kusaka vipaji na alikua hajielewi elewi kwa kiasi flani ni kitu gani alikua anataka kufanya na kama basi kutakua na la kufanya inabidi liwe kutoka WCB na sio sehemu nyengine yoyote na agulia nini kilitokea? WCB aliipata na kilichokua kinatakiwa baada ya hapo ni UVUMILIVU wa HALI YA JUU.
    Kwenye vitabu vyangu vyote Bi Zuhura Othman Soud ndo muandishi wangu BORA wa KIKE kuwahi kutokea katika kizazi chetu hiki cha Bongo Flava, na naweza sema hivyo wakati wowote iwe usiku au mchana, kipaji hicho ndicho kilichonifanya mimi nistaajabu sana na kutaka kuongea nae na kumuuliza yote yale ambayo nilikua nataka kumuuliza, ingawa humo humo nilikua nishajijibu kutoka kwenye historia ya familia atokayo ingawa hiyo haikutakiwa ndo iwe lazima, lazima mtoto wa Khadija Kopa na Othman Soud awe muandishi mzuri maana wazazi wake wamejaa vipaji tena na Baba yake ndo muandishi mkubwa wa nyimbo nyingi za Mama yake zilizowahi kuvuma.
    Kwa umri wake wakati mwengine hujiuliza kajuaje haya maneno yote, anajua maana yake hii? Kasikia wapi hili neno au pengine je huwa anamfikiria Mama yake (ambaye ndo kipenzi chake na ndo amemlea) wakati anaandika hii? Anaona aibu? Je huwa wanaongelea hayo mashairi wanapokua wawili tu? Mazungumzo huendaje?
    Sasa turudi kwenye kazi hiyo ya kuanza kuifanya baada ya kuipata sasa WCB, ukiachana na msoto mrefu alopitia, WCB wenyewe walikua waangalifu sana kwenye mipango ambayo ilikua ikiandaliwa kwaajili yake, yeye ndo msanii wa KWANZA wa KIKE kuwahi kutokea kwenye label kwahiyo ukichana na kipaji pia uwekezaji wa hali ya juu ulitakiwa ufanyike and boy they did that. Toka single yake ya kwanza mpaka wakati naandika hii Zuchu hakuwahi kuwa na kazi chafu, album yake ya kwanza alotoka nayo ya I am Zuchu ilikua na nyimbo 7 ambazo zote zilienda kufanya vizuri, na mpaka leo kila wimbo ambao anaachia ni wa moto, tukisema namba moja nadhani namba zake pia zinasema hivyo za kila sehemu, hakuna chumvi yoyote ndani yake.
    Vipi sasa anaweza ku maintain hii schedule yake ilojaa mambo kuanzia asubuhi mpaka usiku? Kutoka Jumatatu mpaka Jumapili? Je ana muda kwaajili yake? Ana mpenzi? Mipango yake je? Endelevu? Vipi hizi title ambazo tunampa anazichukuliaje? Kuna pressure yoyote? Na kuhusu familia je? Kuna pressure yoyote kwenye baadhi ya mambo na maamuzi? Na kwenye label nako? Watu na furaha na kazi yake?
    Kwa kuanzia msimu wetu wa TANO nadhani introduction ya Ms Zuchu inatufaa sana na yangu matumaini uta enjoy pia.
    Asante kwa support ya toka siku ya kwanza ulipoanza kutupa macho na masikio yako.
    You’re the best, nakukumbusha tu kwamba mengi yajayo yatakufurahisha In Shaa Allah maana kazi ndo kwaanza imeanza.
    Love,
    Salama
  • บันเทิง

ความคิดเห็น • 239

  • @kanyamaladembelesacko2812
    @kanyamaladembelesacko2812 ปีที่แล้ว +25

    Zuchu kuolewa na Simba ni inshu Kali Sana kwasababu zuchu anaakili kdg, anaweza kuongea anaweza kuelezea in shot anajitaidi Sana anafaa kuwa mke wa boss, blessed.

  • @yakobomsafiri692
    @yakobomsafiri692 ปีที่แล้ว +24

    Salama mungu akubariki na akutie nguvu katika kazi yako bado uturetee daimond platnumz

  • @catenzeki678
    @catenzeki678 ปีที่แล้ว +19

    Mimi nakupa SHADA LA MAUA na pongezi nyingi ukiwa hai kwa kazi nzuri.Naomba umlete Harmonize,Roma na Stamina

  • @salajohn6633
    @salajohn6633 ปีที่แล้ว +23

    Amazing interview..Zuchu anaongea vzur sana n yuko real yaan

  • @janethmihayo6337
    @janethmihayo6337 ปีที่แล้ว +17

    Nimekupendq zuchu wew mara ya kwanza leo❤️❤️❤️❤️Nakupenda

  • @charliestyles5535
    @charliestyles5535 ปีที่แล้ว +21

    Bonge la interview! Please we also need interview ya salama na sky tanzania,itakuwa balaa 🙌

  • @fathiyaomar9009
    @fathiyaomar9009 ปีที่แล้ว +29

    Omar aliumwa sana na alikuwa rafikiyangu sana na mara ya mwisho aliimba gofu lakini alikuwa tayari anaumwa mwenyezi mungu amsameh makosa yake na sisi pia amin

    • @rosemahenge9071
      @rosemahenge9071 ปีที่แล้ว +6

      Marehemu anasamehewaje jamani kama hakutubu angali hai ndiyo basi tena ila sisi tulio hai ndio twapaswa kutubu makosa yetu na Mungu mwenye rehema atatusamehe🤲

    • @ukhtyzainab7254
      @ukhtyzainab7254 ปีที่แล้ว +1

      Aamiin

    • @alwatansharyf9294
      @alwatansharyf9294 ปีที่แล้ว +3

      @@rosemahenge9071 sisi waislamu tunayo nafasi ya kuwaombea dua watu wetu waliokwishaondoka duniani ni zawadi pekee Mola wetu alotujaalia kuwatunuku watu wetu

    • @rosemahenge9071
      @rosemahenge9071 ปีที่แล้ว

      @@alwatansharyf9294 Kumbe!!

    • @salomewandya7257
      @salomewandya7257 ปีที่แล้ว +1

      @@alwatansharyf9294 kabisaa na ndiyo maana uwa wanasomewa dua marehemu

  • @yustayusuph9101
    @yustayusuph9101 ปีที่แล้ว +10

    Daaa! hadi mimi nimelia story ya omari 😭😭

  • @AfiSoul103
    @AfiSoul103 ปีที่แล้ว +6

    Nampenda Salama jamani.. she's natural

  • @sarahlondo7597
    @sarahlondo7597 ปีที่แล้ว +27

    Was really waiting for this one😂😂❤️‍🔥❤️‍🔥

  • @diva_20162
    @diva_20162 2 หลายเดือนก่อน +1

    I like her voice jaman Mungu fundi asee ❤❤

  • @aminaomary5567
    @aminaomary5567 ปีที่แล้ว +3

    Huyu mtoto namkumbuka toka akiwa mdogo anakuja na MAMA yake Ushirika Club Mtwara 93.Zuchu anaimba vibaya sana.👍👍👍😁😁😁

  • @jamaalsaleem2926
    @jamaalsaleem2926 ปีที่แล้ว +6

    Wakwanza kucoment🔥🔥

  • @victoriamkumbo5866
    @victoriamkumbo5866 ปีที่แล้ว +1

    Zuchu nakupenda sana kwani uko lmakini hakiwewe mtotowa mtani usiyumbishwe nakupenda asante mwanangu

  • @sifasiraji2903
    @sifasiraji2903 ปีที่แล้ว +10

    Zuchu kama Zuchu❤️

  • @athumanahmadramadhan9220
    @athumanahmadramadhan9220 ปีที่แล้ว +5

    Natamani napenda na nataka sana siku moja umlete Alhaji Dr Sule kwenye interview hii nzuri inayonipa elimu pia ktk maisha haya

  • @somaliandnorway
    @somaliandnorway ปีที่แล้ว +16

    Zuchu i understand your pain my grand ma dies and i was not told and i was also in bording school..it hapoened the same to me and now i lost my mum 4 months ago …death is painful😢😢😢

  • @theodoreconstantine2565
    @theodoreconstantine2565 ปีที่แล้ว +2

    Huyo ndo salama banna lazima akulize alaf akuchekeshe you are the best salamaa I appreciate your work .

  • @ibrahimhumanamicroscopic6515
    @ibrahimhumanamicroscopic6515 ปีที่แล้ว +15

    First time to listen zuchu voice 🥰🥰 that's was nice

  • @sporttv9449
    @sporttv9449 ปีที่แล้ว +5

    Hapo pa "aaaahaa mimba".hiyo nimeipenda ha ha ha

  • @niyonkurufadhoulillah4916
    @niyonkurufadhoulillah4916 ปีที่แล้ว +7

    You know what ? Mimi nazani wawekezaji wawekeze kwenye club ya ma star iwe VIP yani isiw fasi ya show no iwe fasi yao ya ku enjoy tu afu kingilia kiwe ju sana kwa watu wasio kuwa marufu so then wa sani munaweza kua muna enjoy maisha yale munayo ya miss kama watu wangine wote sababu sizani kama msani kama msani ni rahisi kutoka kwenda club ao kwenye migahawa

  • @wakisawakisa5455
    @wakisawakisa5455 ปีที่แล้ว +2

    ckutegemea kama Zuchu angezungumza vzr namna hii, kuna vitu vya msingi ktk tasnia yetu ya muziki na maisha kwa ujumla amevizungumza cjui kama watu wamevinote...anyways, asilimia kubwa ya wanaokuja hapo huwa wanafanya hvyo ila kuna muda hutegemei sana kwa mtu huyo but hii imenifurahisha coz ckutegemea, it's good...Love u Zuu

    • @kantai737
      @kantai737 ปีที่แล้ว +1

      Zuchu is very intelligent na mature, listen to all her interviews and u will be impressed, it’s only that she has a bubbly personality and petite body so ppl think she is childish.

  • @kantai737
    @kantai737 ปีที่แล้ว +12

    Finally was really waiting for this

  • @joysarah
    @joysarah ปีที่แล้ว +33

    You can't get tired listening to her interviews..our smart queen 🔥🔥

  • @shuu62
    @shuu62 ปีที่แล้ว +21

    Finally, it's here‼️ Keep up the great work girls 😊

  • @edgardevis8152
    @edgardevis8152 ปีที่แล้ว +4

    🙌🙌🙌👌👌👌👌🙏 aunt salama respect Sana naomba umlete na marioo plz

  • @mwasitihamisi8421
    @mwasitihamisi8421 ปีที่แล้ว +5

    Ur my best interviewer ❤

  • @supertal2943
    @supertal2943 ปีที่แล้ว +13

    Awesome interview ever👌

  • @princessiyalicious4185
    @princessiyalicious4185 ปีที่แล้ว +8

    Salama unafnya kaz nzur sna....

  • @melangachikubati9253
    @melangachikubati9253 ปีที่แล้ว +4

    Salama please, if posible find time for sky worker a real jita man with wonderful voice ever, i am watching all the way from Ukerewe the sunshine ground.

  • @irenevicky4656
    @irenevicky4656 ปีที่แล้ว +2

    Zuchu you are 👌👍a star lots of love❤❤❤💖💖

  • @sistersade9039
    @sistersade9039 ปีที่แล้ว +30

    Lovely interview and it's wonderful to get to know zuchu closer. Salama wewe ni bigwa wa watangazaji unajua ivyo sio? All the best 🥰

  • @emanuelkiwanuka578
    @emanuelkiwanuka578 ปีที่แล้ว +6

    Asanteni nimeisubili kwa Hamu sana hii

  • @mahmoudaziz4717
    @mahmoudaziz4717 ปีที่แล้ว +13

    Big up salama. Nime enjoy interview mzuri kiswahili safi. Safi zuchu.

  • @hamedabashir9
    @hamedabashir9 ปีที่แล้ว +8

    Niliisumbilia sana 💋🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿♦️❤️😍

  • @mwabiawahadi6247
    @mwabiawahadi6247 ปีที่แล้ว +6

    Nakukubali Sana Zuch

  • @SultanDean
    @SultanDean ปีที่แล้ว +15

    I love your interviews. They are so deep and informational

  • @browngennestone5979
    @browngennestone5979 ปีที่แล้ว +7

    GOOD WORK

  • @radjabreezy5564
    @radjabreezy5564 ปีที่แล้ว

    🇷🇼🇷🇼🇷🇼Salama asante kwaku tuletea Mzee wetu 🇷🇼Sheikh Kipozeo Asante kwa elimu 😊😊😊 ila sijapenda huja mkirimu Sheikh sijapenda lol tumependa kipindi next Time tutapenda kumuona Sheikh Mazinge mbele ya camera love from Rwanda🇷🇼

  • @queenlinda255
    @queenlinda255 ปีที่แล้ว +13

    Amevaa viatu gani jamani huyu binti 😂😂😂

    • @fortunatemushi4943
      @fortunatemushi4943 ปีที่แล้ว

      Yaani mpaka nimecheka! Hayo maviatu hapana hata kama fashion mmh mi hapana

  • @remybuyenzi1856
    @remybuyenzi1856 ปีที่แล้ว +11

    ❤❤❤❤❤❤ nimekua naisubiri kwa ham kubwa

  • @kristofuraha3369
    @kristofuraha3369 ปีที่แล้ว +11

    Nimefurahi sana aisee!!🔥❤👊

  • @maliamjuma9376
    @maliamjuma9376 8 หลายเดือนก่อน +1

    nawapenda sana munguawabariki lnshallah

  • @hildahwangari4337
    @hildahwangari4337 ปีที่แล้ว +1

    She is doing good congrats

  • @samilaamlli3474
    @samilaamlli3474 ปีที่แล้ว +9

    ilove you zuchu

  • @florencekaranja8736
    @florencekaranja8736 ปีที่แล้ว +9

    Everyday I was checking on this interview en now here it is

  • @saudahassan6667
    @saudahassan6667 ปีที่แล้ว +3

    Nakupenda sana salama na zuchu

  • @aishambise6529
    @aishambise6529 ปีที่แล้ว +3

    Nawapenda sanaas ❤❤❤❤🙏🏻

  • @piusphilip307
    @piusphilip307 ปีที่แล้ว +2

    You are really cofident, yaani huigizi, I like you

  • @chaneldici4083
    @chaneldici4083 ปีที่แล้ว +6

    My salama jabir❤❤ from🇧🇮

  • @paulonjozi1638
    @paulonjozi1638 ปีที่แล้ว +7

    Naitaman nakuisubr salama na young killer msodok

  • @eliassanga6907
    @eliassanga6907 ปีที่แล้ว +7

    Joelnanauka na MaxRioba fanya ivi vichwa vidondoke studio vina madini

  • @marymsaid3540
    @marymsaid3540 ปีที่แล้ว +7

    Nampenda sana zuchu ❤❤

    • @foodbasiccourt2028
      @foodbasiccourt2028 ปีที่แล้ว +1

      Hata mimi ila kuwa na mahusiano na kiruka njia diamond i am worried for her career

  • @keyla3641
    @keyla3641 ปีที่แล้ว +2

    Interview nzuri sana

  • @mahfoudh.official7318
    @mahfoudh.official7318 ปีที่แล้ว

    Wa zanzibar 2 🎤🌍

  • @faudhiasalum7279
    @faudhiasalum7279 ปีที่แล้ว +8

    Tuli kata tamaaa kabisa eeh🙄🙄🙄😢😢

  • @jamilamasoud3800
    @jamilamasoud3800 ปีที่แล้ว +10

    Baada yakuisubiri kwa muda mrefu

  • @vanessakiwia7890
    @vanessakiwia7890 ปีที่แล้ว +7

    Zuchu we comedian ila ujijui wallay 🤣🤣🤣 yani mwanzo mwisho nacheka wallay

    • @lulu-xd7to
      @lulu-xd7to ปีที่แล้ว

      Na story ya Omar umecheka

  • @mochakeno9123
    @mochakeno9123 ปีที่แล้ว +7

    My own girl

  • @rosemahenge9071
    @rosemahenge9071 ปีที่แล้ว +7

    Hahaha ila Zuchu na ucomedian anao🤣🤣

  • @zizahissa8642
    @zizahissa8642 ปีที่แล้ว +12

    I was really waiting for loooooog 🙌🙌🙌🙌❤️❤️❤️

  • @samtelah7578
    @samtelah7578 ปีที่แล้ว +6

    Mlete Diamond

    • @wardatkhamis3703
      @wardatkhamis3703 ปีที่แล้ว

      Mtihani eti mungu jaman kweny balaa hili pia mung anashirikishwa??? Au ni bilisi ndio mwenyw jmn

  • @stellah3844
    @stellah3844 ปีที่แล้ว +5

    Zuchu💓💓💓💓

  • @conaddaud9502
    @conaddaud9502 ปีที่แล้ว +4

    🔥🔥

  • @yasintadavid1296
    @yasintadavid1296 ปีที่แล้ว +1

    Thanks

  • @stevennyondo2215
    @stevennyondo2215 ปีที่แล้ว +5

    Kweli mlikuwa closer hadi unamwambia kaka nimevunja ungo!!😂

  • @evanathings9554
    @evanathings9554 ปีที่แล้ว +12

    I love Zuchu ❤

  • @rogersodero3897
    @rogersodero3897 ปีที่แล้ว +3

    Pls bring Esha Buheti

  • @esthermusanga8118
    @esthermusanga8118 ปีที่แล้ว +2

    Hongera zuchu kazi smart

  • @SAVPTVOnline
    @SAVPTVOnline ปีที่แล้ว +1

    good girl

  • @jokhaaliy3720
    @jokhaaliy3720 ปีที่แล้ว +2

    Music na law bora dhambi kubwa ipi

  • @winfridangoloke1916
    @winfridangoloke1916 ปีที่แล้ว +5

    Hatimaeeeeee

  • @japhtv9858
    @japhtv9858 ปีที่แล้ว +4

    Oya kingereza kingi bhana

  • @lareineminah1353
    @lareineminah1353 ปีที่แล้ว +3

    Tuulisubiriii sana😍😘

  • @loganpoul
    @loganpoul ปีที่แล้ว +5

    Salama lakini wajua nakupenda Sana?mamangu pia anaitwa salama so nikikuona naburudika Sana kama namuona mamangu,

  • @hamisamsimbe4613
    @hamisamsimbe4613 ปีที่แล้ว

    Mm mwenyewe nilimpenda sana omary kopo mungu amsamehe dhambi zake

  • @RuzoOwzy
    @RuzoOwzy ปีที่แล้ว +1

    00:50
    Subira yavuta kheri.
    Haraka haraka haina baraka.
    Hizi si zinashabihiana, ziko fresh tu.
    Au kachanganya na
    Ngoja ngoja huumiza matumbo!!!

  • @mammymammy997
    @mammymammy997 หลายเดือนก่อน

    Zuchu Allah amubariki nampenda sana

  • @user-ki9le1jy8e
    @user-ki9le1jy8e วันที่ผ่านมา

    Wanao uliza kuhusu uvaaj miwan sjui nguo sjui viatu jmn hili swal muwaulize mafundi huko viwandan najua wanajua walichokifanya mpk kutengez nasisi kukubali jmn wat mjaj maisha yenu mkuta wengin mnataman kupat alivyo navyo lkn ndo hivyo 😅😅

  • @jennytugara9470
    @jennytugara9470 ปีที่แล้ว

    Go for it girl. elimu haikomi hata kina Kardashian wanafanya urembo na kasoma Sheria juu yake. Music ni era inafika mahali inaisha.

  • @faudhiasalum7279
    @faudhiasalum7279 ปีที่แล้ว +5

    Au bi kikalala au mzeee kikalala tuomba

  • @judithjulius5993
    @judithjulius5993 ปีที่แล้ว +3

    Hivi watu wanaosemaga zuchu ana sura mbaya Wana Nini! Mbona Binti mrembo hivi

    • @EugeneUroki
      @EugeneUroki 7 วันที่ผ่านมา

      Kwasababu anamakali😅

  • @modysaid8439
    @modysaid8439 ปีที่แล้ว +34

    Hy zuu Mimi ni fan wako but kuna kitu naomba urekebishe,ukiwa Kwa interview usionge wakati unaulizwa swali just wait untill swali liishe ulielewe coz sio Kila interviewer ni anakupenda so anaweza kutumia weakness yako ya ku interrupt swali na ku kufanya ujibu kitu ambacho sio sawa so jaribu kuwa calm coz your a superstar my dear

    • @anthonym2542
      @anthonym2542 ปีที่แล้ว +3

      Sijaskiza interview lakini Akili Yako IPO sawa kaka

    • @hawasaid7151
      @hawasaid7151 ปีที่แล้ว

      Good 👏👏

    • @awatifalghanim1106
      @awatifalghanim1106 6 หลายเดือนก่อน

      Ni kweli umesema👍

  • @stevewanga957
    @stevewanga957 ปีที่แล้ว +5

    Si aongee kiswahili tu..

  • @shaluuanthony1836
    @shaluuanthony1836 ปีที่แล้ว +3

    Our zuchu

  • @mwanatumusalim1558
    @mwanatumusalim1558 ปีที่แล้ว +4

    Kiatu sasa zuchu 😁😁😁

  • @yusraramadhan8203
    @yusraramadhan8203 ปีที่แล้ว +2

    😍👏🏿👏🏿

  • @iradukundalvs4423
    @iradukundalvs4423 ปีที่แล้ว

    Vma sana

  • @mwasity2348
    @mwasity2348 ปีที่แล้ว +2

    💕♥️💕💕♥️

  • @abenawemubaraka6681
    @abenawemubaraka6681 ปีที่แล้ว

    Zucu y Lev u 2 am mubaraka from kanpara

  • @edwinmbugua7738
    @edwinmbugua7738 ปีที่แล้ว +3

    Tnaomba Lavalava pia

  • @aishadotto3640
    @aishadotto3640 ปีที่แล้ว

    Pole Zuchu

  • @chimamyatu4124
    @chimamyatu4124 ปีที่แล้ว +2

    ♥️♥️♥️♥️

  • @farajavilla2379
    @farajavilla2379 ปีที่แล้ว +1

    Mziki sio masiharaaa na hanstone kapewa uo mtihani wa kustahmili lkn umemshinda

  • @isihaqkerdehaqker1403
    @isihaqkerdehaqker1403 ปีที่แล้ว +5

    Sauti km mama yake

  • @mercypeter162
    @mercypeter162 ปีที่แล้ว +7

    Viatu vya zuchu sijui V inatokaga kiwanda gain Ahahahahaaaa Salama mulize zuchu Na kuhusu viatu

  • @iddmohammed1086
    @iddmohammed1086 ปีที่แล้ว +2

    Lafudh tamu mno ya kizanzibari baina ya wazanzibari hawa wawili.

  • @basilmwalongo6149
    @basilmwalongo6149 ปีที่แล้ว

    Zuchu♥️♥️♥️

  • @jacintabati6238
    @jacintabati6238 ปีที่แล้ว +10

    I LOVE ZUCHU SO MUCH.....I THINK AM OBSESSED WITH HER 😍🥰😘🤩❤❤❤

    • @robionaire
      @robionaire ปีที่แล้ว +3

      Zuchu is way above Diamond league. She is gorgeous, smart and well educated. Diamond amwachie kina Hamisa na Zari. You deserve so much better Zuchu. Someone at your level.

    • @waridirose8734
      @waridirose8734 ปีที่แล้ว +1

      @@robionaire I my thoughts too. Zuchu has everything to get a higher quality man. Awachane na diamond alee watoto

    • @eysherqdout8361
      @eysherqdout8361 ปีที่แล้ว +1

      Same🥰

  • @BigZhumbe
    @BigZhumbe ปีที่แล้ว +5

    Zuchu namkubali miaka buku... great soul, great mind I love you to death and eternity ❤️ ♥️ 💗 💓 💕